Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117137

SIMANZI YATAWALA JIJI LA ARUSHA KATIKA KUAGA MIILI YA WANAFUNZI 32, WALIMU WAWILI NA DEREVA

$
0
0
 Umati wa wakazi wa Jiji la Arusha na maeneo ya jirani ukiwa umefurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu wa Sheikh Amri Abeid wakati wa zoezi la kuaga miili ya Wanafunzi 32 wa Shule ya Sekondari ya Lucky Vicent, Walimu wao wawili na Dereva waliopoteza maisha kwa ajali ya gari iliyotokea eneo la Rhotia Wilayani Karatu hivi karibuni. Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan ndie aliongonza zoezi hilo la kuaga.
Sehemu ya Jeneza zenye miili ya Wanafunzi 32, Walimu wawili na Dereva waliopoteza maisha kwa ajali ya gari iliyotokea eneo la Rhotia Wilayani Karatu hivi karibuni, zikiwa Uwanja wa Kumbukumbu wa Sheikh Amri Abeid wakati wa zoezi la kuaga lililoongozwa na Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan. 



Viewing all articles
Browse latest Browse all 117137

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>