Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Sianga amesema kuwa vita ya kupambana na dawa za kulevya ni kubwa kutokana na kila siku watu wanabuni njia mpya.
Vita ya dawa za kulevya sio lelema kutokana na kuwa watu ambao wana mbinu nyingi za kufanya hivyo, lakini watakamatwa wote na hatuingii kichwa kichwa katika kufanya kazi hiyo.
Akizungumza leo katika hafla ya Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober House) kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
“Watu watano tumewakamta na mmojawapo aliyekuwa anasambaza dawa za kulevya Tanzania Bara na Zanzibar na jumla zaidi watu 11000 wamekamatwa ’’amesema Sianga.
Sianga amesema mtandao wote unaofanya biashara ya dawa za kulevya wameukamata, na wanaendelea kupokea taarifa mbalimbali za kuweza kutokomeza mtandao wa kuingiza dawa hizo.
Amesema wanatumia njia tatu katika kupata taarifa za watu wanaofanya biashara hiyo moja ni taarifa za watu za moja kwa moja ya pili utafiti pamoja wananchi.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Siangaakizungumza katika hafla ya timu ya Serengeti Boys chini ya miaka 17 kutembelea kituo cha watu waliodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani jana.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum akizungumza katika hafla Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu walioadhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani juu ya viongozi wa dini walivyo mstari wa mbele katika kupambana na dawa za kulevya.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Siangaakimkabidhi cheti , Rais wa TFF, Jamal Malizi katika hafla Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu walioadhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Sianga akimkabidhi cheti , Mwakilishi Michuzi Media Group,Emmanuel Massaka katika hafla ya Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu waliodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober House)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Wadau mbalimbali.