Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117162

DKT SHEIN AFANYA UTEUZI.

$
0
0
Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu namba 17 cha sheria ya utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia namba 6 ya mwaka 2016, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed Shein, amemteua Bwana Omar Zubeir Ismail kuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mamlaka ya Kudhibiti Utafutaji na Uchimbaji wa mafuta na gesi asilia, Zanzibar.

Kabla ya uteuzi huo, Bwana Omar Zubeir Ismail alikuwa Ofisa Mwandamizi katika Idara ya Nishati, Zanzibar.

Uteuzi huo uliosainiwa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, umeanza leo tarehe 18 Machi 2017.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO-ZANZINAR

18 Machi 2017

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117162

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>