Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117380

Watu zaidi ya 40 wamekufa baada ya jengo la ghorofa nane kuporomoka India

$
0
0
Jengo moja la ghorofa nane linalosemekana lilikuwa likijengwa kinyume cha sheria limeporomoka na kuua watu 47 na kujeruhi wengine 70 jijini Mumbai, India siku ya Alhamisi jioni. 

Waokoaji wakiwa na nyundo, misumeno, jeki na bulldozer zipatazo sita walikuwa wakijitahidi kunasua walionasa kwenye jengo hilo lililo maeneo yam situ liiltwalo Thane.

 “Kuna uwezekano kuna watu wamenasa katika kifusi” Kamishna wa Polisi wa eneo hilo Bw. K.P. Raghuyanshi amesema leo mchana. 

Wakati linaporomoka inasemekana ndani ya jengo hilo mlikuwa na watu kati ya 100 na 150, wengi wakiwa ni wakazi wa humo mjengoni na wengine wajenzi. Zaidi ya watu 20 hawajulikani walipo hadi sasa, kwa mujibu wa Bw. R.S. Rajesh, afusa wa kitengo cha majanga na uokoaji. Waliokufa ni pamoja na watoto 17. 

Ghorofa nne za jengo hilo zilikuwa zimeshamalizika kujengwa na watu walikuwa wanaishi humo, ambapo wajenzi walikuwa wakimalizia ghorofa zingine tatu na walikuwa katika kuongezea ya nane ndipo lilipobumburuka.




Viewing all articles
Browse latest Browse all 117380

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>