Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109609 articles
Browse latest View live

CHAMA CHA UKOMBOZI (CHAUMA), CHAZINDUA KAMPENI ZAKE VIWANJA VYA BAKHRESA MANZESE DAR ES SALAAM LEO

0
0
 Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Ukombozi (Chauma), Dk. Hashim Rungwe, akihutubia wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho, uliofanyika viwanja vya Bakhresa Manzese Dar es Salaam leo.


 Mwananchi aliyevalia nguo za Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiondolewa na askari polisi baada ya kujipenyeza kwenye uzinduzi wa kampeni za Chama cha Ukombozi Umma (Chauma), uliofanyika viwanja vya Bakhresa Manzese Dar es Salaam leo.
 Mzee wa chama hicho, Mbwana Hassan Mbwana akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Mgombea ubunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Robinson Fulgence Lembo, akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Mgombea urais wa Zanzibar,  Mohamed Masoud Rashid, akihutubia.
 Wananchi wakishangilia.



 Mgombea Mwenza wa urais kupitia Chama cha Ukombozi (Chauma), Issa Abbas Hussein, akihutubia wakati wa uzinduzi huo.
Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za Chama cha Ukombozi Umma (Chauma), uliofanyika viwanja vya Bakhresa Manzese Dar es Salaam
(Imeandaliwa na mtandao wa 
www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

SIMU TV: HABARI KUTOKA VITUO VYA TELEVISHENI

MISA YA SHUKRANI

0
0
Familia ya Kanali Mstaafu Burchard Mushumbusi, inatoa shukrani za dhati kwa  ndugu, jamaa, marafiki na majirani wote walioshiriki nasi kwa hali na mali katika msiba wa mpendwa wetu Bi. Candida K Mushumbusi aliyefariki tarehe 24 Julai 2015 katika hospitali ya Apollo, New Delhi India na kupumzishwa katika nyumba yake ya milele tarehe 28 Julai 2015 hapa Dar es salaam.


Familia pia inatoa shukrani za dhati kwa Paroko na Mapadre wa Parokia ya Mt. Nicolaus, Kunduchi  Mtongani; Uongozi na jumuiya ya Mt. Yohane Mbatizaji Kunduchi; Mkuu wa Majeshi  ya Ulinzi ya Tanzania; Uongozi na watumishi wa Hari Singh&Sons, Benki Kuu ya Tanzania(BOT), Tanzania Food and Nutrition Centre (TFNC) , Halmashauri ya  Manispaa ya Kinondoni na VASTech.

Tunatoa pia shukrani za pekee kwa Madaktari na wauguzi wote wa hospitali za Apollo New Delhi; Ruby Hall Clinic na Inamdar za Pune; Shree Hindu Mandal, Lugalo na Regency Medical Centre;

Hatutaweza kuwataja wote kwa majina, lakini tunaomba wote mpokee shukrani zetu za dhati kwa upendo wenu kwa familia hii.


Misa ya Shukrani itafanyika siku ya Jumapili tarehe 06 Septemba 2015  katika Kanisa Katoliki la Mt. Nicolaus, Kunduchi Mtongani  saa 3:00 asubuhi.  Familia inawakaribisha wote siku hiyo kanisani na baadae saa 6:00 kwenye chakula cha mchana nyumbani kwa Kanali Mushumbusi, Kunduchi Beach.



Mungu Ailaze Roho ya Bi. Candida Mahala Pema Peponi. 
Apumzike Kwa Amani.
 AMINA

DJ NATURE WA MAGIC FM AFARIKI DUNIA

0
0
Uongozi wa Africa Media Group Ltd kupitia Radio ya Magic Fm unasikitishwa kutangaza kifo cha aliyekuwa mfanyakazi mwenzao upande wa Radio,Geophrey Herry (pichani enzi za uhai wake), al-maarufu kama Dj Nature,  kilichotokea siku ya Jumatatu ya tarehe  31/08/2015  mjini Songea.

Habari ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki 
na majirani popote pale walipo.
Mazishi yatafanyika kesho Songea.

Magic Fm inasikitika sana kwa kupotelewa na jembe, 
lakini hatuna budi kumshukuru Mungu kwa kila jambo.

Mungu ametoa, na Mungu ametwaa. 
jina la Bwana na lihimidiwe.
Amen.

MAGUFULI AFUNGA KAZI MKOANI MTWARA, AAHIDI KUSHUSHA BEI YA VIFAA VYA UJENZI

0
0
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli,akiwahutubia wananchi wa mji wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza kwenye mkutano wa kampeni unaoendelea jioni hii katika uwanja wa Mashujaa. 

Dkt John Magufuli amesema kuwa iwapo atachaguliwa kuwa Rais katika uchaguzi mkuu mwaka huu ,Serikali yake itashusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa bati na saruji,amesema kuwa serikali yake inataka kurahisisha maisha ya watanzania wote na hivyo atapunguza bei ya saruji na bati na hilo litafanikiwa kwa kupunguza ushuru wa vifaa hivyo. 

"Serikali ya Magufuli nataka iwe ya kurahisisha maisha ya wananchi wake.Moja ya mambo ambayo ninedhamiria kuyafanya ni kupunguza bei ya bati na saruji.Nataka kuona watu wanajenga nyumba nzuri na za kisasa, hivyo lazima tushushe bei ya vifaa vya ujenzi,alisema Dk.Magufuli.

Alisema anatambua kiu ya watanzania ni kutaka mabadiliko ya maendeleo na kwamba Serikali yake itasimamia kuleta maendeleo ya wananchi na kazi hiyo anaiweza na ndio maana anaomba urais. " Ndugu zangu watanzania serikali ya Magufuli inakuja kuendelea pale ambapo awamu nyingine zimeishia.Tumetoka mbali ,tupo mbali na tunakwenda mbali.Nataka tuwe na maendeleo makubwa na hilo serikali yangu ndio kazi itakayofanya,"alisema Dk.Magufuli huku wananchu wakimshangilia kwa mayowe.

Dk Magufuli tayari hadi sasa amefanya mikutano ya kampeni katika mikoa 6 ya Katavi, Rukwa, Mbeya, Njombe, Ruvuma na Mtwara. ambapo akishinda uchaguzi ameahidi mambo mbalimbali kama vile Eimu ya bure kutoka darasa la kwanza hadi kidato cha nne, kujenga reli kutoka Mtwara hadi Mbamba Bay mkoani Ruvuma, kushusha bei ya vifaa vya ujenzi na kutoa sh. mil. 50 kwa kila kijiji za kuwakopesha wanawake na vijana kuendeleza miradi na biashara zao kwa lengo la kuwaletea maendeleo

  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli,akiwahutubia wananchi wa mji wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza kwenye mkutano wa kampeni unaoendelea jioni hii katika uwanja wa Mashujaa. 

Dk Magufuli tayari hadi sasa amefanya mikutano ya kampeni katika mikoa 6 ya Katavi, Rukwa, Mbeya, Njombe, Ruvuma na Mtwara. ambapo aakishinda uchaguzi ameahidi mambo mbalimbali kama vile ile ya bure kutoka darasa la kwanza hadi kidato cha nne, kujenga reli kutoka Mtwara hadi Mbamba Bay mkoani Ruvuma, kushusha bei ya vifaa vya ujenzi na kutoa sh. mil. 50 kwa kila kijiji za kuwakopesha wanawake na vijana kuendeleza miradi na biashara zao kwa lengo la kuwaletea maendeleo 
Wakazi wa mji wa Mtwara wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM,unaofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa CCM,wakimsikiliza mgombea Urais wa chama hicho Dkt John Pombe Magufuli.

 Dk Magufuli akizungumza na mtoto Riziki Faraji na pia alimpa kiasi kadhaa  cha fedha kwa ajili ya kununulia sare ya shule alipomuona wakati msafara wake ulipozuiwa na wananchi katika Kijiji cha Kitama A, mkoani Mtwara


  Dk Magufuli akimnadi Mgombea Ubunge Jimbo la Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Kata ya Ziwani Mtwara Vijijini

 Mgombea Ubunge wa jimbo la Mtwara mjini,Murji Hasnein Mohamed akiwasalimia maelfu ya wananchi wa mji wa Mtwara waliofurika kwenye uwanja wa Mashujaa katika mkutano wa kampeni za CCM,jioni ya leo ambapo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli aliwahutubia wananchi hao .
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akijiachia jukwaani pamoja na wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara,ambapo Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao waliofurika kwa wingi.
  Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akijiachia jukwaani pamoja na wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara,ambapo Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao waliofurika kwa wingi.

Mafuriko ya Mama Samia Suluhu Yawavuna Vigogo Chadema Dodoma

0
0
Baadhi ya wanaCCM na wapenzi wa chama hicho wakiwa wamefurika katika mkutano wa hadhara ulofanyika Viwanja vya Chang'ombe mjini Dodoma.Baadhi ya wanaCCM na wapenzi wa chama hicho wakiwa wamefurika katika mkutano wa hadhara ulofanyika Viwanja vya Chang'ombe mjini Dodoma.
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu akiwasili na kuwapungia mkono wananchi katika viwanja vya jangani.Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu akiwasili na kuwapungia mkono wananchi katika viwanja vya jangani.Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu akipokea kadi kutoka kwa  aliyekuwa mgombea wa udiwani wa Chadema Kata ya Mlowa Barabarani baada ya kujiunga na chama hicho.Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu akipokea kadi kutoka kwa aliyekuwa mgombea wa udiwani wa Chadema Kata ya Mlowa Barabarani baada ya kujiunga na chama hicho.
Bi. Samia Suluhu kulia akimtambulisha mgombea ubunge wa jimbo la Mtera, Livingstone Lusinde jimboni humo.Bi. Samia Suluhu kulia akimtambulisha mgombea ubunge wa jimbo la Mtera, Livingstone Lusinde jimMgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu (kulia) akiwatambulisha mgombea ubunge Jimbo la Kibakwe, George Simbachawene (katikati). Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu (kulia) akiwatambulisha mgombea ubunge Jimbo la Kibakwe, George Simbachawene (katikati).boni humo. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA






MABUNGE YATAKIWA KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WA MALENGO MAPYA YA MAENDELEO ENDELEVU

0
0
Na Mwandishi Maalum , New York 
Maspika wa Mabunge kutoka mataifa mbalimbali duniani, wamemaliza mkutano wao wa Nne kwa kupitisha tamko ambalo pamoja na mambo mengine, linayataka Mabunge kuhakikisha yanasimamia na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa Malengo na Ajenda Mpya za Maendeleo Endelevu ( Ajenda 2030). 
Akihitimisha mkutano huo wa Maspika ambao hufanyika kila baada ya Miaka mitano, Rais wa Chama cha Kimataifa cha Mabunge ( IPU) Saber Chowdhur amesema, Maspika na wabunge wanawajibu wa kuhakikisha Serikali zao zinatenga bajeti za kutosha ambazo kwayo zitahakikisha utekelezaji wa malengo na ajenda mpya ya maendeleo endelevu. 
Ajenda 2030 inayochukua nafasi ya Malengo ya Maendeleo ya Millenia ( MDGs) itapitishwa rasmi na Viongozi Wakuu wa Nchi na Serikali katika mkutano wao wa kihistoria na wa Kilele utakaofanyika kuanzia tarehe 25 hadi 26 mwezi huu wa Septemba. 
Miongoni mwa mambo ambayo mabunge yanatakiwa kusimamia ili kuhakikisha kwamba malengo na ajenda hizo mpya yanatekelezwa kikamilifu pasipo kumwacha yeyote nyuma ni pamoja na kuhakikisha uboreshwaji wa vyanzo vya mapato ya ndani pamoja na kuziba mianya ya ukwepaji wa kodi. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Ann Makinda ndiye aliyeongeza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huu muhimu na wa aina yake na ambao umefanyika ikiwa ni wiki chake kabla ya Wakuu wa Nchi na Serikali kukutana kwa mikutano muhimu na inayotarajiwa kuzungumzia mstakabali wa maendelele na ustawi wa watu na utunzaji wa mazingira. 
“ Maspika wa Mabunge ambao tumekutana hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, tumepokea kwa kauli moja, Malengo na Ajenda mpya za Maendeleo Endelevu ambayo wakuu wa nchi na serikali watapisha wiki chache zijazo. 
"Kama wawakilishi wa wananchi na wasimamizi wa Mabunge tunawajibu wa kuhakikisha kwamba, tunakuwa mstari wa mbele katika siyo tu, kuhakikisha tunapitisha mipango na sera za utekelezaji wa malengo na ajenda hii mpya, bali pia kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuziba mianya ya ukwepaji kodi” amesema Rais wa IPU Bwa. Chowdhury. 
 Maspika wa Mabunge kutoka mataifa mbalimbali duniani wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Maspika hao  wamepitisha tamko  ambalo  linatambua na kupokea malengo na ajenda mpya za  maendeleo endelevu, na kuyataka mabunge kuhakikisha utekelezaji  malengo hayo yanayochukua nafasi  ya MDGs. Mhe Ann Makinda ni wa tatu kutoka kushoto mstari wa mbele.

Mhe. Spika  akiwa na  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania Katika Umoja wa Mataifa, Balozi  Tuvako Manongi,  wakati alipofika  katika Ofisi za Uwakilishi na kisha kuzungumza na  Maafisa. Mhe. Spika  ameeleza kuwa  moja ya mambo atakayoshauri ni pamoja na  kutaka  Maafisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  kuwa na fursa ya  kuja katika Umoja wa Mataifa kujifunza na kujijengea uwezo kuhusu   mijadala ya kimataifa inavyofanyika na kufikiwa uamuzi katika Umoja wa Mataifa. Akasema anaamini kabisa kwamba kuna mambo ambayo wanaweza kujifunza.

WATOTO WATATU WAFUTWA MACHOZI NA BIMA YA ELIMU YA BAYPORT BIHARAMULO

0
0
Na Mwandishi Wetu, Kagera 
TAASISI ya kifedha ya Bayport Financial Services inayojihusisha na mambo ya mikopo, jana imewakabidhi hundi ya Sh Milioni tatu watoto watatu wilayani Biharamulo, mkoani Kagera, kwa ajili ya kunufaika na huduma ya Bima ya Elimu iliyoachwa na mzee wao Karume Ochieng aliyefariki Dunia, huku akiwa amejiunga na huduma ya bima kwa ajili ya watoto wake hao.
Mratibu Mauzo wa Bima ya Elimu wa Taasisi ya Kifedha inayotoa Mikopo(Bayport Financial Services, Ruth Bura akikabidhi mfano wa hundi kwa familia ya marehemu Karume ambaye alikuwa amejiunga na bima hiyo katika shule ya msingi Nyamuhuna iliyopo wilayani Biharamulo mkoani Kagera, kushoto ni Meneja Mauzo wa Bayport Kanda ya Ziwa, Lugano Kasambala. Taasisi hiyo imeanzisha bima ya elimu ili kusaidia kiasi cha ada kwa watu wa karibu walioainishwa na mteja wao endapo atakumbwa na umauti.

Watoto hao ambao wamepewa hundi hiyo itakayowawezesha kila mwaka katika vipindi vya miaka mitatu mfululizo kupewa Sh Milioni moja kwa ajili ya kuwalipia ada katika shule wanazosoma ni pamoja na Athieno Karume, Chacha Karume na Aaptalius Karume.
Makabidhiano ya hundi kwa familia ya marehemu Karume yakiendelea wilayani Biharamulo, mkoani Kagera.

Akizungumza katika makabidhiano ya hundi hiyo kwa watoto hao, Mratibu wa Bima ya Elimu ya Bayport Financial Services, Ruth Bura, alisema kwamba kukabidhi hundi hiyo kutawafanya watoto hao wasome kwa raha, baada ya kuwekewa bima hiyo na marehemu baba yao kutokana na mapenzi mema na vijana hao wanaoendelea na masomo.


MKUTANO WA TAKWIMU HURIA KANDA YA AFRIKA (AFRICA OPEN DATA CONFERENCE) ______________________________________

0
0
       Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia itakuwa mwenyeji wa Mkutano wa Takwimu Huria Kanda ya Afrika. 
Mkutano huo utakaofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete utafanyika tarehe 4 – 5 Septemba, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.  Kauli Mbiu ni Tumia Takwimu Huria  Kuendeleza Afrika” (Developing Africa Through Open Data).


Washiriki takriban 400 kutoka Serikalini, Asasi za Kiraia, Sekta Binafsi, Taasisi za Elimu ya Juu na Washirika wa Maendeleo kutoka ndani na nje ya Nchi wanatarajiwa kushiriki.  Miongoni mwa washiriki kutoka Serikalini ni pamoja na Wakurugenzi kutoka Idara za Sera na Mipango, Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA na Maofisa Takwimu Waandamizi wa Wizara zote.


Mkutano wa Takwimu Huria kwa Kanda ya Afrika ni wa kwanza wa aina yake  Barani Afrika Tanzania ikiwa nchi ya kwanza kuwa mwenyeji.  Heshima hiyo imetokana na Tanzania kujiunga na Mpango wa Uendeshaji wa Shughuli za Serikali kwa Uwazi (Open Government Partnership – OGP) unaolenga kuifanya Serikali kuwa wazi zaidi na hivyo kuleta uadilifu na uwajibikaji katika kuwahudumia Wananchi.  Katika utekelezaji wa Mpango wa OGP, Tanzania iliweka kipaumbele katika kuanzisha Tovuti ya Takwimu Huria itakayoweka wazi takwimu mbalimbali za Serikali na Taasisi zake.


Madhumuni ya Mkutano ni kujadiliana kuhusu mfumo wa Takwimu Huria na jinsi utakavyoleta maendeleo hususan kwa nchi za Afrika. 


Mkutano utawawezesha wadau kujadiliana na kubadilishana uzoefu kuhusu mfumo wa Takwimu Huria na kuona jinsi gani Sera za nchi zenye mfumo huo zinavyofanya kazi na kusimamia viwango vya upatikanaji wa Takwimu Huria.


Aidha, Mkutano huo utaihusisha sekta binafsi na wadau wengine katika matumizi ya Takwimu Huria katika kuleta maendeleo ya kasi zaidi Barani Afrika.


Washiriki watajadili jinsi ya kukuza na kuimarisha matumizi ya Mfumo wa Takwimu Huria katika kutoa huduma kwa wananchi hasa katika sekta ya Huduma za Jamii za elimu, afya, maji na kilimo.


Tunaomba ushirikiano wenu ili Mkutano huu ufanyike na kukamilika kwa ufanisi.



Imetolewa na Ofisi ya Rais, Ikulu                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                        





RAIS KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA TAIFA LA BIASHARA TANZANIA (TNBC) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

0
0

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi muda mfupi kabla ya kufungua na kuendesha mkutano wa nane wa Baraza la Taifa la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
 Rais Kikwete akiongoza mkutano wa nane wa Baraza la Taifa la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka, Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi 

  Rais Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na secretariate ya TNBC  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na watumishi wa  TNBC  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka, PICHA ZOTE NA IKULU
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA


Go Taifa Stars! Go!

LOWASSA ATUA MPANDA KWA CHOPA, APATA MAPOKEZI MAKUBWA

0
0
Chopa iliyowabeba Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa pamoja na Mwenyekiti wake, Mh. Freeman Mbowe, ikitua kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kashaulili, Mpanda Mkoani Katavi leo Septemba 3, 2015.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa pamoja na Mwenyekiti wake, Mh. Freeman Mbowe, wakiwasili kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kashaulili, Mpanda Mkoani Katavi leo Septemba 3, 2015, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwapingia wananchi wa Mpanda, Mkoani Katavi.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe, akihutubia kwenye Mkutano huo wa Kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kashaulili, Mpanda Mkoani Katavi leo Septemba 3, 2015.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akizungumza jambo na Mgombea wa nafasi ya Udiwani katika Kata ya Mtapenda, Bi. Pauline Pesnacy, mara baada ya kumnadi kwa wananchi wa Mpanda, waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kashaulili, Mpanda Mkoani Katavi leo Septemba 3, 2015, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni na kunadi sera zake.

KUONA PICHA ZAIDI

BOFYA HAPA AU BOFYA HAPA

DIASPORA YA MONTGOMERY COUNTY YAMUAGA BALOZI AMINA SALUM ALI

0
0
 Bwn. Daniel Korona akisherehesha hafla fupi ya kumuaga Balozi wa Umoja wa Afrika aliyemaliza muda wake Mhe. Amina Salum Ali iliyoandaliwa na Jumuiya ya Diaspora kutoka Afrika wanaoishi Montgomery county iliyofanyika siku ya Jumatano Sept 2, 2015 Silver Spring, Maryland.
Kulia ni mwongozaji maswali Bi. Soffie Ceesay ambaye ni mwanachama mwanzilishi wa Montgomery County's African Affairs Advisory Group na African Immigrant Caucus akimuuliza Mhe. Amina Salum Ali maswali mbalimbali likiwemo nini anajivunia kwenye uongozi wake kama Balozi wa kwanza wa Umoja wa Afrika nchini Marekani. Balozi Amina Salum Ali alieleza ni ushirikiano wa nyanja mbalimbali mabalozi nchi za Afrika zimenufaika na kupata mafanikio na uhusiano wa AU na Marekani kwa kuwezesha kupata Balozi wao nchini Marekani na kikubwa kabisa katika historia ya AU na yeye  kama Balozi kuwezesha Rais Barack Obama kwa mara ya kwanza katika historia kama Rais wa Marekani kuhutubia Umoja huo.
Isiah Leggett ambaye ni Montgomery County Executive akimtunukia cheti Mhe. Balozi Amina Salum Ali

KWA PICHA ZAIDI OFYA HAPA.

WAANDISHI WA HABARI WAELIMISHWA JUU YA SHERIA NA MAKOSA YA MITANDAO

0
0
 Afisa Sheria wa Wizara ya Mawasiliano, Eunice Masigati akizunzungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na sheria za makosa ya mitandao, ambapo sheria hii itatumia Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar wakati wa Tamasha la mtandao wa wanawake na katiba na uchumi linaloendela TGNP jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mawasiliano wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Melkizdeck Karol akiwaelimisha waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya usalama wa sheria za mitandao wakati wa Tamasha la mtandao wa wanawake na katiba na uchumi linaloendela TGNP jijini Dar es Salaam. Pembeni ni Afisa Sheria wa Wizara ya Mawasiliano, Eunice Masigati.
 Afisa Sheria wa Wizara ya Mawasiliano, Eunice Masigati akimsikiliza waandishi wa habari wakichangia mada kuhusiana na sheria za makosa ya mitandao wakati wa Tamasha la mtandao wa wanawake na katiba na uchumi linaloendela TGNP jijini Dar es Salaam. 

TAMASHA LA MTANDAO WA WANAWAKE LAWAELIMISHA WANANCHI NAMNA YA KUIMARISHA AFYA YA AKILI

0
0
 Mwenyekiti wa Basicneed Foundashon Tanzania, Prof. Joseph Mbatia akizungumza juu ya kula vyakula vyenye lishe bora na kunywa maji ya kutosha kufanya mazoezi ya viungo angalau mara tatu kwa wiki, (kujali afya kila siku kujitambua na epuka vitu vinavyoathiri afya yako) ikiwa ni siku ya pili ya muendelezo wa Tamasha la  mtandao wa wanawake na katiba na uchumi linaloendelea kufanyika ndani ya TGNP jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Basicneed Foundashon Tanzania, Prof.Joseph Mbatia akifafanua jambo wakati wa Tamasha la  mtandao wa wanawake na katiba na uchumi linaloendelea kufanyika ndani ya TGNP jijini Dar es Salaam.
Wananchi wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Basicneed Foundashon Tanzania, Prof.Joseph Mbatia akifafanua jambo  ikiwa ni siku ya pili ya muendelezo wa Tamasha la mtandao wa wanawake na katiba na uchumi linaloendelea kufanyika ndani ya TGNP jijini Dar es Salaam.
 (Picha na Emmanue Massaka)
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Bw. Nasifu Ahmed Lema yu taabani Afrika kusini, anahitaji msaada wa ndugu zake Tanzania

0
0
BWANA NASIFU AHMED LEMA


MTAJWA HAPO JUU NI RAIA WA TANZANIA AMBAYE KWA SASA YUKO AFRIKA KUSINI. BW. LEMA ANA HALI MBAYA KIMAISHA. ANADAI KWAMA ALIZALIWA HIMO MAKUYUNI KIJIJI CHA LOTIMA MKOANI KILIMANJARO MWAKA 1968. WAZAZI WAKE NI AHMED LEMA NA ANNA MFINANGA AMBAO KWA SASA WOTE NI MAREHEMU.


UBALOZI WA TANZANIA AFRIKA KUSINI UNAOMBA KAMA KUNA YOYOTE AMBAYE ANAWAFAHAMU NDUGU ZAKE WAPATIWE TAARIFA HII.
WANAWEZA KUWASILIANA NA UBALOZI KITENGO CHA UHAMIAJI KWA NAMBA ZIFUATAZO: +27 12 342 4371 AU +27 12 342 4393

EAGER WAKAA KUJADILI JINSI YA UNDELEZAJI WA NISHATI YA JOTOARDHI

0
0
 Naibu Kiongozi wa Timu ya Shirika linanoshughulikia masuala ya Jotoardhi Afrika Mashariki (EAGER) Bw. John Heath akiwaelimisha wadau mbalimbali wa Kampuni inashughulikia Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Wizara ya Nishati na Madini pamoja na wadau wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) kuhusu Mifumo mbalimbali ya biashara kwa soko la Jotoardhi. Warsha inayofanyika tarehe 2-4 Septemba, 2015 jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wadau mbalimbali kutoka Kampuni ya Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Wizara ya Nishati na Madini pamoja na TANESCO wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa mada kuhusu Mifumo mbalimbali ya biashara kwa soko la Jotoardhi, warsha iliyofanyika siku ya tarehe 2 Septemba, 2015 jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau mbalimbali kutoka Kampuni ya Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Timu ya Shirika linanoshughulikia masuala ya Jotoardhi Afrika Mashariki (EAGER), Wizara ya Nishati na Madini pamoja na TANESCO wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya warsha iliyofanyika siku ya tarehe 2 Septemba, 2015 jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWEGA-MAELEZO.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

HAJA YA HOJA: NI LINI TAJIRI AKAPENDA MASKINI AKAWA TAJIRI KAMA YEYE

0
0
Ni jambo lilo wazi kuwa watu wote hawawezi kuwa sawa, hivyo watu wote hawawezi  kuwa matajiri. Hivyo kulipo na matajiri  wakubwa na  maskini nao ni wengi. Kwa sababu tajiri na maskini wanategemeana.  Utajiri hauwezi kuwepo bila kuwepo umaskini.Kwa mantiki hiyo ili tajiri awepo maskini lazima awepo na   maskini akiwepo  na tajiri atakuwepo, wote wanategemeana. Kanuni hii ni kwa watu na hata nchi.
Ni kweli matajiri wanachukia umaskini  na maskini wenyewe wanatamani utajiri. Hivyo si rahisi kwa tajiri kupenda  maskini awe tajiri.Kwani maskini akiwa tajiri  utajiri wake unakuwa mashakani. 
Hivi karibuni nimesikia kauli za  wagombea uongozi katika taifa letu wakisema wanauchukia umaskini, kitu ambacho ni kizuri, na kwamba wanatamani watu wote wawe matajiri. 
Hapo ndipo nilipopata ukakasi, je hawa wagombea wanalizungumzia jambo hili kwa dhati, wanaelewa kweli miiko na taratibu ya vitu mbalimbali kutegemeana katika maisha? Lakini nikijaribu kuwaangalia wao binafsi, je  ni matajiri au maskini. 
Kama maskini wanaweza kulizungumza hili kwa dhati  na wangependa na wao wawe matajiri. Lakini kama wao ni matajiri, basi hapo tunaogepewa kwani hakuna tajiri anayependa maskini awe tajiri kama yeye. Watanzania tutafakari.
R. Kahwa

AZAM TV HABARI - SHERIA MTANDAO 2015

Casting Call!

0
0


Je, wewe ni kijana wa kiTanzania unaejua kuigiza?

Tunatafuta waigizaji wanaojiamini kwa ajili ya Tamthilia mpya Tanzania.

Tunatafuta wanawake & Wanaume umri kati ya miaka 20-40.

Fika SLIPWAY STUDIO Dar es salaam.

Jumamosi Tarehe 5 September, 2015
Saa sita mchana.
Uje na kitambulisho.
Kwa maelezo zaidi, piga 0754343969.
Viewing all 109609 articles
Browse latest View live




Latest Images