Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live

Job Announcement at the Commonwealth Secretariat

$
0
0

Job Announcement at the Commonwealth Secretariat



The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation call upon qualified Tanzanians to apply for the posts of Adviser-Commonwealth Blue Charter (Ocean Governance)and Outreach Coordinator- Blue Charter available at the Commonwealth Secretariat.

Job descriptions, terms and conditions of services applicable to the stated posts are available through: http://thecommonwealth.org/jobs


The deadline for application is 21st November 2018.


Issued by;

Government Communication Unit,

Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,

Dar es Salaam, 12 November 2018.


WAZIRI UMMY MWALIM ANATARAJIWA KUWA MGENI RASMI MBEZI FUN RUN

$
0
0

MWANDAAJI wa mbio za kujifurahisha maarufu ‘Mbezi Fun Run’  Shomari Kimbau amesema mbio hizo  zimepangwa kufanyika Desemba Mosi, kwenye hoteli ya Ramada Kunduchi, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Kimbau amesema mbio hizo zimeandaliwa na umoja wa wakazi wa Mbezi Beach zikiwa na lengo la kufahamiana na kubadilishana mawazo na kusaidia kwenye changamoto mbalimbali huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu.

Amefafanua mbio hizo zitaanzia kilomita 21, kilomita 10 na kilomita tano ambazo zitashirikisha pia makundi mbalimbali ya watu watakaopenda kushiriki ikiwemo vikundi vya Jogging . "Hizi ni mbio za kujifurahisha, na atakayependa kutembea pia ni sawa, na si kwa wakazi wa Mbezi tu, Wilaya zote tano za mkoa wa Dar es Salaam wanakaribishwa, lengo ni kutuleta pamoja wana Dar es Salaam.”alisema Kimbau na kuongeza

“Kama mnavyojua siku hiyo ya Desemba Mosi itakuwa ni siku ya Ukimwi duniani,  hivyo pia tumemualika Waziri Ummy Mwalimu awe mgeni rasmi na tutafanya nae mazoezi ya pamoja, na pia kutakuwa na zoezi la uchangiaji damu. Damu salama inahitajika kwenye banki ya damu, kama haijanisaidia mimi itamsaidia ndugu yangu, jamaa au mtanzania yoyote yule, hivyo tumeona siku hiyo pia tuitumie kuchangia damu salama na pia kupima afya yetu kwa kupima maambukizi ya virusi ya ukimwi.”amesema.


Kimbau amesema watakaotembea kilomita 21, wataanzia Ramada hoteli, kupitia Whitesand, Mbezi chini, Clouds, Cocacola, Mwenge na hadi Afrikana na kurudi Ramada. Kwa upande wa Mwenyekiti wa bonaza hilo la Mbezi Run Fun Loraa George ‘Robelo’ amesema ni wakati sasa watanzania kufanya mazoezi na ili kuepuka magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo sukari na shinikizo la damu.

“Bonaza hili linajumuisha wana Dar es Salaam yoyote atakayependa kushiriki, lengo ni kujumuika pamoja na kufahamiana, mbali na kukimbia pia kutakuwa na burudani nyingine nyingi ikiwemo mashindano ya kucheza mziki na michezo mbali mbali ya watoto.”alisema Loraa.

Wakati huo huo Msanii Christina Manongi ‘Sinta’amesema burudani katika bonaza hilo itatolewa na K- Mondo Sound na Up town intertaiment. “Wanaopenda kushiriki kuna tisheti zitapatikana kwa shilingi 25,000 na beji za ushiriki zitapatikana kwa shilingi 10,000 ila mtu kama anatisheti zake binafsi anaruhusiwa kushiriki hii ya tisheti ni hiyari.”alisema.
 Mwandaaji wa mbio za kujifurahisha maarufu 'Mbezi Fun Run' Loraa George akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo jijini Dar kuhusu maandalizi ya  Mbezi Fun Run zitakazofanyika Desemba Mosi  jijini Dar es Salaam,(kushoto) ni Mratibu wa mbio hizo Omary Kimbau na kulia ni mmoja wa waratibu wa mbio hizo Sinta Manongi 'Sinta' .
 Mwandaaji wa mbio za Mbezi Fun Run Shomari Kimbau akitoa ufafanuzi zaidi mbele ya Wanahabari kuhusu maandalizi ya mbio za kujifurahisha maarufu ‘Mbezi Fun Run’ zinazotarajiwa kufanyika Desemba Mosi, kwenye hoteli ya Ramada Kunduchi, jijini Dar es Salaam. 
 Mmoja wa Waraibu wa Mbizo Mbezi Fun Run Sinta Manongi 'Sinta' . akifafanua jambo kuhusiana na burudani itakayokuwepo siku ya tukio hilo,amesema burudani katika bonaza hilo itatolewa na K- Mondo Sound na Up town intertaiment. “Wanaopenda kushiriki kuna tisheti zitapatikana kwa shilingi 25,000 na beji za ushiriki zitapatikana kwa shilingi 10,000 ila mtu kama anatisheti zake binafsi anaruhusiwa kushiriki hii ya tisheti ni hiyari.”alisema.

HESLB YATOA ELIMU KWA WANAFUNZI WA MWAKA WA KWANZA WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB) imekutana na wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Akizungumza leo Dar es Salaam na wanafunzi hao katika chuo hicho Meneja wa Upangaji Mikopo wa Bodi hiyo Julitha Miyedu amesema kuwa taratibu za kuomba mikopo ziko wazi kutokana na vigezo na masharti vilivyoanishwa na kwamba bodi hiyo ipo kwa ajili ya wanafunzi kwa lengo la kuhakikisha kila mwenye vigezo vya mikopo anapata kwa wakati ili kuwezesha wanafunzi wasifikirie suala fedha katika kufanya mahitaji.

Miyedu elimu wanayoitoa ya mikopo ni endelevu katika kuhakikisha kila mwanafunzi anapata uelewa wa bodi inavyochakata mikopo kwa wanafunzi kwa kutumia vigezo vilivyoainishwa.“Haachwi mtu kwenye suala la utoaji mikopo ikiwa nia ya bodi kuona kila mtu anapata mkopo kutokana vigezo vilivyoanishwa katika kuijenga nchi yetu na mikopo huyo kwa wanuifaka baada ya kuhitimu kurejesha kwa ajili ya kunufaisha wengine ”amesema Miyedu.

Kwa upande wake Ofisa  Mawasiliano Mwandamizi wa Bodi ya Mikopo Veneranda Malima amesema wanafunzi wanatakiwa kusoma vitu katika mitandao na vipeperushi vya bodi kwa kupata taarifa zinazotokana na bodi. Amesema kuwa bodi imeweka mfumo wa kielekroniki katika kurahisisha malipo ya mikopo kwa wanafunzi kupitia kwa maafisa wa mikopo wa chuo na ndio inakuwa karibu nao kwa kila masuala ya wanafunzi yanayohusiana na mikopo huku akisisitiza bodi kuendelea kutoa taarifa katika utaratibu uliozoeleka, hivyo wanafunzi wajiepushe na kupata taarifa katika sehemu zisizo rasmi

Afisa Mikopo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM); Lugano Mwakyusa akitoa ufafanuzi wamasuala ya Wanafunzi waliojiunga na chuo hicho.

Katibu wa serikali ya Wanafunzi waChuo Kikuu cha Dar es Salaam, Respicious Reginald akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.


Meneja wa Utoaji Mikopo, Neema Nitume akitoa ufafanuzi wa masuala malipo ya Fedha za mikopo kwa Wanafunzi wanaonufaikana mikopo ya elimu ya juu.

Maafisa waandamiziwa HESLB wakiwa na viongozi wa DARUSO baada ya kuanza kwa mhadhara kwa Wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa kulia mstari wa mbele ni Waziri Mkuu wa DARUSO, Paul Goodluck, kulia kwake ni Waziri wa mikopo, LigwaDictaeakifuatiwa na AfisaMawasiliano wa HESLB Veneranda Malima na Menejawa Utoaji Mikopo, Neema Nitume.

MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA CRDB AENDELEA NA ZIARA YA KUJITAMBULISHA KWA VIONGOZI MBALIMBALI WA SERIKALI JIJIJI DODOMA

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) wakati akimkaribisha ofisini kwake, Jengo la LAPF, Jijini Dodoma leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay. Viongozi wa Benki ya CRDB wapo jijini Dodoma kwa lengo la kukutana na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na wateja wa Benki hiyo, sambamba na kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wao mpya ayepokea kijiti kutoka kwa Mtangulizi wake Dkt. Charles Kimei ambaye amestaafu. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kushoto) alipokuwa akizungumzia mikakati mbalimbali ya Benki hiyo pamoja na kujitambulisha kwake, baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Dodoma, Rehema Hamisi.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Alhaj Eng. Mussa Iyombe (katikati) akikabidhi cheti cha shukrani kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, kwa mchango waliotoa kwa Kitengo cha Ukaguzi na Ufuatiliaji Fedha cha TAMISEMI, wakati uongozi wa Benki hiyo ulipomtembelea Katibu Mkuu huyo ofisini kwake, Jijini Dodoma leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa na kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Ukaguzi na Ufuatiliaji Fedha cha TAMISEMI, Miriam Mbaga.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Alhaj Eng. Mussa Iyombe (kushoto) akifafanua jambo mbele ya Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, wakati wa kikao chao kilichofanyika ofisini kwake, jijini Dodoma leo.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay (wa pili kulia) alipokuwa akifafanua jambo wakati wa kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela aliyeteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati) akizungumza jambo wakati wa kikao chake na viongozi wa Benki ya CRDB, waliofika ofisini kwake leo jijini Dodoma kwa lengo la kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela aliyeteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo. 

Wataalam wa Afya Muhimbili Wanaendelea kuwajengea Uwezo Wataalam wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi

$
0
0

Wataalam wa afya wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) pamoja na wataalam wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa Lindi Sokoine wakiendelea kutoa huduma kwa wagonjwa na kuwajengea uwezo wataalam wa hospitali hiyo ili kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda kutibiwa Muhimbili, endelea kufuatilia habari katika picha.

Daktari Bingwa wa macho kutoka Muhimbili Judith Mwende akimpima macho mgonjwa kwa kutumia mashine maalum ya kuangalizia Retina, kushoto ni Dkt. Mwita Machage wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa Lindi Sokoine. 
Dokta Willybroad Massawe ambaye ni Dkt. wa upasuaji, pua, koo na masiko (kushoto) kwa kushirikiana na watalaam wengine wa MNH pamoja na wa hospitali ya Sokoine akimtoa mgonjwa matezi ya koo na matezi ya nyama ya pua (mafindofindo) upasuaji ambao huwa haufanyiki katika hospitali hiyo kutokana na ukosefu wa wataalam. 
Daktari Bingwa wa Patholojia kutoka MNH Innocent Mosha akifanya uchunguzi wa vivimbe ili kujua tatizo alilokuwanalo mgonjwa kwa ajili ya kuwasaidia Madaktari wa upasuaji kuendelea na tiba sahihi. 
Wataalam wa Muhimbili wakimfanyia upasuaji mgonjwa ambaye alikua akisumbuliwa na uvimbe. 

MAKAMU WA RAIS AENDELEA NA ZIARA YAKE WILAYA SIHA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka jiwe la msingi la ufunguzi wa hospitali ya Wilaya ya Siha. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Andrew Method (kulia) wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika hospitali ya Wilaya ya Siha. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Pichani Hospitali ya Wilaya ya Siha inavyoonekana baada ya kufunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 Sehemu ya Wakazi wa Kijiji cha Matabi wilayani Siha wakiwa wamejitokeza kwenye mkutano wa hadhara ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa kijiji cha Matabi wilayani Siha.
 Sehemu ya Wakazi wa Kijiji cha Matabi wilayani Siha wakiwa wamejitokeza kwenye mkutano wa hadhara ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Tanzania kupokea Watalii 10,000 kutoka Shanghai mwaka 2019

$
0
0


Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imesaini makubaliano na kampuni ya Touchroad International Group ya China kwa ajili ya kusafirisha watalii 10,000 kutoka jiji la Shanghai kutembelea Tanzania mwaka 2019 kwa kutumia ndege Maalum (chartered flights).

Makubaliano hayo yalisainiwa sambamba na mikutano ya kutangaza utalii katika soko la China- Tourism Roadshow katika miji mitano ya China iliyoanza katika jiji la Shanghai tarehe 12 Novemba 2018.

Mikutano hiyo ni matokeo ya jitihada za Ubalozi wa Tanzania nchini China kwa kushirikiana na TTB ambapo katika mkutano wa kwanza uliofunguliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki, washiriki mbalimbali zaidi ya 200 walijitokeza wakiwemo makampuni ya utalii (tour operators), mawakala wa usafirishaji (travel agents), mashirika ya ndege (airlines), na vyombo vya habari.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii, Bi. Devotha Mdachi alitoa mada maalum kuhusu vivutio vya utalii vilivyopo nchini Tanzania pamoja na fursa za uwekezaji katika sekta ya utalii. Aidha, makampuni ya utalii kutoka Tanzania yalipata fursa ya kuelezea packages zao za utalii mahsusi kwa soko la China. Kadhalika, Shirika la Ndege la Tanzania lilitumia fursa hiyo kutangaza juu ya mpango wake wa kuanza safari za moja kwa moja kutoka Tanzania hadi China katika mji wa Guangzhou mwezi Februari 2019.

Mikutano ya kutangaza utalii itaendelea kufanyika katika miji mingine ikiwa ni pamoja na Guangzhou tarehe 14 Novemba 2018, Hong Kong tarehe 16 Novemba 2018, Chengdu tarehe 19 Novemba 2018 na Beijing tarehe 20 Novemba 2018.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma, 13 Novemba 2018



Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki akitoa neno la ukaribisho katika mkutano wa kutangaza vivutio vya utalii uliofanyika Shaghai, China tarehe 12 Novemba 2018.

Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bi. Devotha Mdachi, Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki, Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania, Jaji Mstaafu, Thomas Mihayo na viongozi wa kampuni ya Touchroad International Group wakiwa katika furaha baada ya kukamilika uwekaji saini wa makubaliano ambapo kampuni hiyo italeta watalii 10,000 nchini Tanzania mwaka 2019.

Wajumbe wameshika shuka la kimasai ambalo linaonesha utamaduni wa kabila hilo maarufu kutoka Tanzania.

Baadhi ya Washiriki wakiwemo viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii, TTB na Balozi wa Tanzania nchini China wakiwa katika mkutano huo.

MBIO ZA NAMTUMBO SELOUS MARATHON ZAFANA, DC KIZIGO ATOA NENO LA SHUKRANI KWA WATANZANIA ,WANARIADHA

$
0
0
Na Ripota Wetu ,Globu ya jamii

WILAYA ya Namtumbo mkoani Ruvuma imefanya Mbio za Namtumbo maarufu kama Namtumbo Selous Marathon ambapo wanariadha mbalimbali akiwamo Godefrey Masaki wa JKT Arusha walishiriki.

Katika mbio hizo Masaki alishinda kwa kushika nafasi ya kwanza baada ya kushinda mbio za kilometa 21 huku akimuacha Mohemed Dule kutoka kikosi cha KG Songea aliyesgika nafasi ya pili wakati nafasi ya tatu ikishikiliwa na Ostin Kinyunyu kutoka mkoani Njombe.

Pia kwa upande wa wanawake katika mbio hizo Magdalena Crispin kutoka Arusha ameibuka mshindi wa kwanza wa mbio za Kilometa 21 huku mkimbiaji machachari Fabiola John kutoka Jeshi la Polisi Dar es Salaam akiibuka mshindi wa pili na kumwacha Adelina Irasias kutoka Dar es Salaam akishikilia nafasi ya tatu.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mbio hizo Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Mfaume Kizigo aliyeshiriki mbio za kilometa 2.5 akivalia nambari 021 amewashukuru Watanzania hasa wanariadha walioshiriki mbio hizo kwa kujitokeza kwao kushiriki na kuhamasisha malengo ya mbio

“Nashukuru Mungu kuwa miongoni mwa walioshiriki mbio hizi na kumaliza kilometa mbili na nusu.Nawashukuru sana washiriki na Watanzania wote kwa kuja kutuunga mkono katika safari yetu ya kujenga maendeleo ya sekta ya afya,” amesema Kiziga. Pia amepongeza jitihada za wadhamini wa mbio hizo Mantra Tanzania na Uranium One kwa ushirikiano mzuri wanaouonesha kwa wana namtumbo na watanzania kwa ujumla.

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo akimvalisha medali ya dhahabu mshindi wa kwanza KM21 wa Namtumbo Marathon Godfrey John Masaki kutoka JKT Arusha,wemgine ni washindi wa pili na wa tatu
mkuu wa wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo akimkabidhi zawadi mshindi wa kwanza KM21 wa Namtumbo Marathon Godfrey John Masaki kutoka JKT Arusha,  wengine ni washindi wa pili na wa tatu ambao pia walijinyakulia zawadi ya Fedha, Simu ya kisasa pamoja na medali.

Mshindi wa kwanza wa kike KM21 Magdalena Crispin (katikati) baada ya kukabidhiwa zawadi ya ushindi na Andrei Shutov(kulia) mwakilishi kutoka Uranium One Urusi, wa pili kutoka kulia ni mshindi wa pili Fabiola John na wa kwanza kushoto ni mshindi wa tatu Adelina Irasias. 

Picha ya baadhi ya Wanariadha mbalimbali walioshiriki Namtumbo Marathon.


REGIONAL INTEGRATION KEY TO BUILDING MASS OF QUALIFIED SCIENTISTS – HON. MUTIMURA

$
0
0

Kigali, November 13, 2018 - The Eastern and Southern Africa Higher Education Centers of Excellence Project (ACE II) is holding its sixth Technical and Advisory meeting at the Serena Hotel in Kigali, Rwanda, from November 12th to 14th, 2018.

The ACE II project is strengthening 24 competitively selected Africa Centers of Excellence (ACEs) to deliver quality, market relevant post graduate education, and building collaborative research capacity in five regional priority areas of industry, agriculture, health, education and applied statistics. Sixteen universities in eight countries are participating in the ACE II Project.

The five year project is financed by the World Bank to a tune of $140 million in form of credit to the eight countries which include Ethiopia, Kenya, Malawi, Mozambique, Rwanda, Tanzania, Uganda, and Zambia. Burundi, which does not host any ACE, is eligible to access services offered by the ACEs in other countries and regional capacity-building activities under the project.

The first phase, ACE I, was launched in 2013 in West and Central Africa with 22 ACEs and the second phase in Eastern and Southern Africa with 24 ACEs so as to create a collaborative movement across the continent to steer higher education towards science and technology. Combined, ACE I, ACE II and ACE III projects have a total investment of $600 million. 

The Minister of Education, Republic of Rwanda, Hon. Dr. Eugene Mutimura expressed his passion for the ACE II project “because of the potential benefits and outcomes we expect this project to bring to the region.” 

“We cannot develop as islands. Many of the pillars that we are talking about in terms of developing science must be linked to regional integration,” he said. For example, Carnegie Mellon University Africa Center in Rwanda and other ACEs in Rwanda have offered scholarships to several students from the region.

“It would be good to think about regional integration in terms of developing human capital resource required for our region as a bloc,” said Hon. Mutimura. Prof. Alexandre Lyambabaje, the Executive Secretary of Inter-University Council for East Africa (IUCEA), the Regional Facilitation Unit of ACE II, said that the main aim of countries joining the ACE II Project was to create a conducive environment for training highly skilled and competent scientists at Masters and PhD degree levels in identified key strategic areas.

LONGIDO KUPATA MAJISAFI NA SALAMA KWA ASILIMIA 100-PROFESA MBARAWA

$
0
0
Waziri wa Maji Mhe. Profesa Makame Mbarawa (Mb) amesema hali ya upatikanaji majisafi na salama katika mji wa Longido wenye idadi ya wakazi 16, 712 inaongezeka kutoka asilimia 15 ya sasa inayowafikia wananchi 2, 510 hadi kufikia asilimia 100.

Waziri Mbarawa akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo amefafanua kuwa hatua hiyo inamaanisha wananchi wote katika mji huo watapata huduma ya majisafi na salama kupitia mradi mkubwa wa maji wa Longido unaoanzia mto Simba katika wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro wenye uwezo wa kuzalisha maji kiasi cha Mita za ujazo 2,160 kwa siku wakati mahitaji halisi katika mji wa Longido ni Mita za ujazo 1,462.

Waziri Mbarawa ameainisha mradi wa maji Longido unaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 15.7 tayari mabomba yenye urefu wa kilometa 94 yamelazwa kutoka katika chanzo cha maji cha mto Simba wilayani Siha na mkandarasi kampuni ya ujenzi ya STC anatakiwa kukabidhi mradi mwezi ujao Tarehe 15 Desemba 2018. 

Waziri Mbarawa amesema ili kuhakikisha wananchi wa Longido wanapata maji huduma ya maji haraka na kujikita katika shughuli nyingine za maendeleo, Serikali iliamua kandarasi ya mradi huo itekelezwe na Wakandarasi waliopewa kazi tofauti; kazi hizo ni pamoja na kujenga matanki, ujenzi wa mifumo ya kusambaza maji, na ujenzi katika chanzo cha maji.

Waziri Mbarawa amesema Serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma ya majisafi na salama kama ambavyo Sera ya Taifa ya Maji ya mwaka 2002 inavyoelekeza kuwapatia wananchi waishio vijijini majisafi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao. 

Aidha, ameongeza nia hasa ni kufanikisha asilimia 85 ya wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama katika maeneo ya vijijini ifikapo mwaka 2020 na asilimia 95 katika miji. Pamoja na hilo amewataka wananchi kutunza mazingira na kuotesha miti kulinda vyanzo vya maji. 
Waziri wa Maji Mhe. Profesa Makame Mbarawa (Mb) akitoa maelekezo katika kizimba cha kupunguza msukumo wa maji (BPT) katika eneo la mto Simba, wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro. Mradi wa maji wa Longido chanzo chake kipo mkoani Kilimanjaro.
Waziri wa Maji Mhe. Profesa Makame Mbarawa akiangalia ubora wa kizimba na bomba zilizotumika katika kizimba cha kupunguza msukumo wa maji (BTP) katika eneo la mashamba la Simba. BTP moja ya kazi yake ni kuzuia mabomba kupasuka. Mradi wa maji wa Longido mabomba yamelazwa kwa umbali wa kilomita 94 na thamani ya mradi ni kiasi cha Shilingi bilioni 15.7.
Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa (Mb) akishiriki kazi ya kuunga mabomba kabla ya kulazwa eneo la Mbugani, katika mradi wa maji wa Longido . Waziri Mbarawa amemtaka mkandarasi kampuni ya Ujenzi ya STC kukabidhi mradi ifikapo Tarehe 15 Desemba 2018. 

VIONGOZI WA MATAWI WA YANGA SC WASHUSHIWA RUNGU NA KAMATI YA MAADILI YA TFF

TFDA NA ELIMU YA VIFAA TIBA KWA JAMII

MICHUZI TV: KMC WAMTAMBULISHA RASMI ELIUS MAGULI

KAMATI YA BARAZA LA WAWAKILISHI INAYOSIMAMIA OFISI ZA VIONGOZI WAKUU ZANZIBAR YAVUTIWA NA MAFANIKIO YA TASAF.

$
0
0
NA Estom Sanga- TASAF.

Wajumbe wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wamepongeza hatua ya Serikali ya Muungano na ile ya Mapinduzi kwa usimamizi thabiti wa utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF.

Wakizungumza jijini Dar es salaam baada ya kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Shughuli za TASAF mwanzoni mwa ziara ya siku NNE ya kutembelea miradi ya Mfuko huo, Wajumbe hao wameeleza kuridhishwa kwao na namna Mfuko huo ulivyoleta hamasa ya wananchi kujinasua na tatizo la umaskini uliokithiri.

Wamebainisha kuwa miradi iliyotekelezwa na TASAF nchini inaonyesha taswira nzuri ya uwajibikaji na utekelezaji wa maagizo ya serikali yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi na kuondoa kero ya umaskini.

Wametolea mfano wa miradi ya Shule ,Afya,Maji na hata uanzishaji wa miradi ya midogo midogo ya kiuchumi kwa wananchi kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji wa shughuli za kujiongezea kipato .

Aidha Wajumbe hao wameiomba serikali kupitia TASAF kuhakikisha kuwa inatoa fursa nyingine ya Wananchi wanaokabiliwa na umaskini ambao hawakupata fursa ya kuandikishwa kwenye shughuli za Mpango huo unaohudumia takribani Kaya Milioni MOJA na Laki Moja Tanzania Bara ,Unguja na Pemba.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bw. Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akizungumza kwenye kikao cha Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa Zanzibar wa liotembelea taasisi hiyo kuona utekelezaji wa shughuli zake.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kusimamia Ofisi za watendaji wakuu wa kitaifa katika baraza la wawakilishi Mhe. Ali Suleimani Ali akizungumza kwenye kikao na Watendaji wa TASAF baada ya kupokea taarifa ya miradi ya TASAF.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais –Zanzibar Mhe. Mihayo Juma N’hunga akizungumza wakati wa kikao cha pamoja katika wajumbe na menejimenti ya TASAF juu ya utekelezaji wa shughuli za mfuko huo.
Mkurugenzi wa Miradi wa TASAF ,Bw. Amadeus Kamagenge(aliyesimama ) akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za TASAF kwa wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa Zanzibar.
Mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa akichangia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za TASAF kwenye kikao kilichofanyika kwenye ofisi za TASAF jijini Dar es salaam.

Serikali ya Awamu ya Tano yaimarisha matibabu ya Moyo nchini.


SPIKA WA BUNGE APOKEA MSAADA KWA AJILI YA HOSPITALI YA KONGWA

$
0
0

Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akipokea mojawapo ya Mashine maalum ya kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya kufikisha miezi tisa iliyotolewa na Benki ya Diamond Tust kwa Hospitali ya Wilaya ya Kongwa jana. (Picha na Ofisi ya Bunge).
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akitoa shukrani kwa Benki ya Diamond Tust mbele ya Waandishi wa Habari mara baada ya kupokea Mashine maalum ya kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya kufikisha miezi tisa iliyotolewa na Benki hiyo kwa Hospitali ya Wilaya ya Kongwa.
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akisikiliza maelezo kutoka kwa mwanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation Ndg. Doris Mollel kuhusiana na picha inayoonyesha mtoto aliyezaliwa kabla ya muda wake. Taasisi hiyo ikishirikiana na Benki ya Diamond Trust walitoa msaada wa Mashine maalum ya kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya kufikisha miezi tisa kwa Hospitali ya Wilaya ya Kongwa hii leo. (Picha na Ofisi ya Bunge)

MAKAMU WA RAIS ANEDELEA NA ZIARA YAKE HAI,AMSABAHI BIBI SIFAELI KUNDASHUMA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Bibi Sifaeli Kundashuma ambaye ni mmoja walioshiriki katika tukio la kuchanganya mchanga wakati wa Muungano wa Tanzanyika  na Zanzibar.Makamu wa Rais yupo wilayani Hai kwa ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) .
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi mara baada ya kufungua wodi ya Wanawake katika hospitali ya wilaya ya Hai. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

CHANZO KIMOJAWAPO CHA AJALI ZA BARABARANI NI UCHOVU WA MADEREVA -DKT. MPOKI

$
0
0
Na WAMJW, Dar es Salaam.

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa moja ya sababu za ajali barabarani, ni uchovu wa madereva.

Dkt. Mpoki ameyasema leo Novemba 13,2018 wakati wa kufungua mafunzo ya watoa huduma za tiba, uokoaji na usafirishaji wa majeruhi wa ajali na wagonjwa wenye dharura mbalimbali nje ya Hospitali nchini.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo, Dkt. Mpoki amelitaka jeshi la Polisi nchini kuangalia namna ya kuweka utaratibu wa madereva kubadilishana kwani suala la uchovu linachangia kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani.Aidha,akitolea mfano suala la uchovu, dereva kutoka Mwanza au Bukoba kwenda Dar es Salaam, basi ashuke Singida ili aingie dereva mwingine kumalizia safari na hiyo itasaidia kuepusha ajali.

“Tumemuomba Mkuu wa Jeshi la Polisi atusaidie kama mchango wa Polisi katika kupunguza ajali kwa kuhakikisha kwamba wanaweka utaratibu wa madereva wanaendesha kwa muda maalum. Kuliko ilivyo sasa madereva wanaweza kuendesha siku nzima, Hivyo wanakuwa wachovu na kuchangia kwa kiasi kikubwa sana ajali mbalimbali barabarani” amesema Dkt. Mpoki.

Hata hivyo ameeleza kuwa, mpango huo ni hatua ya kwanza ambayo Serikali imewekeza kuingilia kati pale watu wanapokuwa wameumia, ambapo huko nyuma maisha ya watu wengi yalikuwa yakipotea kwa sababu vifaa vilikuwa vinachelewa sana kufika mahali tukio na hivyo kushirikiana na Benki ya dunia kwa kutenga kiasi cha shilingi Bilioni 8 kwa ajili ya uwekezaji na shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya kuendesha shughuli za kila siku za wataalam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akizindua kitabu cha mafunzo ya watoa huduma za tiba, uokoaji na usafirishaji wa majeruhi Wa ajali na wagonjwa wenye dharura mbalimbali nje ya hospitali nchini Tanzania
Mkurugenzi wa idara ya dharura hospitali ya Ta ifa ya Muhimbili Dkt.Juma Mfinanga akipokea kitabu hicho cha mafunzo kutoka kwa Katibu Mkuu Dkt.Mpoki Mara baada ya kukizindua
Picha ya Pamoja ya watumishi toka wizara ya Afya,hospitali,Shirika la msalaba Mwekumdu,Chuo kikuu MUHAS Pamoja na majeshi ambao kwa Pamoja watatekeleza mpango huo nchini.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 14,2018.

MWANAHABARI WA RELI TV BEN MWANANTALA NA SUZAN MAMKWE WAMEREMETA

$
0
0
 Mwandishi machacahri wa wa Shirika la Reli Tanzania Ben  Mwanantala akiwa na mkewe Suzan Mamkwe baada ya kufunga.ndoa katika  kanisa la Mwenge Parokia ya Mwenge jijini Dar es salaan na kufuatiwa na mnuso wa nguvu katika ukumbi  wa Mwenge Hall. Globu ya Jamii inatoa hongera sana kwa Ben ambaye ni mfano wa kuigwa kwa wanahabari wa kwenye taasisi za umma kwa weledi wake na kujituma,
 Ben mwanantala na Suzan Mamkwe katika mnuso wao baada ya  kumeremeta
Ben mwanantala na Suzan Mamkwe wakiwa na furaha kwa kumeremeta
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live




Latest Images