HARUSI YA NIAH ALMASI NA JACKLINE BUKUKU WA NSSF MBEYA
↧
↧
WATEJA WAMIMINIKA BANDA LA NHC NANE NANE, LINDI
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akitia saini kwenye kitabu cha wageni kwenye banda la maonesho la NHC lilikuwapo katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi kulikokuwa kukifanyika maonesho hayo ya Nane Nane kitaifa.
Wateja wakipata maelekezo kutoka kwa maafisa wa mauzo wa Shirika la Nymba la Taifa kwenye maonyesho ya Nane Nane Kitaifa Ngongo, Lindi.
Wateja wakipata maelekezo kutoka kwa maafisa wa mauzo wa Shirika la Nymba la Taifa kwenye maonyesho ya Nane Nane Kitaifa Ngongo, Lindi.
Wateja wakipata maelekezo kutoka kwa maafisa wa mauzo wa Shirika la Nymba la Taifa kwenye maonyesho ya Nane Nane Kitaifa Ngongo, Lindi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akihutbia wakazi wa Lindi kwenye uwanja wa Nane Nane Ngongo ambapo alihitimisha kilele cha sikukuu ya wakulima Nane Nane. Maonesho ya nane nane yaliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akihutbia wakazi wa Lindi kwenye uwanja wa Nane Nane Ngongo ambapo alihitimisha kilele cha sikukuu ya wakulima Nane Nane. Maonesho ya nane nane yaliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
↧
EFM WAANDAA TAMASHA LA PILI LA MUZIKI MNENE BAR KWA BAR
Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa kituo cha Redio cha EFM, Denis Ssebo (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu kuendelea kufanyika kwa Tamasha la Muziki Bar kwa Bar baada ya kumalizika kwa tamasha hilo kwa awamu ya kwanza. Kulia ni Mtangazaji, Dina Marios.
Mtangazaji, Dina Marios akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu kuendelea kufanyika kwa Tamasha la Muziki Bar kwa Bar baada ya kumalizika kwa tamasha hilo kwa awamu ya kwanza. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa kituo cha Redio cha EFM, Denis Ssebo.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa kituo cha Redio cha EFM, Denis Ssebo katika mkutano uliofanyika makao makuu ya EFM-Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
BAADA ya kumalizika kwa Tamasha la muziki mnene Bar kwa bar awamu ya kwanza, na mashabiki kuomba Burudani hiyo iendelea tena, Uongozi Efm umekubali ombi hilo na sasa Tamasha hilo linarudi tena kwa kishindo likiwa limeboreshwa kwakuongeza wigo wa kuwafikia watu wengi zaidi.
Muziki mnene bar kwa bar awamu hii bila kuwasahamu wasikilizaji na mashabiki wa EFM katika wilaya za Kinondoni, Temeke na Ilala kwa umuhimu wake na Wilaya mpya katika mkoa wa Dar es salaam, Muziki mnene sasa utapelekwa pia katika mkoa wa Pwani.
Maeneo ambayo wanatakiwa kukaa tayari kwa Muziki mnene bar kwa bar utakaoporomoshwa na Madjs wakali wa Efm, ni pamoja na Kibaha, Mlandizi, Mkuranga, Bagamoyo, Kisarawe, Kigamboni na maeneo mengine mengi kwa ajili ya kuhakikisha tunakonga nyoyo za mashabiki wetu.
Muziki Mnene bar kwa bar mwaka huu inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 5/09/2015 . Lakini katika kuelekea huko efm imeanza na Muziki mnene bango katika sehemu yako ya biashara ambako bwana E anapita na ukiwa umeweka bango la EFM na unasikiliza matangazo yetu basi utapata kifurushi chenye zawadi kibao.
Na kama ilivyokawaida yetu, mwishoni tutakuwa na Tamasha kubwa la hitimisho ambalo litafanyika jijini Dar es salaam ambalo safari hii limeboreshwa na kuongezwa vionjo vingi sana.
“Ninawaomba wasikilizaji wetu wakae mkao wa kula maana tutawafikia na kuwamiminia Burudani ambayo pia itarushwa live kutoka eneo husika kupitia kituo chao cha 93.7 EFM. Njoo tuonane, tufahamiane na tuijenge Radio yetu efm ambayo kwetu Muziki unaongea”.
LAKINI jambo la pili ambalo ndugu zangu wanahabari tungependa kuwajulisha ni kwamba katika kuhakikisha tunaendelea kukupa kilicho bora zaidi kupitia vipindi vyetu mbalimbali,sanjari na kuwa na watangazaji wenye ushawishi na uwezo mkubwa. leo hii tunamtambulisha kwenu mtangazaji Dina Marios ambaye wengi uwezo wake mnaujua na sasa ameungana na wenzake wenye uwezo mkubwa katika familia ya Efm.
Mwisho niwashukuru sana kwa mwitikio wetu na kwakuwa tumeendelea kushirikiana mara nyingi hivyo naomba tuendelee kushirikiana hivi hivi. Asanteni sana kwakunisikiliza.
↧
JK atua mjini Dodoma leo kuendesha vikao vya chama cha mapinduzi
Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Adam Kimbisa muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma ambapo ataongoza vikao vya Kamati ya Maadili na Kamati kuu ya CCM vitakavyofanyika katika ukumbi wa White House Makao Makuu Dodoma.
Alhaj Kimbisa amekanusha uvumi uliosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa ameihama CCM. Kushoto ni Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (picha na Freddy Maro)
Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na KAtibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahmana Kinana baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma ambapo ataongoza vikao vya Kamati ya Maadili na Kamati kuu ya CCM vitakavyofanyika katika ukumbi wa White House Makao Makuu Dodoma. Picha na Freddy Maro
↧
SSRA katika maonesho ya Sherehe ya wakulima (NANE NANE) Mkoani Morogoro
Afisa uhusiano mwandamizi Bw. Fulgence Sebera akitoa maelezo ya shughuli za Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Majid Mwanga (wa tatu kulia) aliyeambatana na viongozi wengine wa TASO walipotembelea banda la SSRA katika sherehe za maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere mkoani Morogoro.
Mch. Vernon Fernandes (aliyekaa) alipotembelea banda la SSRA katika maonesho ya Nanenane Morogoro, kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasishaji Bi Sarah Kibonde Msika akifuatiwa na mwanasheria mwandamizi Bw. Omar Sururu Khalfan, kushoto ni Afisa matekelezo Bw. David Lyanga.
Mkuu wa kitengo cha uhusiano na uhamasishaji Bi Sarah Kibonde Msika wa kwanza kushoto akitoa maelezo ya masuala ya Hifadhi ya Jamii kwa wadau waliotembelea banda la SSRA, akifuatiwa na afisa matekelezo Bw.David Lyanga na afisa uhusiano mwandamizi Bw. Fulgence Sebera katika maonesho ya Nanenane Morogoro.
Maafisa wa Mamlaka wakikabidhi zawadi ya Mfuko wa SSRA kwa mdau aliyetembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya Nanenane mkoani Morogoro.
↧
↧
NHIF WAIBUKA WASHINDI KWENYE MAONYESHO YA NANE NANE MKOANI LINDI
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti NHIF akipokea Kikombe cha Ushindi wa Kwanza kundi la Mifuko ya Jamii Toka kwa Rais Jakaya Kikwete,kushoto na Kulia kwa Rais wakishuhudia tukio hilo Ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Mwantumu Mahiza na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika,Stephen Wassira katika Ufungaji wa Maonesho hayo katika Viwanja Vya Ngongo Lindi
Meneja wa Mfuko wa NHIF Mkoa wa Lindi,Fortunata Kullaya(Alieshika kikombe)Kwa Pomoja na Mkurugenzi wa Masoko ,Rehani Athumani (kulia) na Grace Kisinga Afisa Uhusiano na mawasiliano Nhif wakishangilia Ushindi wa Kwanza Walioupata katika Maonesho ya Nane Nane Kitaifa katika Viwanja vya Ngongo,Manispaa ya Lindi.
Waziri Mkuu wa Jahuri ya Muungano wa Tanzania,Mizengo Pinda Akisiliza kwa Makini maelezo ya Huduma zinazotolewa na Mfuko wa Bima ya Afya Toka kwa Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti Bima ya Afya Makao Makuu,Bw Rehani Athuman.Huku Mkuu wa mkoa wa Lindi na Mtwara wakifuatilia kwa karibu
↧
Mabalozi na Wafanyabiashara Kutoka Kuala Lumpur watembelea Serengeti, Ngorongoro na Zanzibar
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Aziz Ponary Mlima aliwaalika Mabalozi wa wa nchi mbali mbali kuja kutembelea Tanzania hivi karibuni.
Mabalozi hao kutoka Kuala Lumpur Malaysia walitembelea mbuga za wanayama za Serengeti, Ngorongoro na walifanya ziara mjini Zanzibar.
Mabalozi hao ni Waheshimiwa Viorica na Constantin Nistor (Romania), Stephen Mubiru (Uganda), Dkt. AzizPonary Mlima(Tanzania), Isabela Mhlanga( Afrika Kusini), na Bwana Rogatius Shao (Naibu Balozi-Tanzania).
Mabalozi walipowasili Kibo Palace Hotel, Arusha na kupokelewa na Naibu Waziri wa Maliasili.na Utalii Mheshimiwa Mahmud Mgimwa, Bwana Alan Kijazi Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA na Bwana Pascal Shelutete Meneja wa Mawasiliano na Masoko wa TANAPA.
Tembo mbugani Serengeti
Simba wa Serengeti
Kifaru katika mbuga ya Serengeti
Mabalozi walipowasili kutokea Zanzibar
Sehemu ya mamilioni ya nyumbu na pundamilia Serengeti |
↧
USALAMA MITANDAO: TANZANIA INA CHA KUJIFUNZA KUTOKA KENYA.
Mwandishi wa makala haya Bw. Yusuph Kileo akitoa mada kwenye moja ya vikao vya usalama mitandao jijini Nairobi, Kenya, hivi karibuni |
Nimekamilisha vikao vya usalama mitandao vilivyofanyikia jijini Nairobi kufuatia mualiko maalum nilioupata. Katika vikao hivyo niliwasilisha mada mbili (ya kwanza ikiwa ni namna ya kukabiliana na uhalifu mtandao na mada ya pili ikiwa ni namna ya uchunguzi wa makosa ya digitali kitaalam) katika mada hizo mbili ambazo zilipokelewa vizuri na kupelekea mijadala ya kipekee kuna mengi nikajifunza kutoka kwa washiriki.
Aidha, nilishiriki mijadala duara iliyojikita katika changamototo mbali mbali za uhalifu mitandao na kuiangazia sharia mtandao ya nchi ya Kenya.
Kenya ni miongoni mwa nchi tatu barani afrika ambazo zimeorodheshwa kuwa na uhalifu mkubwa sana wa kimtandao nyingine ni Nigeria pamoja na Afrika ya kusini.
Tukijadili takwimu za kutisha duniani kote, tulishuka na kuangazia bara la Afrika na baadae Afrika mashariki na hatimae kujikita na takwimu za nchi ya Kenya.
Kwa upande wa Kenya kwa mujibu wa takwimu zilizo wasilishwa katika mkutano, hadi kufikia Mwezi wa saba mwaka huu (2015) kuna simu 34.8 Milioni huku watumiaji wakiwa ni 26.0 Milioni. Aidha, matumizi ya intaneti ni 29.1 milioni ambayo ni sawa na 65% “penetration”. Takwimu hizo zinasindikizwa na upotevu wa dola za kimarekani 20 milioni ($20 Mil) kila mwaka kutokana na uhalifu mtandao.
↧
NEWS ALERT: Mzee Paul Sozigwa apotea katika mazingira ya kitatanishi
Mzee Paul Sozigwa (pichani), aliyewahi kuwa Mwandishi wa Habari wa Rais katika serikali ya Awamu ya kwanza chini ya Mwalimu Nyerere, amepotea tangu jana mchana katika mazingira ya kitatanishi.
Kwa mujibu wa taarifa ya familia yake ambayo Globu ya Jamii imeletewa, mara ya mwisho Mzee Sozigwa alionekana kanisani Mbezi Beach BCIC (kwa Gamanywa) jana Jumapili saa nane mchana. Kupotea huku kunaleta mashaka hasa kwa kuwa Mzee Sozigwa ni mgonjwa wa Alzheimer, na mara nyingi anapoteza kumbukumbu. Taarifa ya kupotea kwake imeshatolewa polisi na kufunguliwa RB.
Taarifa hiyo imesema mara ya mwisho Mzee Sozigwa alikuwa amevaa shati jeupe lenye mistari ya bluu na kijivujivu, suruali nyeusi na viatu vyeusi. Anapoulizwa anakaa wapi hujibu Kisarawe ama Vidunda, wilaya ya Kisarawe. Atakayemuona anaombwa kupiga simu zifuatazo:
Mch. Moses Sozigwa 0712 379818, 0755 716158
Mrs. Irene Yussuf 0784 300418
Ms. Lucy Paul Sozigwa 0755 564080, 0717 310783
Mrs. Judith Mlawa 0712 834737
Unaweza pia kuwasiliana nao kwa Whatsapp na Viber
Taarifa hiyo imesema mara ya mwisho Mzee Sozigwa alikuwa amevaa shati jeupe lenye mistari ya bluu na kijivujivu, suruali nyeusi na viatu vyeusi. Anapoulizwa anakaa wapi hujibu Kisarawe ama Vidunda, wilaya ya Kisarawe. Atakayemuona anaombwa kupiga simu zifuatazo:
Mch. Moses Sozigwa 0712 379818, 0755 716158
Mrs. Irene Yussuf 0784 300418
Ms. Lucy Paul Sozigwa 0755 564080, 0717 310783
Mrs. Judith Mlawa 0712 834737
Unaweza pia kuwasiliana nao kwa Whatsapp na Viber
↧
↧
MAKOSA YA KISHERIA KATIKA KUNADISHA NYUMBA YA MKOPAJI.
Na Bashir Yakub
Sheria ya ardhi Sura ya 113 imetoa maelezo kwa upana kuhusu miamala kati ya mtoa mkopo , mkopaji na dhamana inayohusika katika mkopo huo. Mara kadhaa watu binafsi, taasisi za haki za binadamu, asasi za kiraia, na makundi mengine wamekuwa wakitoa maelezo mbalimbali yanayotokana na sheria hii hasa wakilenga kupunguza vitendo vya ukiukaji wa taratibu ambao hufanywa na baadhi yua taasisi za mikopo zikishirikiana na makampuni ya udalali ( Brockers/auctioneers).
Katika kipindi hiki ambapo taasisi za fedha zinazojihusisha na mikopo zimeongozeka watu wengi wamekuwa wakilalamikia mienendo yake hasa pale mtu anaposhindwa kurejesha kwa wakati. Pia wamekuwa wakilalamikia namna taasisi hizi zinavyowakokotolea mahesabu hasa yale ya riba. Jingine ni taratibu zinazotumika katika kuuza/ kunadisha dhamana ya mtu hasa nyumba iwapo mlengwa ameshindwa kurejesha.
http://sheriayakub.blogspot.com/2015/08/makosa-ya-kisheria-katika-kunadisha.htmlKusoma zaidi BOFYA HAPA
↧
NEWS ALERT: MKIMBIZI KUTOKA BURUNDI AFARIKI MKOANI KIGOMA KWA UGONJWA USIOJULIKANA, AZIKWA KWA TAHADHARI KUBWA
Habari na picha na Editha Karlo,
wa Globu ya Jamii Kigoma
MTU mmoja ambaye ni raia kutoka nchi ya Burundi amefariki usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Kigoma kwa ugonjwa usiojulikana.
Mgonjwa huyo amezikwa jana jioni kwa tahadhari zote zihusuzo magonjwa hatari ya kuambukiza.
Nguo, vitanda, mashuka na vitu vyake vyote alivyokuwa akitumia wakati wa uhai wake vimechomwa moto mara tu baada ya mwili wake kuzikwa eneo la Masanga nje kidogo ya mji wa Kigoma.
(Picha zinaonesha hatua mbalimbali toka mwili wa marehemu ulipoondolewa na wataalamu waliovaa mavazi maalumu hadi mazikoni).
Mgonjwa huyo amezikwa jana jioni kwa tahadhari zote zihusuzo magonjwa hatari ya kuambukiza.
Nguo, vitanda, mashuka na vitu vyake vyote alivyokuwa akitumia wakati wa uhai wake vimechomwa moto mara tu baada ya mwili wake kuzikwa eneo la Masanga nje kidogo ya mji wa Kigoma.
(Picha zinaonesha hatua mbalimbali toka mwili wa marehemu ulipoondolewa na wataalamu waliovaa mavazi maalumu hadi mazikoni).
Akiongea na mtandao huu daktari wa wakimbizi kutoka shirika la kusafirisha wakimbizi kwenda nje ya nchi (IOM) Dkt. Beda amesema kuwa marehemu ameishi katika kambi ya wakimbizi ya Nyalugusu Wilayani Kasulu kwa muda wa miaka mitatu yeye pamoja na familia yake.
Dkt Beda amesema kuwa marehemu Buchumi Joely (39) alifika Kigoma mwezi uliopita akiwa yeye pamoja familia yake kwa ajili ya kusafirishwa na shirika la IOM kwenda marekani.
DK Beda alisema kuwa marehemu alianza kuugua tarehe 31 ya mwezi uliopita kwa kutokwa na damu sehemu mbalimbali za mwili wake kama mdomoni, kwenye fizi na machoni.
"Ilipofika tarehe juzi Agosti 8 hali yake ilizidi kuwa mbaya ndipo uongozi ulipoamua kumpeleka katika hospital ya mkoa maweni kwaajili ya matibabu zaidi" alisema Dkt Beda.
Naye Kaimu mganga mkuu wa hospital ya nkoa wa kigoma Dkt Shija Ganai amethibitishia mtandao huu kuwa walimpokea mgonjwa huyo na kumlaza katika wodi namba 8 ya Grade One.
Alisema kuwa usiku wa kuamkia leo hali ya mgonjwa ilizidi kuwa mbaya na damu zilizidi kuongezeka, na walipompima maralia alikuwa na joto la kawaida la nyuzijoto 36.
Dkt. Ganai ameeleza kuwa ilipofika alfajiri ya kuamkia leo mgonjwa huyo alifariki dunia. Amesema kwamba mpaka sasa bado haijadhibitishwa kama mgonjwa huyo amekufa kwa ugonjwa wa ebola japo alikuwa na dalili zote za ugonjwa huo.
"Tumeshatuma sampo ya damu maabara kuu ya Taifa kwa ajili vipimo ili tujue ni ugonjwa gani uliomuuwa"alisema Dkt huyo.
Aliongezea kuwa hivi sasa madaktari, manesi pamoja na ndugu wote waliokuwa wanamuhudumia mgonjwa hivi sasa wapo chini ya uangalizi maalumu wa madaktari kwa muda wa siku 21.
Aliongezea kuwa hivi sasa madaktari, manesi pamoja na ndugu wote waliokuwa wanamuhudumia mgonjwa hivi sasa wapo chini ya uangalizi maalumu wa madaktari kwa muda wa siku 21.
↧
MAGUFULI AWASHUKURU WANA CCM WA MTWARA KWA KUMDHAMINI,WAMUHAKIKISHIA USHINDI WA KISHINDO
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasalimia wanachama na wafuasi wa CCM mkoa wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kumpokea,Dkt Magufuli aliwashukuru wanachama hao kwa kujitokeza kwa wingi na walimuahakikishia ushindi wa kishindo na wa mapema katika uchaguzi mkuu utakaofanyika hapo baadae mwaka huu,pia amewata kuwa na umoja wa kushirikiana na kuweka kando tofauti zao kuhakikisha wanailetea CCM ushindi wa kishindo.
Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini Husnain Murji akiwahutubia wana CCM nje ya ofisi ya CCM Mtwara na kuwaambia kuwa ushindi kwa CCM utakuwa wa kishindo .
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mtwara Ndugu Mohamed Sinani akihutubia wakazi wa Mtwara ambapo alihakikisha kuwa Mtwara itaongoza katika kumpigia kura nyingi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.
Wananchana na Wafuasi wa chama cha Mapinduzi (CCM),wakimshangilia Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwashukuru kwa kumpa udhamni na kujitokeza kwa wingi kumpokea,lakini pia alitumia nafasi hiyo kujitambulisha kwao na kuwaomba wajenge mshikamano na kuweka tofauti zao kando ili kukihakikishia ushindi chama cha CCM katika uchaguzi mkuu utakaofanyika hapo baadae mwaka huu.
Mgombea mteule wa Urais kwa chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu wa CCM mkoa wa Mtwara,Ndugu Shaibu Akwilombe mara baada ya kuwasili katika ofisi za CCM mkoa wa Mtwara kuwashukuru Wanachama na wafuasi wa chama hicho kwa kujitokeza kwa wingi,na pia alitia saini vitabu vya wageni vya ofisi hiyo,kati ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mtwara Ndugu Mohamed Sinani pamoja na Naibu Waziri wa Fedha,ambaye pia aliwahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Mwigulu Nchemba.
Baadhi ya Wanachama na wafuasi wa chama cha CCM wakiwa wamekusanyika nje ya ofisi ya za mkoa huo mjini Mtwara,kabla ya kumsikiliza mgombea Urais wa chama hicho Dkt John Pombe Magufuli,ambaye alifika ofisini hapo kusaini vitabu na pia kuwashukuru wanachama hao kumdhamini na kujitokeza kwa wingi kumpokea
↧
MFUMUKO WA BEI WA TAIFA WAONGEZEKA
Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Ephraimu Kwesigabo akitoa taarifa ya kuongezeka kidogo kwa mfumuko wa bei nchini kwa mwezi Mei 2015 leo jijini Dar es salaam.Mfumuko wa Bei wa bei kwa mwezi Julai ,2015 umefikia asilimia 6.4 kutoka asilimia 6.1 iliyokuwepo Juni 2015.
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu imetangaza Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Julai 2015 na kusema kuwa umeongezeka hadi kufikia asilimia 6.4 kutoka asilimia 6.1 iliyokuwepo mwezi Juni 2015.
Hii inamaanisha kuwa kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa na huduma kwa mwezi Julai 2015 imeongezeka ikilinganishwa na kasi ya upandaji bei ya bidhaa na huduma iliyokuwepo mwezi Juni mwaka 2015.
Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam amesema kuongezeka huko kumesababishwa na kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula katika maeneo mbalimbali nchini.
Amezitaja bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko huo kutokana na upandaji wa bei katika masoko kwa mwezi Julai 2015 kuwa ni mchele kwa asilimia 27.9,mahindi asilimia 2.3, unga wa muhogo asilimia 9.2, nyama asilimia 4.5, samaki 12.2, na maharage asilimia 5.9.
Kuhusu Fahirisi za Bei ambacho ni kipimo kinachotumika kupima mabadiliko ya bei ya bidhaa na huduma zinazotumiwa na kaya binafsi hapa Tanzania, Kwesigabo amesema zimeongezeka hadi kufikia 158.78 kutoka 158:12 za mwezi Juni.
Amesema kuongezeka kwa fahirisi za bei kumechangiwa na ongezeko la bei ya baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula zikiwemo gesi ya kupikia kwa asilimia 3.7, mafuta ya dizeli 5.9, mafuta ya Petroli ailimia 4.9, unga wa mahindi asilimia 2.5, ulezi asilimia 2.9, samaki asilimia 4.8, viazi vitamu asilimia 2.6 na ndizi za kupika asilimia 3.4.
Kwesigabo amesema uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma za mlaji kwa mwezi Julai , 2015 umefikia shilingi 62 na senti 98 ikilinganishwa na kiasi cha shilingi 63 na senti 24 za mwezi Juni 2015.
“Uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma zilezile kwa mlaji kwa mwezi Julai ,2015 na umepungua hii ina maana kuwa sasa mtu anahitaji kuongeza ziada ya shilingi 38 ili aweze kununua bidhaa na huduma sawa na zile alizokuwa na uwezo wa kuzinunua katika mwezi Juni"
Kwa upande wa mfumuko wa Bei kwa nchi za Afrika Mashariki kwa mwezi Julai, 2015 Bw.Kwesigabo amesema kuwa una mwelekeo unaofanana , Kenya umepungua kidogo hadi kufikia asilimia 6.62 na kutoka 7.03 mwezi Juni 2015 huku Uganda ikiwa na mfumuko wa Bei wa asilimia 5.4 kutoka asilimia 4.9 za mwezi Juni, 2015.
↧
↧
Modewjiblog yapatwa na kwikwi, yaomba radhi kwa wasomaji wake
Wapendwa wasomaji wa Modewjiblog tunashughulikia matatizo ya kifundi yaliyojitokeza tangu jana kwenye ‘server’ kiutaalam inaitwa DDOS unaweza kuperuzi link hii kwa taarifa zaidi https://en.wikipedia.org/wiki/ Denial-of-service_attack ambayo yako nje ya uwezo wetu.
Modewjiblog itarudi hewani hivi punde, samahani kwa usumbufu wowote ule uliojitokeza, tunahitaji ushirikiano wenu zaidi.
----------------------------------
There has been an undergoing DDOS attach on the server https://en.wikipedia.org/wiki/ Denial-of-service_attack.
We have taken measures to lighten the effects of this as much as we can. Unfortunately it is something that we don't have much control over, but we will do all in our power to get the blog back to full functionality.
Email: info@modewjiblog.com
↧
Inroducing ROL International Pre-school & Daycare school at Mbweni Mpiji
↧
Jubilee InsuranceTanzania and R&R Insurance Brokers introduce the first-ever Investment Plan for Tanzanians living in the Diaspora
R&R Insurance Brokers Limited (R&R) in partnership with Jubilee Insurance companies in Tanzania announced the first-ever Investment Plan cover that combines both Life Insurance and Repatriation (Funeral) cover for Tanzanians living in the diaspora.
The product named Nyumbani Kwetu, Swahili for My Home has been designed to deliver three components; investment, life and repatriation cover. Nyumbani Kwetu allows access to ones’ funds after the second year, it has a guaranteed life cover, guaranteed funeral cover and a return rate of 4 %.The cover is affordable and accessible with premiums as low as Tsh17,200/- per year. The product is available to all Tanzanians living outside the country with a minimum age of 18 years. Unlike other insurance products, Nyumbani Kwetu has no maximum age of entry.
R&R prides itself on crafting unique insurance solutions. R&R Insurance Brokers Managing Director, Ms. Diana Matondane, said that the firm is thrilled to partner with the number one Insurance Company in East Africa. “This presents us with an opportunity to showcase our products to Tanzanians all over the world. Jubilee’s passion and dedication to underwrite risks and paying claims is well known as the market leaders in Tanzania, It’s an honour to work with them,” said Ms. Matondane.
“We are delighted to partner with R&R and we look forward to introducing various products to the Tanzanian market, and beyond catering for long term life Assurance packages such as school fees and personal investment policies,” said Jubilee Insurance CEO George Alande. Alande further highlighted that Jubilee also offers short term insurance packages such as domestic package insurances for residential houses and their contents, motor vehicle covers specifically for ladies and individual medical insurance covers among others. “There is a synergy between our two brands that we feel will result in a profitable relationship for both of us,” said Alande.
R&R provides a full- brokerage service covering General, Life and Health insurance in a wide range of sectors including aviation, marine, mining, oil, gas and energy, credit and political (investment) risks, surety bonds, terrorism and sabotage as well as micro insurance.
↧
Mkurugenzi wa Ushirikano wa Kimataifa awashauri vijana kufanya kazi na Mashirika ya Kimataifa
Juu na Chini ni picha ya Vijana waliohudhuria Kongamano hilo wakimsikiliza Balozi Mushy (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha mada. |
Balozi Mushy akimwelezea jambo Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi katika Kongamano la Vijana |
↧
↧
WASHIRIKI WA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2015 WAHIMIZA WANAKIJIJI KUFANYA KILIMO CHA BIASHARA, WAWAPA BURUDANI WANAKIJIJI.
Baada ya washiriki wa Shindano la Mama shujaa wa Chakula Shindano linalo endeshwa na Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow na kudhaminiwa na Gates and Melinda Foundation,TBS, Cooperative Bank Great Britain na Care Tanzania, baada ya kuwasili wote sasa wanapangwa makundi makundi kwa ajili ya kuanza mchakato wa siku
Hapa katika kundi la kwanza washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula , Shindano linaloendeshwa na Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow hapa wakiwahamasisha wanakijiji cha kisanga kilimo cha Biashara na kubadilishana mawazo kuhusu nyenzo , mazao na tathimini ya mapato na matumizi.
Kundi la pili wakiendelea kutoa Elimu ya Kilimo kwa Wanakijiji. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
↧
Katibu Mkuu amuaga rasmi Balozi wa Finland aliyemaliza muda wa kazi nchini
Balozi Mulamula akiendelea kuzungumza. |
Sehemu ya Wageni walioudhuria hafla hiyo wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani). BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI |
↧
MFUMUKO WA BEI WA TAIFA WAONGEZEKA
Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Ephraimu Kwesigabo akitoa taarifa ya kuongezeka kidogo kwa mfumuko wa bei nchini kwa mwezi Mei 2015 leo jijini Dar es salaam.Mfumuko wa Bei wa bei kwa mwezi Julai ,2015 umefikia asilimia 6.4 kutoka asilimia 6.1 iliyokuwepo Juni 2015.
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
OFISI ya Taifa ya Takwimu imetangaza Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Julai 2015 na kusema kuwa umeongezeka hadi kufikia asilimia 6.4 kutoka asilimia 6.1 iliyokuwepo mwezi Juni 2015.
Hii inamaanisha kuwa kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa na huduma kwa mwezi Julai 2015 imeongezeka ikilinganishwa na kasi ya upandaji bei ya bidhaa na huduma iliyokuwepo mwezi Juni mwaka 2015.
Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam amesema kuongezeka huko kumesababishwa na kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula katika maeneo mbalimbali nchini.
Amezitaja bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko huo kutokana na upandaji wa bei katika masoko kwa mwezi Julai 2015 kuwa ni mchele kwa asilimia 27.9,mahindi asilimia 2.3, unga wa muhogo asilimia 9.2, nyama asilimia 4.5, samaki 12.2, na maharage asilimia 5.9.
Kuhusu Fahirisi za Bei ambacho ni kipimo kinachotumika kupima mabadiliko ya bei ya bidhaa na huduma zinazotumiwa na kaya binafsi hapa Tanzania, Kwesigabo amesema zimeongezeka hadi kufikia 158.78 kutoka 158:12 za mwezi Juni.
Amesema kuongezeka kwa fahirisi za bei kumechangiwa na ongezeko la bei ya baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula zikiwemo gesi ya kupikia kwa asilimia 3.7, mafuta ya dizeli 5.9, mafuta ya Petroli ailimia 4.9, unga wa mahindi asilimia 2.5, ulezi asilimia 2.9, samaki asilimia 4.8, viazi vitamu asilimia 2.6 na ndizi za kupika asilimia 3.4.
Kwesigabo amesema uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma za mlaji kwa mwezi Julai , 2015 umefikia shilingi 62 na senti 98 ikilinganishwa na kiasi cha shilingi 63 na senti 24 za mwezi Juni 2015.
“Uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma zilezile kwa mlaji kwa mwezi Julai ,2015 na umepungua hii ina maana kuwa sasa mtu anahitaji kuongeza ziada ya shilingi 38 ili aweze kununua bidhaa na huduma sawa na zile alizokuwa na uwezo wa kuzinunua katika mwezi Juni"
Kwa upande wa mfumuko wa Bei kwa nchi za Afrika Mashariki kwa mwezi Julai, 2015 Bw.Kwesigabo amesema kuwa una mwelekeo unaofanana , Kenya umepungua kidogo hadi kufikia asilimia 6.62 na kutoka 7.03 mwezi Juni 2015 huku Uganda ikiwa na mfumuko wa Bei wa asilimia 5.4 kutoka asilimia 4.9 za mwezi Juni, 2015.
↧
More Pages to Explore .....