Na Karama Kenyunko
Mshtakiwa Mary Amokowa, ameiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imuachie huru kwani hakuhusika na tuhuma za kusafirisha wasichana 10 kutoka Tanzania Kwenda Kenya kwa ajili ya biashara ya ngono.
Mshtakiwa huyo ambaye ni raia wa Kenya ameiomba mahakama imuachie huru kwa kuwa madai ya kesi hiyo ni ya uongo na ya kutengenezwa.
Ameyasema hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godifrey Mwambapa wakati akitoa utetezi wake dhidi ya kesi hiyo inayomkabili yeye,Jackline Milinga na Simon Alex Mgawe.
Akiongozwa na wakili wake Nehemia Nkoko,Mary amedai kuwa yeye ni mfanyakazi wa kampuni ya simu ya safari Com iliyopo Nairobi Kenya. Amedai kuwa, Septemba 4,2015 akiwa na rafiki yake Jackline walisafiri kwa kutumia basi la Mordem Coast kutoka Dar es Salaam kwenda Nairobi.
Ameongeza kuwa walikuwa na tiketi na pasi za kusafiria lakini walipofika Namanga mpakani mwa Kenya na Tanzania, akiwa tayari amekwisha gongewa mhuri wa kutoka Tanzania na akiwa katika foreni ya kusubiri kugongewa muhuri wa kuingia Kenya, askari wawili wa Uhamiaji wa Tanzania walimkamata Jackline.
Amedai walipomkamata walimwambia wana wasiwasi na hati yake ya kusafaria kwa sababu alikuwa na hati ya kusafiria ya kidiplomasia na baadaye walibaini haijaghushiwa ni halali.
Amedai kuwa, baada ya pasi ya rafiki yake kuonekana kuwa ni halali na wote wakati huo walikuwa chini ya ulinzi aliomba waachiwe huru, baada ya kutuchukua maelezo lakini hawakutuachia. Badala yake wakatuweka sehemu moja na hao wasichana 10, ambao tulikaa nao siku nne Uhamiaji Makao Makuu na kwamba walipohamishiwa uhamiaji mkoa hawakuwa na hao wasichana.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Mshtakiwa Mary Amokowa, ameiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imuachie huru kwani hakuhusika na tuhuma za kusafirisha wasichana 10 kutoka Tanzania Kwenda Kenya kwa ajili ya biashara ya ngono.
Mshtakiwa huyo ambaye ni raia wa Kenya ameiomba mahakama imuachie huru kwa kuwa madai ya kesi hiyo ni ya uongo na ya kutengenezwa.
Ameyasema hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godifrey Mwambapa wakati akitoa utetezi wake dhidi ya kesi hiyo inayomkabili yeye,Jackline Milinga na Simon Alex Mgawe.
Akiongozwa na wakili wake Nehemia Nkoko,Mary amedai kuwa yeye ni mfanyakazi wa kampuni ya simu ya safari Com iliyopo Nairobi Kenya. Amedai kuwa, Septemba 4,2015 akiwa na rafiki yake Jackline walisafiri kwa kutumia basi la Mordem Coast kutoka Dar es Salaam kwenda Nairobi.
Ameongeza kuwa walikuwa na tiketi na pasi za kusafiria lakini walipofika Namanga mpakani mwa Kenya na Tanzania, akiwa tayari amekwisha gongewa mhuri wa kutoka Tanzania na akiwa katika foreni ya kusubiri kugongewa muhuri wa kuingia Kenya, askari wawili wa Uhamiaji wa Tanzania walimkamata Jackline.
Amedai walipomkamata walimwambia wana wasiwasi na hati yake ya kusafaria kwa sababu alikuwa na hati ya kusafiria ya kidiplomasia na baadaye walibaini haijaghushiwa ni halali.
Amedai kuwa, baada ya pasi ya rafiki yake kuonekana kuwa ni halali na wote wakati huo walikuwa chini ya ulinzi aliomba waachiwe huru, baada ya kutuchukua maelezo lakini hawakutuachia. Badala yake wakatuweka sehemu moja na hao wasichana 10, ambao tulikaa nao siku nne Uhamiaji Makao Makuu na kwamba walipohamishiwa uhamiaji mkoa hawakuwa na hao wasichana.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA