Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

KAMPUNI YA LAFARGE NA HOLCIM ZAUNDA KAMPUNI MOJA YA LAFARGEHOLCIM, ITAKAYOSHUGHULIKA NA VIFAA VYA UJENZI

$
0
0
Kiwanda cha saraji cha Lafarge kilichopo Mbeya. Kiwanda hiki ni maarufu kwa utengenezaji wa saruji, kokoto na zege.
Wafanyakazi wa kiwanda cha saruji cha Lafarge kilichopo Mbeya wakiwa kwenye picha ya pamoja. Lafarge ni mdau mkubwa katika bishara ya Saruji, Kokoto na Zege.

Kampuni mbili zinazoongoza katika sekta ya ujenzi hapa nchini, Lafarge S.A. na Holcim Ltd zimekamilisha muungano wao uliosubiriwa kwa muda mrefu na kuunda kampuni moja itakayo fahamika kwa jina la LafargeHolcim.

Vigezo muhimu vya kukamilisha muungano huo vimeafikiwa hivi karibuni kufuatia ubadilishaji wa umiliki pamoja na kutolewa kwa hisa mpya za Holcim kwenda kwa wanahisa wa Lafarge.

Wanahisa wa kampuni ya Holcim walipitisha azimio hilo la muungano katika mkutano mkuu uliofanyika Mei 8, 2015.  

SOMA ZAIDI HAPA

MSANII MAARUFU WA FILAMU AJIUNGA NA ACT WAZALENDO, KALENDA YA UCHUKUAJI FOMU YA CHAMA HICHO YATANGAZWA

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa (kushoto) akimkabidhi kadi msanii maarufu wa filamu nchini, Mohamed Mwikongi jina la sanaa 'Frank' alipotambulishwa mara baada ya kujiunga na chama hicho. Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa (kushoto) akimkabidhi kadi msanii maarufu wa filamu nchini, Mohamed Mwikongi jina la sanaa 'Frank' alipotambulishwa mara baada ya kujiunga na chama hicho.Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa (kushoto) akimkabidhi aliyekuwa Mwenyekiti wa kitengo cha vijana Taifa wa NCCR Mageuzi, Deo Meck alipotangazwa kujiunga na chama hicho rasmi leo jijini Dar es Salaam.Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa (kushoto) akimkabidhi aliyekuwa Mwenyekiti wa kitengo cha vijana Taifa wa NCCR Mageuzi, Deo Meck alipotangazwa kujiunga na chama hicho rasmi leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa (kushoto) akimkabidhi kadi na katiba msanii maarufu wa filamu nchini, Mohamed Mwikongi jina la sanaa 'Frank' alipotambulishwa mara baada ya kujiunga na chama hicho. Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa (kushoto) akimkabidhi kadi na katiba msanii maarufu wa filamu nchini, Mohamed Mwikongi jina la sanaa 'Frank' alipotambulishwa mara baada ya kujiunga na chama hicho.Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa akizungumza na waandishi wa habari leo alipowapokea baadhi ya wanachama wapya wa ACT-Wazalendo. Kushoto ni Katibu wa Kampeni na Uchaguzi, Mohamed Masaga na kulia ni Deo Meck mwanachama mpya wa ACT Wazalendo.Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Msafiri Mtemelwa akizungumza na waandishi wa habari leo alipowapokea baadhi ya wanachama wapya wa ACT-Wazalendo. Kushoto ni Katibu wa Kampeni na Uchaguzi, Mohamed Masaga na kulia ni Deo Meck mwanachama mpya wa ACT Wazalendo.



 Akizungumzia mchakato wa uchukuaji fomu kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho, Mtemelwa alisema Julai mosi mwaka huu Chama Cha ACT-Wazalendo kilifungua rasmi pazia la uchukuaji fomu za kugombea nafasi mbalimbali zikiweno za Udiwani, Ubunge na Urais. 

Alisema tangu kuanza kwa uchukuaji huo wa fomu kumekuwa na mwitikio mkubwa wa wanachama kuchukua fomu na hadi sasa kuna baadhi ya majimbo na kata zina watia azma kuanzia wanne mpaka tisa jambo ambalo alidai ni faraja kwa ACT Wazalendo. 
"Kati ya majimbo 265 yakiwamo majimbo mapya 26 yaliyoongezwa hivi karibuni na Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), ACT-Wazalendo tumeshakuwa na waweka azma zaidi ya mmoja katika majimbo 226 kwa nchi nzima na tunaamini mpaka kufikia mwisho wa uchukuaji fomu ndani ya Chama majimbo yote 265 yatakuwa yanawatia azma mbalimbali wanaosubiri kupitishwa na chama kwa ajili ya uchaguzi mkuu," aliongeza Naibu Katibu Mkuu huyo wa ACT Wazalendo. 
Alibainisha kuwa kichama mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu kwa nafasi ya udiwani ni julai 24, kwa nafasi ya Ubunge mwisho ni Julai 31 na kwa nafasi ya Urais mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Agosti Mosi, 2015. 
"Kwa ngazi ya Taifa Halmashauri kuu itakutana Agosti 13 kwa ajili ya kuteua jina la mgombea Urais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, pamoja na kupendekeza majina ya wagombea Urais kwenye mkutano mkuu,
Agosti 13, Mkutano mkuu utamchagua mtu atakayepeperusha bendera ya Chama cha ACT Wazalendo katika mbio za urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania." 
"Hivi karibuni tumepokea taarifa kutoka katika miji ya Tarime na Rorya Mkoani Mara kuwa kuna watu wanapita na kutangaza kuwa Chama chetu kimezuiwa kushiriki Uchaguzi kwa muda wa miezi sita. 
"Tumebaini lengo la upotoshaji huu ni kuwakatisha watanzania tamaa juu ya ukuaji wa Chama Cha ACT-Wazalendo pamoja na dhamira yake nzuri ya kuirudisha nchi katika misingi iliyoachwa na hayati Mwalimu Julius Nyerere. "Tunawataarifu wananchi kuwa Chama chetu kitashiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu kwa kuweka wagombea wa nafasi zote na Chama hakitakuwa tayari kuona sehemu yoyote ya nchi mgombea wa CCM anapita bila kupingwa," alisisitiza Naibu Katibu Mkuu huyo wa ACT Wazalendo.


WAKILI EMMANUEL TAMILA MAKENE AJITOSA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KINONDONI

$
0
0
Kada wa Chama cha Mapinduzi CCM na Wakili  wa siku nyingi, Emmanuel Tamila Makene (kulia) akipokea fomu za kugombea kuteuliwa kugombea kuteuliwa kuwania Ubunge Jimbo la Kinondoni katika uchaguzi Mkuu utakao fanyika Oktoba 25 Mwakahuu nchini kote. Makene ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Kinondoni amechukua fomu hiyo leo, Ofisi za Chama Kinondoni Mkwajuni Dar es Salaam.
Makene akisaini kitabu kabla ya kuchukua fomu hiyo leo katika Ofisi za CCM Wilaya ya Kinondoni.

 Makene akisikiliza maelezo kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni juu ya kanuni za kufuata kama muonesha nia.
Makene akionesha fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kugombea Ubunge jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CCM.

JARIDA LA WIKI NISHATI NA MADINI TOLEO LA 76

bbc dira ya dunia alhamis 16/07/2015

Dkt. John Pombe Magufuli na Mh. Samia Suluhu Hassan wapokelewa kwa shangwe Zanzibar

$
0
0
Wananchi na Wafuasi wa chama cha Mapinduzi CCM wakiwapokea kwa shangwe Mgombea Urais kwa tiketi ya chama hicho Dkt John Pombe Magufuli na Mgombea mwenza Mh.Samia Suluhu Hassan mapema asubuhi hii mara baada ya kuwasili mjini Unguja -Zanzibar kujitambulisha kwa chama na Wananchi kwa ujumla.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwa kwenye gari la wazi pamoja na mgombea mwenza Mhe.Samia Suluhu Hassan kwenye mitaa ya Michenzani Zanzibar.

Mhe. Magufuli aliwasili Zanzibar kwa lengo la kutambulishwa kwa wanachama wa CCM Zanzibar akiongozana na mgombea mwenza Mhe.Samia Suluhu Hassan ambapo wote kwa pamoja walipata kuwasalimia wananchi wa Zanzibar kwenye viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.


 Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Magufuli nje ya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar kwenye sherehe fupi ya kutambulishwa wagombea wa CCM kwa wanachama wa CCM.

 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John P.Magufuli pamoja na mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan wakiomba dua mbele ya kaburi la Hayati Abeid Aman Karume muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar.

 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Mhe. John Magufuli akiwasalimu wananchi waliojitokeza kwenye sherehe fupi za kumtambulisha kwenye viwanja vya Afisi Kuu CCM Zanzibar.

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

KIWANJA KIPYA CHA MAISHA CLUB BASEMENT CHAANZA KUPIGA MZIGO USIKU HUU

$
0
0
 Kiwanja  kipya cha Maraha kifahamikacho kwa jila la Maisha Club Basement kimeanza kupiga kazi usiku huu kwenye jengo jipya la LAPF, Makumbusho jijini Dar es salaam. Kiwanja hiki ambacho ni cha kisasa kabisa ni mbadala wa Maisha Club iliyokuwepo Masaki, hivyo sasa kila kitu kinapatikana hapa.
 Ndani ya Kiwanja hicho maalum kwa kuruka majoka kunaonekana namna hii.

THE STARS BAND KUZINDULIWA RASMI EID MOSI NDANI YA MZALENDO PUB

$
0
0
IMG-20150715-WA0008
Na Andrew Chale, Modewjiblog
Bendi mpya ya muziki wa dansi ijulikanayo kama The Stars Band iliyo chini ya Anneth Kushaba inatarajiwa kuzinduliwa rasmi Jumamosi ya Julai 18, siku ya Idd-Mosi ndani ya kiota cha Mzalendo Pub, Kijitonyama jijini Dar es Salaam huku ikitarajiwa kusindikizwa na mwanamuziki Barnabas pamoja na bendi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’

Kiongozi wa Stars Band, Kushaba anasema kuwa, tayari wapo katika mazoezi mbalimbali na ‘crew’ nzima ya bendi hiyo ambayo inaunganisha wanamuziki wenye uzoefu mkubwa katika uimbaji, upigaji vifaa na kushambulia jukwaa ndani na nje ya Tanzania.

“Wadau wa burudani ni nafasi ya kipekee kujitokeza kushuhudia uzinduzi wa bendi yao mpya iliyojaa kila aina ya burudani kuanzia uimbaji, kumiliki jukwaa na vyombo vilivyopangika.. burudani itakayoanza kuanzia saa moja jioni hadi majogoo” anasema Kushaba.

Anaongeza kuwa, uzinduzi huo pia utapambwa na bendi ya Fm Academia ‘Wazee wa NGWASUMA na mwanamuziki Barnabas Classic huku kiingilio mlangoni kitakuwa sh 10,000.

Kushaba anasema kuwa, miongoni mwa wanaounda bendi hiyo wapo wakali katika upande wa uimbaji kama Mao Santiago, Felly Kano, Alawy Junior, Khajanito (Khadija Maumivu) na Aneth Kushaba.

Kwa upande wa vyombo bendi hiyo inaundwa na mpiga drum wa zamani wa Twanga Pepeta, James Kibosho akiwa pamoja na Zaid Sato (Base), Othuman Majuto, Sebastian na Denis ‘Keyboard’, pamoja na Chacha ‘Tumba’.

Stars Band ndio inakuwa bendi ya kwanza ya dansi nchini kuja na mitindo mipya ya Utamaduni na bongo fleva (None stop!!) jukwaani.
Stars Band pia baada ya uzinduzi huo itakuwa inapiga kila Jumamosi ndani ya kiota hicho cha Mzalendo Pub.

ZIJUE SABABU KUMI KWA NINI NYWELE ZAKO ZINANYONYOKA

$
0
0
   
Kama umegundua  nywele  zako  zinanyonyoka, usi-panic. Sababu  inaweza  kuwa  rahisi. 
Inaweza kuwa  ni  ukosefu  wa  vitamin  au  sababu  za  kinasaba ( urithi ). Zifutazo  ni  sababu  kwa nini  nywele  zako  zinanyonyoka:
1. Stress
Kila  aina  ya   physical and emotional pain   inaweza  kusababisha  kunyonyoka  kwa  nywele.  . Ajali  ya  gari  au  kufanyiwa  upasuaji   vinaweza  kukusababishia  stress  ambayo  itakuletea kunyonyoka  kwa  nywele  zako.   Emotional stress  hazisababishi  kunyonyoka  kwa  nywele   lakini inaweza  kutokea  pale  unapokuwa  katika  wakati  mgumu  kisaikolojia  kama  vile  kumpoteza mtu  wako  wa  karibu  kutokana  na  kifo  au  kuachwa  kimapenzi. Hata  hivyo,. Baada  ya  wakati huo  mgumu, nywele  zako  zitaanza  kuota  tena   baada  ya  miezi  sita.
 2. Homoni
 Kunyonyoka  kwa  nywele  kunaweza  kuwatokea  wanawake  w alio  katika  menopause  kutokana na  kuadilika  kwa  viwango  vya   homoni.  Inaweza  kutokea  pia  kwa  wanawake  wanaotumia vidonge  vya uzazi  wa  mpango  hususani  wanapokuwa  wana  ahirisha  mara  kwa  mara  zoezi  la kutumia  vidonge  hivyo.  Unashauriwa  kama  unatumia  vidonge  kwa  uzazi  wa  mpango, basi hakikisha  unazingatia  ratiba  na  usiahirishe  hata  mara  moja.
3. Ukosefu  wa  Protini  au  Hamirojo
 Ukosefu  wa  protini  unaweza  kudhoofisha   ukuaji  wa  nywele au  kusababisha  kunyonyoka  kwa nywele kabisa  na  hatimaye  kuwa  na  kipara  kabisa.

Mkurugenzi TBL afanya ziara Daily News na Mwananchi

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa  kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL) Roberto Jarrin (kushoto) akisalimiana na Mhariri Mkuu wa kampuni ya magazeti ya serikali ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayochapisha magazeti ya Daily News ,Habari Leo na Spoti Leo,Bw.Gabriel Nderumaki(wa pili kulia) alipofanya ziara ya kutembelea ofisi hizo zilizopo eneo la Tazara barabara ya Sam Nujoma jijini Dar es Salaam, wengine pichani wa kwanza kushoto ni Afisa Uhusiano wa TBL Emma Oriyo aliyesimama nyuma kulia ni Meneja wa Media wa kampuni ya Aggrey&Clifford Bw.Oliver Mutere.
 Mkurugenzi Mkuu wa  kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL) Roberto Jarrin (kushoto) akibadilishana mawazo na Mhariri Mkuu wa kampuni ya magazeti ya serikali ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayochapisha magazeti ya Daily News ,Habari Leo na Spoti Leo,Bw.Gabriel Nderumaki(kulia) alipofanya ziara ya kutembelea ofisi hizo zilizopo eneo la Tazara barabara ya Sam Nujoma.
 Ujumbe wa TBL ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Roberto Jarrin katika mazungumzo na watendaji waandamizi wa kampuni ya Tanzania Standard wakiongozwa na Mhariri Mtendaji Gabriel Nderumaki.

Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Breweries Limited (TBL) Roberto Jarrin  (Kushoto) akitembezwa katika eneo la ofisi za kampuni ya Mwananchi Communications na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Bwana Francis Nanai (kulia)  alipofanya ziara kwenye ofisi za  kampuni hiyo zilizopo Mabibo Relini jijini Dar es Salaam wengine kwa nyuma ni Maofisa waandamizi wa kampuni ya Mwananchi.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Breweries Limited (TBL) Roberto Jarrin  (Kushoto) akipata maelezo ya jinsi habari za digitali zinavyotengenezwa kutoka kwa Mhariri Mkuu wa magazeti ya Mwananchi Bw. Bakari Machumu (kulia)  alipofanya ziara kwenye ofisi za  kampuni hiyo zilizopo Mabibo Relini jijini Dar es Salaam .

WAZIRI MKUU MHE MIZENGO PINDA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YA ELIMU WILAYANI MLELE

$
0
0
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa amekalia oja ya madwati mapya ya plastiki yaliyowekwa kwenye moja ya madara ya shuley amsingi ya Kakuni  wilayani Mlele akiwa katika mapumziko mafupi kijijini kwake Kibaoni Julai 16, 2015
Waziri Mkuu, Mizengo  Pinda akikagua ujenzi wa nyumba za walimu katika shule ya msingi ya Kakuni wilayani Mlele Julai 16, 2015. Picha na PMO

MDAU EMMA BARNABAS ACHUKUA FOMU KUWANIA UDIWANI KATA YA KIPAWA

$
0
0
 
Kada wa chama cha mapinduzi Emmanuel Barnabas Maro anayewania kuteuliwa na chama chake kugombea nafasi ya udiwani katika kata ya Kipawa wilayani Ilala jijini Dar akionesha fomu alizokabidhiwa leo na Katibu wa CCM wa kata ya Kipawa Amina Sebo hayupo pichani.

MWanahabari Kambi Mbwana achukua fomu ya ubunge Handeni Vijijini

$
0
0
Mwandishi wa Habari za Michezo na mdau wa maendeleo ya wilaya ya Handeni, Kambi Mbwana, mwenye fulana ya CCM, akikabidhiwa fomu ya kuwania Ubunge, Jimbo la Handeni Vijijini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu Msaidizi wa CCM wilayani Handeni, Asha Muya, wilayani Handeni, mkoani Tanga. Kulia kwa Mbwana ni Jerome Mhando, mmoja wa wadau waliomsindikiza katika tukio la uchukuaji fomu ya kuwania nafasi ya kuwatumikia wana Handeni. Picha na Mpiga Picha Wetu.


Na Mwandishi 

Wetu, Handeni

MWANDISHI wa habari za michezo na mdau wa maendeleo wilayani Handeni, mkoani Tanga, amejitokeza rasmi katika mbio za kuwania ubunge jimbo la Handeni Vijijini kwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Makabidhiano hayo ya fomu yalifanyika mbele ya Katibu Msaidizi wa CCM wilayani Handeni, Asha Muya, ikiwa ni siku chache baada ya milango ya uchukuaji fomu za kuwania nafasi za Ubunge na udiwani kufunguliwa rasmi.Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Mbwana alisema kwamba ameamua kujitokeza katika mbio hizo za ubunge ili afanyie kwa vitendo yale aliyokuwa anayapenda, hususan katika suala zima la maendeleo, huku wachache wao wakishindwa kuelewa faida ya harakati zake, zikiwapo zile za kuitangaza Handeni kwa njia mbalimbali.

Alisema wilaya yao imekuwa na changamoto kadhaa zinazohitaji nguvu za pamoja katika suala zima la shida ya kubwa ya maji, migogoro ya ardhi, ukosefu wa huduma bora za kijamii, hivyo kunahitajika jitihada na mipango ya pamoja kufanikishaji mambo hayo.

“Nilikuwa kimya kwa siku kadhaa nikiangalia akina nani wapo katika mchakato wa kuhitaji nafasi ya kuwatumikia wananchi wa Handeni Vijijini na kusikitishwa na watu wasioishi huku na wasiokuwa na uchungu wala dhamira ya kuwakwamua wananchi wakijitokeza kwa wingi kuwania nafasi ya ubunge, inaonyesha wapo kwa maslahi yao zaidi.


BASATA YAPIGA MARUFUKU DISKO TOTO NA UKIUKAJI WA SHERIA ZA UENDESHAJI KUMBI ZA SANAA NA BURUDANI KIPINDI HIKI CHA SIKUKUU YA EID-EL-FITR

$
0
0


download (9)
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambalo ni msimamizi wa sekta ya Sanaa na burudani nchini linawakumbusha wamiliki na waendeshaji wa kumbi za burudani kufuata sheria, kanuni na taratibu walizopewa kwenye vibali vyao vya uendeshaji wa kumbi.
Wanaelekezwa kuhakikisha wanakuwa na vibali halali vya uendeshaji wa kumbi zao, kuzingatia muda wa matumizi ya kumbi, kuepuka kelele zinazosumbua kwenye maeneo maalum hasa makazi ya watu na kuhakikisha ulinzi na usalama wa maisha ya watu.
Aidha, BASATA linawakumbusha wamiliki wote wa kumbi za burudani kwamba ni marufuku kukusanya watoto katika kumbi zao kupitia kile kinachoitwa ‘Disko Toto’ ili kuepuka maafa yanayoweza kujitokeza.
Uzoefu unaonesha kwamba, nyakati za sikukuu kama hizi wamiliki wa kumbi wamekuwa wakijisahau na kutamani kutengeneza faida katika biashara zao kiasi cha kuandaa disko kwa watoto hali mbayo imekuwa ikisababisha maafa makubwa ambayo yangedhibitika kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu.
BASATA kama mtoaji wa vibali vya kumbi za sherehe na burudani linasisitiza kwamba halitafumbia macho ukumbi wowote utakaokiuka maelekezo haya sambamba na kuruhusu maonesho machafu yenye kudhalilisha utu wa binadamu hasa yale yanayoonesha maungo ya ndani. Hatua kali na za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayekiuka maagizo haya.
BASATA linawatakia wasanii na wadau wote wa Sanaa sherehe njema ya Eid El Fitr na yenye furaha tele.

Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini
Godfrey Mngereza
KATIBU MTENDAJI

Rais Kikwete azungumza na Watanzania waishio Uswisi

$
0
0

 k
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na watanzania waishio  Switzerland katika hoteli ya Intercontinental jijini Geneva-Julai 16, 2015.
mail.google.com9
Watanzania waishio Switzerland.
j

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa ofisi ya mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa  Geneva jana baada ya kuzungumza nao na kisha kupata futari katika Hoteli ya Intercontinental jijini Geneva Uswisi.(picha na Freddy Maro)

MWANASHERIA MAKENE AREJESHA FOMU KUGOMBEA JIMBO LA KINONDONI

$
0
0
Mwansheria na Kada wa Chama cha Mapinduzi, Emmanuel Makene (katikati) akiwa ameambata na mkewe Dk. Sarah Makene kurejesha fomu za kuomba ridhaa ya wana CCM Kinondoni kuteuliwa kugombea Ubunge katika Jimbo la Kinondoni. Anaepokea fomu hizo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe. Wengine ni wapambe wa mgombea huyo waliomsindikiza kurejesha fomu hizo leo.
Emmanuel Tamila Makene ambae ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya na Katibu wa Usalama na Maadili taifa wa Umoja wa vijana (UVCCM) akisaini kitabu cha kurejesha fomu huku mkewe Dk Sarah Makene akimwangalia kwa makini na Katibu wa CCM Wilaya akikagua fimu. Dk Sarah Makene ni Daktari katika Hospitali ya Mwananyamala anaeshughulika na wagonjwa wa Ukimwi na wWaathirika na dawa za kulevya.
Dk Sarah Makene ni Daktari katika Hospitali ya Mwananyamala anaeshughulika na wagonjwa wa Ukimwi na wWaathirika na dawa za kulevya, akipeana mkono na Katibu wa CCM Wilaya baada ya kupokea fomu za Muwewe.

RAIS KIKWETE ATOA MKONO WA EID EL FITR KWA WATOTO YATIMA ,MAHABUSU YA WATOTO PAMOJA NA WAZEE WASIOJIWEZA

$
0
0
Watawa wa kituo cha kulea watoto yatima cha Mburahati wakipokea msaada wa Mbuzi,Mchele na Mafuta uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete, kutoka kwa Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii, Beatrice Fungamo katika hafla iliyofanyika leo katika Mahabusu ya Watoto Jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Kituo cha Darul Alqam, Shaban Mohamed akipokea msaada wa Mbuzi,Mchele na Mafuta uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete, kutoka kwa Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii, Beatrice Fungamo katika hafla iliyofanyika leo katika Mahabusu ya Watoto Jijini Dar es Salaam.
Kamishina Msaidizi wa Ustawi wa Jamii, Beatrice Fungamo akizungumza na waandishi wa habari juu ya msaada uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete. (picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii)

Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii

RAIS Jakaya Kikwete ametoa mkono wa Edd El-Fitri katitka vituo mbalimbali vya kulea watoto yatima pamoja wazee wasio na uwezo ili waweze kusherehekea sikukuu hiyo ambayo inatarajiwa kufanyika kesho.

Akizungumza na waandishi habari wakati wa kukabidhi zawadi hizo, kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete, Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii wa  Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ,Beatrice Fungamo  amesema kuwa kufanya hivyo ni utamaduni uliowekwa na Rais Kikwete kukumbuka makundi maalum katika siku za sikukuu.

Beatrice amesema zawadi hizo zimetolewa katika mikoa ya Dar es Salaam,Arusha,Kilimanjaro ,Mbeya,Morogoro ,Tanga,Pemba pamoja na Unguja. Ambapo zawadi hizo ni kama Mbuzi, Mchele pamoja na mafuta ya kupikia.

Amesema kwa waliopata msaada huo watumie vizuri katika kuwafanya watoto washerekee  sikukuu kama watu wengine.

President Kikwete meets WHO Director General Margaret Chan in Geneva

$
0
0
President Dr .Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with World Health Organization(WHO) Director General Margaret Chan at the UN Headquarters in Geneva this morning during an on going consultative sessions of the High Level Panel on the Global response to Health Crises.(photos by Freddy Maro)

NMB YAKABIDHI MADAWATI KWA SHULE YA MSINGI KISEKE

$
0
0
Mmoja wa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kiseke - Elias Sita anaye soma darasa la Nne, akifurahi pamoja na Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB - Bw. Waziri Barnabas baada ya shughuli ya makabidhiano ya madawati shuleni hapo.
Bw. Daniel Makorere, Afisa Elimu Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza  akimshukuru Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB Bw. Waziri Barnabas(kushoto) baada ya kupokea madawati yenye thamani ya shilingi milioni 5 kutoka benki ya NMB. Msaada huo wa madawati ulikabidhiwa kutoka NMB kwa Shule ya Msingi Kiseke ili kupunguza uhaba wa madawati unaoikumba shule hiyo. Wakishuhudia kutoka kulia ni Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa Bw. Abraham Augustino pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kiseke Bw, Denitrus Wima.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kiseke Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza, wakiwa wameketi kwenye madawati 64 yenye thamani ya shilingi milioni 5 waliyokabidhiwa na Benki ya NMB kama sehemu ya msaada kwa shule hiyo.

Kambi Mbwana achukua fomu ya ubunge Handeni Vijijini

$
0
0
Mwandishi wa Habari za Michezo na mdau wa maendeleo ya wilaya ya Handeni, Kambi Mbwana, mwenye fulana ya CCM, akikabidhiwa fomu ya kuwania Ubunge, Jimbo la Handeni Vijijini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu Msaidizi wa CCM wilayani Handeni, Asha Muya, wilayani Handeni, mkoani Tanga. Kulia kwa Mbwana ni Jerome Mhando, mmoja wa wadau waliomsindikiza katika tukio la uchukuaji fomu ya kuwania nafasi ya kuwatumikia wana Handeni. Picha na Mpiga Picha Wetu.

Kambi Mbwana ajitosa Ubunge Handeni Vijijini


MWANDISHI wa habari za michezo na mdau wa maendeleo wilayani Handeni, mkoani Tanga, amejitokeza rasmi katika mbio za kuwania ubunge jimbo la Handeni Vijijini kwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Makabidhiano hayo ya fomu yalifanyika mbele ya Katibu Msaidizi wa CCM wilayani Handeni, Asha Muya, ikiwa ni siku chache baada ya milango ya uchukuaji fomu za kuwania nafasi za Ubunge na udiwani kufunguliwa rasmi. Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Mbwana alisema kwamba ameamua kujitokeza katika mbio hizo za ubunge ili afanyie kwa vitendo yale aliyokuwa anayapenda, hususan katika suala zima la maendeleo, huku wachache wao wakishindwa kuelewa faida ya harakati zake, zikiwapo zile za kuitangaza Handeni kwa njia mbalimbali.

Alisema wilaya yao imekuwa na changamoto kadhaa zinazohitaji nguvu za pamoja katika suala zima la shida ya kubwa ya maji, migogoro ya ardhi, ukosefu wa huduma bora za kijamii, hivyo kunahitajika jitihada na mipango ya pamoja kufanikishaji mambo hayo.

“Nilikuwa kimya kwa siku kadhaa nikiangalia akina nani wapo katika mchakato wa kuhitaji nafasi ya kuwatumikia wananchi wa Handeni Vijijini na kusikitishwa na watu wasioishi huku na wasiokuwa na uchungu wala dhamira ya kuwakwamua wananchi wakijitokeza kwa wingi kuwania nafasi ya ubunge, inaonyesha wapo kwa maslahi yao zaidi.


“Hii haiwezi kukubalika, ukizingatia kwamba wananchi wameendelea kuishi maisha ya mashaka kwa kukosa maji safi, elimu, afya, michezo, utamaduni na mambo mengine yanayopaswa kufanyiwa kazi kwa kushirikiana na watu wote, wakiwamo viongozi wa kisiasa, watendaji wa serikali na Watanzania kwa ujumla,” alisema Mbwana.


Licha ya kuonekana mpya katika ulingo wa kisiasa hususan kwa nafasi ya ubunge, Mbwana anakumbukwa na kushukuriwa na wengi kutokana na mradi wake wa Tamasha la Handeni Kwetu linalofanyika kila mwisho wa mwaka, kuasisi Taasisi ya Handeni Kwetu Foundation, bila kusahau kuandika kitabu kinachojulikana kama Dira na Tumaini Jipya Handeni kilichopokewa kwa hisia tofauti, haswa kutokana na kilichoandikwa kwenye kitabu hicho.

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images