Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

Dk. Shein akutana na Balozi wa Urusi Nchini

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Balozi wa Shirikisho la Urusi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Yuri Fedorovich Popov alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa mazungumzo na Rais leo asubuhi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na mgeni wake Balozi wa Shirikisho la Urusi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Yuri Fedorovich Popov alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi.Picha na Ikulu, ZANZIBAR.

WASANII WA KUCHORA KUFANYA MAONYESHO BUSTANI ZA POSTA YA ZAMANI

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Wasanii wa Sanaa ya uchoraji nchini wanataraji kufanya maonyesho ya wazi ya uchoraji katika bustani ya NBC iliyopo Posta ya zamani jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kiongozi wa umoja wa wasanii hao wa kuchora, Amani Abeid amesema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kuweza kuonyesha umma umuhimu wa sanaa za uchoraji katika majengo na ofisi za serikali.

“wachoraji wote maarufu hapa nchini na walioweza kufanya kazi nyingi za kimataifa watakuwepo hapo kuonyesha umuhimu wa sanaa hii ya uchoraji kwa taifa” amesema Abeid.

Kwa upande wake mchoraji vibonzo maarufu nchini , Nathan Mpangala amesema kuwa wasani hao kwa umoja wao watachora kasha baadae kufanya maonyesho ya picha hizo katika makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam

Nathani ametoa wito kwa wakazi wote wa jiji la Dar es Salaam kufika katika maonyesho hayo ambayo yataanza kuanzia saa 2 mpaka saa 6 mchana.
Mchoraji wa Vibonzo Nathan Mpangala akizungumza juu ya uwepo wake katika Tamasha hilo la uchoraji.
Kiongozi wa kundi la Wasanii wa Sanaa ya Uchoraji, Amani Abeid akizungumza na Waandishi wa habari juu ya maonyesho ya uchoraji katika eneo la bustani ya Posta ya Zamani. 

KIPINDI MAALUMU CHA MAMA JANETH MAGUFULI NA MAMA MARY MAJALIWA ZIARA SINGIDA NA TABORA FEBR 12 - 17 ,2017

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA HOYCE TEMU

$
0
0
 Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimkaribisha ofisini kwake  Mkuu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Nchini Hoyce Temu, Ikulu jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).
 Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizungumza na  Mkuu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Nchini Hoyce Temu (kushoto) aliyemtembelea Makamu leo ofisini kwake, Ikulu jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Nchini Hoyce Temu mara baada ya mazungumzo, Ikulu jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha ofisini kwake Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Mwigulu Nchemba tayari kwa mazungumzo Ikulu jijini Dar Es Salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na  Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Mwigulu Nchemba , Ikulu jijini Dar Es Salaam


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na  Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Mwigulu Nchemba , Ikulu jijini Dar Es Salaam ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

MREMA AMSHUKURU RAIS MAGUFULI KWA MATIBABU NCHINI INDIA

$
0
0
Na Eliphace Marwa -Maelezo

Mwenyekiti wa Bodi ya Parole ya Taifa, Dkt. Augustine Lyatonga Mrema amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufanikisha safari ya kwenda nchini India kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.

Dkt. Mrema ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waaandishi wa habari kuhusu uteuzi uliofanywa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kwa kuwateua wajumbe wawili wa bodi hiyo.

“Nachukua nafasi hii kumshukuru Rais Magufuli , Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Wizara ya Afya na Ikulu, kwa kunipeleka nchini India kufanyiwa uchunguzi wa afya yangu na kupatiwa matibabu na sasa afya yangu imeimarika na niko tayari kutekeleza majukumu yangu”, alisema Dkt. Mrema.

Akizungumzia uteuzi uliofanywa na Waziri Nchemba, Mrema amesema kuwa toka alivyoteuliwa na Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Taifa, Bodi hiyo haikukaa vikao kutokana na baadhi ya wajumbe wa Bodi hiyo kumaliza muda wao.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Parole ya Taifa, Dkt. Augustine Lyatonga Mrema (katikati) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitangaza tarehe ya uzinduzi wa bodi mpya ya parole taifa tarehe 3 na 4 Machi 2017 mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Msaidizi wake Bw. Clemence Munisi na kulia ni Mkewe Bi. Rose Augustino Mrema.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Bodi ya Parole ya Taifa, Dkt. Augustine Lyatonga Mrema (katikati mwenye kofia) wakati akitangaza tarehe ya uzinduzi wa bodi mpya ya parole taifa tarehe 3 na 4 Machi 2017 mapema hii leo jijini Dar es Salaam.Picha na Eliphace Marwa - Maelezo.


WACHIMBAJI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA KUEPUSHA AJALI MIGODINI

$
0
0

Wachimbaji wadogo wa madini nchini wametakiwa kufanya shughuli za uchimbaji kwa kuzingatia sheria na kanuni za usalama migodini ili kuepusha ajali.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani alipokuwa akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu kwenye mgodi wa Musasa uliopo Kata ya Makurugusi, wilayani Chato.

Dkt. Kalemani alisema njia bora ya kuepukana na ajali migodini ni kufanya shughuli za uchimbaji kwa kutii sheria za uchimbaji madini bila shuruti na kuzingatia kanuni za usalama kwenye maeneo ya machimbo na wakati wa shughuli za uchimbaji.

Aliwaasa wachimbaji wadogo wa madini kote nchini kujifunza kutokana na ajali mbalimbali zilizotokea migodini ili kuepuka sababu zilizopelekea kutokea kwa ajali hizo kutojirudia tena kwenye maeneo mengine.

Aidha, Dkt. Kalemani aliwasisitiza wachimbaji wa madini kote nchini kuhakikisha wanafanya shughuli za uchimbaji kwa kutunza mazingira na afya zao pamoja na afya za wengine wanaozunguka machimbo husika.

Alisema suala la mazingira linapaswa kupewa kipaumbele wakati wa shughuli husika, na kwamba ni jukumu la kila mchimbaji na kila anayeishi ama kufanyia shughuli zake maeneo ya machimbo kuhakikisha anaboresha mazingira ili kuepusha majanga mbalimbali ikiwemo ya magonjwa ya mlipuko.

“Chimbeni madini kwa kutunza mazingira na afya zenu ili mpate kufaidi matunda yatokanayo na shughuli hii, alisema Dkt. Kalemani.
Kwa wakati huohuo, Naibu waziri huyo aliwakumbusha wachimbaji wadogo wa madini kulipa kodi na ushuru stahiki ili kuepuka usumbufu.
Aliwahakikishia wachimbaji wadogo wa madini kufanya shughuli zao bila kubughudhiwa endapo watafuata maelekezo ya sheria.

“Mkitaka kuishi salama na kufanya shughuli zenu bila kubughudhiwa, hakikisheni mnalipa kodi na tozo mbalimbali mnazopaswa kulipa,” alisema.
Dkt. Kalemani alizipongeza kampuni za watanzania zinazomiliki leseni kwenye machimbo hayo ya Musasa ambazo ni Godfrey and Partners, Kilimo Kwanza Group na Hapa Kazi Tu Group kwa kuonesha njia na kutunza usalama kwenye machimbo hayo na hivyo kuwataka wachimbaji wengine kuiga mfano huo.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akizungumza na wachimbaji wadogo kwenye machimbo ya dhahabu ya Musasa yaliyopo kwenye Kata ya Makurugusi, Wilayani Chato. Nyuma yake ni baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini.
 Baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini kwenye machimbo ya dhahabu ya Musasa katika Kata ya Makurugusi, Wilaya ya Chato wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani).
 Baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini kwenye machimbo ya dhahabu ya Musasa katika Kata ya Makurugusi, Wilaya ya Chato wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani).

Muonekano wa baadhi ya maeneo ya machimbo ya dhahabu ya Musasa katika Kata ya Makurugusi, Wilaya ya Chato.

Serikali yaunga Mkono uzinduzi wa Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (TDF).

$
0
0

Na Lorietha Laurence-WHUSM
Serikali imeunga mkono uwanzishwaji wa Bodi ya Maendeleo ya Mpira wa Miguu (TDF)  wenye lengo la kuratibu vyanzo mbalimbali vya mapato ili kutekeleza maendeleo ya mpira nchini ikiwemo  kukuza vipaji vya michezo kwa vijana wa kike na wa kiume.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipozindua Bodi hiyo iliyo chini ya uratibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania leo Jijini Dar es Salaam ambapo aliwataka wadau wa michezo,wananchi na sekta binafsi kuunga mkono jitihada  hizo.
“Jambo hili ni jema sana katika sekta  ya michezo nchini hivyo ni jukumu letu sote kuhakikisha tunaunga mkono juhudi hizi zenye lengo la kuleta matokeo chanya katika sekta hii muhimu mfano mzuri ni vijana wetu wa Serengeti Boys  wameshatuonyesha kuwa tunaweza kufika mbali” alisema Waziri Nnauye.
Aidha, aliitaka Bodi hiyo kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu ili kuhakikisha mfuko huu unakua na hivyo kuwezesha utendaji fanisi wa kukuza vipaji vya michezo wa kike na wa kiume na kwa wale watakaokiuka miiko ya kazi uongozi usisite kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yao.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  Mhe. Nape Moses Nnauye akiongea na wadau wa michezo katika  ufunguzi  wa Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) ulioanzishwa na  Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo  Jijini Dar es Salaam.
  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akimkabidhi nyaraka za Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) kwa  Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa Meshack Bandawe (kushoto), ambaye ni mjumbe wa bodi hiyo ,katikati ni  Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.Jamal Malinzi.Leo Jijini dar es Salaam.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akimkabidhi nyaraka za Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) kwa  Meneja Mwandamizi wa Benki ya NBC Salmi Rupia(kushoto), katikati ni   Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.Jamal Malinzi.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF)  mara baada ya kuuzindua leo Jijini Dar es Salaam .(Picha na Lorietha Laurence-WHUSM).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

JOH MAKINI,DONGO JANJA KUPAMBA KILI MARATHON 2017

$
0
0
Wasanii Joh Makini na Dogo Janja wanatarajiwa kutoa burudani ya nguvu katika mbio za Kilimanjaro Marathon 2017 zinatarajiwa kufanyika Februari 26, Mkoani Kilimanjaro.

Akizngumza Mjini Moshi, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli aliwataka wakaziwa Moshi kujitokeza kwa wingi katika mbio hizo ambazo ndio kubwa Tanzania kwa sasa.

“Wasanii hawa wawili wanakubalika Moshi na tuna uhakika wakazi wa Moshi na wangeni wengine kutoka sehemumbalimbali watapata burudani ya aina yake mara baada yam bio hizi kukamilika siku ya Jumapili,” alisema nakuongeza kuwa burudani hii itaenda sambamba na Kilimanjaro Premium Lager za baridi za chupa zenye ujazo wa 375ml ambazo zinauzwa Tsh 2000.

“Hii ni chupa mpya ambayo kwa sasa tunaiuza Moshina Arusha na tuna uhakika wateja wetu watafurahia,” alisema.

Akizungumza, msanii Joh Makini alisema amejiandaa vizuri kukonga nyoyo za mashabiki wake na kuwataka wakazi wa Moshi wajitokeze kwa wingikushuhudiamuziki wa aina yake.

“Moshi ni nyumbani na nina uhakika mbioza Kilimanjaro marathon mwaka huu zitakuwa za aina yake kwani maandalizi  ni mazuri na tayari tunahisi jotolake Moshi,” alisema.

Naye Dogo Janja alisema, “Kati ya mikoa ambayo ina muamko mkubwa ni Kilimanjaro na ni faraja kutumbuiza katika hadhara kama hii ya watu kutoka pembe mbalimbali wanaokuja kushiriki Kilimanjaro Marathon 2017.”

Wakati huo huo usajili Mjini Moshi umeshaanza huku wakaziwa Moshi na wageni kutoka sehemu mbalimbali wakijitokeza kujisajili huku zikiwa zimebakizsiku mbili tu kabla yam bio hizo ambazo zitafanyika katika viwanja vya Chuo Cha Ushirika Moshi Jumapili Februari26 kuanzia saa kumi na mbili asubuhi.

Wadhamini wa mbio za mwaka huu ni Kilimanjaro Premium Lager-42km, Tigo 21km, GAPCO 10 km-walemavu, Grand Malt-5km. Wengine ni KK Security, TPC Limited, FNB, Kibo Palace, Kilimanjaro Water, CMC Automobile, Rwandair, Keys Hotel and new sponsors Anglo Gold Ashanti na KNAUF Gypsum.

NAMAINGO BUSSINESS AGENCY NA NHIF YAWAKUTANISHA WAJASIRIAMALI WA MKOA WA TANGA PAMOJA LENGO KUHAMASISHA KUJIUNGA NA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF)

$
0
0


MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wajasiriamali na Taasisi ya Kibiashara ya Namaingo Bussiness Agency uliokuwa na lengo la kuwahamasisha kujiunga na bima ya Afya na kuhalalisha biashara zao

Mkurugenzi wa Kampuni ya Namaingo Business Agency, Bi Ubwa Ibrahima akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali wa wafanyabiashara na wajasiamali mkoani Tanga leo

Mkurugenzi wa Kampuni ya Namaingo Business Agency, Bi Ubwa Ibrahim akisisitiza jambo kwenye mkutano huo wa pamoja.

Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga(NHIF) Miraji Kisile akifafanua namna ya wajasiriamali na wafanyabiashara wanavyoweza kunufaika na huduma mbalimbali ikiwemo za matibabu kupitia mfuko huo.

MAWAZIRI 15 WA NCHI ZA SADC KUKUTANA DAR KESHO

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Mawaziri 15 wa Nchi Wananchama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika ( SADC), wanatarajia kufanya mazungumzo kesho jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiao wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga alisema kuwa mawaziri hao wanatarajiwa kuzungumza masuala mbalimbali ikiwemo elimu, ushiriki wanchi za SADC, ikiwa ni pamoja na kuzungumzia haliinayoendelea nchini Msumbiji.

“Tanzani ni mwenyeji na wenyekiti wa Mkutano huo, ambapo pia inaongoza Kitengo Maalumu cha Masuala ya Ulinzi,Usalama pamoja na Siasa, pia kamati ya siasa na diplomasia inatarajiwa kukutana pia wiki hii” alisema Waziri Mahiga

Kila mwaka mawaziri hao hukutana mara moja, kwa lengo la kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu nchi wanachama wa umoja huo.Katika hatua nyingine, Waziri Mahiga alisema kuwa ,Tanzania inashirikiana na Msumbiji kufanyia kazi suala la watanzania walihamishwa nchini.

“ Hili ni zuala gumu kidogo tusitoe majibu rahisi, na hivyo Serikali zote mbili zinaendelea kufanya mazungumzo zaidi juu ya suala hili” alisema Waziri Mahiga.

MARAIS WA NCHI MBILI WANATARAJIA KUFANYA ZIARA NCHINI

$
0
0

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Marais wa nchi mbili wanatarajia kufanya ziara nchini na kufanya mazungumzo na Rais Dk. John Pombe Magufuli katika masuala ya uchumi pamoja masuala ya uhusiano wa kidiplomasi katika nchi hizo.

Marais hao watakaofanya ziara hiyo,ni Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni  pamoja na Rais wa Visiwa vya Shelisheli, Danny Faure.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema ziara hizo zinafaida kwa watanzania katika uchumi.
Rais wa Yoweri Kaguta Museveni anatarajia kuwasili kati ya Februari 25 na kuondoka February 26 na Rais  wa Shelisheli, Danny Faure anatarajia kuwasili February 27 na kuondoka February 28.

Makonda amesema kuwa ziara hiyo inatokana na Mkutano wa Umoja wa Afrika uliofanyika  ambapo Rais Dk. John Pombe Magufuli alikutana na baadhi ya marais ambao wametaka kuja kufanya ziara nchini kwa faida katika nchi hizo.

 Amewataka wakazi wa jiji la Dar es Salaam kujitokeza katika kuwalaki viongozi hao kama uzalendo uliozoeleka.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza  na waandishi  wa habari (hawapo pichani) juu ya ugeni wa marais wawili kutoka nchi za Uganda na Visiwa vya Shelisheli leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii)

MUSEUM ART EXPLOSION POSTER

RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 25 YA CSSC

$
0
0
Rais Mstaafu wa Serikali ya awamu ya pili, Alhaji Alli Hassan Mwinyi, ameipongeza Tume ya Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC) kwa kutimiza miaka 25 tangu ilipoanzishwa mwaka 1992.  Akiongea katika maadhimisho hayo, Mzee Mwinyi amesema kuwa Serikali imekuwa ikitambua na kuthamini mchango wa makanisa na Taasisi za dini katika kuboresha huduma za Jamii.

“Nimefarijika sana kwa kupata taarifa kuwa hadi kufikia Septemba 2016, hospitali za Kanisa 87 na vituo vya afya 45, vimeingia Mkataba na Serikali katika kutoa huduma za afya”, alisema Rais Mstaafu Mwinyi.

Katika hatua nyingine, Mzee Mwinyi aliongeza kuwa kwa upande wake yeye amekuwa mstari wa mbele kwa kuwaasa ndugu jamaa na marafiki zake na Watanzania wote kwa ujumla, kutumia huduma zitolewazo na hospitali za kanisa kwa kuwa wanatoa huduma bora, kwa kuzingatia upendo

“ Ikiwa mnaona kazi zinawazidia na mnafikia sehemu mnanung’unika kwa kuzidiwa na kazi nyingi, basi ningesema mgomvi wenu ni mie. Maana nawaambia ndugu na Watanzania wenzangu, kuwa huduma nzuri za afya zinapatikana katika hospitali za Kanisa, kwa kuwa unahudumiwa kwa upendo pamoja na tabasamu,” aliongeza Rais Mstaafu, Mwinyi.

 Rais Mstaafu Alhaji Ally Hassan Mwinyi akitembelea  mabanda mbalimbali katika maadhimisho ya miaka 25 ya Tume ya Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC) yaliyofikia kilele siku ya tar 22/02/2017 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
 Mkuu wa Shirika la "Pressures Blood" Tanzania Padre Chesco Msanga, akimkabidhi zawadi ya picha Rais Mstaafu Mzee Mwinyi kama kumbukumbu alipoifungua Hospital ya St. Gaspar Itigi inayoendeshwa na shirika hilo
 Mzee Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Tume ya Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC).
Mzee Mwinyi akitoa Cheti kwa  Profesa Costa Mahalu, moja ya watu waliyotoa msaada mkubwa wa masuala ya Sheria kipindi Tume hiyo ilipokuwa inaanzishwa.

RAIS MUSEVENI KUWASILI NCHINI JUMAMOSI

$
0
0

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni anatarajiwa kufanya ziara ya siku mbili nchini kuanzia Jumamosi wiki hii.

Taarifa hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiao wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuendeleza uhusiano mzuri uliopo baina ya Uganda na Tanzania, pamoja na kujadili masula mbalimbali ya kikanda, kimataifa na sekta mbalimbali za ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususani katika sekta za nishati, biashara na uchukuzi.

“ Mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Uganda yameendelea kuimarika katika miaka ya hivi karibuni, ambapo mwaka 2016 Tanzania ilifanya mauzo nje kwa Nchi hiyo ya kiasi cha shilingi bilioni 66.849, ikilinganishwa na shilingi bilioni 78.31 za mwaka 2015” alisema Waziri Mahiga.

Aliongeza kuwa Uganda ni muhimu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo haina Bandari na hivyo inategemea Tanzania kwa ajili ya kupitisha mizigo yake.

Nchi ya Uganda imezidi kuwa na umuhimu kufuatia uamuzi wa kupitisha bomba la mafuta nchini Tanzania, kutoka Kabaale –Hoima, Uganda hadi Bandari ya Tanga, ambapo bomba hilo lina urefu wa kilimeta 1443 na kipenyo cha inchi 24.Bomba hilo la mafuta litakalokamilika mwaka 2020 limnatarajiwa kupatia nchi hizi mbili fursa mbalimbali.

“ Utekelezaji wa mradi huu utafungua fursa za ajira kwa watanzania, kuchochea shughuli za kiuchumi kwa mikoa inayopita bomba hilo, pamoja na kufungua ukanda wa biashara wa kaskazini mwa Tanzania na Uganda pamoja na kuimarisha uhusiano katika soko la Afrika Mashariki” alifafanua Waziri Mahiga.

Katika hatua nyingine, Waziri Mahiga alisema kuwa kuhusu mgogoro wa nchini Burundi, kumekuwepo na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Rais Museveni pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin Mkapa ili kuhakikisha amani inarejea nchini humo.

Katika ziara hiyo ya Rais Museveni nchini, atapokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Johm Magufuli ambapo atatembelea Bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kuangalia maboresho yaliyofanywa katika bandari hiyo, pamoja na Kiwanda cha kutengeneza Juisi cha Azam kilichopo Vingunguti jijini Dar es salaam.

DCB YAKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA DROO YA PILI YA WEKA NA AMANA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

WASHINDI wa bahati nasibu ya kampeni ya kuweka amana DCB inayojulikana kama Boresha maisha na DCB wamekabidhiwa zawadi zao  na Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya DCB Said Kapilima leo Jijini Dar es salaam.

Akizungumza kabla ya kutoa zawadi kwa washindi hao, Kpilima amesema kuwa hii ni droo ya pili ya bahati nasibu kwa wateja wa benki hiyo kunufaika na kampeni ya kuweka amana kwa akaunti za Akiba binafsi, akaunti za watoto na WAHI iliyoanza mwezi Novemba mwaka jana.

Kapilima amesema kuwa, lengo kuu la kampeni hii ni kuboresha maisha ya wateja wa benki hiyo kwa kuwapatia zawadi mbalimbali pindi mteja anapokuwa anaweka fedha mara kwa mara na inawadsaidia kuongeza ukubwa wa amana na kuwajengea utamaduni wa kujiwekea akiba benki kwa matumizi ,mengine.

Katika droo ya pili iliyochezwa mbele ya mkaguzi kutoka michezo ya bahati nasibu ya Taifa Bakari Maggid iliweza kutoa washindi wawili wa simu za mkononi, washindi wa tatu wa fedha taslimu za ada na washindi ishirini wa tshirt.
  Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya DCB Said Kapilima akimkabidhi zawadi ya simu Mercelina Haule wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa bahati nasibu ya  kuweka amana DCB inayojulikana kama Boresha maisha na DCB leo Jijini Dar es salaam.

  Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya DCB Said Kapilima akimkabidhi zawadi ya fedha taslimu kwa ajili ya ada ya watoto, Ziada Haule wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa bahati nasibu ya  kuweka amana DCB inayojulikana kama Boresha maisha na DCB leo Jijini Dar es salaam.
   Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya DCB Said Kapilima  akikabidhi zawadi za Tshirt kwa wateja waliofanikiwa kushinda bahati nasibu ya  kuweka amana DCB inayojulikana kama Boresha maisha na DCB leo Jijini Dar es salaam.
Baadhi ya washindi wakiwa katika picha ya pamoja na  Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya DCB Said Kapilima   (katikati), Meneja mwandamizi wa benki na matawi Haika Machaku(wa kwanza kulia) wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa bahati nasibu ya  kuweka amana DCB inayojulikana kama Boresha maisha na DCB leo Jijini Dar es salaam. 

ZIFAHAMU FAIDA ZITOKANAZO NA RASILIMALI ZA BONDE LA MTO NILE KWA TANZANIA

$
0
0


Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Mto Nile ni miongoni mwa mito mikubwa iliyopo upande wa Mashariki ya Bara la Afrika naDuniani kote ukiwa na urefu wa kilomita 6,695 ambapo beseni ya Nile hukusanya maji ya eneo linalojumuisha 10% za eneo la Afrika yote.

Kwa muonekano wa juu Mto Nile unaonekana kama pembetatu wakati upande wa chini wa eneo la Nile (Kaskazini) na upande wa juu (Kusini) kuna mimea mbalimbali inayoota kwa wingi pia katika kipindi cha mwisho wa mwaka eneo la mto Nile huwa linakuwa na mwonekano mwekundu na kuwa na maua yanayojulikana kama lotus flowers.

Japokuwa mimea hii haioti kwa wingi wakati huu kama ilivyokuwa hapo awali, mimea inayoota kwa wingi katika eneo la Mto Nile kwa upande wa chini ni yale yanayojulikana kama Egyptian lotus na kwa upande wa juu hujawa na mimea inayoitwa Cyperus papyrus.

Chemchemi za Nile ni mito yote inayopeleka maji kwenda Ziwa Viktoria katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda na Kenya na kwa upande mwingine wa Nile unaanzia Ethiopia ukiitwa Abbai au Nile ya Buluu unatoka katika Ziwa Tana wakati chanzo cha mbali kabisa ni mto wa Luvironza huko Burundi unaoingia katika mto wa Kagera na kufika Ziwa Viktoria.

Mto huo ambao unaanzia Ziwa Victoria nchini Tanzania, ni chanzo  kikubwa cha maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, viwandani, kilimo cha umwagiliaji na kuzalisha umeme kwa wakazi wa nchi za bonde hilo.

Kutokana na nchi nyingi kuzungukwa na mto Nile, suala la ushirikiano katika kusimamia na kuendeleza rasilimali za Bonde la Mto huo limepewa kipaumbele ili kuzuia migogoro inayoweza kuzuka baina ya nchi ambazo wanatumia mto huo.

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi inayosimamia shughuli za wanachama wa Bonde la Mto Nile (NBI), Innocent Ntabana anasema kuwa azma ya kusimamia na kuendeleza rasilimali za Bonde la Mto Nile limepewa kipaumbele na nchi zote zinazozungukwa na mto huo, jambo hilo ndilo limesababisha kuanzishwa kwa Sekretarieti ya NBI mwaka 1999 jijini Dar es Salaam.

NBI ina jukumu la kusimamia na kuendeleza rasilimali za maji za Bonde la Mto Nile kwa niaba ya nchi wanachama zipatazo 10 ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Sudan, Sudan ya Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Misri,” anasema Ntabana.

Kwa upande wa Mratibu wa Kanda wa Kitengo cha Uratibu cha Bonde la Mto Nile (NELSAP-CU), Elicad Nyabeeya anasema kuwa mto huo una manufaa makubwa kwa nchi wanachama kwani muunganiko wa nchi hizo umeleta mawasiliano mazuri ambayo yanapelekea kuinua uchumi wa nchi hizo pia kwa upande mwingine uwepo wa ushirikiano huo umesaidia nchi wanachama kufahamu tamaduni za watu tofauti tofauti.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA GUINEA CONAKRY

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri Mkuu wa zamani wa Guinea Conakry Mhe. Kabine Komara ambaye sasa ni Balozi wa Taasisi ya Maendeleo ya Bonde la Mto Senegal, Ikulu jijini Dar es salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri Mkuu wa zamani wa Guinea Conakry Mhe. Kabine Komara ambaye sasa ni Balozi wa Taasisi ya Maendeleo ya Bonde la Mto Senegal, Ikulu jijini Dar es salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa zamani wa Guinea Conakry Mhe. Kabine Komara ambaye sasa ni Balozi wa Taasisi ya Maendeleo ya Bonde la Mto Senegal, Ikulu jijini Dar es salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

TANZANIA DAY IN DALLAS, TEXAS

$
0
0

Last year on April 29th the Mayor of Dallas Declared that day as Tanzania Day in Dallas. Come join the community this May as we celebrate the day as well as learn more about this land of Mwalimu Julius Nyerere.
About Tanzania: Tanzania occupies a total land of 364,898 square miles in East Africa, south of Kenya and Uganda, and east of Burundi, Rwanda and Congo—with an estimated population of 50 million people (slightly less than twice that of Texas). Tanzania is a founding member of the East Africa Community and home the Community’s headquarters.  English and Kiswahili are both official languages; ethnic composition include native Africans, Asians, Europeans and Arabs.  These groups have diverse religious believes including 35% Islam, 30% Christians, and about 35% indigenous and other religions.
Tanzania has three of Africa's best-known lakes—Victoria (is Africa's largest lake by area, the world's largest tropical lake), Tanganyika (second largest freshwater lake in the world by volume, the second deepest and the world's longest freshwater lake), and Nyasa. It is also the home of Mount Kilimanjaro (19,340 feet), a snow-caped, highest point on the continent. Tanzania’s Serengeti reserves is the continent’s most diverse and largest concentration of plains animals – a breathtaking spectacle that features more than one million wildebeest, 500,000 gazelles and 250,000 zebras on the move.
The famous Olduvai Gorge, the cradle of mankind is in northern Tanzania; it is an internationally recognized for Louis and Mary Leakey’s famous discoveries of early humans. Research at Olduvai has produced an unparalleled wealth of archaeological data for the study of some key phases of early human evolution.

For more information: www.tzdallas.com

KANUSHO: RAIS MSTAAFU ALHAJ ALLY HASSAN MWINYI YU SALAMA NA BUHERI WA AFYA - KATIBU

$
0
0


Hiyo Story inyayozagaa mitandaoni kupitia link hio hapo juu ni Uzushi na iipuuzeni.  Rais Mstafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi yuko salama nyumbani kwake, na jana alikuwa kwenye hafla hiyo hapo chini. Jioni hii ataungana na Jumuiya ya Mabalozi pamoja na wadau wengine katika kusherehekea Siku ya Taifa ya Kuwait iliyoandaliwa na Balozi wa nchi hiyo hapa Dar es Salaam. Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie afya na siha njema na umri mrefu - Amin

Dkt Abdullah H. MAKAME_

 Katibu wa Rais Msaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi.
  Rais Mstaafu Alhaji Ally Hassan Mwinyi akitembelea  mabanda mbalimbali katika maadhimisho ya miaka 25 ya Tume ya Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC) yaliyofikia kilele jana tarehe 22/02/2017 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
  Mkuu wa Shirika la "Pressures Blood" Tanzania Padre Chesco Msanga, akimkabidhi zawadi ya picha Rais Mstaafu Mzee Ally  Hassan Mwinyi kama kumbukumbu alipoifungua Hospital ya St. Gaspar Itigi inayoendeshwa na shirika hilo

Mzee Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Tume ya Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC). 
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images