Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live

POLEPOLE AENDELEA KUVUNA WANACHAMA WAPYA MKOANI KIGOMA

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma, 

JUMLA ya wanachama 27 kutoka Chama cha NCCR-Mageuzi  akiwemo aliewahi kuwa Diwani Kupitia Chama hicho Kata ya Kitagata  wilayani Kasulu mkoani Kigoma wamejiunga CCM.Miongoni mwa hao walijiunga CCM wapo pia wanaotoka Kata ya Nyakitonto na wamefikia uamuzi kutokana na utendaji kazi unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli.
Wanachama hao wapya wamejiunga CCM leo mbele ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Humphray Polepole ambaye yupo mkoani Kigoma akikagua  utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya mwaka 2015-2020.Wakizungumzungumza  mara baada ya kujiunga na CCM, wachama hao wamesema wamefikia uamuzi huo baada ya kuona kazi inayofanywa na uongozi wa awamu ya tano na viongozi wanavyozunguka kutatua kero za wananchi na kuchochea Maendeleo na kuinua uchumi wa wananchi.

Damiani Cosmasi ambaye aliwahi kuwa Diwani kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi amesema yeye amekuwa kiongozi katika chama hicho na hajawahi ona viongozi wa chama hicho  kufika kuwatembelea na kuwasaidia katika masuala ya maendeleo.Pia amesema wanapowachagua viongozi  hawawaoni hadi hapo wanapoanza kuomba kura tena ndipo wananza kuwatembelea.
Amefafani Serikali ya CCM imejitahidi kuyafanyia kazi yale yote yaliyo ahidi wakati wa kampeni na wameanza kuona mabadiliko na maendeleo mpaka vijijini. "Kila mtu ni lazima amuunge mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania kutokana na kazi kubwa anayoifanya ya kuwahudumia wanyonge ambapo ndicho kilicho kuwa kilio cha wananchi wengi," amesema.

Akizungumza baada ya kushiriki ujenzi wa Shule ya Msingi  Kasasa Kijiji cha Kasasa kata ya Kitagata a Wilaya ya Kasulu  na wananchi wa Kijiji hicho, Polepole amesema Serikali imeamua kuwasaidia wananchi kuwatoa katika dimbwi la umasikini na kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na shule na wanafunzi wote wanaofikia umri wa kwenda shule waende kama Ilani ya CCM  inavyoeleza.
Amesema kwa kazi kubwa inayofanywa na CCM na Serikali hiyo ni lazima wananchi wakubaliane nae kwakuwa anachokifanya  ndilo lililokuwa hitaji la wananchi wengi."Na Serikali imeandaa fedha nyingi kwaajili ya kuinua uchumi wa wananchi na kuhakikikisha wanaondokana na umasikini kupitia miradi ya maendeleo inayoanzishwa na Serikali ya CCM.


RAIS MAGUFULI AFUNGUA KIWANDA CHA SIGARA MANSOOR INDUSTRIES LTD KILICHOPO KINGOLWIRA MOROGORO

$
0
0


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage mara baada ya kufungua kiwanda cha Sigara cha Mansoor Industries ltd kilichopo chini ya leseni ya Phillip Morris Tanzania katika eneo la Kingolwira mkoani Morogoro. Wa kwanza kushoto ni Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Phillip Morris Tanzania Dagmara Piasecka akipiga makofi, wengine katika picha ni Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt. Steven Kebwe pamoja na Mmiliki wa kiwanda cha Sigara Mansoor Shanif Hirani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Tumbaku inayotumika katika utengenezaji wa Sigara hizo za Marlboro mara baada kufungua kiwanda hicho cha Sigara mkoani Morogoro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mapakiti ya sigara hizo za Marlboro wakati akikagua utendaji kazi wa shughuli mbalimbali za kiwanda hicho mara baada ya kukifungua.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mojawapo ya hatua katika utengenezaji wa Sigara mara baada ya kufungua kiwanda hicho mkoani Morogoro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mojawapo ya vifungashio vya Sigara hizo kiwandani hapo mara baada ya kukifungua.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

IGP SIRRO AKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAKAO MAKUU YA POLISI DODOMA

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akikagua mradi wa maendeleo wa  Makao Makuu ya Jeshi hilo unaotekelezwa katika mkoa wa Dodoma, leo mradi ambao unatarajiwa kukamilika hivi karibuni. 
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akitoka kukagua mradi wa maendeleo wa  Makao Makuu ya Jeshi hilo unaotekelezwa katika mkoa wa Dodoma, leo mradi ambao unatarajiwa kukamilika hivi karibuni. Picha na Jeshi la Polisi.

TPSF, WADAU WAKUTANA KUJADILI MAFANIKIO YA KUONDOLEWA VIKWAZO VYA KIBIASHARA

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

TAASISI ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), imesema vikwanzo vilivyokuwa katika biashara kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki vimepungua na hivyo kuongezeka kwa fursa za kibiashara.

Hayo yamasemwa na Mkurugenzi wa Sera TPSF, Gilliard Telly wakati wa Warsha kuongeza fursa za biashara katika mipaka ulioandaliwa TPSF kwa kushirikiana Taasisi ya Biashara na Uwekezaji ya East Afrika Mashariki (East Afrika Trade & Investiment Hub) iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Telly amesema changamoto zilizokuwepo katika soko biashara katika nchi za Afrika Mashariki zimeondoka kutokana na kufanya utafiti pamoja na kuzungumza na Serikali kuhusu vikwanzo vya biashara katika tozo.

Amesema tozo hizo zilikuwa kwenye mazao ya mchele iliyokuwa asilimia 10 katika soko la Kenya hali inayofanya wafanyabiashara kushindwa kufanya biashara hiyo.“Moja ya changamoto ilikuwa ni kuchelewa kwa taarifa kuwafikia wafanyabishara lakini kwa sasa taarifa zinawafikia kwa wakati,”amesema.

Telly amesema kuondolewa kwa tozo katika bidhaa za Kilimo katika soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki nako kunafanya kuinuka kwa kiuchumi.Amesema kwa upande wa bidhaa za vyakula Tanzania ndio inayolisha Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivyo biashara inazidi kukua kwa wafanyabiahara na kutanua masoko.
 Mkurugenzi wa Sera Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Gilliard Telly akizungumza katika warsha ya kuhitimisha mradi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na mafanikio ya mradi huo leo jijini Dar es Salaam.
.Mchumi wa East Africa Trade & Investiment Hub, Alfred Kombudo akizungumza mazingira ya biashara katika jumuiya ya Afrika Mashari leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Mkurugenzi wa masuala ya Uchumi wa USAID , Michelle Corzine akizungumza kuhusiana na biashara katika soko la Afrika Mashariki.
 Mkurugenzi wa Huduma za Jamii, Loius Accaro akizungumza kuhusiana na wafanyabiashara kushiriki katika masoko mbalimbali leo jijini Dar es Salaam. Leo jijini Dar es Salaam. 
 Baadhi ya wafanyabiashara na watendaji wa TPSF wakisikiliza maada mbalimbali.

RC Shinyanga akagua upanuzi wa kituo cha afya wilayani Kishapu

$
0
0
Na Robert Hokororo, Ofisi ya Mkurugenzi 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack amekagua maendeleo ya mradi wa upanuzi wa miundombinu ya kituo cha afya Songwa pamoja zahanati ya Maganzo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu.
Katika ziara hiyo Telack alikagua ujenzi wa chumba cha upasuaji na maabara katika kituo hicho cha afya ambayo unaotekelezwa kwa fedha zilizotolewa na Benki ya Dunia (WB) sh. milioni 400.
Akiwa Songwa aliwapongeza wananchi kwa akujitolea katika shughuli za maendeleo umoja na kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha wanapata maendeleo katika maeneo yao ikiwa ni kuboresha huduma.
“Niwapongeza wananchi kwa kujitolea kushiriki shughuli za ujenzi na tumekuja hapa tumeona mmejitokeza kwa wingi kujenga kituo chenu siku. Siku zote umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu kazi itakwenda haraka na kwa muda mfupi kwa sababu ninyi mmeamua kusema kile kitu ni cha kwenu,” alisema.
Mhe. Telack aliwataka wananchi kuwapa ushirikiano watumishi wa afya ambao wanawahudumia na kutoa taarifa kwa viongozi wao endapo wanaona wanakwenda kinyume cha taratibu za kazi.
Pia aliwataka watumishi wasivunjike moyo kutokana na baadhi ya changamoto zinazojitokeza pindi wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao huku akiwaahidi kuwa Serikali iko nao bega kwa bega.
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akizungumza na watumishi pamoja na wananchi katika viwanja vya kituo cha afya cha Songwa alipofanya ziara kukagua mradi wa afya. Wengine pichani kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba na diwani wa kata ya Songwa, Abdul Ngoromole.
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akizungumza na wananchi wanaojitolea nguvu kazi akiwa katika mradi wa upanuzi wa kituo cha afya Songwa wilayani Kishapu.
 Sehemu ya watumishi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao viwanja vya kituo cha afya Songwa.
 Mganga mfawidhi wa zahanati ya Maganzo, Sam Phillip akitoa maelezo kuhusu kituo hicho kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack alipokitembelea.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MAKONDA APOKEA TANI 120 ZA SARUJI KUTOKA VYAMA VYA USHIRIKA 27 VYA MKOA WA DAR

$
0
0
Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amepokea tani 120 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 2,400 ya saruji kutoka kwa Vyama vya ushirika 27 vya Mkoa huo vilivyoguswa na kempeni ya ujenzi wa ofisi 402 za walimu Dar es salaam.

Mifuko hiyo 2,400 ina uwezo wa kufyatua tofali 70,000 ambazo zitejenga ofisi 14 za kisasa kwa ajili ya Walimu. 

Akizungumza baada ya kupokea mifuko hiyo Makonda amesema shughuli ya ujenzi wa ofisi za walimu inaendelea vizuri na amewashukuru wadau wote wanaoendelea kuchangia kampeni hiyo inayolenga kuboresha mazingira ya kazi kwa walimu ili waweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la Ushirika Dar es salaam Tumaini Wilfred amesema wameguswa na jitiada zinazofanywa na Makonda katika kuboresha mazingira ya walimu.

Amesema ndio maana wameona umuhimu wa wao kama ushirika wasibaki nyuma katika kufanikisha jambo hilo ambalo ni jema na na la ukombozi wa fikra na kuongeza ushirika utaendelea kuunga mkono kwa kila hali juhudi zinazifanywa na Makonda.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda wakwanza kulia akizungumza machache leo jijini mara baada ya upoea kupokea tani 120 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 2,400 ya saruji leo jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wakiwasiri 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akipokea tani 120 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 2,400 ya saruji kutoka kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Ushirika Dar es salaam Tumaini Wilfred leo jijini Dar es Salaam.

BODI YA WADHAMINI HOSPITALI YA MUHIMBILI YAZINDUA KAMATI MBILI, YAJIWEKEA MIKAKATI YA MIAKA MITANO

$
0
0

BODI ya wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili pamoja na Menejimenti yake imejiwekea mikakati mbalimbali katika mpango mkakati wake wa miaka mitano kuanzia mwaka 2017 hadi mwaka 2022 unaolenga kuimarisha utawala bora ambao ni muhimu katika utekelezaji wa mikakakati mingine inayolenga kuboresha huduma kwa wagonjwa.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Ellen Mkondya-Senkoro wakati akizindua Kamati mbili ya Kudhibiti Uadilifu na Uratibu.

Amesema pamoja na ueledi wa kazi, uadilifu katika utumishi wa umma ni pamoja na kutokuomba rushwa au kutoa rushwa wakati watumishi wa umma wanapotekeleza majukumu yao. "Hospitali ya Taifa Muhimbili inaunga mkono mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa na mpango mkakati wa utekelezaji wa awamu ya tatu (2017-2022).

"Nina imani kwamba kamati hizi zitatekeleza majukumu yake ipasavyo kuhakikisha kwamba mkakati huu unatekelezwa kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali," amesema Dk. Mkondya-Senkoro.

akamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini (MNH), Dkt. Ellen Mkondya-Senkoro wakati akizindua Kamati mbili ya Kudhibiti Uadilifu na Uratibu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru (katikati) akitambulisha viongozi na wajumbe wa Kamati mbili ya Kudhibiti Uadilifu na Uratibu.

Viongozi wa kamati ya Kamati mbili ya Kudhibiti Uadilifu na Uratibu wakijitambulisha.
Viongozi wakifuatilia uzinduzi huo.
Kiongozi kutoka idara ya utawala bora, ofisi ya Rais, Ikulu kwa kushirikiana na taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wakitoa mafunzo elekezi na wawezeshaji kwa kamati zilizochaguliwa.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Ellen Mkondya-Senkoro (wa tatu toka kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wajumbe wa kamati mbili zilizochaguliwa. Picha/Habari: Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.

KAMATI YA MAADILI YAMFUNGIA MAISHA MICHAEL WAMBURA

$
0
0
Kamati ya Maadili ilikutana tarehe 14/3/2018 kupitia shauri linalomhusu Ndugu Michael Richard Wambura, Makamu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) ambaye anashtakiwa na Sekretarieti ya TFF kwa makosa matatu ya kimaadili.

TUHUMA ZILIZOWASILISHWA
Sekretarieti ya TFF iliwasilisha mbele ya Kamati mashtaka matatu (3) ambayo ni;

1.    Kupokea/kuchukua fedha za Shirikisho (TFF) za malipo ambayo  hayakuwa halali ikiwa ni kinyume na kifungu cha 73(1) cha Kanuni za Maadili za TFF Toleo la 2013.

2.    Kughushi barua ya kuelekeza alipwe malipo ya kampuni ya JEKC SYSTEMS LIMITED huku akijua malipo hayo sio halali ikiwa ni kinyume na kifungu cha 73(7) cha Kanuni za Maadili za TFF Toleo la 2013.

3.    Kufanya vitendo vinavyoshusha Hadhi ya Shirikisho ikiwa ni kinyume na ibara ya 50(1) ya Katiba ya TFF (kama ilivyorekebishwa 2015)

MAELEZO YA KOSA

Ndugu Michael Richard Wambura alichukua fedha isivyo halali kwa kughushi barua ya kampuni ya JEKC SYSTEMS LIMITED ya kujipa mamlaka ya kulipwa kwa kula njama na waliokuwa Viongozi Wakuu wa TFF; Rais na Katibu Mkuu waliopita. Kitendo hiki ni kuvunja maadili na kushusha hadhi ya Taasisi ya TFF.

SHAURI LILIVYOENDESHWA

Ndugu Wambura alipelekewa wito wa kufika mbele ya Kamati siku ya tarehe 14/3/2018 ili awasilishe utetezi kuhusu tuhuma zinazomkabili. Ndugu Wambura alipewa hiari ya kutoa utetezi huo kwa mdomo, kutuma kwa maandishi, kuleta mashahidi au kutuma mwakilishi kama kifungu cha 58 cha Kanuni za Maadili za TFF toleo la 2013 kinavyoelekeza. Ndugu Wambura alimtuma mwakilishi wake, Wakili Emanuel Muga, aliyefika na kuthibitisha kuwa ametumwa na mteja wake (Ndugu Michael Richard Wambura) kuwasilisha utetezi wake mbele ya Kamati.

Baada ya kuelezwa mashtaka yanayomkabili mteja wake, Wakili Muga aliiomba Kamati kuwa mteja wake anaomba kupewa muda wa kupitia shauri hilo ili aandae utetezi, vielelezo, na mashahidi. Mara baada ya kutoa ombi hilo Kamati ilimruhusu asubiri ili ipitie kabla ya kufanya uamuzi. Baada ya majadiliano wajumbe walikubaliana kuwa suala hili si geni kwa Ndugu Wambura; hivyo siyo kweli kuwa hana ufahamu nalo. 


Pia moja ya vielelezo vilivyowasilishwa mbele ya Kamati ni utetezi wa maandishi wa Ndugu Wambura kuhusiana na suala hilo ulioandikwa 4/12/2017. Hivyo Kamati ilijiridhisha kuwa Ndugu Wambura anao ufahamu wa kutosha wa suala hilo na alikuwa na uwezo wa kufika mbele ya Kamati ili kutoa maelezo ya ziada.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KAMISHNA UHAMIAJI, DKT MWIGULU WAMSHUKURU RAIS KWA KUTOA FEDHA BILILIONI 10/- KWA AJILI YA KUJENGWA OFISI ZA IDARA YA UHAMIAJI DODOMA

$
0
0
Na Ripota Wetu, Blogu ya jamii

KAMISHNA wa Uhamajia nchini, Dk.Anna Makakala na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk.Mwigulu Nchemva wamemshukuru Rais Dk.John Magufuli kwa kuwapa fedha Sh.bilioni 10 kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa ofisi za Idara ya Uhamiaji mkoani Dodoma.

Kwa upande wake Dk.Makakala ametoa shukrani hizo kutokana na uamuzi wa Rais kutoa fedha hizo Sh.bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi huo ambapo ameagiza zijengwe ofisi za idara hiyo ambazo zitakuwa za kisasa.Dk.Makakala amefafanua tayari wameshapata eneo kubwa kwa ajili ya kujenga ofisi zao.
"Sisi Idara ya Uhamiaji tunajukumu la kufuata taratibu zote kwa haraka iwezekanavyo ili jengo hili ndani ya mwaka wa fedha ujao liwe limekamilika kwsababu tayari fedha zipo,"amesema Dk.Makakala.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk.Mwigulu Nchemba aambaye naye ametembelea eneo hilo la Mtaa wa NCC lililopo Manispaa ya Dodoma Mjini, ambako ndiko patajengwa ofisi hizo ambapo naye amemshukuru Rais kwa kutoa fedha hizo.

Dk. Mwigulu amemshukuru Rais, kwa kuwapa fedha hizo kwa ajili ya ujenzi makao makuu ya Uhamiaji na tayari kwa sasa eneo kubwa lenye mita za mraba 9,777 limepatikana kwa ajili ya kujenga jengo kubwa na la kisasa kwa Idara hiyo.
"Tunashumkuru Rais Magufuli kwa kutoa fedha ambazo zitatumika kwenye ujenzi wa ofisi za Idara ya Uhamiaji ambazo zitakuwa za kisasa.Eneo ambalo tumepata ni kubwa na litatosha kujengwa ofisi hizo,"amesema Dk.Mwigulu.

Amefafanua ni eneo ambalo lipo karibu na ofisi nyingine muhimu ikiwamo ya Ofisi ya vitambulisho vya Taifa, Zimamoto na ofisi nyingine za Serikali ambapo zitasaidia mtu anapofika eneo hilo kupata huduma kadri anavyohitaji.

Dk.Migulu ametoa rai kwa idara ya Uhamiaji kuendelea kuchapa kazi kwa bidii kwani kuchapa kazi kwao ndio kumefanya wao kupata fedha hizo za ujenzi kwa haraka na fedha za kununua nyumba za makazi ya askari Dodoma.
"Iwapo fedha ambazo Rais amezitoa wangefuata utaratibu wa bajeti basi ingechukua muda mrefu kuzipata lakini uchapakazi wao umemfanya Rais kutoa fedha hizo,"amesema Dk.Mwigulu.

Mobile Week to Offer Brand New Smartphones at Throw Away Prices

$
0
0
Tigo's Corporate Communications Manager, Woinde Shisael (centre) briefs journalists on the Mobile Week that will happen on March 24 - 30 via the Jumia online shopping network www,jumia.co.tz , and give great offers and discounts on smartphones. Flanking her are Jumia Tanzania's CEO, Zadok Prescott (right) and Tecno Tanzania's Public Relations Officer, Eric Mkomoye (left).
Jumia Tanzania's CEO, Zadok Prescott (second right) briefs journalists on the Mobile Week that will happen on March 24 - 30 via the Jumia online shopping network www,jumia.co.tz , and give great offers and discounts on smartphones. Flanking him are Samsung Tanzania's Country Head, Suleiman Mohammed (far right), Tigo's Corporate Communications Manager, Woinde Shisael (second left) and Tecno Tanzania's Public Relations Officer, Eric Mkomoye (far left).
Samsung Tanzania's Country Head, Suleiman Mohammed (far right) briefs journalists on the Mobile Week that will happen on March 24 - 30 via the Jumia online shopping network www,jumia.co.tz , and give great offers and discounts on smartphones. Flanking him are Jumia Tanzania's CEO, Zadok Prescott (second right) , Tigo's Corporate Communications Manager, Woinde Shisael (second left) and Tecno Tanzania's Public Relations Officer, Eric Mkomoye (far left).

mbinu sahihi zatakiwa kutumika ili kuimarisha afya kinywa na meno

$
0
0
 Daktari bingwa wa meno kutoka Chuo kikuu cha AJMANI cha Falme za kiaarabu,  Zaid Mohammed Hassan akimfanyia uchunguzi wa meno mwanafunzi wa skuli ya Mwanakwerekwe H Juma Hassan katika zoezi la kutoa matibabu yaliofanyika skulini hapo.

Na Kijakazi Abdalla-MAELEZO
JAMII imetakiwa itumie mbinu sahihi ili kuimarisha afya kinywa na meno na kupunguza mzigo mkubwa wa kutibu maradhi ya meno.  

Akizungumza katika kampeni maalum juu ya kujikinga na maradhi yanayoathiri kinywa na meno katika skuli ya msingi Mwanakwerekwe ‘E’, Daktari Dhamana Kanda ya Unguja Muhidin Abdalla Mohammed, amesema wananchi wengi wamebainika kuathiriwa na maradhi ya kinywa na meno.

Kwa hivyo amesema ipo haja ya kuchukua tahadhari ili kupunguza tatizo hilo. Aidha, alisema lengo la kampeni hiyo ni kuinua uwelewa wa watu ambao hawatoi kipaumbele kwa afya ya kinywa na meno, na hivyo kujikuta wakisumbuka kuhahangaikia matibabu.

 Dkt. Muhidini Abdalla wa meno kanda ya Unguja  akiwapatia elimu fupi wanafunzi wa skuli ya Mwanakwerekwe E namna ya kusafisha meno.

Dk. Muhiddin pia amesema hatua ya kufanya kampeni hiyo katika skuli, inalenga kuwapa elimu wanafunzi juu ya namna bora na sahihi za kutunza meno na kupiga mswaki ili waimarishe afya ya meno yao.

Alisema katika umri mdogo, ndipo watoto hupitia mabadiliko makubwa kimwili, hivyo kuwapa taaluma kutawawezesha kufahamu mbinu sahihi za kuimarisha afya na kujikinga wanapokua wakubwa.

Hata hivyo, ameiomba Serikali iongeze juhudi zaidi kufikisha huduma za meno kila eneo ingawa kunahitaji gharama kubwa, lakini akasema kuacha watu waugue bila tiba ni gharama zaidi.

Alieleza kuwa, tangu kuanza kampeni hizo kuelekea maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa na meno kimataifa, zaidi ya watoto 1,000 wametibiwa kwa kushirikiana na madaktari kutoka Ujerumani, Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE) pamoja na Wizara ya Afya.

 Daktari dhamana wa Meno kanda ya Unguja alievalia vazi jeupe Muhidini Abdalla akishirikiana na madaktari bingwa kutoka Ujerumani na Falme za Kiarabu wakimng’oa jino mwanafunzi Aisha Makame wa skuli ya Mwanakwerekwe H katika matibabu yaliofanyika skulini hapo.

Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Msingi Mwanakwerekwe ‘E’ Khitiyar Haidhuru Ramadhani,  alisema ujio wa madaktari hao umewapa faraja  wanafunzi na elimu sahihi ya kutunza meno yao.

Aidha aliwataka wazee kujenga utamaduni wa kuwanunulia watoto vitu vinavyoweza kuwaepusha na maradhi ya meno kama vile pipi, biskuti na chokoleti ambavyo huchangia zaidi maradhi hayo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

MAKAMU WA RAIS KUONGOZA HARAMBEE YA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA MUHEZA

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mhandisi Mwanasha Tumbo (kulia) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu maandalizi ya Harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga. Kutoka kushoto ni Katibu wa Kamati ya Harambee hiyo, Hassan Msumari na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hamis Mgoda. IMeandaliwa na Richard Mwaikenda;Kamanda wa Matukio Blog;0715264202,0689425467

Na Mwandishi Wetu

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan, kuongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Hospitali mpya ya Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga. Akizungumza katika mkutano na wanahabari, jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhandisi Mwanasha Tumbo alisema kuwa hafla hiyo itakayoanza Kesho Ijumaa saa 12 jioni kwenye Hoteli ya Golden Tulip ya Masaki, Dar es Salaam itaambatana na chakula cha usiku kwa wageni waalikwa.

Hivi sasa Wilaya hiyo haina Hospitali ya Wilaya na wananchi wanaohitaji huduma za afya wamekuwa wakitumia hospitali teule ya Kanisa la Anglikana ambayo imeingia mkataba na Serikali na kutokana na idadi ya wananchi wa wilayani hapo hospitali hiyo imezidiwa.

Hayo yamesemwa leo na Mhandisi Tumbo wakati akizungumzia harambee ya kuchangisha fedha inayotarajia kufanyika kesho jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufanikisha ujenzi wa Hospitali mpya ya Wilaya hiyo.

Wajumbe wa Kamati ya Harambe hiyo wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa mkutano na wanahabari kwenye Hoteli ya Golden Tulip, katikati ya Jiji la Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Juma Mgazija, Mwenyekiti wa Kamati, Hamis Mgoda, Mkuu wa Wilaya, Mhandisi Mwanasha Tumbo, Katibu Tawala wa Wilaya, Desderia Haule na Katibu wa Kamati, Hassan Msumari.

Mhandisi Tumbo amesema kutokana na Wilaya ya Muheza kutokuwa na Hospitali ya Wilaya tangu kuanzishwa kwake mwaka 1974, wananchi wamekuwa wakiteseka pindi wanapohitaji huduma za afya na hivyo wakaamua kuchanishana fedha ili kuanza ujenzi wa hospitali hiyo.

Amefafanua tayari wananchi na wadau wa maendeleo wilayani Muheza mkoani Tanga na Watanzania kwa ujumla wameanza kuchingiaa ujenzi huo na hadi kukamilika kwake zinahitajika fedha Sh.bilioni 11.1, hivyo wakati wakisubiri fedha za Serikali Kuu na zile za kwenye bajeti wameamua kuanza kwa kuchangisha fedha hizo.

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMIS MACHI 15, 2018

BALOZI WA KUWAIT NCHINI AKABIDHI MASHINE ZA WATOTO NJITI KWA TAASISI YA DORIS MOLLEL

$
0
0
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jassim Al-Najim (kushoto) akikabidhi mashine maalum za kuwasaidia Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), kwa Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njiti, Doris Mollel ambazo zimetolewa na Ubalozi huo jana jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Rahma Amoud na Maryam Gerion wote kutoka Taasisi ya Doris Mollel. 

The Ambassador of Kuwait to Tanzania, HE Jassim Al-Najim (L) handing over the machines for preterm Babies, to the Founder of Doris Mollel Foundation, Doris Mollel, at the Kuwait Embassy Office in Dar es salaam Yesterday. Others are Rahma Amoud and Maryam Gerion all from the Doris Mollel Foundation.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jassim Al-Najim akiwa katika mazungumzo na Ujumbe kutoka Taasisi ya Doris Mollel, uliomtembelea ofisini kwake, Jijini Dar es salaam jana.

TFF YAMFUNGIA MAISHA MAKAMU WAKE WA RAIS MICHAEL WAMBURA


KUTOKA MAKTABA: MWALIMU NYERERE ATEMBELEA IKULU YA MAREKANI YA WHITE HOUSE JULAI 15, 1963

MAGAZETI YA IJUMAA LEO MARCH 16,2018

WANANCHI WA ARUMERU WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI

$
0
0

 Wananchi wilayani Arumeru Mkoani Arusha wamempongeza Rais John
Magufuli kwa wema wake katika kuwajali wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo wakati akikagua ujenzi unaoendelea katika Kituo cha Afya cha Usa river kinachoboresha kwa kukijengea jengo la upasuaji, wodi ya wazazi, maabara, nyumba ya daktari na maboresho
mengine ya majengo ya kituo hicho.

Katika ziara hiyo, wananchi walionyesha furaha yao kwa kumshukuru Rais Magufuli kwa kuwa ameonyesha kuwajali sana kwa kuwafanyia maendeleo makubwa sana katika kituo cha cha afya. Akizungumza katika ukaguzi huo, Waziri Jafo amewataka wananchi wa Arumeru kuendelea kushirikiana na serikali kwa hali na mali kwa ajili ya maendeleo yao na Tanzania kwa ujumla.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selamani Jafo akitoa maelekezo alipokuwa akikahua ujenzi unaoendelea wa Kituo cha Afya Usariver mkoani Arusha.
Wataalam wa Afya wa Kituo cha Afya Usariver mkoani Arusha wakiwa katika picha na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selamani Jafo huku wakionesha furaha yao baada ya kujengewa majengo mapya.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selamani Jafo akipokea taarifa kutoka kwa wataalam wa ujenzi wa Kituo cha Afya Usariver mkoani Arusha.
Moja ya majengo mapya yanayojengwa kituo cha Afya Usariver mkoani Arusha.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selamani Jafo akikagua maeneo mbalimbali ya ujenzi wa kituo cha Afya Usariver mkoani Arusha unaoendelea.

INTRODUCING DIAMOND PLATNUMZ ft OMARION - African Beauty (Official Music Video)

A Boy From Tandale - Diamond Album Launch

Viewing all 110182 articles
Browse latest View live




Latest Images