Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Serikali ya Korea kupitia mradi wa ''Thank you Small Ribray program'' leo imekabidhi Vifaa na kuzindua maktaba ndogo ya kisasa katika ofisi za makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo balozi wa Korea nchini Song Geum Young amesema kuwa serikali yake licha ya kusaidia serikali katika miradi mingi lakini kwa sasa wameamua kusaidia katika kuwawezesha watoto kupata elimu inayoendana na wakati.
"sisi kama korea tunaamini kuwa ukimpa mtoto elimu umeweza kumpa maisha ya kesho, hivyo vifaa hivi vitaweza kuwasaidia katika kukuza taaluma yao " amesema Balozi.Balozi ametoa wito kwa wazazi kuwaleta watoto waweze kutumia maktaba hiyo kwa kutumia sehemu hiyo kwa ajili kukuza taaluma yao .
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akiwa na Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young na Mama Anna Abdalah Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Makumbusho ya Taifa wakikata utepekuashiria uzinduzihuo.
Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young akizungumza kabla ya uzinduzi wa wa Maktaba ya kisasa ambayo imetolewa na Serikali ya korea.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo, akikabidhi vitabu kwa Mwenyekiti wa bodi ya Makumbusho ya Taifa , Mama Anna Abdalah
Mkurugenzi Mtendaji wa Makumbusho ya Taifa , Audax Mabula akizungumza kabla ya uzinduzi wa Maktaba ya Kisasa katika Makumbusho ya Taifa.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akizungumza kabla ya uzinduzi wa Maktaba ya Kisasa katika ukumbi wa Makumbusho ya taiafa kwa msaada wa Serikali ya watu wa Korea.