Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117024

Lake Cement inalinda mazingira ya wananchi wa Kimbiji –Katemba

$
0
0
 
Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii 

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni , Stephen Katemba amesema kiwanda cha Lake Cement kinafuata sheria za utunzaji wa mazingira kwa wananchi wa Kimbiji. 

Katemba amesema hayo wakati alipokwenda kusherekea siku ya wafanyakazi na kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii zinazofanywa na Lake Cement, amesema kuwa kiwanda kwa kufuata sheria ya mazingira na sheria za wafanyakazi kamwe migogoro haiwezi kutokea. 

Amesema kuwa wafanyakazi lazima wafanye kazi kwa kujituma ili kiwanda kiweze kujiendesha katika kuweza kufikia malengo ya kutimiza kwa wafanyakazi wake. 
Katemba amesema wakati kitendo cha Kiwanda kudhamini mashindano mbalimbali katika eneo la kimbiji ni kuonyesha kiwanda kinajua wajibu wake. 

Makamu wa Rais wa Lake Cement , Afroz Ansary amesema wanawajibu wa kuwa karibu na jamii ya Kimbiji katika shughuli za kijamii . Mafanikio ya kiwanda yanatokana na jamii inayozunguka kushirikiana katika masuala mbalimbali ya kijamii. 

Nae Afisa Utumishi wa Kiwanda hicho, Ahmed Mstapha amesema kuwa kiwanda cha Nyati Cement kinatekeleza majukumu yake kwa jamii inayozunguka kiwanda hicho. 

Amesema kuwa wataendelea kuwa karibu na wananchi katika shughuli mbalimbali ambazo zinajitokeza katika eneo la Kimbiji.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni, Stephen Katemba akizungumza na wafanyakazi mara baada kutembelea kiwanda hicho katika siku ya wafanyakazi na kushiriki shughuli mbalimbali ikwemo ya upandaji jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Lake Cement, Afroz Ansary akizungumza juu ya udhamini wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na kiwanda hicho.
Meneja Rasilimali Watu wa Lake Cement, Julieth Domel akizungumza juu jinsi wanavyoshugulika na wafanyakazi wa kiwanda kwa kufuata sheria za Kazi. 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117024

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>