Na Mwandishi wetu,Globu ya Jamii
KUONGEZEKA kwa ndoa za utotoni inatokana na sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kuendelea kutumika wakati hali yake ni mbaya kwa watoto wakike kushindwa kufikia ndoto zao.
Akizungumza na katika mdahalo wa Nijali uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Regency ,Mratibu wa Utetezi Taifa ,SOS Tanzania/Zanzibar ,John Batista amesema kuongezeka kwa mimba za utotoni inatokana na sheria ya ndoa kuendelea kutumika.
Amesema kuwa kuendelea kwa mimba za utotoni pamoja kuolewa kunatokana sheria kutamka kuwa mtoto anaweza kuolewa kwa miaka 14 kwa ridhaa ya wazazi.
Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya Watu (UNFPA) inaonyesha watoto 1,3822 ambao wamezaliwa katika mwaka 2005 na 2010 ifikapo 2030 watakuwa wameolewa chini ya miaka 18.
Katika ripoti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inaonyesha wasichana 8000 wanapata ujauzito wakiwemo wanafunzi wa Shule ya msingi 3000 na ,sekondari 5000.
Mratibu wa C-SEMA,Michael Kihongoh amesema kampeni hii ni endelevu na waandishi wametakiwa kuweka kipaumbele kupigania sheria ya ndoa ya mtoto kuondolewa kabisa ili watoto wa wakike waweze kulindwa.
Amesema kuwa watoto wa kike wako katika hatari ambapo elimu inatakiwa kutolewa kwa jamii ikiwemo malezi kwa waoto wa kike wasiweze kuingia katika vishawishi.
Mratibu wa Utetezi Taifa, SOS Tanzania/Zanzibar, John Batista, akizungumza katika Mdahalo wa Nijali uliolenga ndoa za utotoni na mimba za utotoni kwa kushirikisha Chama cha Waandishi wa Habari za Watoto, (TAJOC) na wengine, uliofanyika leo katika Hoteli Regency jijini Dar es Salaam. Mshauri Mkuu Mwandamizi na Msimamizi wa Huduma ya Simu kwa Mtoto wa C-SEMA, Fatuma Ahmad akizungumza na waandishi wa habari katika mdahalo wa Nijali uliofanyika katika leo Hoteli ya Regency Jijini Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Watoto (TAJOC), Chalila Kibuda akizungumza na waandishi wa habari katika mdahalo wa Nijali uliofanyika katika leo Hoteli ya Regency Jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa Mdahalo wa Nijali ulioshirikisha Chama cha Waaandishi wa habari za Watoto (TAJOC) na wadau wengine uliofanyika leo katika Hoteli ya Regency jijini Dar es Salaam.