Benki ya NMB imemwakikishia Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kuwa itaendelea kutumia mifumo ya kiteknolojia ili kuwawezesha wateja wa benki hiyo kutumia Zaidi mifumo ya kietroniki kuliko unaotumika Zaidi kwa sasa wa malipo kwa kutumia pesa taslim.
Hayo ya mesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa NMB, Ineke Bussemaker wakati wa ufunguzi wa Kituo cha Kibiashara cha Mtwara na kueleza kuwa nia ya benki ni kuendelea kukua Zaidi huku ikitoa suluhu ya vipau mbele vya serikali na kujikita katika ukusanyaji wa mapato ya serikali kwa njia zakielektroniki.
“Kwa kutumia teknolijia mbalimbali, NMB tumewekeza Zaidi kwenye kutatua changamoto mbalimbali za wateja wetu na hivyo kutoa fursa za kutumia Zaidi njia za benki kuliko kutumia njia za malipo kwa kutumia pesa taslim,” alisema Ineke.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Prof. Joseph Semboja alisema kuwa NMB imefanya maboresho makubwa na hivyo kuwa na uwezo mkubwa wa kutoa huduma za kifedha kwa kila kada ya watanzania na serikali kwa ujumla.
Prof. Semboja alisema kuwaSerikali kwa sasa inamiliki hisa asilimia 32 ndani ya benki ya NMB zenye thamani ya Zaidi ya Bilioni 430 hivyo kuiwezesha serikali kupata gawio la Zaidi ya bilioni 75 ndani ya miaka mitano.
“Kwa mwaka huu mheshimiwa raisi, kama mkutano mkuu wa wanahisa utakaokaa mwezi wa sita mwaka huu, utabariki Kiwango cha gawio, serikali itapata gawio la shilingi Bilioni 16.5 zinazotokana na faida iliyopatikana mwaka 2016,” alisema Prof. Semboja.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB Ineke Bussemaker mara baada kukifungua rasmi kituo cha Biashara cha NMB mjini Mtwara kijulikanac ho kama Mtwara Business Centre. Pamoja na mambo mengine, rais magufuli alimuagiza Waziri wa fedha Dr Philip Mpango kuhakikisha kuwa fedha zote za serikali zinapita NMB.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkurgenzi wa NMB – Ineke Bussemaker wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa kituo cha kibiashara cha NMB – NMB Business Centre mjini Mtwara juzi. Kutoka kulia niAfisa Mkuu wa wateja wadogo na wa kati – Abdulmajid Nsekela, Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi – Prof Joseph Semboja na kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara – Halima Dendegu na Waziri wa Fedha na Uchumi – Dr Philip Mpango.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkurgenzi wa NMB – Ineke Bussemaker wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa kituo cha kibiashara cha NMB – NMB Business Centre mjini Mtwara juzi. Kutoka kulia niAfisa Mkuu wa wateja wadogo na wa kati – Abdulmajid Nsekela, Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi – Prof Joseph Semboja na kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara – Halima Dendegu na Waziri wa Fedha na Uchumi – Dr Philip Mpango.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA