Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117117

Bondia Iddy Kipandu na Bahati Mwafyela kuzichapa idd pili jijini dar

$
0
0

 kocha kwame mkuluma kulia akimwelekeza Bondia Iddy Kipandu 'Iddy Bonge' jinsi ya kutupa makonde mazito mazito.


 Bondia  Iddy Kipandu 'Iddy Bonge' yupo kambini kwa ajili ya kupambana na bondia Bahati Mwafyela mpambano utakaofanyika siku ya sikukuu ya Iddi pili jijini Dar es salaam,katika ukumbi wa friends Corner Manzese.

 akizungumzia maandalizi ya mpambano huo mtaalishaji wa Mpambano huo,Waziri Rosta amesema mpambano huo wa uzito wa juu umekuwa gumzo katika jiji la Dar es salaam na vitongoji vyake kwani mabondia hao wanatafutana kwa muda mrefu sana na sasa wamekutana kwa ajili ya mchezo huo.

Mpambano huo wa raundi 8 siwakukosa kwani ndio mpambano pekee kwa mwaka huu kukutanisha uzito wa juu kwani mabondia wa uzito huu  wanaotamba viwango vyao ni vidogo ukizingatia kuwa wapo wachache nchini.

aliongeza kuwa mbali na mpambano huo kutakuwa na mapambano mengine ya mabondia chipkizi na wanaotamba hapa nchini.

Na kwa upande wa kocha anaemnoa bondia  Iddy Kipandu 'Iddy Bonge' amesema kuwa bondia wake alikuwa na manyama nyama mengi lakini kwa sasa hakuna kutokana na mazoezi anayompatia kwani kwa sasa dozi yake ni kutwa mara tatu na mpaka siku ya mchezo nahisi mambo yatakuwa safi.

Mpambano huo utakao sindikizwa na mabondia Hassani Mandula atakae pambana na Twalib Mchanjo na Fadhili Majia atakae menyana na Ally Mahiyo na Mustapha Doto atapambana na Hashimu Mjeshi mapambano yote ya utangulizi itakuwa ni ya raundi sita.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117117

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>