Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Kilimanjaro na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Said Meck Sadik pamoja na viongozi wengine wa Serikali pamoja na Chama Cha Mapinduzi katika uwanja wa ndege wa KIA. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).Makamu wa Rais atahudhuria sherehe za wafanya kazi Mei Mosi zitakazofanyika kitaifa mkoani Kilimanjaro.
