Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117138

DC WA SAME MHE. ROSEMARY SENYAMULE AKAMATA SHAMBA LA MIRUNGI NA WAKULIMA WAKE

$
0
0
Na MatukiodaimaBlog Same 
MKUU wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro Mhe. Rosemary Sitaki Senyamule ambae ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ameendelea na mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa kukamata shamba la mirungi. 
 Mkuu huyo wa wilaya amesema  kuwa Shamba hilo limekamatwa leo kata ya Vudee, kijiji cha Kisesa wilayani humo pamoja na mtuhumiwa aliyekuwa mmiliki wa shamba hilo. 
 "Tunaendelea na utekelezaji wa agizo la Rais Dkt John Magufuli la kupambana na dawa za kulevya na mbali ya misako endelevu tumekamata pia miche 1450 iliyokuwa ikimwagilia..... analitunza sana shamba lama kama vile ni la  mazao ya chakula"
"Tumewapa siku 2 ndugu zao wahakikishe wameng'oa mirungi hiyo na kuiteketeza" mkuu huyo alisema na kuongezea kwamba  bado kazi ya kuwasaka wote wakulima wa bangi, mirungi na Viroba inaendelea 
 "Watu wamekuwa wagumu sana kuacha hii biashara. Na sisi tutapambana kwa kutolala mpaka mirungi inaisha Ardhi ya Same" alitoa wito kwa wana Same kulima mazao sahihi ya chakula na biashara badala ya kulima bangi na Mirungi ambayo amesema mwisho wake ni jela

Mkuu wa wilaya ya Same Mhe. Rosemary Sitaki Senyamle akiwa na mtuhumiwa mkulima wa Mirungi. 


.
mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamle akiwa katika shamba la Mirungi baada ya kukamata kwa watuhumiwa wakulima wa zao hilo haraamu 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117138

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>