Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117374

WANAWAKE JIKITENI KATIKA UJASIRIAMALI, UTAWAKOMBOA

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO.

Dunia ya sasa inapigania haki sawa kwa wanaume na wanawake ili waweze kushiriki kwa pamoja kwenye nyanja zote za kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa ajili ya kuchangia kwenye ukuzaji wa pato la taifa na kupelekea kukua haraka kwa maendeleo ya nchi.

Tumeshuhudia wanawake wengi nchini wakijikita katika kufanya biashara na ujasiriamali wa bidhaa na huduma mbalimbali ambazo zinawakomboa kiuchumi na kuwafanya waweze kujitegemea kama walivyo wananume. 

Wanawake hao waliojiamini na kuamua kuanzisha biashara zao wameonekana kuwa na mafanikio makubwa ambayo yanasaidia kuinua uchumi wa mtu binafsi na wa nchi kwa ujumla.

Kwa upande mwingine, baadhi ya wanawake wamekua bado hawana ujasiri wa kuanza kufanya ujasiriamali kwa kuhofia kuwa hawataweza kuendelea na wengine wakihofia waume zao kuwakataza.

Dhima ya kujirudisha nyuma waliyonayo baadhi ya wanawake ndio inayorudisha nyuma hata maendeleo ya nchi hasa kwa wakati huu ambao Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kujikita katika kukuza uchumi wa viwanda.

SOMA ZAIDI HAPA

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117374

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>