Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117045

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA PROF PALAMAGAMBA KABUDI AWASILI OFISINI MJINI DODOMA

$
0
0
Waziri wa Katiba na Sheria Prof.Palamagamba Kabudi amewasili katika Ofisi za Makao makuu ya Wizara zilizoko ndani ya Chuo Kikuu cha Dodoma na kulakiwa na watumishi wa Wizara walioko makao makuu ya Serikali mjini Dodoma. 

Prof Kabudi aliapishwa tarehe 24/03/2017 Ikulu jijini Dar Es Salaam kuchukua nafasi hiyo baada ya Mhe.Rais kufanya mabadiliko madogo kwenye Baraza la Mawaaziri ambapo Dkt. Harrison Mwakyembe alihamishiwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. 

Nje ya Ofisi za Wizara Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi alilakiwa na Naibu Katibu Mkuu, Bw. Amon Mpanju, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bw. Aloyce Mwogofi, Jaji Mfawidhi Kanda ya Dodoma na wafanyakazi wengine wa Wizara waliopo Makao Makuu ya Serikali mjini Dodoma.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.Palamagamba Kabudi akipokea shada la maua kutoka kwa mtumishi Joyce Mtuma mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.Palamagamba Kabudi akiangaalia kadi ya Pongezi iliyoasiniwa na watumishi wa wizara mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma
WaziriwaKatibanaSheriaMhe. Prof.Palamagamba Kabudi akisalimiana naNaibu Katibu Mkuu Bw. Amon Mpanju mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma


Waziri wa Katiba na SheriaMhe. Prof.Palamagamba Kabudi akisalimiana na Jaji mfawidhi Kanda ya Dodoma Mhe. Mwanaisha Kwariko alipowasili Wizarani mjini Dodoma




Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.Palamagamba Kabudi akisikiliza maelezo mbalimbali alipokutana na watendaji wa Wizara na Mahakama katika ukumbi wa mikutano Wizarani mjini Dodoma

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117045

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>