Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 120484 articles
Browse latest View live

SERIKALI YAZIHAKIKISHIA KAMPUNI ZA USWISI MAZINGIRA SALAMA YA BIASHARA, UWEKEZAJI

$
0
0

Serikali ya Tanzania imezihakikishia kampuni za Uswisi mazingira salama ya biashara na uwekezaji nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) alipokutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Uswisi Bi. Patricia Daanzi katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi Mulamula amesema kuwa Serikali ya awamu ya Sita imetilia mkazo katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ikiwa ni pamoja na kupitia sheria na kuondoa baadhi ya kodi zilizokuwa ni kikwazo kwa wawekezaji.

“Serikali imepitia sheria zetu na kuweza kuondoa kodi zilizokuwa kero na kupitia pia sheria ya uwekezaji kwa lengo la kuboresha zaidi mazingira ya biashara na uwekezaji hapa nchini,” amesema Balozi Mulamula

Balozi Mulamula ameongeza kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Uswisi pamoja na ujumbe wake wameoneshwa kuridhishwa na juhudi za Serikali ya Tanzania katika kuboresha mazingira ya biashara na kuahidi kuendelea kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Uswisi kuja kuwekeza Tanzania.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Uswisi Bi. Patricia Daanzi amesema pamoja na mambo mengine, wamejadiliana mazingira ya biashara na uwekezaji na vitu ambavyo kampuni za Uswisi zinahitaji ili kuwekeza zaidi Tanzania.

“Tumeridhishwa na juhudi za Serikali ya Tanzania za kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na tumemhakikishia Waziri Mulamula kuwa tutaendelea kuwahamasisha wafanyabiashara kutoka Uswisi kuja kuwekeza Tanzania,” amesema Bi. Daanzi

Bi. Daanzi ameongeza kuwa mbali na kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji pia kuna maeneo ya ushirikiano ambayo Serikali ya Uswisi itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha maisha ya watanzania.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China Nchini Mhe. Chen Mingjian katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Viongozi hao pamoja na mambo mengine, wamejadili kuhusu Mkutano wa nane (8) wa Wakuu wa Nchi wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 - 30 Jijini Dakar nchini Senegal.

Katika Mkutano huo Rais wa China Mhe. Xi Jinpign anatarajiwa kuhutubia kwa njia ya Mtandao ambapo Tanzania itawakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula.

Mkutano huo utawajumuisha viongozi na wawakilishi kutoka Bara la Afrika na China ambapo utatoa fursa ya viongozi hao kujadili na kuangalia jinsi ambavyo China ilivyotekeleza hatua za ushirikiano kwa kipindi cha miaka mitatu 2018 - 2021 kwenye maeneo ya ujenzi wa maeneo maalum ya viwanda barani Afrika, ujenzi wa miundombinu ya nishati, usafirishaji, habari na mawasiliano, kukuza wigo wa biashara kati ya China na mataifa ya Afrika.

Maeneo mengine ni kampeni ya mapinduzi ya kijani, mpango maalum wa mafunzo ya ufundi, kuboresha sekta ya Afya, ulinzi na usalama na ushirikiano katika masuala ya habari, utamaduni sanaa na michezo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Uswisi Bi. Patricia Daanzi akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zaadi ya picha Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Uswisi Bi. Patricia Daanzi


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Uswisi Bi. Patricia Daanzi, Balozi wa Uswisi Nchini Mhe. Didier Chassot, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Swahiba Mndeme. Wengine ni ujumbe ulioambatana na Bi. Daanzi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Balozi wa China Nchini Mhe. Chen Mingjian katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa China Nchini Mhe. Chen Mingjian akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

WAZIRI SIMBACHAWENE AZINDUA MCHORO WA BARABARANI UNAOONESHA ENEO MAALUM LA KUSIMAMA PIKIPIKI JIJINI ARUSHA

$
0
0

 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo na kulia kwake ni Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mkadam Mkadam ambae ni Afisa Mnadhimu wa Kikosi cha Usalama Barabarani wakiwa katika picha ya pamoja na Wadau mbalimbali katika uzinduzi (MOTORCYCLE BUFFER ZONE) katika eneo la Sanawari mkoani Arusha.(Picha na Jeshi la Polisi).

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe, George Simbachawene, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo na Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mkadam Mkadam, ambae ni Afisa Mnadhimu wa Kikosi cha Usalama Barabarani na Wadau mbalimbali wakikata utepe katika uzinduzi wa mchoro wa Barabarani unaoonesha eneo maalum la kusimama Pikipiki (MOTORCYCLE BUFFER ZONE) katika eneo la Sanawari mkoani Arusha.(Picha na Jeshi la Polisi).

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Simbachawene akisalimiana na moja wa madereva Bodaboda kabla ya uzinduzi wa kivuko cha mchoro wa Barabarani unaoonesha eneo Maalum la Kusimama Pikipiki (MOTORCYCLE BUFFER ZONE) katika eneo la Sanawari mkoani Arusha. (Picha na Jeshi la Polisi).

WAJASIRIAMALI WADOGO NA WA KATI WAHAMASISHWA KUSHIRIKI MAONESHO YA 21 YA NGUVU KAZI/JUA KALI JIJINI

$
0
0


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Robert Gabriel akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu Maonesho ya 21 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Afrika Mashariki (Nguvu Kazi/ Jua Kali) hii leo Novemba 25, 2021 Jijini Mwanza.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Robert Gabriel (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi Msaidizi Uratibu na Uwezeshaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Eliakim (kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wajasiriamali Tanzania Bw. Joseph Rweyemamu (katikati) mara baada ya mkutano huo uliofanyika hii leo Novemba 25, 2021 Jijini Mwanza.

PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

***********************

Na: Mwandishi Wetu – MWANZA

Wajasiriamali Wadogo na wa Kati nchini wamehasishwa kushiriki kwa wingi kwenye Maonesho ya 21 ya Wajasiriamali maarufu kama Nguvu Kazi au Jua Kali yatakayofanyika Desemba 2 hadi 12 mwaka huu, katika viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa huo wa Mwanza Mhe. Robert Gabriel wakati wa mkutano na Waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi yake hii leo Novemba 25, 2021.

Alieleza kuwa maonesho hayo ya 21 ambayo hujulikana kama maonesho ya Jua Kali au Nguvu Kazi yatafanyika nchini Tanzania yanalenga hasa wajasiriamali Wadogo na wa Kati waliopo katika sekta isiyo rasmi ili kuwawezesha kurasimisha shughuli zao kwa kuwapatia fursa ya kutangaza bidhaa zao, kubadilishana taarifa, kukuza ujuzi, kukuza masoko ya bidhaa na kukuza teknolojia ya utengenezaji wa bidhaa pamoja na kuongeza fursa za ajira za staha kwa vijana.

“Serikali inayachukulia maonesho haya kama fursa ya kuwawezesha Wajasiriamali Wadogo na wa Kati pamoja na vijana wabunifu kutangaza kazi zao na kutafuta masoko kwa wenzetu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,” alisema

Aliongeza kuwa Maonesho hayo yanaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa pamoja zimejipanga kutekeleza azma ya Serikali katika kukuza fursa za ajira hususan kwa wajasiriamali, vijana wabunifu wa makundi yote wakiwemo wenye Ulemavu.

“Maonesho haya hufanyika sambamba na makongamano ya kuwajengea uwezo wajasiriamali na wabunifu kuhusu masoko, ubora wa bidhaa, urasimishaji biashara na kuongeza thamani ya bidhaa, hivyo ni vyema wajasiriamali na vijana wabunifu nchini wakatumia fursa hii kujiletea maendeleo,” alieleza

Sambamba na hayo alieleza kuwa Fomu za maombi pamoja na maelekezo kwa wajasariamali na wabunifu wanaokusudia kushiriki maonesho hayo zinapatikana katika Ofisi za Wakuu wa Mikoa kupitia Afisa Biashara, Halmashauri zote nchini na Ofisi za Mameneja wa Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) ambapo muda wa kurejesha fomu hizo ni Novemba 28, 2021.

Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Robert Gabriel alitimia fursa hiyo kusisitiza Kamati ya Uratibu kuhakikisha inaibua na kuteua wajasiriamali na vijana wabunifu kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa. Pia amehamasisha wajasairiamali na vijana wabunifu kujitokeza na kushiriki kwa wingi katika maonesho hayo. Pamoja na hayo alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wananchi kutembelea maonesho hayo na kujionea bidhaa zinazotengenezwa na wajasiriamali wa ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwa maonesho hayo hayana kiingilio.

“Tumejipanga katika kuhakikisha masuala ya afya yanazingatiwa wakati wote wa maonesho hususan kuchukua tahadhari dhidi ya changamoto ya UVIKO – 19,” alisema

Kauli mbiu ya Maonesho ya 21 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati ni: “Kuhamasisha ubora na uvumbuzi ili kuongeza Ushindani wa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Afrika Mashariki na hatimaye kuwainua kiuchumi hasa kutokana na janga la UVIKO 19”

Serikali ya awamu ya Sita imeweka mikakati ya kupambana na ukatili wa kijinsia -Mratibu Kulaya

$
0
0
Na Chalila Kibuda ,Michuzi TV
SHIRIKA la Wanawake katika sheria na Maendeleo Afrika WilDAF chini ya Mratibu wa Kampeni Siku 16 za ukatili dhidi ya Wanawake Kitaifa Anna Kulaya amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Hassan Suluhu ameiongoza Serikali yake kwa jitihada za dhati za kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia na kuhakikisha vinatokomezwa kabisa.

Amesema kuwa ukomeshwaji huo unawezesha wanawake na mabinti kushiriki kwenye shughuli za maendeleo na kwamba kwa mwaka huu kumeazishwa Mahakama maalum ya kushughulikia masuala ya familia ili kuongeza upatikanaji wa haki kwa wakati kwa wanawake na watoto.

Anna ameyasema haya jijini Dar es salaam mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wa uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za uharakati dhidi ya ukatili wa kijinsia ambapo alisema wameipongeza Serikali kwa kuwaruhusu mabinti wanaopata mimba wakiwa masomoni kuendelea na shule baada ya kujifungua.

"MKUKI tunatoa wito kwa Serikali na wadau wote kuongeza jitihada za kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia ili kuharakasha kufikia lengo kubwa la kupunguza, hivyo kwa asilimia 50 kufikia mwaka 2022 kama ilivyoainishwa na MTAKUWWA, zaidi kumaliza vitendo hivi na kufikia maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030." amesema Anna

Nakuongeza kuwa "Sisi kama wana MKUKI tunaamini kuwa muda sasa umefika kutengeneza kizazi kipya kinachothamini usawa wa kijinsia." alisisitiza

Anna amesema Kauli mbiu ya Mwaka huu kuhusu ukatili wa kijinsia ni'' EWE MWANANCHI KOMESHA UKATILI WA KIJINSIA SASA.'' Kupitia kauli mbiu hiyo wanaiomba Serikali kutunga sheria ya kudhibiti ukatili wa kijinsia ( Gender Based Violence Violence Act) kwani ukosefu wa sheria mahususi ya makosa ya ukatili ni changamoto kubwa katika upatikanaji wa haki kwa watendewa na kuwatia hatiani watuhumiwa.

Pia amesema kuharakishwa kwa mabadiliko ya sheria ya ndoa juu ya mwaka 1971 ili kuokoa mabinti dhidi ya ndoa za utotoni .kuboresha muundo na kutengwa bajeti ya kutosha kwa ajili ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto MTAKUWWA.

Pia amesema kuna umuhimu wa kufuta sheria zote za kibaguzi mathalani sheria ya kimila ya mirathi, tangazo la serikali Namba 436 la mwaka 1963 ambayo inanyima wanawake haki yao ya kikatiba ya kumiliki Mali kupitia urithi.

Anna akizungumzia siku 16 alisema kutakuwa na shughuli mbalimbali na midahalo ili kuleta mabadiliko katika nchi nakwamba shughuli hizo ni pamoja na maonesho ya matumizi ya digitali, kukuza usawa wa kijinsia na utawala bora ,kongamano la kitaifa kujadili ukatili wanaofanyiwa wanawake wenye ulemavu, msafara wa kijinsia (Caravan Route) kuhamasisha uanzishwaji wa madawati ya kushughilikia ukatili.

Amesema kongamano kwa viongozi wa dini kushiriki katika harakati za kukomesha ukatili wa kijinsia na tuzo kwa vinara 16 wa kupinga ukatili wa kijinsia zitatolewa, lakini pia alibainisha kwamba matukio ya ukatili kwa watoto yaliyoripotiwa na jeshi la polisi kati ya kipindi cha januari 2021 hadi septemba 2021 yanaonyesha kuwa watoto 6168 kati yao wasichana 5287 na wavulana 88.

Amefafanua kuwa wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kati ya hao watoto 3524 walibakwa 637 walilawatiwa 1887 walipata mimba na 130 walichomwa moto na kinachosikitisha zaidi ni kati ya visa vilivyoripotiwa watuhumiwa waliofikishwa mahakamani ni 3800 kesi zilizofanyiwa upelelezi ni 2368 na zilizotolewa hukumu 88.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuzindua Mwongozo wa Kushughulikia Ukatili wa Kijinsia katika Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati nchini, kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, Novemba 25, 2021. Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamisi na kulia ni Wakili Anna Kulaya ambaye ni Mratibu wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo. 
Mratibu wa Ukatili wa Kampeni ya Siku 16 ya kupinga Ukatili wa Kijinsia Wakili Anna Kulaya akizungumza wa uzinduzi wa kampeni iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo Novemba 25,2021.

ZIARA YA KUTEMBELEA VISIMA VYA MAJI SAFI NA SALAMABBUMBWISUDI MAGHARIBI “A”

$
0
0
 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (wa pili kulia) akizungumza na Wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya Visima vya Maji Safi na Salama (ZAWA)Bumbwisudi Wilaya ya Magharibi”A” Mkoa wa Mjini Magharibi wakati alipofanya ziara ya ghafla leo kuangalia tatizo lililopelekea kukosekana kwa huduma hiyo (kulia)Waziri wa Maji,Nishati na Madini Mhe.Suleiman Masoud Makame,(wa pili kushoto) Dkt.Mngereza Mzee Miraji).[Picha na Ikulu] 25/11/2021.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akisisitiza jambo kwa watendaji wakati alipofanya ziara ya Ghafla kwa kutembelea visima vya Maji Safi na Salama Bumbwisudi Wilaya ya Magharibi “A” Mkoa Mjini Magharibi leo (katikati) Waziri wa Maji,Nishati na Madini Mhe.Suleiman Masoud Makame,(wa tatu kulia) Mkuu wa Wilaya ya Magharibi”A” Mhe.Suzan Peter Kunambi.[Picha na Ikulu] 25/11/2021.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akitoa maelekezo kwa Waziri wa Maji,Nishati na Madini Mhe.Suleiman Masoud Makame (katikati) pamoja na watendaji wengine wakati alipofanya ziara ya Ghafla kwa kutembelea visima vya Maji Safi na Salama Bumbwisudi Wilaya ya Magharibi “A” Mkoa Mjini Magharibi leo.[Picha na Ikulu] 25/11/2021.








Mlinzi katika Visima vya Maji Safi na Salama (ZAWA) Bw.Hussein Ismail akitoa changamoto zinazowakabili katika kazi zao wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) alipofika maeneo ya Visima vya Maji Safi na salama (ZAWA)Bumbwisudi Wilaya ya Magharibi”A” Mkoa wa Mjini Magharibi kuangalia tatizo lililopelekea kukosekana kwa huduma hiyo.[Picha na Ikulu] 25/11/2021.

MANISPAA KAHAMA YATAKIWA KUONGEZA KASI YA UKUSANYAJI KODI YA ARDHI

$
0
0

Na Munir Shemweta, WANMM KAHAMA


Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga kuongeza kasi ya ukusanyaji kodi ya pango la ardhi.

Hatua hiyo inafuatia Dkt Mabula kutoridhishwa na kasi ya ukusanyaji mapato yatokanayo na kodi ya ardhi ambapo Manispaa hiyo ya Kahama hadi kufikia Novemba mwaka huu imekusanya milioni 460,328,934 kati ya bilioni 3.5 ilizopangiwa kukusanya katika mwaka wa fedha 2021/2022.

Kwa mujibu wa Afisa Ardhi Mteuli Manispaa ya Kahama Bw Yusufu Luhumba., katika kipindi cha mwaka uliopita wa 2020/2021 Halmashauri ya Manispaa hiyo ya Kahama ilipangiwa kukusanya bilioni 2.5 lakini ilifanikiwa kukusanya shilingi bilioni 1.330 sawa na asilimia 53.25.

Aidha, Manispaa hiyo inawadai wamiliki wa ardhi kiasi cha bilioni 1.6 ambapo Naibu Waziri wa Ardhi alielekeza manispaa hiyo kuhakikisha anawachukulia hatua wale wote walioshindwa kulipa madeni ya kodi ya pango la ardhi kwa wakati kwa kuwa wamevunja masharti ya umiliki.

Hata hivyo, Dkt Mabula aliwataka watendaji wa sekta ya ardhi kabla ya kuwafikisha wadaiwa katika mabaraza ya ardhi kuzungumza nao ili kuangalia namna bora ya kulipa madeni hayo na kuongeza kuwa, iwapo wapo wadaiwa wanaoweza kulipa kwa awamu basi mazungumzo yafanyike lakini kwa kuzingatia fedha kulipwa kwa kuzingatia kipindi cha mwaka wa fedha husika.

Akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri ya Manispaa ya Kahama akiwa katika ziara yake ya siku mbili katika mkoa wa Shinyanga tarehe 24 Novemba 2021 Dkt Mabula alisema, wale wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi walioshindwa kulipa madeni yao wanatakiwa kufikishwa katika mabaraza ya ardhi ili washitakiwe kwa kushindwa kulipa.

" Maelekezo yangu wale wote walioshindwa kulipa madeni yao basi sheria ichukue mkondo wake ikiwemo kuwafikisha katika Mabaraza ya Ardhi ambako huko maamuzi ni kulipa ama mali za wahusika kupigwa mnada kufidia deni" alisema Dkt Mabula.

Aidha, Dkt Mabula aliitaka halmashauri ya Manispaa ya Kahama kuhakikisha inatumia vyombo vya habari pamoja na ujumbe wa simu kuwakumbusha wamiliki wa ardhi katika Manispaa hiyo kulipa kodi ya pango la ardhi ili waweze kulipa kwa wakati na kuiwezesha serikali kupata mapato.

Awali, Afisa Ardhi Mteule Yusufu Luhumba alisema, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama imeendelea na utaratibu wa kuwafuatilia wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi na jumla ya thamini 37 za wadaiwa kati ya 103 zimekwishakabidhiwa kwa dalali wa mahakama kwa utekelezaji.

" Wakati thamini 54 zimekwisha andaliwa na kukamilika, kwa sasa zinasubiri kusainiwa na mthamini Mkuu wa serikali kisha kupelekwa kwa dalali wa mahakama kwa utekelezaji wa uuzaji" alisema Luhumba.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Clemence Nkusa wakati akielekea ofisi za ardhi katika Manispaa hiyo tarehe 25 Novemba 2021.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akikagua majalada ya ardhi katika ofisi ya ardhi Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga tarehe 25 Novemba 2021. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Clemence Nkusa na kulia ni Afisa Ardhi Mteule wa Manispaa hiyo Yusufu Luhumba.

 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Clemence Nkusa wakati wa ziara yake katika manispaa hiyo tarehe 25 Novemba 2021.


POLISI WATAKIWA KUONGEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO

$
0
0



Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani, Naibu Kamishna wa Polisi Fulgence Ngonyani akiwasilisha mada katika Mkutano wa Maafisa Wanadhimu wa mikoa, Wakuu wa Usalama barabarani wa mikoa na Wahasibu wa Polisi unaofanyika Mkoani Kilimanjaro kwa lengo la kutathmini mfumo wa ukusanyaji mapato ya Serikali kwa njia ya mtandao. (Picha na A/INSP Frank Lukwaro wa Jeshi la Polisi


Mkurugenzi Udhibiti Usafiri Ardhini kutoka LATRA Johanesy Kahatano akiwasilisha mada katika Mkutano wa Maafisa Wanadhimu wa mikoa, Wakuu wa Usalama barabarani wa mikoa na Wahasibu wa Polisi unaofanyika Mkoani Kilimanjaro kwa lengo la kutathmini mfumo wa ukusanyaji mapato ya Serikali kwa njia ya mtandao. (Picha na A/INSP Frank Lukwaro wa Jeshi la Polisi


Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Leonard Ngasa akichangia mada katika Mkutano wa Maafisa Wanadhimu wa mikoa, Wakuu wa Usalama barabarani wa mikoa na Wahasibu wa Polisi unaofanyika Mkoani Kilimanjaro kwa lengo la kutathmini mfumo wa ukusanyaji mapato ya Serikali kwa njia ya mtandao. (Picha na A/INSP Frank Lukwaro wa Jeshi la Polisi)


Kamishna wa Fedha na Lojistiki Hamad Hamis Hamad akizungumza na Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi DCP Antony Ruta wakati wa Mkutano wa Maafisa Wanadhimu wa mikoa, Wakuu wa Usalama barabarani wa mikoa na Wahasibu wa Polisi unaofanyika Mkoani Kilimanjaro kwa lengo la kutathmini mfumo wa ukusanyaji mapato ya Serikali kwa njia ya mtandao. (Picha na A/INSP Frank Lukwaro wa Jeshi la Polisi

*******************

Na. A/INSP Frank Lukwaro- Jeshi la Polisi.

Mkutano wa Maafisa Wanandhimu, Wakuu wa Usalama barabarani na Wahasibu wa Polisi kutoka mikoa yote Tanzania bara na Zanzibar wametakiwa kuongeza kasi katika kukusanya maduhuli ya serikali ikiwemo kuwasimia walio chini yao ili kuepusha hoja za kiukaguzi ambazo zinaweza kujitokeza kutokana na usimamizi usioridhisha kwa baadhi ya Viongozi.

Hayo yamesemwa na Kamishna wa Fedha na Lojistiki Hamad Hamis Hamad wakati wa siku ya pili ya mkutano huo unaoendelea Mkoani Kilimanjaro kwa lengo la kuboresha utendaji kazi kwa washiriki hao pamoja na kujiimarisha katika utumiaji mifumo ya kidigitali katika kukusanya mapato ya serikali ikiwemo tozo za barabarani.

Amesema ni vizuri washiriki wa mkutano huo kuhakikisha kuwa mkutano huo utakapomalizika mabadiliko yaweze kuonekana kwa vitendo kwakuwa kila mmoja anatakiwa kutambua wajibu wake katika kuhakikisha kuwa mapato ya Serikali yanakusanywa na kufikishwa katika mamlaka husika kwa wakati.

“Kila mmoja aone umuhimu wa kuongeza bidii katika ukusanyaji wa mapato na kuimarisha usimamizi wa matumizi ya fedha na rasilimali za umma ili kufikia malengo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” Alisema Kamishna Hamad.

Mkutano huo pia umeshirikisha wadau wa nje wakiwemo Wizara ya Fedha na Mipango, Mamlaka ya udhibiti wa Ardhini (LATRA), Ofisi ya Mhakiki mali wa Serikali ambapo wameweza kuwasilisha mada zao na kufanya majadiliano ya pamoja ili kuboresha ushirikiano uliopo baina ya taasisi hizo na Serikali.

Vilevile Wajumbe hao wameweza kuelimishwa kuhusu ufanyaji kazi wa mashine mpya za ukusanyaji wa tozo za serikali (POS) ambapo zimeboreshwa katika ufanyanyaji wa kazi ambapo jumla ya mashine hizo 2,050 zimenunuliwa ili kuendeleza zoezi hilo la ukusanyaji wa tozo hususani za barabarani.

Mkutano huo ulifunguliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na unatarajia kufungwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini unabebwa na kauli mbiu ya Kusanya mapato, Simamia fedha na mal iza Umma kwa maendeleo ya Taifa.

KILI MARATHON YAWATAKA WASHIRIKI WA KANDA YA KASKAZINI KUJISAJILI MAPEMA

$
0
0



Na Mwandishi Wetu.

MAANDALIZI ya mbio maarufu za Kilimanjaro Premium Lager Marathon ambazo zinatimiza miaka 20 tangu kanzishwa kwake, yamefikia hatua nzuri huku waandaaji wakitoa wito kwa washiriki kutoka Kanda ya Kaskazini wajisajili mapema kuepuka usumbufu dakika za mwisho.

Wito huo umetolewa kutokana na uzoefu wa miaka ya mnyuma ambapo washiriki kutoka kanda hiyo ya kaslkazini ambayo ndio mwenyeji wa mbio hizo,  wamekuwa wakisubiri hadi dakika za mwisho ili wajisajili jambo ambalo huwaacha baadhi na masikitiko baada ya kukuta namba zote zimeshauzwa.

“Tunatoa wito kwa washiriki kutoka Kilimanjaro, Arusha, Tanga na Manyara kujisajili kwa njia ya mtandao kupitia Tovuti yetu Au kwa njia ya Tigopesa kwa kupiga *149*20#,” alisema Aggrey Marealle ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Executive Solutions, waratibu wa mbio hizo kitaifa.

Alisema mbio hizo za mwakani zinategemewa kuwa kubwa zaidi kwa sababu itakuwa ni mwaka wa 20 tangu kuanzishwa kwake kwa hivyo washiriki wana kila sababu ya kujisajili na kuhakikisha wanathibitisha ushiriki wao kwa kujisajili.

“Huwa inasikitisha sana kuona washiriki kutoka Moshi au Arusha wanakosa namba wakati wanatokea katika kanda mwenyeji wa mbio hizi. Namba zikishaisha usajili huwa unafungwa. Kwa kawaida hakuna namba zinazouzwa katika vituo vya kutolea namba isipokuwa tu kwa mbio za KM 5 kama zitakuwa zimebakia,” alisema.

Alisema kujisajili ni rahisi mno na kwa sasa kuna punguzo la bei la asilimia 20 lakini ifikapo Januari 7, 2022 bei zitapanda kwani hakutakuwa na punguzo tena.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa mbio hizo, Bw. John Bayo alisema washiriki wote wa mbio za Kilimanjaro Premium Lager 42km , Tigo 21km na Grand Malt 5km waanze mazoezi mapema ili wajiandae na mbio hizi za 20 za Kilimanjaro Marathon ambazo ni za kihistoria.

“Tunataka mbio hizi ziwe za ushindani zaidi na ziache kumbukumbu ya aina yake miongoni mwa washiriki kwa hivyo maandalizi ni muhimu sana. Ni matumaini yetu kuwa zawadi nyingi zitabaki hapa nyumbani safari hii. Kama waandaaji tutafanya sehemu yetu  na tunatoa wito kwa washiriki wafuate maelekezo ili kufanya mbio za mwakani ziwe za kufana zaidi kwani tunatarajia washiriki kutoka nchi zaidi ya 55 na umati unatarajiwa kuwa mkubwa zaidi kuliko miaka ya nyuma,” alisema.

Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania Bw. Jackson Ndaweka alisema wameridhishwa na maandalizi hadi sasa kwani wamekuwa wakipokea taarifa kutoka kwa waandaaji wa Kilimanjaro Marathon.

“Hili ndio tukio kubwa kabisa la riadha nchini ambalo huwaleta pamoja zaidi ya washiriki 12,000 kutoka ndani na nje ya Tanzania kwa maana hiyo tunashirikiana na waandaaji kwa karibu kuhakikisha mbio hizi zinafanikiwa na zinaweka riadha ya Tanzania katika kiwango cha kimataifa. Wanariadha wa hapa nchini hujipatia kipato kwa kushiriki mbio hizi lakini pia huwandaa vizuri katika mashindano ya nje ya nchi.Mbio hizi pia zinachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la nchi kwa sababu ya watalii ambao hutembelea vivutio mbalimbali,” alisema.  

Alisema RT pia imefarajika kusikia kuhusu maonesho yaliyoandaliwa na wandaaji wa Kilimanjaro Marathon kama sehemu ya madhimisho ya miaka 20 ya mbio hizo. “Maonesho hayo yatatoa fursa nzuri kwa wadhamini kujitangaza vizuri na pia wananchi watapata maelezo mengi kuhusu Kili Marathon na riadha kwa ujumla. Tutakuwepo kutoa mchango wetu katika suala hili,” alisema.

Wadhamini wa Kilimanjaro Marathon  2022 ni Kilimanjaro Premium Lager- 42km, Tigo- 21km, Grand Malt -5km wadhamini wa meza za maji ni Absa, Unilever, TPC Sugar, Simba Cement, Kilimanjaro Water, na wasambazaji maalumu Kilimanjaro Leather Industries Company Limited, GardaWorld Security, Keys Hotel, Kibo Palace Hotel na CMC Automobiles.

Mbio za mwakani zitafanyika katika Chuo Kikuu Cha Ushirika Moshi Februari 27, 2022.

Mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon huandaliwa na kampuni ya Kilimanjaro Marathon Company Limited na kuratibiwa kitaifa na kampuni ya Executive Solutions Limited.


ZIMAMOTO YAPATA UGENI KUTOKA HAMBURG, UJERUMANI

$
0
0


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga (Kushoto), akikabidhi zawadi ya kikombe chenye maneno “Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na namba ya Dharura 114” kwa mgeni wake ndugu Reinhard Paulsen (Kulia) kutoka Jiji la Hamburg Nchini Ujerumani leo tarehe 25 Novemba, 2021 Makao Makuu ya Zimamoto na Uokoaji Jijini Dodoma.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga (Kushoto), Akizungumza na Ndugu Reinhard Paulsen (Katikati) kutoka Jiji la Hamburg Nchini Ujerumani alipomtembelea ofisini kwake leo tarehe 25 Novemba, 2021 Jijini Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga (Katikati) akiongoza kikao na wageni kutoka Jiji la Hamburg Nchini Ujerumani walipomtembelea ofisini kwake leo tarehe 25 Novemba, 2021 Jijini Dodoma; Kikao ambacho kilihudhuriwa pia na Viongozi Waandamizi wa Jeshi hilo.


Picha ya pamoja ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga, Viongozi Waandamizi wa Zimamoto Na Uokoaji pamoja na wageni kutoka Jiji la Hamburg Nchini Ujerumani katika Ofisi za Makao Makuu ya Zimamoto Na Uokoaji Jijini Dodoma leo tarehe 25 Novemba, 2021. (Picha zote na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji)

********************

Dodoma, 25 Novemba 2021.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga, leo tarehe 25 Novemba, 2021 amepokea Wataalamu wa Uzimaji Moto na Maokozi kutoka Jijini Hamburg, Ujerumani na kufanya nao kikao kifupi akiwa pamoja na Viongozi Waandamizi wa Jeshi hilo.

Kamishna Jenerali amepokea ugeni huo akiwa ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dodoma. Ugeni huo uliongozwa na Ndugu Reinhard Paulsen akiongozana na Nobert Sorge pamoja na Dennis Rosenthal hao ambao ni wazimamoto wa kujitolea chini ya program ya ‘’sistership cities’’ na kuwashukuru sana kwa misaada mbalimbali ya vifaa pamoja na mafunzo ambayo yamekuwa yakitolewa nchini Ujerumani.

“Baadhi ya maafisa na askari wamefaidika sana na mafunzo ya maokozi pamoja na huduma ya kwanza, lakini pia imekuwa ni fursa kwa Jeshi kupokea wakufunzi mbalimbali ambao wamekuwa wakitoa mafunzo hapa nchini” alisema Kamishna Jenerali Masunga. Aliendelea kusema kwamba bado Jeshi linahitaji msaada mkubwa sana katika mafunzo ya maokozi angani ‘’High Angel Rescue’’, mafunzo ya utoaji huduma ya kwanza pamoja na misaada ya vifaa vya maokozi na uzimaji moto.

Naye kiongozi wa ugeni huo, Ndugu Reinhard Paulsen, alimshukuru sana Kamishna Jenerali na kusema; “Tunashukuru sana kwa mapokezi mazuri lakini pia kwa namna ambavyo Jeshi limepiga hatua kubwa ya mabadiliko chanya kwa kipindi kifupi na kutunza vifaa mbalimbali ambavyo vimekuwa vikiletwa kutoka nchini Ujerumani”.

Paulsen alisema kupitia mpango wa Sistership Cities tuko tayari kuendelea kutoa misaada ya vifaa pamoja na mafunzo kwa maafisa na askari. Aidha kwa sasa tunaendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa huu wa Uviko ambao ni janga la kidunia na tunaahidi kushirikiana kwa kadiri itakavyowezekana.

Kamishna Jenerali alihitimisha ziara ya ugeni huo kwa kufanya kikao kifupi na baadhi ya Viongozi Waandamizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na wageni hao.

WATANZANIA WAUSHUKURU UBALOZI WA TANZANIA UBELGIJI

$
0
0

Afisa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Mh:Juma Ali Salum{mwenye miwani} akiagana na watanzania waliofika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zaventem nchini Ubelgiji kumsindikiza ndugu Othman{mwenye kofia} aliyefiwa na mkewe siku ya jumapili nchini Luxembourg.Ubalozi wa Tanzania ulifika uwanjani hapo kuhakikisha raia wake hapati usumbufu wowote na walimsaidia mpaka mwisho aliposafiri.




Pichani kaimu balozi nchini Ubelgiji Mh:Juma Ali Salumu{kushoto}aliyefika uwanja wa ndege Zaventem nchini Ubelgiji kuhakikisha mtanzania aliyefiwa na mkewe nchini Luxembourg ndugu Othman{Pichani wa tatu kutoka kushoto}anampatia msaada stahiki ili asafiri na mwili wa marehemu mkewe kwenda nyumbani Tanzania bila usumbufu.



Watanzania wanaoishi nchini Ubelgiji wameupongeza ubalozi wa Tanzania nchini hapo kwa hatua zote walizosaidia mpaka mwili wa marehemu kusafiri.

Shukrani za pekee kwa Mh:Balozi Jestas Abouk Nyamanga

Kaimu Balozi Mh: Juma Ali Salum,

Watanzania wote nchini Luxembourg,Watanzania wote nchini Uingereza,Watanzania wote nchini Ujerumani,Watanzania wote nchini Tanzania Bara na Zanzibar

MILIONI 950 KUJENGA VITUO VIWILI VYA AFYA MANISPAA YA SONGEA

$
0
0

Na Muhidin AmriSongea,

SERIKALI imetenga Sh.milioni 950 wa ajili ya kujenga vituo viwili vya Afya katika kata ya Msamala na Lilambo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, ikiwa ni mkakati wake wa kusogeza huduma za matibabu kwa wananchi wa kata hizo.

Hayo yamesemwa jana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt Frederick Sagamiko, wakati akitoa taarifa ya ujenzi wa kituo cha Afya Msamala kwa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge.

Alisema, kati ya fedha hizo Sh.milioni 500 zitatumika kujenga kituo cha afya Msamala na Sh.milioni 450 kwa ajili ya kujenga kituo cha afya Lilambo kata ya Lilambo.

Dkt Sagamiko alisema,mradi wa ujenzi wa kituo cha Msamala umeibuliwa na wananchi wenyewe kwa madhumuni ya kupunguza kero ya kutembea umbali mrefu hadi kituo cha afya Mjimwema na Hospitali ya rufaa Songea kufuata matibabu.

Dkt Sagamiko alisema,ujenzi wa mradi huo utahusisha jengo la maabara,upasuaji,jengo la wagonjwa wa n je,wodi ya wanawake,choo cha nje,kichomeo taka,shimo la kondo na shimo la maji taka.

Kwa mujibu wa Dkt Sagamiko,katika utekelezaji wa mradi huo Serikali imetoa Sh.milioni 500 ambapo wananchi wa kata hiyo wamechangia kiasi cha Sh.milioni 2 na unatekelezwa kwa mfumo wa force akaunti na umewezesha wananchi hasa wanaoishi kata hiyo kushiriki katika shughuli za ujenzi na kujipatia kipato.

Dkt Sagamiko alitaja manufaa ya mradi huo mara utakapokamilika ni upatikanaji wa huduma bora ya mama na mtoto na hivyo kupunguza vifo vya akina mama na mtoto kutoka 202 hadi 190 kwa vifo 100,000 kwa mwaka.

Faida nyingine ni upatikanaji wa huduma ya dharura ya upasuaji kwa akina mama wajawazito,kupungua kwa magonjwa ya kuambukiza na yasioambukiza pamoja na wananchi watapa elimu ya lishe,hivyo kupunguza tatizo la utapiamlo kwa Watoto.

Aidha huduma nyingine zitakazo patikana ni chanjo,huduma ya tohara huduma ya upimaji wa VVU/ukimwi na kuzuia maambukizi pamoja na kupunguza mzigo wa wagonjwa uliokuwa unaielemea Hospitali ya mkoa na kituo cha afya Mjimwema.

Pia alisema, katika bajeti ya mwaka 2021/2022 Manispaa hiyo imepanga kutumia Sh.450,000,000.00 ikiwa ni fedha za mapato ya ndani kujenga kituo cha Afya Lilambo na wananchi wamechangia Sh.3,295,000.00 ambapo Sh.160,000,000.00 zimetolewa kutekeleza kazi hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,amemtaka fundi anayesimamia mradi huo kuhakikisha unajengwa kwa viwango na unakamilika kwa wakati ili uweze kuleta tija kwa wananchi ambao walisubiri mradi huo kwa

Alisema,lengo la Serikali ya awamu ya sita ni kuwatatua kero wananchi zilizokuwepo ikiwemo huduma za matibabu,ambapo amewapongeza wananchi wa kata ya Msamala kwa kuibua mradi huo na kushiriki katika shughuli za ujenzi.

Brigedia Jenerali Ibuge alisema,Serikali ya mkoa itakuwa bega kwa bega na wananchi hao na kufuatilia kwa karibu mradi huo ili ukamilike haraka.

Diwani wa kata ya Msamala Michael Mbano alisema, kata ya Msamala ni kubwa na yenye wakazi wengi,hata hivyo kwa muda mrefu haikuwa na huduma zozote za matibabu badala yake wananchi walilazimika kwenda kutibiwa Hospitali ya mkoa na kituo cha Afya Mjimwema.

Mbano ameishukuru Serikali kutoa fedha za ujenzi wa kituo hicho, kwani kitakapo kamilika wananchi wa watapata matibabu karibu na kuwa na afya njema itakayowawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo.





DC TANDAHIMBA AIPONGEZA REA

$
0
0




Kazi ya kusimika nguzo za umeme ikiendelea katika kijiji cha Mtua, wilayani Nachingwea, Mkoa wa Lindi. Taswira hii ilichukuliwa wakati wa ziara ya Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy (hawapo pichani), Novemba 24, 2021.




Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy (hawapo pichani). Viongozi hao wa REA walimtembelea Mkuu wa Wilaya ofisini kwake, Novemba 24, 2021 wakiwa katika ziara ya kazi.




Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala (kushoto) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo, Kitabu kinachoelezea utamaduni wa eneo hilo. Wakili Kalolo alimtembelea Mkuu wa Wilaya akiwa katika ziara ya kazi, Novemba 24, 2021.




Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy Kitabu kinachoelezea utamaduni wa eneo hilo. Mhandisi Saidy alimtembelea Mkuu wa Wilaya akiwa katika ziara ya kazi, Novemba 24, 2021.


Kazi ya kusimika nguzo za umeme ikiendelea katika kijiji cha Mtua, wilayani Nachingwea, Mkoa wa Lindi wakati wa ziara ya Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo (mwenye fulana ya mistari) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy (fulana ya njano), Novemba 24, 2021.



Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala (katikati) akionesha vijiji vya wilaya hiyo vilivyofikiwa na umeme na ambavyo havijafikiwa kwa kutumia ramani ya mkoa wa Mtwara kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (kushoto). Viongozi hao wa REA walikuwa katika ziara ya kazi Novemba 24, 2021.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mtwara, Yusuf Nannila (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy (kushoto). Viongozi hao wa REA walikuwa katika ziara ya kazi Novemba 24, 2021.


Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala (kulia) akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy pamoja na watalaam kutoka REA na TANESCO. Viongozi hao wa REA walikuwa katika ziara ya kazi Novemba 24, 2021.


Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo (wa pili-kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (wa tatu-kushoto), wakikagua shimo lililoandaliwa kwa ajili ya kusimika nguzo ya umeme katika kijiji cha Mtunungu, wilayani Masasi, Mkoa wa Mtwara. Viongozi hao wa REA walikuwa katika ziara ya kazi Novemba 24, 2021.




Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo (wa tatu-kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (wa tatu-kulia) na wataalam kutoka REA na TANESCO, Novemba 24, 2021. Ujumbe wa REA ulikuwa katika ziara ya kazi.
………………………………………………………………………

Na Veronica Simba, REA – Mtwara

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala ametoa pongezi kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutokana na kazi nzuri inayofanyika kupeleka umeme vijijini.

Alitoa pongezi hizo ofisini kwake wakati akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, waliokuwa katika ziara ya kazi, Novemba 24, 2021.

“Tunawapongeza na kuwashukuru REA kwa kushirikiana na TANESCO. Tunatambua kazi kubwa mnayoifanya na tunafarijika sana,” alisema Kanali Sawala.

Aidha, Mkuu wa Wilaya alipongeza kasi ambayo REA imeanza nayo katika kutekeleza Mradi wa REA Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili wilayani humo na kusisitiza kuwa iendelee hivyo ili vijiji vilivyosalia vipate umeme kwa wakati uliopangwa.

Vilevile, alipongeza maelekezo yaliyotolewa na Uongozi wa REA kwa mkandarasi anayetekeleza miradi ya umeme vijijini wilayani humo, kuandaa Mpango Kazi na kuuwasilisha katika ofisi yake, ofisi ya mbunge, diwani na serikali za mitaa akisema kuwa itarahisisha ufuatiliaji wa utendaji kazi hatua kwa hatua.

Akifafanua zaidi, Kanali Sawala alisema kuwa wananchi wanapaswa kufahamu kinachofanyika, namna watakavyonufaika na mradi husika na kwa wakati gani kwani kwa namna hiyo watatoa ushirikiano mzuri katika utekelezaji wake.

Pia, alitoa rai kwa Wakala kutekeleza kwa haraka kazi ya kupeleka umeme katika vijiji vya wilaya hiyo vilivyoko mpakani mwa nchi ili kuwezesha uimarishaji zaidi wa ulinzi na usalama wa nchi.

Katika hatua nyingine, viongozi hao wa REA walimtembelea Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mtwara, Yusuf Nannila na kuzungumza naye kuhusu utekelezaji wa Ilani ya CCM hususan katika sekta ya nishati vijijini.

Mwenyekiti huyo wa CCM alieleza kuwa Uongozi wa Chama unafarijika kuona maelekezo yaliyotolewa katika Ilani kuhusu sekta ya nishati vijijini, yanatekelezwa kwa vitendo.

“Leo tunashuhudia kwamba Ilani yetu haikuwa maneno matupu bali ni matendo kama inavyojidhihirisha sasa,” alisema.

Hata hivyo, Nannila alitoa wito kwa watendaji wa serikali kuendelea kuchapa kazi kwa bidii ili vijiji vyote vifikiwe na umeme ifikapo mwishoni mwa mwezi Desemba, 2022 kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya CCM.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mwenyekiti wa Bodi, Wakili Kalolo na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Saidy, walimhakikishia Mkuu wa Wilaya na Mwenyekiti wa CCM kuwa watatekeleza maagizo yote waliyowapatia.

Walieleza kuwa REA imejipanga kuhakikisha inatekeleza azma ya serikali kufikisha umeme katika vijiji vyote ifikapo mwishoni mwa Desemba, 2022.

Aidha, walieleza kuwa Wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini nchini, wameshajulishwa kuwa hakutakuwa na ongezeko la muda wa kukamilisha miradi hiyo, hivyo wanapaswa wajipange kuhakikisha miradi inakamilika kwa muda uliopangwa.

Wakili Kalolo alimwomba Mwenyekiti wa CCM kufikisha salamu za shukrani kutoka REA kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kuendelea kuwezesha utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini na kwamba REA inaahidi haitamwangusha.

Akifafanua zaidi kuhusu utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili mkoani Mtwara, Mhandisi Saidy alieleza kuwa umelenga kuvifikishia umeme vijiji 402 vilivyosalia.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy wako katika ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini katika mikoa ya Ruvuma, Mtwara, Lindi na Pwani.


UCHUMI WA TANZANIA UNATARAJIWA KUKUA KWA KASI...

$
0
0

Uchumi wa Tanzania unatarajiwa kukua kwa kasi na kufikia zaidi ya asilimia 8 katika kipindi Cha miaka mitano ijayo

Matarajio hayo yanatokana na kuongezeka kwa Matumizi ya rasilimali na ongezeko la tija katika shughuli za uzalishaji.

Akifungua Mkutano wa 20 wa Taasisi za fedha nchini uliofanyika leo November 25, 2021 Jijini Dodoma, Gavana wa Benki Kuu Tanzania Profesa florens Luoga amesema ili kusaidia hilo wanatekeleza hatua za kisera ikiwemo zinazolenga kupunguza riba za mikopo na kuongeza ukwasi katika mabenki.

Amesema kwa sasa wanahakikisha mfumuko wa bei nchini unakuwa wa kiwango cha chini,thamani ya Shilingi dhidi ya Fedha za kigeni inaendelea kuwa imara ili kuongeza mikopo kwa Sekta binafsi na kuchangia ukuaji wa uchumi.

"Tanzania pia itaendelea na maandalizi ya kununua dhahabu yenye ubora unaotakiwa kutoka viwanda vya kusafisha dhahabu vilivyopo nchini,"alisema.

Profesa Luoga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muunganano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake alizofanya kuhusiana na fedha za IFM kwa ajili ya kushughulikia changamoto UVICO19.

SHIRIKA LA POSTA, MRISHO MPOTO WAINGIA MAKUBALIANO YA KUTANGAZA BIDHAA NA HUDUMA

$
0
0
 SHIRIKA la Posta Tanzania limeingia makubaliano ya pamoja kati ya shirika hilo na msanii wa nyimbo za asili na Mshairi balozi mteule Mrisho Mpoto 'Mjomba' kwa lengo la kutangaza huduma na bidhaa za shirika hilo ambalo lipo katika mabadiliko makubwa ya utoaji huduma ndani na nje ya nchi kwa teknolojia ya hali ya juu.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla iliyoambatana na utiaji saini wa makubaliano hayo Posta masta mkuu Macrice Mbodo amesema,lengo la kuingia makubaliano hayo ni kulitangaza shirika hilo ambalo lipo katika mabadiliko makubwa na limekuwa shirika la kidigitali katika utoaji huduma.
''Makubaliano haya ni kwa ajili ya kulitangaza shirika letu la Umma ambalo kwa sasa ni shirika la kidigitali na sio shirika la barua kama wengi wanavyodhaani.... Makao makuu wa Posta Afrika yapo jijini Arusha hapa Tanzania hii nafasi adhimu kwetu kujifunza kupitia Posta zote Afrika, Haya ni mageuzi ya fasta na yenye tija kwa uchumi wa taifa na tunawahimiza wananchi kutumia huduma za Posta kama nchi nyingine wanavyofanya.'' Amesema.

Mbodo amesema, shirika hilo lina fursa nyingi ambazo jamii inatakiwa kuzifahamu na kuzitumia ikiwemo huduma ya duka mtandao ambayo huwezesha kuuza na kununua bidhaa kwa njia ya mtandao kote duniani.

''Posta ina miundombinu ya usafrishaji nchini na nje ya nchi tunasafirisha hadi samaki na dagaa kupeleka nje ya nchi tutumie fursa hii, pia kuna huduma za kifedha zinazotolewa katika shirika hili, huduma za pamoja (One Stop Centre) zinapatikana katika ofisi za Posta nchi nzima hivyo ni vyema wananchi wakatumia fursa hizo kupitia shirika hilo.'' Amesema.

Aidha amesema kuwa shirika hilo linaendelea kuimarika vyema na wanategemea kupokea ujumbe kutoka shirikisho la Posta duniani ambapo Tanzania ni mwanachama hai.

''Kupitia balozi mteule Mpoto, watanzania watapata fursa ya kulifahamu shirika la Posta  na huduma zinazotolewa kwa uaminifu na gharama nafuu kama nchi nyingine wanavyotumia na kuthamini mashirika yao ya Posta kama DHL ya Ujerumani na Royal Mail ya Uingereza ambalo pia lilitushirikisha katika kusafirisha kifimbo cha Malkia hadi hapa nchini, hivyo niwaombe watanzania wenzangu tuunge mkono juhudi za Serikali kupitia shirika hili.'' Amesema.

Kwa upande wake balozi mteule Mrisho Mpoto ameshukuru kwa kupewa nafasi hiyo na kuwashauri watanzania kupenda na kuthamini vitu vya nyumbani ili waheshimwe duniani na kukuza kipato na soko.

Mpoto amesema shirika la Posta ni  la  kidigitali, salama na wanamtandao mkubwa wa usafirishaji wa bidhaa ndani na nje ya nchi na kuahidi kuwafikia watanzania wengi na kuwafahamisha juu ya huduma na bidhaa za shirika hilo zenye uhakika na viwango vya kimataifa.
Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Macrice Mbodo (kulia) pamoja na Balozi mpya wa Shirika la Posta Tanzania, Mshahiri Mrisho Mpoto wakisaini hati za makubaliano mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani)  katika hafla fupi ya kumtambulisha Balozi wa Posta, iliyofanyika kwenye makao makuu ya Shirika hilo, jijini Dar es salaam leo.
Balozi mpya wa Shirika la Posta Tanzania, Mshahiri Mrisho Mpoto (kushoto), akizungumza jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye makao makuu ya Shirika hilo, jijini Dar es salaam leo.
Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Macrice Mbodo akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa hafla fupi ya kumtambulisha Balozi wa Posta, Mshahiri Mrisho Mpoto (kushoto), iliyofanyika kwenye makao makuu ya Shirika hilo, jijini Dar es salaam leo.

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA YAIPATIA TANZANIA MKOPO WA DOLA MILIONI 116.34 KUJENGA BARABARA MKOANI MTWARA

$
0
0

Na Josephine Majura, WFM Dar es Salaam


Tanzania imesaini makubaliano ya mkopo wenye masharti nafuu wa thamani ya dola za Marekani milioni 116.34 (takribani shilingi bilioni 268.18) kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kutoka Mnivata-Newala-Masasi mkoani Mtwara yenye urefu wa kilomita 160 kwa kiwango cha lami.

Mkataba wa msaada huo umesainiwa jijini Dar es Salaam, na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Bw. Emmanuel Tutuba, kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kanda ya Mashariki Dkt. Abdul Kamara.

Bw. Tutuba alisema kuwa kusainiwa kwa mkataba huu utaongeza kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya miradi inayoendelea kutekelezwa na Serikali kupitia ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kutoka takribani dola za Marekani bilioni 2.27 hadi kufikia dola za Marekani bilioni 2.39.

“Hiki ni kiashiria tosha cha ushirikiano mzuri na wa muda mrefu wa maendeleo tangu mwaka 1971 kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Maendeleo ya Afrika”, alisisitiza.

Alieleza kuwa fedha hizo pia zitatumika kujenga daraja la mto Mwiti lenye urefu wa mita 84, ujenzi wa stendi mpya za mabasi katika wilaya tatu (3) za Tandahimba, Newala na Masasi zinazonufaika na mradi, ununuzi wa magari mawili (2) ya kubebea wagonjwa na mashine mbili (2) za X-ray za kupima wagonjwa na utekelezaji wa mikakati ya usalama barabarani pamoja na mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake na vijana.

Bw. Tutuba alisema kuwa gharama za utekelezaji wa mradi ni dola za Marekani milioni 119.65 ambapo Benki ya Maendeleo ya Afrika imetoa dola za Marekani milioni 116.34 na Serikali ya Tanzania itachangia dola za Marekani milioni 3.31.

Aliongeza kuwa utekelezaji wa mradi huo unalenga kuimarisha miundombinu ya usafirishaji katika Ushoroba wa Maendeleo wa Mtwara ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii na kupunguza umaskini kwa wananchi.

Bw. Tutuba, alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo utaunganisha Bandari ya Mtwara na Mikoa ya Kusini mwa Tanzania na kufungua masoko ya kikanda katika nchi za Msumbiji na Malawi.

Aidha, alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutarahisisha shughuli mbalimbali za uchumi ikiwemo utafiti wa gesi, usafirishaji wa saruji, bidhaa za viwandani, pamoja na mazao ya kilimo likiwemo zao la korosho.

Bw. Tutuba alisema Serikali itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Benki ya Maendeleo ya Afrika ili kuimarisha ushirikiano wa kimaendeleo.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo wa Benki ya Maendeleo (AfDB) Kanda ya Mashariki Dkt. Abdual Kamara, alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo kutawezesha kuendeleza maeneo ya vijijini kwenye Ukanda huo wa Maendeleo wa Mtwara na kufanya eneo lote la barabara ya lami kufikia kilometa 816 hivyo kuchochea maendeleo ya maeneo hayo ikiwemo Bandari za Mtwara na Mbamba Bay katika Ziwa Nyasa.

“Mradi huo utarahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo katika ukanda wa Afrika na nchi jirani ya Msumbiji, Malawi na Zambia ambazo zitahudumiwa na Bandari ya Mtawara”, alisisitiza Dkt. Kamara.

Dkt. Kamara alisema kuwa mradi huo unatarajiwa kuleta manufaa makubwa katika uchumi wa nchi ambapo inakadiriwa kuwa utachangia uchumi kwa zaidi ya asilimia 20.6 utakapo kamilika.

Kusainiwa kwa mkataba huo utaongeza ufadhili wa benki hiyo hapa nchini, kwenye Sekta ya barabara kwa kiwango cha dola za Marekani bilioni 1.52 ikiwa sawa na asilimia 82 ya fedha zilizowekezwa na benki hiyo hapa nchini unaofikia takribani dola za Marekani bilioni 2.47 ambazo kwa kiwango kikubwa zimeelekezwa kwenye Sekta ya miundombinu ikiwemo usafirishaji , nishati pamoja na maji na usafi wa mazingira.

Dkt. Kamara, ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kufanikisha upatikanaji wa mkopo huo na kusisitiza umuhimu wa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mradi huo ili ulete manufaa yaliyokusudiwa kwa wakati.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi huo, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania, Mandisi Rogatus Mativila alisema kuwa wamegawanya katika awamu mbili na kwa kuanzia wataanza na kipande cha Mnivata hadi Mitesa kilomita 100 kupitia Newala na awamu ya pili itakua kipande cha kutoka Mitesa hadi Masasi kilomita 60 ikihusisha ujenzi wa daraja la Mwiti.

Aidha mradi huo utahusisha pia ujenzi wa miradi mbalimbali ya kijamii ikiwemo vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na madaktari na mashine za kubangulia korosho na maghala ya kuhifadhia korosho.

Aliahidi pia kusimamia utekelezaji wa mradi huo kwa weledi kwa kuzingatia vigezo vyote vilivyowekwa ili uweze kukamilika kwa wakati kama ilivyokusudiwa.



Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba (kulia) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kanda ya Mashariki Dkt. Abdul Kamara, wakisaini mkataba wa mkopo nafuu wa dola za Marekani milioni 116.34 (tshs bilioni 268.18) kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mnivata – Newala – Masasi mkoani Mtwara, yenye urefu wa kilometa 160 kwa kiwango cha lami, Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba (katikati) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kanda ya Mashariki Dkt. Abdul Kamara (kushoto), wakisaini mkataba wa mkopo nafuu wa dola za Marekani milioni 116.34 (tshs bilioni 268.18) kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mnivata – Newala – Masasi, mkoani Mtwara, yenye urefu wa kilometa 160 kwa kiwango cha lami, Jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania Mhandisi Rogatus Mativila.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba (kulia) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kanda ya Mashariki Dkt. Abdul Kamara, wakibadilishana Hati za Mkataba wa mkopo nafuu wa dola za Marekani milioni 116.34 (tshs bilioni 268.18) kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mnivata – Newala – Masasi, mkoani Mtwara, yenye urefu wa kilometa 160 kwa kiwango cha lami, Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba (kulia) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kanda ya Mashariki Dkt. Abdul Kamara, wakionesha Hati za Mkataba wa mkopo nafuu wa dola za Marekani milioni 116.34 (tshs bilioni 268.18) kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mnivata – Newala – Masasi mkoani Mtwara yenye urefu wa kilometa 160 kwa kiwango cha lami, Jijini Dar es Salaam.


Maafisa wa Serikali ya Tanzania wakiwa katika tukio la kusainiwa kwa mkataba wa mkopo nafuu wa dola za Marekani milioni 116.34 (tshs bilioni 268.18) kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mnivata – Newala – Masasi mkoani Mtwara, yenye urefu wa kilometa 160 kwa kiwango cha lami, Jijini Dar es Salaam.

Maafisa wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) wakiwa katika tukio la kusainiwa kwa mkataba wa mkopo nafuu wa dola za Marekani milioni 116.34 (tshs bilioni 268.18) kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mnivata – Newala – Masasi mkoani Mtwara, yenye urefu wa kilometa 160 kwa kiwango cha lami, Jijini Dar es Salaam.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango-Dar es Salaam)

UTT AMIS YADHAMINI WIKI YA NENDA KWA BARABARANI JIJINI ARUSHA

$
0
0
Kampuni ya UTT AMIS ikiwa ni mdau mkubwa wa Usalama Barabarani imedhamini Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Kitaifa jijini Arusha.

Inawakumbusha wawekezaji wake na watanazania wote kwa ujumla kujali usalama wao wawapo barabarani na kujali usalama wa wengine.

 Sambamba na udhamini huo UTT AMIS inashiriki maonyesho yanayoambatana na maadhimisho hayo katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

UTT AMIS inawakaribisha wakazi wa Arusha kutembelea banda lao ili kujifunza juu ya uwekezaji wenye tija kwenye mifuko inayosimamiwa na UTT AMIS. Maadhimisho hayo yameanza rasmi Novemba 23 na yatafikia kilele chake Novemba 28.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia katika maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani yaliyoanza Novemba 23-28 katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha.
Wananchi wakimsikiliza Afisa Uendeshaji wa Kampuni ya UTT AMIS, Hilder Lyimo wakati akiwaelezea fursa zinazopatikana katika kampuni hiyo.
Afisa Uendeshaji UTT AMIS ofisi ya Arusha, Wishiko Makumbati, akitoa maelezo kuhusu faida na fursa zinazopatikana katika mifuko inayosimamiwa na UTT AMIS.

Benki ya Exim Yatangaza washindi wa droo ya kwanza ya ‘Weka Mkwanja Tukutoe!’

$
0
0

 Benki ya Exim imetangaza washindi wa droo ya kwanza ya kampeni ya ‘Weka Mkwanja Tukutoe!’inayoendeshwa na benki hiyo ikilenga kuhamasisha watanzania kujiwekea amana huku wakipata fursa za kunyakua zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu pamoja na gari aina Toyota Vanguard.


Akitangaza washindi wa droo ya kwanza ya kampeni hiyo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko na Mawasiliano Msaidizi wa Benki hiyo Bi Mariam Mwapinga alisema jumla ya washindi 6 walipatikana kupitia droo hiyo na kujishindia zawadi ya shillingi million sita fedha taslimu.

“Katika droo ya leo jumla ya washindi sita (6) wamepatikana na wameweza kujishindia zawadi za fedha taslimu kiasi cha sh mil 6. Washindi hawa sita watakabidhiwa zawadi zao katika maeneo yao waliopo na tutaendelea na droo kama hizi kila mwezi na washindi wataendelea kuingia kwenye droo itakayowawezesha kushinda zawadi kubwa ya gari aina ya Toyota Vanguard.’’

“Wateja wetu wa sasa na wale wapya watakuwa kwenye nafasi ya kujishindia zawadi hizi kila wakapojiwekea akiba ya kuanzi Tsh. 500,000 na kuendelea. Kadili wanavyojiwekea amana kubwa zaidi ndivyo wanavyojiweka kwenye nafasi ya kushinda zawadi kubwa zaidi,’’ alisema Bi Mariam wakati wa droo hiyo iliyohudhuriwa pia na muwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini.

Akifafanua zaidi kuhusu kampeni hiyo Bi Mariam alisema inalenga kuleta mabadiliko kwenye mtazamo wa uhifadhi wa amana miongoni mwa watanzania kutoka kuhifadhi pesa majumbani na badala yake wazihifadhi kupitia benki hiyo kwa usalama wa fedha zao sambamba na faida nyingine nyingi ikiwemo riba.

“Lengo si tu kuhamasisha watanzania kujenga utamaduni wa kujiwekea amana, tunachohitaji ni kuona kwamba Watanzania wengi wanajiwekea amana zao sehemu salama ili kujiendeleza kukua kiuchumi ndio maana tumejipanga kuwahamasisha watumie akaunti zetu mbalimbali ikiwemo akaunti ya mshahara inayotumika kwa matumizi mbalimbali ya kila siku,’’ alitaja.

Alitaja akaunti nyingine kuwa ni pamoja na akaunti ya mzalendo inayoendeshwa bila makato ya kila mwezi, akaunti ya haba na haba, akaunti ya faida ambayo inakuruhusu kuweka akiba na kupata riba pamoja na akaunti ya Nyota ambayo ni akaunti maalum kwa ajili ya Watoto pamoja na akaunti ya wajasiriamali inayowahudumia wafanyabiashara na mahitaji yao tofauti tofauti ya kibiashara.

Kwa upande wake Ofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Bi Bi Neema Tatock alitoa pongezi kwa washindi wa promosheni hiyo huku akiwahamasisha walengwa kushiriki kwa wingi na kwamba wana nafasi kubwa ya kujishindia zawadi lukuki katika droo zinazofuata huku akiwahakikishia kuwa Bodi hiyo imejipanga kuhakikisha zoezi la kupata washindi linafanyika kwa kwa uwazi na kwa kufuata misingi halali ya kubahatisha.


Meneja Masoko na Mawasiliano Msaidizi wa Benki ya Exim Bi Mariamu Mwapinga (wa kwanza kushoto) akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani ) zawadi kubwa ya gari aina ya Toyota Vanguard itakayotolewa kwa mshindi wa kampeni  ya benki hiyo inayofahamika ‘Weka Mkwanja Tukutoe!’inayolenga kuhamasisha watanzania kujiwekea amana kupitia benki hiyo. Wengine ni pamoja na Wengine ni ofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha  Bi Neema Tatock (wa pili kushoto) na maofisa  wa benki hiyo.


Meneja Masoko na Mawasiliano Msaidizi wa Benki ya Exim Bi Mariamu Mwapinga (Katikati) akiongea kwa njia ya simu na mmoja wa washindi wa droo ya kwanza ya  kampeni  ya ‘Weka Mkwanja Tukutoe!’ inayolenga kuhamasisha watanzania kujiwekea amana kupitia benki  hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni ofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha  Bi Neema Tatock (Kulia) na Ofisa Bidhaa za Rejareja, Callist Butinga (Kushoto)

VIONGOZI UBUNGO WANOLEWA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA KIDIGITALI KULIPIA FEDHA ZA MAEGESHO YA MAGARI

$
0
0


WAKALA  wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeendesha semina elekezi ya kuwajengea uwezo na kutoa elimu kwa viongozi wa Wilaya ya Ubungo mkoani Dar es Salaam kwa Madiwani na Wawakilishi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama.

Semina hiyo ilijikita katika kufafanua kwa kina  kuhusu mfumo mpya wa Kielektroniki wa malipo ya Ushuru wa maegesho ya magari ambao unatarajia kuanza Desemba 1,2021.

Akifungua semina Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kheri James ameipongeza TARURA kwa kuandaa semina hiyo na amehaidi kutoa ushirikiano.Ofisi ya Rais ya Rais TAMISEMI, TARURA kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango wameboresha mfumo, sasa kumbukumbu namba (Control number) itapatikana ndani ya dakika moja kwa kutumia njia ya kutolewa ankara kupitia kwa Mkusanya Ushuru 

 Kwa kutumia TeRMIS App (inayopatikana PlayStore), Kwa kutumia GePG App (inayopatikana PlayStore & AppStore), Kwa kutumia simu ya mkononi Piga *152*00# kisha fuata maelekezo na Kwa kutumia Wavuti ya mfumo inayopatikana kwa www.termis.tarura.go.tz.

Pia, TARURA imeboresha eneo la utoaji wa Elimu kwa kuanzisha Dawati la Malalamiko na kuweka namba za simu ambazo ni 0733-149658, 0733–149659 au 0733-149660 na kupitia namba hizi mteja atapiga simu na kutatuliwa changamoto yake. Pia anaweza kuwasilisha lalamiko lake katika Ofisi za TARURA zilizopo karibu yake.

Katika semina hiyo washiriki wa semina hiyo wameelezwa jinsi ambavyo unatakiwa kulipa maegesho kidigitali ambapo mhusika atatakiwa  kutumia simu ya mkononi

Piga *152*00#

1. Chagua 4 (Nishati, Madini na Usafiri)

2. Chagua 2 (TARURA)

3. Chagua 1 - Lipia Maegesho

4. Ingiza namba ya chombo cha Moto

5. Utapokea ujumbe mfupi

6. Bonyeza 1 Kuendelea

7. Ingiza namba ya Siri

8. Bonyeza 1 Kuthibitisha malipo ya Serikali.


MADAKTARI WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA

$
0
0

WAMJW-Dodoma

Wanataaluma ya Udaktari wametakiwa kuzingatia Sheria, Kanuni Na Maadili ya taaluma hiyo katika utendaji kazi wao kama inavyoainishwa katika kifungu cha Sheria ya Madaktari, Madaktari wa Meno na Wataalamu wa Afya Shirikishi.

Hayo yamesemwa leo na Msajili wa Baraza la Madaktari Tanganyika Dkt. David Mnzava alipokuwa anaongea na waandishi wa Habari jijini Dodoma.

Dkt. Mnzava amesema kumekuwa na uvunjifu wa Sheria kwa baadhi ya wanataaluma kwa kukiuka Kanuni za Madaktari, Madaktari wa Meno na wanataaluma wa Afya Shirikishi, hivyo amewataka kuzingatia sheria hizo.

Sheria ya mwaka 2017 inasimamia utendaji Kazi wa kada ya Udaktari, Udaktari wa Meno, Wataalamu wa mazoezi ya tiba, Wataalamu wa viungo bandia, Wataalamu wa Magonjwa ya Akili na utengemao, Matabibu, Matabibu Wasaidizi na Wataalamu wa Meno wasaidizi.

Aidha Dkt. Mnzava amesema Uvunjwaji wa Kanuni hizi utasababisha kosa la Kimaadili kama inavyonukuliwa katika kifungu cha 41 (2).

"Kifungu hicho kinasema Mtaalamu wa Udaktari, Udaktari wa Meno au Afya Shirikishi ataonekana kukosa sifa ya kutoa huduma, chini ya Sheria hii atakuwa amekiuka Sheria za Maadili." Amesema Dkt. Mnzava.

Hata hivyo Baraza limetoa wito kwa wasimamizi wa Mikoa na Wilaya kuweka mipango thabiti ya kusimamia utendaji wa wanataaluma katika maeneo yao



SERIKALI KUSAIDIANA NA WAPIMA ARDHI KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi  (wa kwanza kulia) akipewa maelezo juu ya kifaa cha kupimia ardhi na Mpima Ardhi Degratias Karulama wa Kampuni ya Trade Investment.
Mpima Ardhi Msungu Daudi wa Kampuni ya Global Survey (kulia) akitoa maelezo kwa Waziri Lukuvi akilezea jinsi vifaa vya kisasa vya upimaji wa ardhi vinavyofanya kazi.
Bwana Alfan Ngowo na Bi. Hellen wa Kampuni ya Esri Eastern Afrika wakitoa maelezo kwa Waziri Lukuvi.
Makamu wa Rais wa Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania IST, Bille Mussa akitoa hotuba yake.
Wanachama wa Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania IST wakifuatilia mkutano huo.
Meza kuu.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akitoa hotuba yake.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akitoa zawadi ya cheti kwa Mpima Ardhi wa muda mrefu.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/Michuzi Tv
SERIKALI imesema itaendelea kusimamia upangaji na uratibu wa kisheria katika matumizi ya ardhi nchini ili miongozo hiyo itoe huduma bora kwa wananchi pamoja na kumaliza migogoro ya ardhi ambayo imekua ikijitokeza kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akiwa kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania IST ambapo pamoja na mambo mengine amesema uwepo wa matumizi sahihi wa Sheria ya ardhi mbali na kusaidia kuweka usawa kwa wamiliki utasaidia pia migogoro ya hapa na pale.

Waziri Lukuvi amesisitiza kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kisheria wapima ardhi ambao watabainika kufanya kazi zao bila kufuata sheria na taratibu za kazi yao kwa maslai binafsi.

Amesisitiza umuhimu kwa wana taaluma hao kujitangaza wenyewe ili kufuta sifa mbaya iliyopo miongoni mwa Watanzania kuhusu utendaji kazi wao. Amesema sifa mbaya inasambaa zaidi kuliko utendaji kazi bora wa IST ambao unafanywa siri.

Lukuvi amesema hatua hiyo itasaidia, kuondoa dhana potofu iliyojengeka kwa wananchi kuwa IST ni walanguzi au wapimaji ni watu waharibifu na kwamba watanzania wataona kazi nzuri inayofanywa chama hicho.

“Bado wana dhana ya kwamba ukimkuta mpima ardhi basi ni yule anayepima mara mbili. Imezoeleka zamani eneo moja linapimwa mara mbili, lakini hatuja wao kuona kazi nzuri inayofanywa na wapima ardhi na ramani.

Ameongeza kuwa wapo wapima ardhi na ramani walioshiriki na kufanya vizuri katika miradi mbalimbali ikiwemo ya bomba la mafuta, barabara, mradi wa kusambaza umeme vijijini, lakini hawajahi kuonekana au kutambuliwa na wananchi wa maeneo mbalimbali.

“Nimewaambia viongozi wenu wajenge utaratibu wa kuratibu shughuli zinazotekelezwa na mwanachama mmoja mmoja ili Watanzania wazijue. Watanzania walio wengi wanajua nyinyi ni walanguzi tu hasa wale wa halmashauri,” alisema.

 “Tengenezeni mtandao wenu, sasa hivi watu wanasoma sana na muweke utaratibu wa kila mwanachama akiwa kazini atume picha ya namna anavyotekeleza majukumu yake ili ikifika siku kama ya leo  watu waone kazi  bora zilizofanywa kwa mwaka huu. Lazima mjisafishe watu waone kuna kazi nzuri mnafanya.

“Vinginevyo mtabaki na kashfa zenu kuwa ni walanguzi, uko nje tuna wajua bahati mbaya sekta yangu kila mmoja ana sehemu yake mbaya ambayo haijafutika.Maofisa mipango miji wana sifa zao wanaweza kubadilisha hata eneo la makaburi kuwa kituo cha mafuta, ndipo wanapokula wao,” alisema Lukuvi.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa IST, Bille Mussa ameiomba Serikali kuzifanyia marekebisho ya baadhi ya sheria za ardhi ili ziendane na wakati na kuifanya Sekta hiyo kutoa huduma zake kwa ufanisi kwaajili ya maslai ya wapima ardhi na Taifa kwa Ujumla.

Amesema mkutano huo, una malengo mbalimbali kiujadili changamoto mbalimbali za kitaalamu wanazokutana nazo kwa nyakati tofauti katika shughuli zao za kila siku.

Lengo jingine ni pamoja na kukumbushana wajibu na nidhamu ya kazi kwa anachama wao kuhusu utoaji huduma kwa wananchi. 

“Pia tutajadili kwa pamoja mabadiliko ya teknolojia na changamoto kwa wana taaluma na kuweka mikakati ya namna kukabiliana nazo. Pia tutajadili namna taaluma ya upimaji ardhi na ramani inavyoshiriki katika utekelezaji wa mkakati wa maendeleo endelevu ya nchi”

Kila mwaka Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania IST hufanya Mkutano Mkuu kwaajili ya kujadili masuala mbalimbali ambapo kwa mwaka 2021 mkutano huo unakwenda na Kauli mbiu isemayo " Jukumu la Taaluma ya Upimaji na Ramani katika ujenzi wa Miundombinu na Maendeleo Endelevu Tanzania.
Viewing all 120484 articles
Browse latest View live
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>