Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109610 articles
Browse latest View live

BUNGE LA VIJANA LAENDELEA BUNGENI DODOMA

0
0
BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia mradi wake wa kuwajengea Uwezo Wabunge na Watumishi (LSP) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP kwa mara ya Pili mwaka huu limeratibu Bunge la Vijana kwa kushirikisha Wanafunzi zaidi ya 100 kutoka Taasisi za Elimu ya Juu hapa Nchi ambao ni viongozi katika Serikali zao. Bunge hilo ambalo limeanza Jumamosi tarehe 15 Julai, 2015 na linatarajiwa kumalizika tarehe 19 Julai 2015.

 Spika wa Bunge la Vijana kwa mwaka 2015 Baraka Thomas (UDSM) akiongoza vikao vya Bunge
 Waziri Mkuu katika Bunge la Vijana kwa mwaka 2015 Alexandra Wasonga (ARDHI) akijibu Maswali ya papo kwa papo Bunge wakati wa Kipindi cha Masuali kwa Waziri Mkuu.
 Mwanasheria Mkuu katika Bunge la Vijana kwa mwaka 2015 Gama Zulu Leonidas (SAUT) akiwasilisha Muswada wa Serikali wa Kuanzisha sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa Mwaka 2015 Bungeni jana. 
 Wajumbe wa Bunge la Vijana wakishiriki Vikao vya Bunge hilo Mjini Dodoma.
Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge.


RADIO CALL ZA KISASA ZAINGIA NCHINI

0
0
Na Mwandishi Wetu,Globu ya Jamii
MAJANGA mbalilmbali nchini ambayo yamekuwa  yakitokea  na kushindwa kupata msaada ni kutokana na kuwa vifaa duni vya mawasiliano ya radio.
Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam wa Maonyesho na Mkutano wa Mawasiliano ya Radio za Kisasa ‘Radio Call’ 

Naibu Mkurugenzi wa Masafa wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Libena Denis amesema kuwa kazi kubwa na kuona mawasiliano ya radio yanakua  na hivyo TCRA lazima isimamie.

Denis amesema kuwa kampuni ya Airsys  kuleta mawasiliano ya radio za kisasa na kuondokana na radio za kizamani ambazo kwa mabadiliko ya kitekonojia haziwezi kuhimili.
Aidha amesema  kuwa nchi za ulaya zimekuwa zikitumia mawasiliano hayo hivyo kuingia nchini itasaidia katika mawasiliano ya radio.

Amesema Meneja Mkuu wa  Airsys  Communication Technology Ltd,Sanctus Mtsimbe amesema mawasiliano ya matumizi ya radio yatakuwa nchini na kutoa urahisi wa upatikanaji wa huduma na mafunzo kwa wateja.

Amesema Tanzania imepewa kuwa kanda ya Afrika Mashariki  kwa kuwa na huduma ya Radio Call hivyo watumiaji watapata msaada na kuondokana na usumbufu wa kuagiza radio nje.
 Balozi wa Uingereza,Dianna Melrose akizungumza wakati wa kuzindua mkutano wa kampuni ya Airsy katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo.
 Afisa mtendaji mkuu,Hans Beckers akionyesha redio call ambazo zinatengenezwa na kampuni ya Airsy ambazo zitakuwa zikisaidia katika ulinzi katika nchi mbalimbali ambazo zitakuwa zikisambazwa hapa nchini alionyesha redio hizo katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya serena jijini Dar es Salaam leo.
 Naibu Mkurugenzi wa Masafa wa Mamlaka ya mawasiliano (TCRA), Libena Denis akizungumza katika mkutano wa kuwaonyesha watanzania jinsi redio hizo zinavyo fanya kazi katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam leo.
Msemaji wa kampuni ya Airsys, Sanctus Mtsimbe akizungumza na waandishi wa habari leo katika hoteli ya serena jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa mtendaji mkuu,Hans Beckers wa kampuni ya Airsy.

 KWAPICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

AIRTEL YATOA MIKOPO KWA MAWAKALA WA AIRTEL MONEY

0
0
 Afisa Mkuu wa Biashara wa Airtel Tanzania, Arindam Chakrabarty
(kushoto), Kamishna Msaidizi wa Wizara ya Fedha, Ridhiwan Masudi
(kulia) na Mkurugenzi wa Afb Tanzania, Wayne Stocks  wakionyesha bango
kama ishara ya uzinduzi wa huduma mpya ya mikopo kwa mawakala wa
Airtel Money ijulikanayo kama ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, katika hafla
iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano Mallya
akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya mikopo kwa mawakala wa Airtel Money ijulikanayo kama ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kutoka (kulia) ni
Mkurugenzi wa Afb Tanzania, Wayne Stocks, Kamishna Msaidizi wa Wizara
ya Fedha, Ridhiwan Masudi na Afisa Mkuu wa Biashara wa Airtel
Tanzania, Arindam Chakrabarty.
3) Afisa Mkuu wa Biashara wa Airtel Tanzania, Arindam Chakrabarty
akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya mikopo kwa mawakala wa Airtel Money ijulikanayo kama ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kutoka (kulia) ni
Mkurugenzi wa Afb Tanzania, Wayne Stocks na Kamishna Msaidizi wa
Wizara ya Fedha, Ridhiwan Masudi.
Baadhi ya mawakala wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya
uzinduzi wa huduma ya Timiza Mkopo kwa wakala, huduma itakayowawezesha
kupata mikopo isiyo ya dhamana kupitia huduma ya Airtel Money.

Airtel yatoa Mikopo kwa Mawakala wa Airtel Money
*          Mikopo isiyo na dhamana
*          Zaidi ya mawakala 20,000 kunufaika
 KAMPUNI ya simu za mkononi
ya Airtel kwa kushirikiana na Afb Tanzania imezindua huduma ya mikopo
kwa wateja wa Airtel Money ijulikanayo kama "Timiza Mkopo kwa Wakala",
 itakayowawezesha  mawakala wa Airtel Money nchini nzima kupata mikopo
isiyo na dhamana ya kuanzia shilingi 50,000 hadi 500,000.

Akiongea wakati wa uzinduzi, Afisa Mkuu wa Biashara Airtel , Bwana
Arindam Chakrabary alisema" Airtel inatambua kuwa mawakala wetu
wanatafuta fursa ya kukuza biashara zao na kuongeza mitaji. Na leo
tunayo furaha kuzindua huduma ya kwanza Tanzania na Afrika "Timiza
Mkopo kwa Wakala" mikopo isiyo na masharti mahususi kwa mawakala wetu.

Huduma hii ya mikopo kwa mawakala  itawanufaisha mawakala zaidi ya
20,000 nchi nzima,  na tunaamini mikopo hii itasaidia kukuza biashara
za mawakala wetu , kuwaongezea faida zaidi na hatimaye kuboresha
upatikanaji wa huduma za kifedha"

Chakrabarty aliongeza kwa kusema" Mwaka jana tulizindua huduma ya
Timiza kwa wateja wetu nchini nzima,  ambayo kwa sasa ina zaidi ya
wateja milioni 7 wanaoweza kupata mikopo ya haraka isiyo na masharti
kwa urahisi , mikopo ambayo inawasaidia kutatua changamoto za kijamii
na kiuchumi.

 "Timiza Mkopo kwa Wakala" itatoa kwa mawakala wetu wa
Airtel Money uhuru wa kupata mikopo ya  haraka isiyo na masharti bila
kupitia njia ndefu zakupata mikopo katika mfumo wa kawaida. Tunaamini
huduma hii inatasaidia na kuwawezesha mawakala wa Airtel Money kupata
fedha za kutatua mahitaji yao ya muda mfupi na mrefu wakati wote.

AliongezaNaye Msimamizi  Mkuu Afb Tanzania, Rwebu Mutahaba, amesema  " Mawakalawanapata mikopo kulingana na matumizi yao ya simu ndo mana tumeweza kuwaamini na  kuwapatia mikopo isiyo na masharti.  Lengo kubwa ni kuwapatia watu fulsa ya kupata huduma ya kisasa na kibunifu ambayoa haijawahi kutolewa kabla. 

 Afb Tanzania tunajivunia ushirika huu na Airtel ambao umetuwezesha kutoa suluhisho kwa wateja wa Airtel , mikopo kwa mawakala ni moja ya huduma nyingi za kibunifu tulizonazo na tunazopanga kuzindua katika mienzi ijayo nchini Tanzania".

Timiza Mkopo kwa Wakala" ina viwango na riba tofauti zenye marejesho
ya ndani ya siku saba, wiki mbili au mwezi mmoja. 

Kiasi cha kukopa
kitategemeana na matumizi simu ya wakala na jinsi anavyorudisha mkopo
wake kwa wakati. Mteja atakapo rudisha mkopo wake ndani ya siku 7,14
au 28 mojakwamoja atawezeshwa kupata mkopo mwingine.

 Inachukua dakika moja kwa mteja kujaza fomu ya kuomba mkopo kupitia simu yake  na kisha mara baada ya kujaza pesa zinawekwa kwenye akaunti yake ya Airtel Money hapohapo".

alisema Mutahaba 
Kwa upande wake, kwa niaba ya Katibu Mkuu, Kamishna Msaidizi Wizara ya 
Fedha, Bwana Ridhiwan Masudi alisema"  sisi kama Serikali tumefurahishwa na hatua walioichukua Airtel katika kuboresha mfumo rasmi wa kifedha kupitia huduma ya Airtel Money.  Tunafurahi  kuona huduma ya Airtel Money  ikikuwa kwa haraka na kuwafaidisha watanzania wakawaida hususani wanaoishi katika maeneo ya pembe zoni mwa nchi.

Napenda kuchukua fulsa hii kuwaomba Airtel waendelee kuleta bidhaa na
huduma za kibunifu ili kuweza kuipatia jamii huduma bora za
mawasiliano na kukuza zaidi huduma za kifedha."

Mawakala wa Airtel Money wanaweza kujipatia mikopo kwa kupiga
*150*60#, na kuchagua 4  ili kupata orodha ya mikopo kwa wakala , na
kisha kuingiza namba ya simu na namba ya siri  na baada ya hapo

wataunganishwa kwenye orodha ya mikopo ya Timiza.

WAFANYAKAZI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI WAHAMASISHWA KUPIMA AFYA

0
0
 Daktari Hafidh Ameir toka Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) akitoa elimu juu ya umuhimu wa kupima afya kwa wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Semina iliyofanyika Makao Makuu ya Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
   Mfanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marcelina Henry akichukuliwa vipimo vya shinikizo la damu na Muuguzi toka Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam, Asma Msimbe wakati wa zoezi la kupima afya kwa wafanyakazi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
   Bwana Ponela John wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akichukuliwa vipimo vya urefu na Bwana John Joseph wa Timu ya Wataalamu waliofika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa ajili ya kupima afya za wafanyakazi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Mfanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bi. Radhia Said akichukuliwa vipimo vya urefu na Bwana John Joseph wa Timu ya Wataalamu waliofika Wizara hapo kwa ajili ya kuendesha zoezi la kupima afya za wafanyakazi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam. 

MONICA MBEGA- DR MAGUFULI NA MWAKALEBELA NAWAUNGA MKONO KWA ASILIMIA 100

0
0
Aliyekuwa  mgombea wa nafasi ya Urais Monica Mbega jukwaani  akimwombea  kura  mgombea  urais wa  CCM na mgombea  ubunge jimbo la Iringa mjini Frederick Mwakalebela (aliyekaa katikati kulia) leo  baada ya  mwakalebela  kuchukua  fomu ya ubunge.
Monica  Mbega  akimpongeza  Mwakalebela
Monica  Mbega  akijiandaa kumsalimia Kiponza.
Mwenyekiti wa CCM Iringa mjini Bw  Abeid Kiponza  (kulia) akimtambulisha mgombea  ubunge jimbo la Iringa mjini Frederick Mwakalebela  leo.

Mgombea udiwani wa kata ya Mtwivila Bw Jose Mgongolwa (kulia) akitambulishwa na Mwakalebela.
Mgombea  udiwani wa kata ya Mkimbizi Bi Farida Mpogole  akitambulishwa na Mwakalebela
Mwakalebela  akimtambulisha mgombea udiwani wa kata ya Gangilonga Bw Nicholina Lulandala
Mwakalebela  akimtambulisha mgombea udiwani wa Kwakilosa Bw Himid Mbata (kulia)
Mwenyekiti  wa CCM wilaya ya  Iringa mjini Bw Abeid  Kiponza  akimtambulisha  mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia  CCM Bw  Frederick Mwakalebela (kushoto)

MUZIKI MNENE BANGO BOKO

0
0
Jimmy Jiam akiwa na washindi wa Muzuki Mnene Bango  eneo la Kisarawe. Washindi hao walitokana na kuwenga bango la EFM katika sehemu zao mbalimbali  na kama wanavyoonekana tayari wamekabidhiwa zawadi zao.





SERIKALI YAKANUSHA CHADEMA KUTUMIA UWANJA WA TAIFA KUZINDUA KAMPENI ZAKE.

0
0
Na Benedict Liwenga, MAELEZO.
SERIKALI imekanusha taarifa zilizojitokeza kwenye Vyombo vya habari yakiwemo magazeti na mitandao ya kijamii kwamba Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kitafanya mkutano hadhara Uwanja wa Taifa Dar es Salaam tarehe 22 Agosti, 2015.

Akizungumza na vyombo vya habari jana, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene alisema serikali haijatoa ruhusa kwa chama chochote cha siasa kutumia uwanja wa taifa kwa ajili ya shughuli za kisiasa.

Alikiri kwamba ni kweli kwamba CHADEMA waliiandikia Wizara tarehe 12 Agosti, 2015 kutaka kutumia uwanja wa taifa katika uzinduzi wa kampeni lakini ombi lao lilikataliwa kwa maelezo kwamba uwanja ule kwa mazingira ya sasa hauruhusiwi kutumika kwa ajili ya mihadhara ya vyama vya siasa.

“kwa kipindi haturuhusu uwanja wa taifa kutumika kwa mihadhara ya kampeni za vyama vya siasa. Uamuzi huu unalenga kuweka uwanja katika mazingira rafiki ya michezo na kuepuka athari zozote zinazoweza kujitokeza kutokana na mihemuko ya kisiasa” alisema Bwana Mwambene.

Mwambene ameeleza kuwa, Serikali imeamua uwanja huo ubaki kwa ajili ya kufanyia shughuli zake za msingi za kimichezo ili kuepuka mihemuko na athari yoyote inayoweza kujitokeza kutokana na hamasa za kisiasa.

“Ni kweli kwamba tulipata barua ya Chadema kuomba Uwanja kutumika kwa ajili ya mhadhara ya kisiasa wa CHADEMA hasa kuzindua Kampeni zao kwenye Uwanja tayari tumeshawaandikia kuwaarifu kuwa Uwanja ule hauwezi kutumika kwa ajili ya shughuli zozote za kisiasa” alisema Bwana Mwambene.

Alisema vyama vyovyote vitakavyoomba kutumia Uwanja ule kwa shughuli za kisiasa havitaruhusiwa.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) akikanusha kuhusu Chadema kutumia Uwanja wa Taifa kuzindua kampeni zake siku ya tarehe 22 Agosti, 2015 jijini Dar es Salaam. Kanusho hilo lilitolewa katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) uliopo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia taarifa kutoka Serikalini kuhusu Chadema kutumia Uwanja wa Taifa kuzindua kampeni zake siku ya tarehe 22 Agosti, 2015 jijini Dar es Salaam. Kanusho hilo lilitolewa katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) uliopo jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA.

FAINALI ZA SHINDANO LA TMT KUFANYIKA AGOSTI 22 MWAKA HUU

0
0
 Wawezeshaji na Wadhamini wa shindano la Tanzania Movie Talent (TMT),Jaji Mkuu,Loy Sarungi(wa kwanza kutoka kushoto),Jaji katika shindano hilo Single Mtambalike(wa kwanza kutoka kushoto),Meneja Mawasiliano na Masoko wa Proin Promotion,Josephat Lukaza,Meneja Bidhaa wa Paisha,Godfrey Fataki na Meneja Masoko wa ITV,Ernest Dilli wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talent (TMT) litakalofanyika Agosti 22 katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
 Meneja Mawasiliano na Masoko wa proin Promotion,Josephat Lukaza akizungumza na Wanahabari kuhusu Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talent (TMT) litakalofanyika Agosti 22 katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
 Meneja Mradi wa Proin Promotion,Saul Mpock akizungumza juu ya Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talent (TMT) litakalofanyika Agosti 22 katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Jaji katika shindano hilo, Single Mtambalike akizungumza na Wanahabari katika mkutano uliohusu Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talent (TMT) litakalofanyika Agosti 22 katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

KAMATI YA UCHAGUZI DRFA YAELEKEZA UCHAGUZI WA TEFA KUFANYIKA AGOSTI 23 MWAKA HUU

0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI         
KAMATI 
ya uchaguzi DRFA inaelekeza kamati ya uchaguzi ya TEFA kufanya uchaguzi wa viongozi,jumapili tarehe 23/08/2015 katika ukumbi wa JKT kama ilivyopangwa kufanyika hapo awali.
Kamati pia inapenda  kuutarifu umma kuwa mchakato huu una Baraka zote kutoka TFF,hivyo uingiliaji wowote unakwenda kinyume na ibara ya 6(1)ya kanuni za uchaguzi za TFF 2013 na ibara za 52(6) na 56(6)(a) za katiba ya TFF ambazo zinaelekeza kuwa majukumu ya uchaguzi yapo chini ya kamati ya uchaguzi.
Itakumbukwa uchaguzi huo uliokuwa ufanyike jumapili ya tarehe 16,08,2015 uliahirishwa na kamati ya uchaguzi ya Tefa licha ya shirikisho la TFF kuagiza ufanyike,na hivyo mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi DRFA wakili Rashid Saadallah akaitaka kamati hiyo ya TEFA kumuandikia barua kueleza sababu ya kuahirisha uchaguzi huo.
baada ya kupitia sababu hizo,ndipo DRFA ikatoa majibu kwa kuelekeza uchaguzi huo sasa kufanyika jumapili hii.
KOZI YA MAKOCHA LESENI ‘C’ ILIYOANDALIWA NA  DRFA SASA YAIVA,WADAU WAOMBWA KULIPIA  ADA ZAO  MAPEMA.
kozi ya ukocha leseni C inatarajiwa kufanyika kuanza tarehe 28. 08. 2015,katika ukumbi wa TFF Uwanja wa Karume, ambapo washiriki wanakumbushwa kulipia ada zao za ushiriki ambayo ni shilingi  TZS 250,000.
Katika kzoi hiyo inategemewa kuwepo na madarasa mawili ya wanafunzi 30 kila darasa.
NB;NIMEAMBATANISHA NA MAJINA YA WASHIRIKI HAPO CHINI.
IMETOLEWA NA CHAMA CHA SOKA DAR ES SALAAM DRFA

Omary Katanga mkuu wa Habari na Mawasiliano DRFA

NHIF yaombwa kufika nchi nzima

0
0
Na Grace Michael, Arusha

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya umeombwa kutekeleza zoezi la upimaji wa afya za wananchi katika Halmashauri zote nchini ikiwa ni pamoja na utoaji wa elimu ya namna ya kuepukana na magonjwa hayo ili kuliwezesha Taifa kuwa na wananchi wenye afya imara.

Rai hiyo imetolewa na watumishi mbalimbali katika mkutano wa kwanza wa mwaka wa Serikali Mtandao uliofanyika mkoani hapa ambapo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulitoa huduma za upimaji afya bure katika magonjwa yasiyoambukiza.

Akizungumzia hilo, Godfrey Luguma kutoka Halmashauri ya Wilaya Munduli alisema kuwa ni vyema NHIF ikawa na ratiba ya kuzunguka katika maeneo yote ili fursa hii iwafikie Watanzania wote.

“Upimaji na uhamasishaji wa wananchi kujiunga na Mifuko hii ikiwemo ya Afya ya Jamii iendelee ili kila mwananchi aweze kutambua hali ya afya yake hatua itakayomuwezesha kuwa na mipango imara ya kimaendeleo,” alisema Bw. Luguma.

Naye Nkide Mwaikuka kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa alitoa mwito kwa wananchi kuhakikisha wanajiunga na utaratibu wa bima ya afya ili wawe na uhakika wa kupata matibabu wakati wote.

“Bima ya Afya ni mpango mzuri sana kwa watumishi wa umma na hata wananchi wa kawaida, hivyo NHIF ongezeni elimu kwa wananchi hususan vijijini ili watambue umuhimu wa kuwa au kutumia mpango huu,” alisema Bw. Mwaikuka. Aidha washiriki wengine wametumia fursa hiyo kupima afya zao huku wakiupongeza Mfuko kwa kuanzisha zoezi hilo kwa lengo la kuhakikisha afya za watanzania zinabaki kuwa bora.

Akizungumzia rai iliyotolewa ya upimaji ndani ya halmashauri zote, Mkurugenzi wa Mifumo Habari wa NHIF, Othman Ali alisema kuwa mpango huo unafanyika katika maeneo mengi ya nchi hii hivyo akawaomba wananchi kutumia fursa hizo wakati zinapokuwa zimejitokeza.

“Tunazo ofisi katika kila mkoa ambazo zinafanya haya majukumu kupitia mpango wa Elimu ya Kata kwa Kata ambapo zoezi la upimaji wa afya kwa wananchi hufanyika,” alisema Bw. Othman.
Maofisa wa Serikali kutoka Wizara, Idara na Taasisi mbalimbali za Serikali wakiwa kwenye foleni ya kupima afya zao kwenye banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya katika Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Serikali Mtandao mjini Arusha.
Huduma za kupima shinikizo la damu zikiendelea.
Dawati la elimu kwa Umma likiwa kazini

NAPE ACHUKUA FOMU ZA UBUNGE PAMOJA NA SAID MTANDA LINDI LEO

0
0
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akikabidhiwa fomu za uteuzi kwa nafasi ya ubunge na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Olliver Vavunge.
Mbunge wa Jimbo la Mchinga Said Mtanda akipokea fomu za uteuzi kwa nafasi ya ubunge na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Olliver Vavunge.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akisalimina na wananchi waliojitokeza kumsindikiza kwenda kuchukua fomu za uteuzi wa ubunge za Tume ya Taifa ya Uchaguzi .Nape Nnauye ndie  mgombea aliyependekezwa na Chama Cha Mapinduzi kugombea jimbo la Mtama mkoani Lindi.

ZANTEL DONATES 10MILLION SHILLINGS IN PEMBA SCHOOL

0
0
Pemba, August 19, 2015: Zantel Tanzania has today donated 10 million Tshs as a contribution to build 6 classrooms of Mkanyageni Primary School in Pemba.

The donation aims at improving education standards to local communities through rendering support and providing school requirements such as infrastructure construction and renovations, the contribution will be used for finishing a building containing 6 class rooms covering costs of fitting windows and doors, cementing floor of 6 class rooms, plastering of 6 classrooms walls, painting of 6 classrooms walls and labor for the work.

Zantel is keen to empower the societies we are serving, and this donation is aimed to contribute to national building by improving the lives of future leaders to have better environment to acquire education, Government alone cannot successfully fund a functional educational system, so it’s important for us to assist youths become the best in their various endeavors through education.

Mkanyageni school head master Mr. Ramadhani Ngwali Makame, giving a speech during the handover ceremony
that took place at Mkanyageni primary school in Pemba.


Mr. Mohammed Mussa Zantel Government relations coordinator handing over dummy cheque to Mr. Ally Ngwali Vuai Mkanyageni school committee chairman, looking on are Zantel Acting CCO Mr. Bajwa,PembaSales Manager Farouk Ahmed and Mkanyageni pupils.

  

IDADI YA WAGONJWA WA KIPINDUPINDU YAONGEZEKA KINONDONI

0
0

Chalila Kibuda,Globu ya jamii
UGONJWA wa kipindupindu unazidi kusambaa katika manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi habari leo Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni,Aziz Msuya watu waliofariki katika manispaa hiyo watatu.
Amesema idadi ya wagonjwa katika manispaa imezidi kuongezeka kutoka 34 hadi kufikia 43.

Amesema dalili za huo ni  homa kali ,kuharisha pamoja na kutapika na kuongeza kuwa mtu akifikia dalili hizo awahi katika kituo cha afya.

Aidha amesema kujiepusha na ugonjwa huo ni kuzingatia usafi wa vyakula ,maji pamoja na kunawa mikono kwa usafi wakati wa kula.

Msuya amesema watu waliokuwa wamelalazwa na ugonjwa huo watatu wamerusiwa.

Katika zahanati ya Mburahati wagonjwa wa kipindupindu waliolazwa ni  21.

Muuguzi Mkuu wa Zahanati hiyo, Nusra Kessy amesema kuwa wagonjwa hao wanaendelea kutibiwa katika zahanati hiyo.
  Usafi ukiendelea katika Zahanati ya Mburahati katika kukabiliana na Ugonjwa Kipindupindu mara baada ya Globu ya Jamii kutembelea kujionea hali halisi ya ugonjwa huo leo jijini Dar es Salaam.
 Wakati ugonjwa wa kipindupindu ukiwa umeshika kasi lakini watu bado wanakula holela kama walivyokutwa na Kamera yetu leo jijini Dar es Salaam.
Usafi wa Mazingira katika Zahanati ya Mburahati ukiendelea kama walivyokuwa na Globu ya Jamii leo jijini Dar es Salaam.picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)

LOWASSA, BABU DUNI WASAINI HATI YA KIAPO YA KUGOMBEA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAHAKAMA KUU JIJINI DAR LEO

0
0
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akisaini fomu za hati ya Kiapo kwenye ofisi za Jaji wa Mahakama ya Tanzania, Jijini Dar es salaam leo Agosti 19, 2015. Hati ambayo kila mgombea wa nafasi ya urais anatakiwa kusaini katika mahakama kuu jijini Dar es Salaam .
Mgombea mwenza wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Juma Haji Duni akisaini fomu za hati ya Kiapo kwenye ofisi za Jaji wa Mahakama ya Tanzania, Jijini Dar es salaam leo Agosti 19, 2015. Kushoto kwake ni Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama hicho, Mh. Edward Lowassa.
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni wakiwa kwenye ofisi za Jaji wa Mahakama ya Tanzania, Jaji Suleiman Said Komu (mbele) wakati wa kusaini fomu za hati ya Kiapo, leo Agosti 19, 2015. Kulia ni Mwanasheria wa CHADEMA, Mh. Mabele Marando.

Mdau Lusekelo Ambokile alamba nondozz katika Chuo Kikuu cha Middlesex, UK

0
0
 Mdau Lusekelo Ambokile akionekana ni mwenye furaha sana mara baada ya kulamba Nondozz yake ya BA-Marketing katika Chuo Kikuu cha Middlesex University, nchini Uingereza.
Mdau Lusekelo Ambokile akiwa na Dada zake mara baada ya kulamba Nondozz yake ya BA-Marketing katika Chuo Kikuu cha Middlesex University, nchini Uingereza.
Mdau Lusekelo Ambokile akiwa na Mama yake mzazi.

RAIS KIKWETE AMTAMBULISHA MGOMBEA URAIS WA CCM KWA WAZEE WA DAR ES SALAAM

0
0
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Mhe Samia Suluhu Hassan, Mgombea mwenza wa ugombea Urais kwa tiketi ya Chama hicho tawala Dkt John Pombe Magufuli leo Agosti 19, 2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam
 :Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM  tawala Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wazee wa Dar es salaam leo Agosti 19, 2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
 Meza Kuu ikimfurahia Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM  tawala Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wazee wa Dar es salaam leo Agosti 19, 2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
 Mwenyekiti wa Wazee wa CCM wa Dar es salaam akipeana mikono na Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM  tawala Dkt John Pombe Magufuli baada ya kuongea na wazee wa Dar es salaam  leo Agosti 19, 2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
 Mwenyekiti wa Wazee wa CCM wa Dar es salaam akipeana mikono na Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM  tawala Dkt John Pombe Magufuli baada ya kuongea na wazee wa Dar es salaam  leo Agosti 19, 2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam
 Mwenyekiti wa Wazee wa CCM wa Dar es salaam akipeana mikono na Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM  tawala Dkt John Pombe Magufuli baada ya kuongea na wazee wa Dar es salaam  leo Agosti 19, 2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
Meza Kuu ikimfurahia Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM  tawala Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wazee wa Dar es salaam  leo Agosti 19, 2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.PICHA NA IKULU

WAJASIRIAMALI KUONYESHA BIDHAA ZAO JIJINI MWANZA, SEPTEMBA 26, 2015.

0
0

Baadhi ya Wajasiriamali wakiwa katika maonyesho ya bidhaa mbalimbali kwenye kongamano la wajasiriamali lililofanyika Hoteli ya Mbezi Garden mapema mwaka huu. Kongamano la namna hiyo linatarajiwa kufanyika Septemba 26, 2015 jijini Mwanza  Ukumbi wa  Benki Kuu (BoT), Capripoint.

Na Dotto Mwaibale

WAJASIRIAMALI  zaidi ya 250 wanatarajia kuonyesha bidhaa zao mbalimbali katika kongamano la mafunzo ya ujasiriamali litakalofanyika jijini Mwanza.

Akizungumza na Dar es Salaam leo, Mratibu wa kongamano hilo, Getrude Kilyabusebu alisema lengo la kongamano hilo ni kutoa mafunzo ya ujasiriamali ili kuwajengea uwezo wajasiriamali hao.

"Wajasiriamali hao katika kongamano hilo watapata fursa ya kuonesha bidhaa zao mbalimbali na pia watapata mafunzo ya jinsi ya kukuza mitaji yao na mbinu zingine za biashara" alisema Kilyabusebu.

Alisema makongamano ya namna hiyo yamekuwa yakiwasaidia wajasiriamali hao kujuana na kubadilishana uzoefu wa kibiashara na utengeneza wa bidhaa zao zikiwemo mbinu za ufugaji na kilimo.

Alisema mafunzo hayo utolewa na wataalamu waliobobea katika shughuli za ujasiriamali na matunda ya mafunzo ya  makongamano hayo yamewanufaisha wajasiriamali  wengi wajasiriamali.

Kilyabusebu alisema kongamano hilo lililoandaliwa na  Jumuiya ya Wanawake Wajasiriamali Tanzania (Tanzania Business Entrepreneurs Women) lita Septemba 6, 2015 jijini Mwanza  katika ukumbi wa Benki Kuu (BoT) Capripoint.

Mratibu huyo alisema kuwa pamoja na mambo mengine kila mshiriki atalazimika kuchangia gharama kidogo ili kufanikisha kongamano hilo ambapo katika mafunzo na chakula atatakiwa kulipia sh.30,000, meza ya kuuzia bidhaa na kuzitangaza sh. 20,000 na mafunzo na meza sh.50,000.

Kilyabusebu alitumia fursa hiyo kuwaomba wajasiriamali wa kanda ya ziwa kuweza kushiriki katika kongamano hilo ambalo ni muhimu kujifunza stadi za kazi zao.


















IRELAND YAWADHAMINI WATANZANIA 14 KWA SHAHADA YA UZAMILI

0
0
Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Bi. Fionnuala Gilsenan, akitoa hotuba yake wakati wa maonyesho ya sayansi kwa wanafunzi wa sekondari yanayoandaliwa na shirika la YST ambayo pia Ubalozi wake unadhamini kila mwaka.

Na Daniel Mbega

UBALOZI wa Ireland nchini Tanzania, umewapatia scholarship Watanzania 14 ili kusoma kozi mbalimbali za shahada ya uzamili (masters) na huku wanne kati yao wakienda kusoma vyuo vya nje ya nchi hasa University College Dublin, Dublin Institute of Technology na National University of Ireland Maynooth. 

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ubalozi wa Ireland nchini, scholarship hizo zimetolewa na ubalozi huo kama sehemu ya Mpango wa Mafunzo wa Kila Mwaka (Fellowship Training Programme), ambapo wataalamu wanne waliobahatika kwenda ng’ambo watakwenda kusomea kozi za Maendeleo Endelevu (Sustainable Development), Kilimo na Maisha ya Vijijini (Agriculture and Rural Livelihoods), Rasilimali Watu (Human Resource Management), na Immunolojia na Afya ya Binadamu (Immunology and Human Health).

Watanzania wengine 10 wamedhaminiwa kusomea kozi mbalimbali katika vyuo vikuu vya hapa nchini.Taarifa hiyo inasema, sherehe za kuwapokea wale walihitimu na kuwakabidhi scholarship wale wanaokwenda kuanza, zitafanyika kesho mchana katika ofisi za Ubalozi zilizoko Masaki, jijini Dar es Salaam ambapo Balozi wa Ireland nchini, Fionnuala Gilsenan, ndiye atakayetoa scholarship hizo.

Mpango huo wa Mafunzo wa kila Mwaka, kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwa kiasi kikubwa unahusisha Mfuko wa Misaada wa Ireland (Irish Aid) kupitia program ya maendeleo ya Ubalozi huo nchini Tanzania.

Wanufaika wa mpango huo wameteuliwa na washirika wa maendeleo wa Ireland nchini Tanzania, zikiwemo wizara mbalimbali za Serikali, halmashauri za wilaya na mashirika yasiyo ya kiserikali, ambayo shughuli zao zinawiana na maeneo ya vipaumbele vya Irish Aid, hususan Kilimo, Afya, Lishe na Utawala.


WAKAZI WA KIJIJI CHA KISANGA WATOA MAONI YAO KUHUSU WASHIRIKI WA SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2015 (VIDEO)

0
0
   Ni Siku ya 16 huku Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 Msimu wa nne shindano linalo endeshwa na Shirika la Oxfam kupitia Kampeni yake ya Grow,  Likiwa linaelekea Ukingoni ambapo katika siku hii tunaona Maisha ya Mama Shujaa wa Chakula  walivyo ishi kwa Siku 15, lakini kubwa zaidi ni wakazi wa Kijiji cha Kisanga hususani wale ambao ndio waliokuwa wanaishi na Akina mama hao katika Kaya zao kutoa maoni yao jinsi walivyo ishi na akina Mama hao. Pia hapa tutaona wasifu wa Washiriki wote wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula ambapo kauli mbiu ni 'Wekeza kwa wakulima wadogo wadogo wanawake inalipa'
Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula katika picha ya pamoja.

MAGUFULI ASAINI HATI YA KIAPO YA KUGOMBEA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAHAKAMA KUU JIJINI DAR LEO.

0
0
Viewing all 109610 articles
Browse latest View live


Latest Images