Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeboresha ofisi zake za kanda za ardhi zilizopo nchini ili kuongeza ufanisi katika kutoa huduma za ardhi karibu zaidi na wananchi.
Wizara imegawa magari katika kanda zake zote ili kurahisisha utekelezaji wa kazi za ardhi na kuharakisha huduma za sekta nzima ya ardhi katika maeneo yote ya nchi badala ya wananchi kuja ofisi za Dar es Salaam ambazo kwa sasa zinahamia makao Makuu ya Nchi Dodoma.
Hatahivyo, huduma nyingine za kisekta kama vile za malipo ya kodi ya pango la ardhi, kituo cha huduma kwa mteja na ofisi za kanda za Dar es Salaam zitaendelea kufanyika kama ilivyokuwa awali.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wakati akitangaza kuhamia rasmi kwa Wizara yake mkoani Dodoma amesema kuwa Wizara imepanga kuwaweka wataalam wa sekta nzima ya ardhi katika ofisi za kanda ili kuondoa usumbufu uliokuwepo wa kufuata huduma za hati, usajili, Uthamini upimaji na ramani na mipango miji na vijiji – Dar es Salaam na Dodoma.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi, Naibu wake Mhe. Dkt. Angeline Mabulla, Katibu Mkuu; Dkt Yamungu Kayandabila na Viongozi wengine wakuu wa wizara wakikagua magari ya kuhudumia ofisi za ardhi za kanda nchini.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akikabidhi funguo ya gari kwa Kamishna wa kanda ya Dar es Salaam; Matthew Nhone.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi, Naibu wake Mhe. Dkt. Angeline Mabulla, Katibu Mkuu; Dkt Yamungu Kayandabila na Viongozi wengine wakuu wa wizara wakikagua magari ya kuhudumia ofisi za ardhi za kanda nchini.