Quantcast
Viewing all articles
Browse latest Browse all 118057

Mhe. Membe azungumza na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini

Image may be NSFW.
Clik here to view.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (katikati) akizungumza na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali ya kikanda na kitaifa. Katika Mkutano huo Mhe. Membe alifafanua juu ya hali ya kisiasa nchini Madagascar na Zimbabwe na kutoa taarifa za kuwasili kwa vikosi vya kulinda amani vya Tanzania huko Mashariki mwa DRC. Kuhusu masuala ya kitaifa Mhe. Membe alilitolea ufafanuzi suala la shambulio la bomu lilitokea hivi karibuni huko Arusha ambapo alisema kuwa Serikali inaendelea na uchunguzi  na kwa ujumla hali nchini ni tulivu. Wengine katika picha ni Bw. John Haule (kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mhe.Khalfan  Juma Mpango (kulia), Mkuu wa Mabalozi na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hapa nchini. Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Mei, 2013.


Image may be NSFW.
Clik here to view.
Baadhi ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na Wakurugenzi wa Idara mbalimbali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa  wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)

Image may be NSFW.
Clik here to view.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajab Gamaha (wa pili kushoto) kwa pamoja na baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakimsikiliza mhe. Waziri Membe (hayupo pichani) wakati alipozungumza na Mabalozi hao.


Image may be NSFW.
Clik here to view.
Mabalozi wengine na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Mambo ya Nje wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)

Image may be NSFW.
Clik here to view.
Sehemu nyingine ya Mabalozi wakati Mhe. Membe alipozungumza nao.


Image may be NSFW.
Clik here to view.
Balozi Mpango akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Mabalozi wenzake mara baada ya Mhe. Membe kumaliza mazungumzo nao.



Image may be NSFW.
Clik here to view.
Picha zaidi za mkutano huo wa Mhe. Membe na Mabalozi.


Image may be NSFW.
Clik here to view.
Mhe. Membe akizungumza na Waandishii wa Vyombo mbalimbali vya Habari juu ya mazungumzo yake  na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hao hapa nchini.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 118057

Trending Articles