Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117374

MAKALA YA SHERIA: JE NI MTOTO WA UMRI GANI ANATAKIWA KUKAA NA MAMA?.

$
0
0
Na  Bashir  Yakub.
Mara  nyingi  wazazi  wanapotengana  huwa  tunashuhudia  mabishano  ya  nani  anatakiwa  kukaa  na  mtoto. Ni  mama au  baba.  Kwa  suala  hilihili wapo  watu  wako  mahakamani  na  wengine  hawako  mahakamani  lakini  wako  katika  ugomvi  mkubwa  wa  nani  haswa  akae  na mtoto.

Wapo  ambao  walikuwa  katika  ndoa  na  sasa  ndoa  imevunjika,  wapo  ambao  walikuwa wakiishi  kama  mke  na  mme  lakini  bila  ndoa  na sasa  mahusiano  yao  yamekwisha  na  wapo  ambao  hawakuwahi  kufunga  ndoa  wala  kuishi  kama  mke  na  mme ila  walizaa  tu  ila  kwasasa  wapo  katika  mgogoro  wa  nani  akae  na  mtoto.

Makala  yataeleza namna  sheria  inavyozungumza  kuhusu  umri  wa  mama  kukaa  na  mtoto  lakini  kabla  ya hilo  ni  vema  pia  kutizama  ni  wapi  waweza  kupeleka malalamiko  ya  jambo  hili. Sheria  ya  Mtoto ,  namba 21 ya  mwaka  2009 ndiyo  inayohusika  katika  jambo  hili.

1.WAPI  UKALALAMIKE  UKITAKA  KUKAA  NA  MTOTO.

Zipo  sehemu  mbili  ambazo  waweza  kupeleka malakamiko  yako  ili  uweze  kupatiwa  haki  ya  kukaa  na  mtoto.  Kwanza  ni  ustawi  wa  jamiii  na  pili  ni  mahakamani. 

Mahakama  yoyote  ya  mwanzo,  wilaya,  hakimu  mkazi  hata  mahakama kuu  unaweza  kupeleka  mombi  haya.  Ila  ni vema  ukaanza  mahakama  ya  mwanzo  au  wilaya. 

Tofauti  ya  ustawi  wa  jamii  na  mahakamani   ni kuwa mahakama  wana  amri  wakati   ustawi  wa jamii  hawana  amri( order) .  


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117374

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>