
Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili ukumbini kuendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM-Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Mwenyekiti wa chama cha CCM, Rais Dkt Magufuli akiwakaribisha wajumbe kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM na kufungua kikao hicho mapema leo asubuhi,kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar).Dkt Shein,wa tatu kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman .

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza jambo wakati wa kikao cha Kamati Kuu kilichoongozwa na Rais Dkt Magufuli,leo mkoani ni Dodoma,Kulia Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar).Dkt Shein.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi,Rais Dkt John Pombe Magufuli akiongoza Kikao cha kamati kuu ya CCM, mapema leo Mkoani Dodoma.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, anayeshughulikia Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga akizungumza jambo na Katibu wa Itikadi na Uenezi Hamphrey Polepole mapema leo kabla ya kuanza kikao cha kamati kuu,mjini Dodoma

Wajumbe wa Sekretarieti wakijadiliana jambo ukumbini kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma

Kikao cha kamati kuu ya CCM kikendelea.