
Mpango wa kufikia uchumi wa kati unalenga kuiwezesha serikali kujitegemea na tayari hatua mbalimbali zimechukuliwa ili kuweza kufikia azma hiyo.
Dira ya Taifa ya Maendeleo, imeainisha malengo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujenge uchumi imara wenye uwezo wa kukabiliana na ushindani.
Katika kuhakikisha mkakati huo unafanikiwa Serikali imeweka sera na mazingira mazuri kwa ajili ya kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza kwenye viwanda.
Hivi karibuni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikwenda nchini Mauritius kumwakilisha Rais Dk. John Magufuli kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Uchumi Barani Afrika (AEP).
Baada ya kumaliza uzinduzi huo Waziri Mkuu alipata fursa ya kutembelea viwanda mbalimbali nchini Mauritius na kuhamasisha wawekezaji waje nchini ili kuongeza uzalishaji utakaokuza uchumi na kuongeza pato la taifa.
KUSOMA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA