Spika wa Bunge Job Ndugai akimkabidhi kikombe Naodha wa timu ya Bunge Sports Club ambaye ni Mbunge wa Mbiga, Sixtus Mapunda baada ya timu hiyo kuifunga NMB Magori 2-0 wakati wa mchezo wa kirafi uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.
Timu ya kwanza ya Bunge kushinda kikombe ilikuwa timu ya mpira wa pete ambaye iliifunga timu ya pete ya NMB magoli 19 kwa 2, ikifuatiwa na timu ya mpira wa kikapu kwa wanaume ambayo iliwafunga wapinzani wao timu ya mpira wa kikapu ya NMB kwa jumla ya vikapu 37 kwa 28.
Kikombe cha tatu kwa timu ya Bunge kilipatikana kwa timu ya mpira wa miguu ambayo iliwafunga NMB goli 2-0 na hivyo kuendeleza rekodi ya kutopoteza mchezo wowote ambao timu hizo zimekutana.
Timu ya Bunge Sports Club na NMB Sports Club zimekuwa zikikutana zikicheza michezo mbalimbali ikiwa na lengo ya kuboresha uhusiano baina ya Bunge na NMB ambapo kwa mwaka huu bonanza hilo limefanyika katika uwanja wa Jamhuri uliopo makao makuu ya nchi, Dodoma.
Kikombe cha tatu kwa timu ya Bunge kilipatikana kwa timu ya mpira wa miguu ambayo iliwafunga NMB goli 2-0 na hivyo kuendeleza rekodi ya kutopoteza mchezo wowote ambao timu hizo zimekutana.
Timu ya Bunge Sports Club na NMB Sports Club zimekuwa zikikutana zikicheza michezo mbalimbali ikiwa na lengo ya kuboresha uhusiano baina ya Bunge na NMB ambapo kwa mwaka huu bonanza hilo limefanyika katika uwanja wa Jamhuri uliopo makao makuu ya nchi, Dodoma.

Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Straton Chilongala akimkabidhi nahodha wa mpira wa Pete wa Bunge Sports Club ambaye pia ni Mbunge wa Tarime Esther Matiko.
Abdulmajid Nsekela akikabidhi kikombe cha mpira wa Kikapu kwa washindi Bunge Sports Club.
Wachezaji wa Bunge Sports Club na NMB mpira wa pete wakiwania mpira wakati wa mchezo wa kirafi uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma.