Sisi watanzania tunaoishi Sweden kwa majonzi na masikitiko makubwa tunatoa pole zetu kuwafikia familia zilizoguswa na msiba, shule ya Lucky Vicent Arusha na Taifa kwa ujumla kwa kupoteza watoto, dereva, na waalimu.
Habari hizi zimetugusa sana na kuleta simanzi na masikitiko makubwa katika jamii ya Watanzania hapa Sweden. Tunapendelea pia kuipongeza serikali yetu kwa jitihada zake za kukabiliana na janga hilo bila kupoteza wakati na pia kuwafariji wafiwa katika wakati huu mgumu.
TUNATANGULIZA UPENDO NA MSHIKAMANO KWA TAIFA LETU
KWA NIABA YA WATANZANIA SWEDEN
MWENYEKITI
NORMAN JASSON