Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117046

TIC YAINGIA MAKUBALIANO YA MRADI EAST AFRICA AND INVESTIMENT HUB

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) kimesaini makubaliano ya Mradi wa East Africa and Investiment Hub kwa ajili ya uchocheaji wa uwekezaji nchini.

Akizungumza wakati wa makubaliano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari amesema kuwa makubaliano hayo yatachochea uwekezaji pamoja na upatikanaji wa masoko nje ya nchi.

Tandari amesema katika kufanya kazi ya mradi huo utasaidia Tanzania kupata wawekezaji kutokana na wigo uliopo katika mradi unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID).

Aidha amesema mradi huo ni wa miaka mitano ambao TIC  inaingia katika makubaliano, tayari  miaka mitatu umefanya kazi katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Aliongeza kuwa mpaka kumalizika kwa mradi huo nchi itanufaika na kodi pamoja na kuongezeka kwa ajira kwa  vijana.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Cliford Tandari akizungumza na Mkurugenzi wa Mradi wa East Africa and Investiment Hub, Kanini Mutooni baada ya kusaini makubaliano ya mradi huo leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari akibadilishana hati na Mkurugenzi wa Mradi wa East Africa and Investiment Hub, Kanini Mutooni leo Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Watendaji wakuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini, wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari akiwa katika picha ya pamoja na watu wanaotekeleza mradi East Africa and Investiment Hub pamoja na watendaji wa TIC leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massak,Globu ya jamii.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117046

Trending Articles