Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

TUME YA MIPANGO YATEMBELEA KIWANDA CHA MAFUTA YA ALIZETI SINGIDA

$
0
0
 Mkurugezi Mkuu wa Kiwanda cha kukamua mafuta cha Singida Fresh Oil Mills Khalid Omary (mwenye kanzu) akimwonesha Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Mha. Happiness Mgalula sindano iliyochambuliwa na mashine ya kuchambua uchafu kwenye alizeti inayoletwa kiwandani hapo. Anayetazama ni Mha. Omari Athumani, Mchambuzi Sera Mkuu, Tume ya Mipango  
 Baadhi ya wakulima wanaoleta alizeti kiwandani hapo wakisubiri huduma ya kukamua mafuta kiwandani hapo. Takribani asilimia 80 ya wakulima wanaoleta alizeti kiwandani hapo wanataka kukamua mafuta ambapo kiwanda kinawalipisha gharama ya kukamua lakini wao wanaondoka na mafuta yao. Jumla ya wakulima 500 wanaleta alizeti kiwandani hapo
 Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda cha kukamua mafuta cha Singida Fresh Oil Mills Khalid Omary akiwaonesha wajumbe wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Tume ya Mipango machine ya kukamua mafuta ya alizeti
 
 Baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha kupakia mafuta kwenye madumu wakiendelea kupakia mafuta ya ujazo wa lita tano kiwandani 
Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha kukamua mafuta cha Singida Fresh Oil Mills Khalid Omary akionesha dumu la mafuta yanayozalishwa na kiwanda chake tofauti na yale ambayo ni feki ambapo watu wasio waaminifu wanatumia nembo ya kiwanda hicho.  

BBC DIRA YA DUNIA JUMANNE 14.07.2015

HABARI TOKA VITUO VYA TELEVISHENI

MAGUFULI AJITAMBULISHA KWA WANANCHI WA JIJI LA DAR

$
0
0
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Dar es Salaam kwenye viwanja vya Zakheem Mbagala kwenye mkutano wake wa kujitambulisha kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambapo aliahidi kuwatumikia wananchi na kutenda haki.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wakazi wa jiji la Dar es Salaam kabla ya kumkaribisha mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli kujitambulisha na kuwasalimia wakazi wa Dar es Salaam.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akiwatambulisha viongozi mbali mbali waliomsindikiza mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli kwenye viwanja vya mikutano vya Mbagala Zakheem.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akipiga ngoma za tumba pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye kwenye jukwaa la bendi ya TOT mara baada ya kumaliza kujitambulisha na kuhutubia  wakazi wa jiji la Dar es Salaam.
Waandishi wa habari wakiwa kazini kwenye mkutano wa Dk. John Pombe Magufuli jijini Dar es salaam.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa mkutano wa Mbagala Zakheem tayari kwa kujitambulisha kwa wakazi wa Dar es Salaam.
 PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

SIMU TV: DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI ALIYOPOKELEWA NA KUHUTUBIA DAR ES SALAAM

Tanzania hosts dinner reception for Head of public services in the Commonwealth in Dar es salaam

$
0
0
Tanzania's Chief Secretary Amb. Ombeni Sefue (seventh from right) and Commonwealth Deputy Secretary-General Ms. Josephine Ojiambo (sixth from right) and Ag. Head of Tanzania Public Services Mr. HAB Mkwizu (third from left) pose with Head of public services from 18 African countries in the Commonwealth are gathered  in Dar es Salaam for a  major intergovernmental forum to improve the efficiency and impact of public services. This was on Monday night during a dinner reception hosted by Tanzania at the Akemi Restaurant.
The Forum of Commonwealth Heads of African Public Service is convened by the Commonwealth Secretariat and hosted by President Dr Jakaya Mrisho Kikwete of the United Republic of Tanzania.
The theme of the forum is ‘From Good Plans to Effective Execution: Anchoring Policy Coherence, Strategy and Execution for a High Performance Culture in the Public Service’.

Speakers include heads of public services, permanent secretaries and chairs of public service commissions, as well as senior representatives of organisations such as the African Union and UONGOZI Institute of African Leadership for Sustainable Development. For more pictures CLICK HERE


POLISI MKOANI DODOMA WAFAFANUA KUHUSU MABAURUNGUTU YA NOTI YALIYOKUTWA KWA MFANYABIASHARA

$
0
0

Kamanda wa Polisi Mkoa wa 

Dodoma, SACP David Misime


Napenda kutoa taarifa fupi kuhusu tukio lililotokea tarehe 11/07/2015 majira ya saa 10:00 hrs huko katika Hoteli ya St. Gasper hapa mjini Dodoma, kuwa wananchi walitoa taarifa majira ya saa nne asubuhi kwamba kuna mtu mmoja mwenye asili ya Kiasia amekamatwa na wananchi akiwa na fedha nyingi na kuna vurugu kubwa. 
Baada ya kupata taarifa hizo Jeshi la Polisi Mkoani hapa lilifika eneo la tukio ili kuona kama taarifa hizo ni za kweli. 
Askari walithibitisha kuwa ni kweli walimkuta mtu mmoja mwenye asili ya Kiasia ambaye alijulikana kwa jina la AMIT KEVALRAMANI mwenye umri wa miaka 31, Mhindi, Mfanyabiashara, Mkazi wa Dar es Salaam   akiwa na fedha kiasi cha Tshs. 722,500,000/= ambacho alipohojiwa alisema kuwa tarehe 10/07/2015 alifika Dodoma kwa ajili ya ununuzi wa mazao ya nafaka. 
Alipofika Dodoma tarehe 10/07/2015 majira ya asubuhi alifikia katika Hoteli ya St. Gasper na tarehe 11/07/2015 aliamua kurudisha fedha benki kutokana na kuona mkusanyiko wa watu wengi wasioeleweka na wenye viashiria vya vurugu. 
Akiwa katika harakati ya kurejesha fedha hizo benki, ndipo kundi la watu waliokuwa katika eneo la Hoteli ya St. GASPER walimtilia mashaka na kumzuia asiondoke na ndipo taarifa zilitolewa polisi. Mashaka ya watu hao yalitokana na vuguvugu za kisiasa/mchakato wa uchaguzi kati ya makundi mbalimbali kuwa kuna watu wanahonga wajumbe. Taarifa za aina hiyo ambazo hata Jeshi la Polisi lilikuwa limepokea bila uthibitisho. 
Katika tukio hili na uchunguzi tulioufanya tumebaini kuwa hakuna kosa la jinai lililothibitika licha ya kukutwa na kiasi hicho cha fedha, tuhuma za rushwa ambazo ndiyo zilikuwa msingi wa ukamataji wa mtu huyo hazikuthibitika, kwa kuwa hakuna aliyeona akizigawa fedha hizo wala hakuna aliyedai kushawishiwa au kugawiwa fedha hizo. 
Aidha imethibitika fedha hizo ni mali yake halali na kwa kuwa hakuna ushahidi mwingine uliyo thibitisha vinginevyo amerejeshewa fedha zake.


mtangazaji mahiri wa ITV na Radio One Isaack Muyenzwa Gamba ahamia DW Ujerumani

$
0
0
Aliyekuwa mtangazaji wa ITV na Radio One Isaack Muyenzwa Gamba (wa pili kulia) akiwa na watangazaji wakongwe wa DW jijini Bonn, Ujerumani alikohamia hivi karibuni. Wengine kutoka kulia ni Mohamed Dahman, Sudi Mnete, Sekioni Kitojo, Abdul Mtulya na mdau.

MONUSCO YAHITAJI USHIRIKIANO ZAIDI NA MAMLAKA ZA DRC

$
0
0
 Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika DRC  Bw. Martin Kobler akiwasilisha taarifa mbele ya  Baraza  Kuu la  Usalama  la Umoja wa  Mataifa siku ya  Jumanne kuhusu  mchakato wa  uchaguzi mkuu, hali ya   usalama na  mkakati wa kupunguza  walinzi wa amani. na   Kueleza kwamba utekelezaji  wa mamlaka ya MONUSCO  unahitaji ushirikiano endelevu kati yake na  mamlaka za DRC
Mwenyekiti wa  Kamati ya  Vikwanzo dhidi ya  Jamhuri ya  Kidemokrasia ya Kongo,   Dina Kawar akiwasilisha taarifa ya Kamati yake mbele ya Baraza Kuu la Usalama  la Umoja wa  Mataifa, ambapo pamoja mambo mengine  ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa  kumkamata na kisha kumpeleka nchi Uganda  kiongozi la kundi la  wanamgambo la Allied Democratic  Forces ( ADF) Bw. Jamil Mukulu ambaye alikuwa katika orodha ya watu waliowekewa vikwazo na   Kamati hiyo. 

TANZANIA YAELEZEA MATUMAINI YAKE KWA MKUTANO WA UFADHILI WA MAENDELEO

$
0
0
Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Saada  Mkuya Salum akizungumza  katika siku ya pili ya mkutano wa tatu wa kimataifa kuhusu ufadhili wa  maendeleo ( FFD3) unaoendelea jijini Addis Ababa- Ethiopia.

Na   Mwandishi Maalum, 
New York

Mkutano wa tatu wa kimataifa  kuhusu ufadhili wa maendeleo, ( FFD3) jana (jumanne) umeingia siku yake   pili ambapo  Waziri wa  Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Saada   Mkuya Salum alielezea matumaini ya   Tanzania  juu ya matokeo ya mkutano huo katika kusukuma mbele ajenda ya maendeleo endelevu.
 Waziri   wa Fedha ambaye anamwakilishi  Mhe. Rais Jayaka Mrisho Kikwete katika mkutano huo,  amesema kuwa,  Tanzania  inaamini  kwamba ufadhili wa  maendeleo ni moja ya ajenda muhimu kwa Bara la Afrika .  Kwa sababu hiyo Tanzania,   inategemea  kuona ufadhili huo  unakuwa na  matokeo makubwa   katika kuondoa umaskini katika   nchi nyingi za Afrika. Taarifa kamili BOFYA HAPA

UPDATES YA UKAWA USIKU HUU: MGOMBEA URAIS WA UKAWA KUTANGAZWA NDANI YA SIKU SABA

$
0
0
Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA umesema kuwa mgombea wao wa Urais watamtoa baada ya siku saba.

Akizungumza na Waandishi wa Habari usiku huu,Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, Mhe. James Mbatia amesema kuwa kuchukua muda mrefu kwa kikao hicho imetokana na kuandaa utaratibu jinsi ya kumtoa mwali wao  wa Urais kwa tiketi ya UKAWA aliye bora. Amesema kuwa mkutano huo pia umechukua muda mrefu  kutokana na mambo mengi ikiwemo mgawanyo wa majimbo.

Afisa Habari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Tumaini Makene akizungumza na waandishi habari  hivi punde juu kinachoendelea katika mkutano wa kutafuta mgombea wa Urais kwa tiketi ya UKAWA, uliofanyika katika Hoteli ya Colesseum jijini Dar es Salaam,Makene amesema majadiliano hayo sio urais tu bali kuna mipaka ya majimbo mapya jinsi watavyojipanga katika kushiriki uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu. Makene amezidi kuwataka waandishi wawe na subira kusubiri maamuzi yatakayotoka katika kikao hicho ambacho kimeanza tangu asubuhi ya leo. 
Baada ya kusubiri kwa muda mrefu tangu mchana,Waandishi wa Habari waliopiga kambi wakisubiri kupata jina la mgombea Urais kwa tiketi ya UKAWA katika Hoteli ya Colosseum Masaki leo jijini Dar es Salaam,wakajikuta wanaacha stendi za Camera zao na kukaa pembeni wakisubiri lolote litakalojiri.
Waandishi wa Habari wakiwa wameweka kambi tangu saa saba mchana wakisubiri kupata jina la mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA katika Hoteli ya Colosseum Masaki leo jijini Dar es Salaam, hiyo inatokana na taarifa zilizotolewa na UKAWA kuwa leo ndio siku rasmi ya kutangaza jina hilo lakini masaa yanazidi kwenda huku kikao chao kikiwa kinaendelea.
Waandishi wakisubiri mtu wa kutoa taarifa juu ya jina la mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA, ambapo taarifa hizo za kuja mtu huyo ziligonga mwamba na kuambiwa kilichobaki ni makubaliano suala jinsi kuendesha uchaguzi katika majimbo.

CYBER DEFENCE EAST AFRICA 2015 SUMMIT “PROTECTING THE INTERCONNECTED WORLD”

$
0
0

 NRDEA in collaboration with TCRA together are organizing the Cyber Defense East Africa Summit which will be held at Mlimani City Conference Hall from 11thto 13th August 2015 with the theme “PROTECTING THE INTERCONNECTED WORLD. The guest of honor will be Hon.Ambassador Ombeni Sefue the Chief Secretary to the Cabinet and head of the public service. Experienced   Speakers on Business transformation, technology and cyber security from within and outside the country will attend and   speak at the event.  

 Business leaders including CEOs’, Directors, CIOs’, CFOs’, Auditors, lawyers; information security experts from various industries in east Africa will also exchange their business knowledge and network with the rest of the participants. 

With over 6 leading security and technology vendors/companies in the world will be available for exhibition and showcase their product with open discussion from any participants.

To get a ticket call +255 719 253 037 / +255 222 110 895 or send an email to info@nrd.co.tz



UK offers security equipment to Tanzania Civil Aviation Authority

$
0
0
Acting UK High Commissioner to Tanzania Ms Penny Smith hands over aviation security equipment to Director General of Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA), Mr. Charles Chacha

Acting  UK High Commissioner to Tanzania Ms. Penny Smith hands over a certificate to one of the participants of the training course.


Acting UK  acting High Commissioner to Tanzania Ms Penny Smith giving her keynote address during closing of training course and handling of aviation security equipments along side are Vicky Hutchinson (RASLO) and TCAA Director General, Mr Charles Chacha and Director Safety Regulations, Mr Redemptus Bugomola (dressed in tie)
 D&T Certified Trainer, Mr. Simon C. Bolt show-case the usage of one of the aviation security equipment . Looking are; Vicky Hutchinson, (RASLO), Acting High Commissioner, Ms. Penny Smith and Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) Director General, Mr. Charles Chacha.

CCM TAWI LA CHINA WAPONGEZA UTEUZI WA DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KUGOMBEA URAIS

$
0
0
CCM TAWI LA CHINA TUNATOA PONGEZI KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA, WAJUMBE WA KAMATI YA MAADILI NA USALAMA, KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA, HALMASHAURI KUU YA TAIFA NA MKUTANO MKUU WA TAIFA KWA KUTUPATIA MGOMBEA MWADILIFU, MAKINI, MZALENDO WA KWELI NA MCHAPAKAZI HODARI AMBAYE ATAPEPERUSHA BENDERA YA CHAMA CHETU KWA NAFASI URAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA 2015, TUNATARAJIA KUPATA USHINDI WA KISHINDO. HONGERA SANA MH. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI ( JEMBE ). WEMBE KULIKO ULE USHINDI.......................................!

VIONGOZI WA CHAMA CHA ACT WAZALENDO WAALIKWA UJERUMANI

$
0
0
MWENYEKITI wa Chama cha ACT Wazalendo mama Anna Mghwira (kulia) akiongozana na katibu mkuu  Ndugu samson mwigamba na katibu wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa ndugu Venance Msebo leo tarehe 15 julai 2015 wameanza ziara ya siku saba nchini ujerumani kwa mwaliko wa chama rafiki cha kijamaa (Die Linke Party).

Katika ziara hiyo pamoja na kutembelea die linke party, watapata fursa ya kutembelea ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani na pia watafanya mkutano na watanzania wanaoishi nchini ujerumani.
 katika mikutano hiyo na watanzania waishio nchini Ujerumani lengo kuu litakuwa kuwahamasisha kuchangia maendeleo ya nchi yao na pia kutafuta fursa kurudi nyumbani kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura pamoja na kupiga kura ifikapo Oktoba mwaka huu.

Imetolewa na Afisa Habari,
ACT Wazalendo
Abdallah Khamis
15 julai 2015

nyalandu arudi jimboni kutetea kiti chake cha ubunge singida kaskazini

$
0
0
 Waziri wa Maliasili na Utalii ambayre ni Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro nyalandu akizungumza katika kijiji cha Muvae wilayani Singida juzi alipokwenda kutangaza nia ya kutetea kiti chake katika uchaguzi mkuu ujao.
 Waziri wa Maliasili na Utalii ambayre ni Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro nyalandu akizungumza katika kijiji cha Muvae wilayani Singida juzi alipokwenda kutangaza nia ya kutetea kiti chake katika uchaguzi mkuu ujao.
 Waanchi wa kijiji cha Muvae wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii ambayre ni Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro nyalandu juzi alipokwenda kutangaza nia ya kutetea kiti chake katika uchaguzi mkuu ujao.
Waanchi wa kijiji cha Muvae wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii ambayre ni Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro nyalandu juzi alipokwenda kutangaza nia ya kutetea kiti chake katika uchaguzi mkuu ujao.

Kipindi cha Niambie Live

$
0
0
Karibu kwenye kipindi hiki cha NIAMBIE LIVE
Kipindi kinachozungumzia mambo mbalimbali yaliyochukua nafasi za juu kwenye mitandao ya kijamii.
Wiki hii mada ni SIKU YA KINABABA DUNIANI.
Na mgeni mwalikwa ni Mayor Mlima
Ni Niambie Live....
KARIBU

KILIMANJARO FILM INSTITUTE

NORWAY GRANTS UN TANZANIA 3.1 MILLION US DOLLARS to support the UN’s Refugees response, governance initiatives, and UN Partnership Building in Zanzibar

$
0
0
IMG_2156_1
Ambassador of Norway, H.E Hanne-Marie Kaarstad, (left) and UN Resident Coordinator, Mr. Alvaro Rodriguez, signing agreement of USD 3.1 million for Grants to support the UN’s Refugees response, governance initiatives, and UN Partnership Building in Zanzibar as well as on Human Rights, at the ceremony which was held at the UN offices in Dar es Salaam.
------------------------------
*Refugees and Governance programs among key areas of support
The Norwegian Embassy today has signed an agreement with One UN Tanzania to release USD 3.1 million (approximately 6.9 billion Tshs).The signing ceremony was held at the UN offices in Dar es Salaam between the Ambassador of Norway H.E Hanne-Marie Kaarstad and the UN Resident Coordinator Mr. Alvaro Rodriguez. The contribution will focus on providing support to the UN’s refugee response, governance initiatives, and UN partnership building in Zanzibar as well as on human rights.
Emphasizing on the Embassy support to the One UN, Ambassador of Norway H.E Hanne-Marie Kaarstad stated that Tanzania has set a good example of UN Agencies working together with coherence, efficiency and effectiveness. 
She added; “The UN has always been a vital and highly valued partner for Norway. The implementation of the new Sustainable Development Goals, which we hope will be adopted by the UN General Assembly in September, will require hard work. It is not business as usual and requires concerted efforts from us all. We wish to support the UN in assisting the people and the Government of United Republic of Tanzania in their effort to achieve these goals and fulfil their international obligations, including giving a voice to the most marginalised and vulnerable.”
IMG_2163
Ambassador of Norway, H.E Hanne-Marie Kaarstad, (left) and UN Resident Coordinator, Mr. Alvaro Rodriguez, shake hands after affirming their signatures on the agreement.
Thanking the government and people of the Kingdom of Norway for their continued support, the UN Resident Coordinator, Mr. Alvaro Rodriguez, stated that Norway has been a supportive and constructive partner of One UN and Tanzania for decades. “The contribution of USD 3.1 Million will be used to strengthen partnerships, enhance democratic governance interventions by UN agencies and provide urgent relief to Burundian refugees in Tanzania”. He added that the One UN looks forward to a continued collaboration with Norway in the years to come.
Norway has been a major supporter of the UN reform agenda and the upcoming Sustainable Development Goals (SDGs) and with other development partners, is committed to the development vision of the government and the people of Tanzania.

ALL WHITE PARTY YA WABONGO HOUSTON TX JUMAMOSI HII

$
0
0
Jumamosi Hii Ndani ya Houston Texas USA 18th (Eid El Fitri) "MoFLAVA ALL WHITE PARTY/TOUR" @ PURE, 505 Main TX 77002 (Downtown Houston). Hosted by Zey Misstanga. $400 for VIP section of 8 people ( 2 Bottles, Snacks & Cover). Regular entry $20 per person. ‪#‎RedCarpet‬ event. Dresscode: Strictly "ALL WHITE". Buy advance ticket here http://allwhitehouston.eventbrite.com/?s=40265011 ‪#‎Bolingo‬‪#‎Mayenu‬ ‪#‎Naija‬ #‎BongoFlava‬ ‪#‎Genge‬ ‪#‎Oldskool‬ (80s, 90s & 00s) ‪#‎Hiphop‬‪#‎House‬ ‪#‎Taarabu‬ ‪#‎Mipasho‬ & ‪#‎EDM‬. KARIBUNI WOTE!
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images