Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117409

RC SHINYANGA ATOA MABATI 171 KWA SHULE TATU WILANI KISHAPU

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack ametoa msaada wa mabati 171 kwa shule za msingi tatu wilayani Kishapu mkoani hapa kwa ajili ya kuezekea vyumba vya madarasa pindi yatakapokamilika ujenzi wake.

Telack alitoa ahadi hiyo jana wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ilobi, kata ya Mwaweja wilayani hapa alipofanya ziara ya kikazi ambapo pia alitumia nafasi hiyo kusikiliza kero zao.

Katika msaada huo jumla ya shule tatu za Nyenze iliyopo kata ya Idukilo, Mwasubi kata ya Bunambiyu na Ilobi kwenye kata ya Mwaweja zitanufaika na msaada huo wa mabati 57 kila moja.

Akiwa katika ziara hiyo ya kikazi wilayani hapa, Telack aliagiza wazazi wote kijijini hapo wawapeleke watoto wao na kuwaandikisha shuleni ambapo alisisitiza umuhimu wa elimu kwao.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ilobi kata ya Mwaweja alipofanya ziara ya kikazi. Kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya, Shadrack Kengese.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya wakifuatilia mkutano wa hadhara kijiji cha Ilobi kata ya Mwaweja wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wilayani Kishapu,mkoani Shinyanga.
Mmoja wa wananchi wa kijiji cha Ilobi akitoa kero yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack wakati wa mkutano wa hadhara kijijini hapo.
Wananchi wa kijiji cha Ilobi wakimsikiliza mkuu wa mkoa wakati akizungumza nao kuhusu maendeleo alipofanya ziara ya kikazi.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117409

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>