Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendesha semina ya kunoa weledi wa taaluma ya uandishi wa habari kwa waandishi wa habari na baadhi ya watumishi wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd, Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, leo katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam. Dk. Ryoba ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), ana shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika Sayansi ya Jamii aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendelea kutoa 'nondoz' kwa wafanyakazi hao wa UPL, huku wafanyakazi hao wakimsikiliza kwa makini sana
Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akifafanua mada zake kwenye semina hiyo ya kunoa weledi wa kitaaluma