Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

PPRA YAWAPIGA MSASA WAFANYAKAZI WA TIA KUHUSU SHERIA MPYA YA MANUNUZI JIJINI DAR

$
0
0
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania(TIA) Dkt.Joseph .M.Kihanda mwenye suti nyeusi(waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo maalum kuhusu sheria mpya ya manunuzi ya umma yaani PPA 2011 na kanuni zake PPR.2013 ambao ni wadau wa kitengo cha manunuzi kinachosimamiwa na Bi.Juliana Musomi,Pius Seda,Salha Tego,Dickson Biya,Ezra Obilla,Kennedy Ndosi,Zubeda Mohamed,Alton Kumburu  na Stephen Mahinya),wajumbe wa bodi ya zabuni ya Taasisi hiyo ambao ni Bw.Zodo .M.Zodo,Bi.Linah Tumwidike,Bajjet Naresho,Anthony Mzurikwao,Said Mayunga,Lucina Comino na Burkad Haule pamoja  na wawezeshaji toka Mamlaka ya udhibiti wa ununuzi wa umma (PPRA) ambao ni Bw.Gilbert Kamnde akishirikiana na ,Onesmo France,pia washiriki wengine walikuwa ni mkurugenzi wa biashara wa Taasisi hiyo Bw.Mzee Boma na  mameneja wote wa matawi ya Taasisi hiyo ambao ni  Ndugu John Boneka(Kigoma)Bw.Emmanuel Kingu (Singida),Luciana Hembe Mwanza)Bw.Mugisha Kamala (Mbeya na Bw.Matei Mapunda(Mtwara).
Wasiriki wakiwasikiliza wawezeshaji kabla ya kumalizika kwa mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa baraza la maaskofu wa kanisa katoliki Tanzania T.E.C Kurasini jijini Dar es Salaama kwa siku tano kuanzia tarehe 25/5/2015 hadi tarehe 29/5/2015 ambapo washiriki watatunukiwa vyeti vya mahudhurio toka PPRA.
Mkuu wa kitengo cha Manunuzi wa Taasisi hiyo akiwa anaendelea kufuatilia kwa makini mafunzo hayo ambapo amekiri yatasiadia kuongeza ufanisi katika kitengo chake na Taasisi kwa ujumla hivyo kuomba Afisa mtendaji mkuu kuwawezesha mafunzo mbalimbali yanayohusu manunuzi ili Taasisi iendelee kufanya manunuzi kwa kuzingatia thamani ya pesa yaani '' Value for Money Procurement'' na kuiletea Taasisi Sifa nje na ndani ya Nchi kwani inatoa pia mafunzo katika ngazi ya cheti hadi Postgraduate kwa masomo hyo ya ugavi,ughasibu na mengine mengi katika nynja ya biashara.
\
Hivyo ni wito pia kwa watanzania wote wanaohitaji kusomesha watotot wao katika chuo kinachotambuliwa na serikali kuwaleta watoto wao waje kusoma TIA...kwa maelezo zaidi na form za kujiunga chuo bonyeza hapa chini..





TAARIFA RASMI KUTOKA KWA KAMATI YA JUMUIYA NA USULUHISHI WA MIGOGORO

$
0
0
Kufuatia mgogoro  wa kisiasa, jaribio la kumtoa madarakani Raisi wa Jamhuri ya Burundi, Pierre Nkurunziza na maelfu ya wananchi wa nchi hiyo kukimbilia nchi jirani za Tanzania na Rwanda. Hali ya kambi zinazopokea wakimbizi zinaonekana kuelemewa na kupelekea kuhatarisha hali za wakimbizi hao.

Kutokana na hali hiyo, Bunge la Afrika ya Mashariki kupitia kamati yake ya Masuala ya Jumuiya na Usuluhishi wa Migogoro imeteua wajumbe watakaokwenda kutembelea kambi hizi zilizopo Kigoma-Tanzania na Mashariki mwa nchi ya Rwanda kwa madhumuni yafuatayo;

1.     Kujiridhisha na hali ya mazingira ya kambi hizo na kuangalia mipango kutatua mgogoro huo.
2.     Kuangalia na kutimiza jukumu la Bunge la Afrika Mashariki kupata suluhisho la kudumu la mgogoro ulioko sasa nchini Burundi.
3.     Kuwatemebelea na kuwafariji wananchi wote wa Burundi walioko kwenye kambi hizo.

Wajumbe wa kamati teule wamegawanyika katika makundi mawili, wajumbe watakaokwenda Kigoma-Tanzania wataongozwa na Mhe. Abdullah Mwinyi ambae ni menyekiti wa kamati hiyo na wajumbe watakaokwenda Mashariki mwa Rwanda wataongozwa na Mhe. Abubakar Zein.

Imetolewa na;
Mhe. Abdullah Mwinyi
(Mwenyekiti wa Kamati ya masuala ya Jumuia na Usuluhishi wa Migogoro)

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA KUAPISHWA RAIS WA NIGERIA LEO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na mtoto Ernest Nkayala alipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Mkewe Mama Asha Bilal, wakiwasili kwenye Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea shada la maua kutoka kwa Mtoto Elin Mwandobo alipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia ngoma za kabila la Kinigeria alipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
(Picha na OMR).

Maadhimisho ya SIKU YA AFRIKA yafanyika Washington DC

$
0
0
Balozi wa Misri nchini Marekani Mhe. Mohamed Tawfik akiongea kufungua sherehe ya African Union iliyofanyika siku ya Alhamisi May 28, 2015 katika hotel ya JW Marriott, Washington DC
Balozi wa Morocco nchini Marekani Mhe. Rashad Bouhlal akiongea machahce.
Msemaji mkuu wa sherehe ya siku ya Afrika Mhe. Donald Tetelbaum.
Mchungaji Jesse Jackson akiongea kwenye sherehe ya siku ya Afrika.
Mambalozi wa Afrika nchini Marekani wakiwa katika picha ya pamoja
Wageni waalikwa wakifuatilia hotuba.

WANAHABARI MKOA WA IRINGA NA POLISI WAKUTANA KATIKA KIKAO CHA MAHUSIANO MEMA

$
0
0
Baadhi ya wanahabari  mkoa  wa Iringa  wakiwa katika picha  ya pamoja na viongozi  wa  jeshi la polisi mkoa wa Iringa mara baada ya  kumalizika  kikao  chao cha mahusiano mema na kutambulishana kati ya wanahabari na viongozi wapya wa  jeshi  la Polisi waliokaa ni kamanda wa polisi Ramadhan Mungi wa tatu  kushoto akifuatiwa na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) Frank Leonard na katibu wa IPC Francis Godwin na maofisa wengine wa polisi mkoa.
 Na FG BLOG.
Wanahabari wa mkoa wa Iringa leo wamekutana na kamanda wa polisi na maofisa wa jeshi la polisi Mkoani hapa ili kuendelea kufanya Kazi kwa ushirikiano kwa faida ya Mkoa wa Iringa.

Katika kikao hicho kilichoambatana na semina fupi ya kukumbushana wajibu wa Kazi za wanahabari na askari.

Akitoa mafunzo hayo kamanda wa polisi wa Mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi amesema kuwa ili kuufanya Mkoa wa Iringa uweze kufanikiwa ni lazima wabahabari na polisi kufanya Kazi zao kwa kuzingatia maadili na kutofanya upendeleo katika utendaji wao.

Mungi alisema kuwa mbali ya kazi kubwa ambazo vyombo vya habari mkoani hapa vinafanywa bado jeshi lake limeamua kukutana na wanahabari hao ili kizidi kuufanya Mkoa kuwa na taswira nzuri ktk mahusiano Kati ya pande hizo mbili kama njia ya kuwatumikia wananchi.

Alisema kwa Mkoa wa Iringa vyombo vya habari vimeonyesha mchango mkubwa zaidi zaidi na kutaka mchango huo na jitihada hizo kuendelea zaidi .

Kamanda Mungi amesema kuna haja ya wanahabari na askari polisi kuendelea kujenga mahusiano kwa kukutana na viongozi wao kabla ya kufanya mapambano yasiyo na tija.

Alisema kuwa wao kama jeshi la polisi wanatambua kuwa vyombo vya habari ni muhimu kwa jamii hivyo lazima kujenga mahusiano mema na kuwa askari polisi hawanasababu ya kuendeleza mivutano 

Alisema kuwa kuna wakati mwingine ajali imetokea na Kazi ya mwanahabari ni kuhabarisha umma na polisi kuokoa hivyo lazima kufanya Kazi kwa karibu na kutoa majibu stahiki kwa wanahabari na wanahabari kutotumia jazba katika utendaji Kazi zao .

ANDIKENI WOSIA KUEPUSHA MIGOGORO - WAZIRI MKUU

$
0
0
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka Watanzania wote nchini wajenge tabia ya kuandika wosia ili kuondoa matatizo ya mirathi pindi mume anapoaga dunia.

Ametoa wito huo leo mchana (Ijumaa, Mei 29, 2015) wakati akizindua kampeni ya kuandika wosia kwenye maadhimisho ya miaka 25 ya Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) yaliyofanyika katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya kushuhudia uandishi wa wosia mbele ya wakili, Waziri Mkuu alisema uandishi wa wosia ni suluhisho la migogoro mingi inayosababishwa na wanandigu ambao wakati mwingine wala hawakushiriki kuchuma mali wanayogombea.

“Kuandika wosia siyo uchuro kama ambavyo watu wengi wanadhani… ninatoa kwa Watanzania kuandoak wosia mapema kwani inasaidia kuondoa matatizo ya mirathi baada ya mmoja wao kuondoka duniani,” alisema.

“Mtua anapaswa kutamka mali nilizonazo ni kadhaa na endapo nitakufa mali hii apewe fulani, na hii fulani na nyingine fulani. Hati hii inapaswa kutunzwa kwa mwanasheria, benki au kwa Kabidhi Wasii. Tusipolifanya hili, matatizo yataendelea kuwakumba wajane na watoto walioachwa na marehemu,” alisema.

Aliipongeza TAWLA kwa kuchukua jukumu la kuhamasisha umma kuhusu suala la uandishi wa wosia lakini pia akawataka wanachama wa TAWLA wajikite zaidi kwenye kutetea haki za makundi maalum kama walemavu wa ngozi, vikongwe na watu kutoka makabila madogodogo. “Haya makundi yana shida zao ambazo hazifanani na watu wengine. Nendeni vijijini, mkatoe elimu, jueni changamoto wanazokabiliana nazo, wasikilizeni shida zao na muone ni njia gani mnaweza kuwasaidia,” alisema.


TAASISI ZA SERIKALI ZAASWA KUBINI MBINU MKAKATI KATIKA UFANISI WA KAZI-BALOZI SEIF ALI IDDI

$
0
0
Na Othman Khamis Ame Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Watendaji wa Taasisi za Serikali wana wajibu wa kutumia vipaji walivyojaaliwa kuwa navyo katika kubuni mbinu na mikakati watakayohisi kwamba inaweza kutaleta faida na ufanisi katika maeneo yao ya kazi sambamba na Serikali  Kuu kwa jumla.

Alisema faida ya ubunifu watakaoutumia watendaji hao utaongeza kasi ya uwajibikaji endapo wataendelea kushikamana baina yao katika kufanya kazi kwa juhudi, maarifa na nidhamu kwa kutumia vipaji hivyo.

Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati wa hafla maalum ya chakula cha usiku alichowaandalia watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi yake kufuatia kukamilisha  na hatimae kupita kwa Bajeti ya Wizara hiyo pamoja na kuagana baada ya kufanya kazi pamoja katika kipindi chote cha miaka mitano tokea mwaka 2010.

Hafla hiyo ya chakula cha usiku iliyofanyika katika Makaazi ya Balozi Seif Mazizini Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar ilijumuisha pia baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa Serikali, wafanyakazi wa Baraza hilo wakiwemo wawakilishi wa taasisi tofauti za ndani na nje ya nchi wanaofanya kazi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.

Balozi Seif aliwapongeza watendaji wa taasisi zote zilizo chini ya Ofisi yake kwa kufanya kazi nzuri katika utekelezaji wa majukumu yao likiwemo pia suala  la kutengeneza Bajeti na hatimae kupita bila ya vikwazo katika Kikao cha Bajeti cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea.
 Kikundi cha Muziki wa Morden Taarab cha Big Staa chenye mastakimu yake Ofisi ya Mkoa Mjini Amani kikitoa burdani kwenye tafrija ya kuwapongeza Viongozi na watendaji wa Taasisi zilizochini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar baada ya kupita kwa Bajeti ya Wizara hiyo pamoja na kuagana kwa kukaribia kukamilika kwa kipindi cha miaka mitano.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar  Balozi Seif Ali Iddi  aliyepo mwanzo kushoto akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Serikali Kushoto yake Mh. Hamza Hassan Juma na Mjumbe wa Kamati hiyo Mh. Makame  Mshimba Mabrouk  kwenye tafrija ya kuwapongeza watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
 Seif wapili kutoka kushoto akijumuika pamoja na Viongozi na watendaji wa Ofisi yake kwenye tafrija aliyowaandalia baada ya kupita kwa Bajeti ya Wizara hiyo katika Kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea.
  Baadhi ya Watendaji wa Taasisi zilizochini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wakijipatia mlo kwenye tafrija hiyo iliyofanyika katika Makazi ya Balozi Seif yaliyopo Mazizini nje kidogo ya M,ji wa Zanzibar.
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed akizungumza kabla ya kumkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kuzungumza na Viongozi na watendaji wa Ofisi yake.
 Balozi Seif akitoa nasaha zake mara baada ya kuwaandalia chakula cha usiku Viongozi na Watenmdaji wa Taasisi zilizochini ya Ofisi yake kufuatia kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara hiyo pamoja na kuagana baada ya kufanyakazi pamoja katika kipindi cya miaka mitano iliyopita.
 Balozi Seif kati kati akiwa pamoja na wake zake Mama Pili Seif Iddi na Mama Asha Suleiman Iddi wakijumuika pamoja katika kusakata rumba kwenye tafrija ya kuwapongeza watendaji wa Ofisi yake hapo Nyumbani kwake Mazizini nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Picha na – OMPR – ZNZ.

BONDIA FRANSIC CHEKA KUZIPIGA KESHO MEI 30 UKUMBI WA P.T.A SABASABA

$
0
0

Mabondia Francis Cheka kushoto na Kiatchai Singwancha wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa Mei 30 utakaofanyika katika ukumbi wa P.T.A sabasaba .
PICHA NA SUPER D BOXING NEWS
Mabondia Francis Cheka kushoto na Kiatchai Singwancha wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa jumamosi ya May 30 utakaofanyika katika ukumbi wa P.T.A sabasaba .
HABARI ZAIDI INGIA HAPA

APICO KUZINDUA KALENDA YA KIISLAM 7JUNI MWAKA HUU.

$
0
0
 Mwenyekiti wa maandalizi taasisi ya Kiislamu ya APICO Tanzania Ltd Habibu Masano akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO JIJINI Dar es Salaam leo, wakati wa kutoa taarifa ya uzinduzi wa Kalenda ya Kiislam itakayo tumiwa na madhehebu yote ya Dini ya Kiislam duniani,inayotarajiwa kuzinduliwa Juni 7 Mwaka huu katika viwanja vya Karimjee jijiji Dar es Salaam.
Mratibu wa taasisi ya Kiislamu ya APICO Tanzania Ltd,Abasi Said Mzeri  akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti wa wa maandalizi wa taasisi ya Kiislamu ya APICO Tanzania Ltd, Habibu Masano,Mjumbe wa Taasisi ya Kiislamu ya APICO Tanzania Ltd,Kalama Mkali na wa mwisho ni Mjumbe wa taasisi ya Kiislamu ya APICO Tanzania Ltd,Salumu Lukungu.PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZUNGUMZA NA WATANZANIA WANAOISHI NCHINI NIGERIA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 29,2015.
 Balozi wa Tanzania Nchini Nigeria Mhe. Danniel Ole Njolai akimkabidhi zawadi ya saa iliyotolewa na Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, baada ya kuzungumza na Watanzania hao katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 29,2015.
 Baadhi ya Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, alipokua akizungumza nao leo May 29,2015  katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 30,2015.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, katikati akiwa katika picha ya pamoja na  Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria Baada ya kuzungumza nao katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 29,2015. (Picha na OMR).

RATIBA NA TAREHE MPYA ZA MoFLAVA ALL WHITE USA TOUR/PARTIES

$
0
0
ATANZANIA WAISHIO MAREKANI TUNAPENDA KUWAKUMBUSHA KUWA TOUR YA MoFLAVA ALL WHITE PARTY INAANZA HIVI KARIBUNI IN USA CITIES. TUNAOMBA USHIRIKIANO WENU AS WE BRING ENTERTAINMENT & GOOD TIME TO YOUR CITY OR CITY NEAR YOU. THIS IS THE UPDATED SCHEDULE FOR UPCOMING PARTY & CITIES

SATURDAY 06/06/2015  CINCINNATI OHIO
SATURDAY 06/20/2015  DALLAS TEXAS
SATURDAY  07/18/2015 (EID AL FITR)  HOUSTON TEXAS
SATURDAY  08/01/2015  WASHINGTON DC
SATURDAY  08/22/2015  WICHITA KANSAS
ATLANTA GA & COLUMBUS OHIO DATES TO BE ANNOUNCED SOON
 

NAIBU WAZIRI MKUU WA AUSTRALIA MAGHARIBI KIM HAMES AFANYA ZIARA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

$
0
0
Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Afya na Utalii kutoka Australia Magharibi Kim Hames (kushoto) akimweleza Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (Kulia) maeneo ambayo nchi ya Australia ingependa kuwekeza.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (Kulia) akimshukuru Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Afya na Utalii kutoka Australia Magharibi Kim Hames (kushoto) mara baada ya kumkabidhi zawadi. Wengine ni ujumbe ulioambatana na Naibu Waziri Mkuu huyo.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene ( wa pili kutoka kulia) Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Afya na Utalii kutoka Australia Magharibi Kim Hames ( wa tatu kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Australia uliohudhuria kikao hicho.

Na Greyson Mwase, Dar es Salaam

Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene ameitaka nchi ya Australia kuimarisha uwekezaji katika sekta za nishati na madini nchini ili ziweze kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi.

Simbachawene aliyasema hayo katika kikao chake na Naibu Waziri Mkuu wa Australia Magharibi, Kim Hames na ujumbe wake aliyemtembelea ofisini kwake kwa ajili ya kupata taarifa za maeneo yanayohitaji uwekezaji nchini.

PPF YANYAKUA TUZO YA UBORA WA HUDUMA YA ISO KIMATAIFA

$
0
0
MFUKO wa Pensheni wa PPF, umepewa cheti cha ubora wa utoaji huduma kimataifa kwa wananchi (ISO) baada ya kukidhi mashariti na vigezo.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio alitoa taarifa hiyo leo Ijumaa  na kusema kuwa walipewa tangu Machi 28, mwaka huu.


Alisema wamepewa cheti chenye namba 9001:2008 na kuanzia mwezi Mei, mwaka huu huduma za PPF zinaza kutambulika kimataifa.

“ISO walikuja nchini wakatukagua wakalidhika na viwango vya huduma zetu tunazotoa na wakatupatia cheti cha ubora,” alisema Erio.


Alisema kwa sasa wanachma wa PPF wategemee kupata huduma bora pamoja na uwajibikaji ulio bora.

Alisema kila baada ya miezi sita ISO watakuwa wanatembelea PPF na kukagua kama huduma bora bado zinatolewa, na kila baada ya miaka mitatu PPF watatakiwa ku-renew maombi ya ISO.



Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio (katikati) akizungumza wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya cheti cha ubora wa utoaji huduma kimataifa kwa wananchi (ISO) walichokipata baada ya kukidhi mashariti na vigezo

Mameneja wa PPF, na waandishi wa habari wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio juu ya tuzo hiyo
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio (katikati), Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Julius Mganga (kushoto) na Mkurugenzi wa Udhibiti Majanga (risk management), Ufoo Swai wakionyesha cheti cha ubora wa utoaji huduma kimataifa kwa wananchi (ISO) wakati wa mkutano na waandishi wa habari makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Mei 29,2015.

China signals end to domestic ivory market during destruction of illegal stockpile

$
0
0
Beijing, China, 29 May 2015 —The Chinese government indicated today that it was planning to eventually phase out its domestic ivory market. 

According to the announcement by the administrator of the State Forestry Administration during the public destruction of 662kg of confiscated illegal ivory, the Chinese authorities will “strictly control ivory processing and trade until the commercial processing and sale of ivory and its products are eventually halted.”

“This is a very positive signal, and WWF applauds the Chinese government’s determination to conserve wildlife and combat the illegal trade in wildlife and wildlife products, including ivory,” said Lo Sze Ping, Chief Executive Officer of WWW China. “This decision will have profound impact on wild elephant conservation and ivory trafficking.”


Today’s destruction of tusks and ivory carvings that were seized since 2014 follows an ivory destruction event held in Guangdong, China, in January 2014 when 6.15 tonnes of confiscated ivory were crushed. Other nations and territories to destroy ivory stockpiles recently include Belgium, Republic of Congo, France, Gabon, Hong Kong, Kenya, UAE and the USA.


“The decision to phase out China’s ivory market as well as today’s destruction of the confiscated ivory are powerful indications of the government’s commitment to support international action against elephant poaching and the illegal ivory trade,” said Zhou Fei, Head of TRAFFIC’s China Office.

“However, ivory destructions should not be an end in themselves—any such events should be followed by actions to ensure countries continue to comply with their international commitments under the Convention on International Trade in Endangered Species of Wild Fauna and Flora (CITES) to shut down the illegal ivory trade.” 

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA WIZARA YA USHIRIKIANO AFRIKA MASHARIKI ZALENGA KUBORESHA UHUSIANO WA TANZANIA KIMATAIFA.

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2015/2016 bungeni leo mjini Dodoma.  Mabalozi wa Tanzania kwenye nchi mbalimbali duniani wakifuatilia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka 2015/2016 iliyowasilishwa leo bungeni mjini Dodoma. Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Harrison Mwakyembe akimsikiliza kwa makini mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere (kushoto) nje ya ukumbi wa bunge leo mjini Dodoma. Kulia ni mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. ShyRose Bhanji. Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju (kulia) akisisitiza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati) kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma jana.  Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Harrison Mwakyembe akifurahia jambo na wabunge wa bunge la Afrika Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere (kushoto) na Mhe. ShyRose Bhanji (kulia) mara baada ya kuwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2015/2016  leo bungeni mjini Dodoma. PICHA ZOTE NA FATMA SALUM - MAELEZO.

Kaa tayari kwa 'Movement' mpya ya WBTA na Tanzania mpya!!!

$
0
0
Monika & Us_00000 copyMiongoni mwa viongozi waandamizi wa WBTA, ambao ni mapacha, Frank na Francis (kulia). Kushoto kwao ni mdogo wao, Monica Ntevi.

WBTA Ni harakati zilizoanzishwa na vijana watatu Frank & Francis Ntevi na Eben Had, ambao wote ni wanafunzi wanaosoma chuo kikuu UDSM, kwa lengo la kuwanyanyua, kusapoti wasomi wote wenye moyo na Sanaa.

Kwa sasa wameanzia ndani ya UDSM, ikiwemo wameanza kusaidia kutoa sapoti kwa UDSM X BAND kwa kuwatengenezea albamu art kwa kushirikiana na mwanafunzi mwingine Papushka ambaye naye yupo kwenye harakati hizo kwa kufaanya video.

Katika haarakati hizo, muunganiko wa wasanii wa chuo kikuu UDSM ALL STARS, wameachia wimbo unaitwa ‘Tanzania mpya’ uliotoka hivi karibuni na pia wapo katika hatua za kutoa video ya wimbo huo.

..Bado haijaanza kupigwa kwenye vituo vya radio kwa sababu wanasubiria video yake kwaza.

TASWIRA MBALI MBALI ZA BARABARANI LEO

$
0
0
Pichani ni Gari mbili zikijaribu kulipita lori kwenye sehemu yenye kona, huku pembeni kule wazee wa feva wakiwa hawana habari. Hapa ni nje kidogo na mji wa Same, Mkoani Kilimanjaro.
 Pamoja na kuwepo na kibao cha tahadhali, lakini dereva wa gari hii hata hakujali na kuamua kulipita lori lililokuwa mbele yake.
 Hivi ndivyo mambo yanavyokuwa wakati mwingine, kwenye barabara zetu.

NEC YAKAMILISHA MAANDALIZI UBORESHWAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA KWA MIKOA 4

$
0
0
Maandalizi ya Kanda ya 5 Tano kati ya Sita yamekamilika leo 29/5/2015 zaidi ya BVR 1492 zinaanza kusambazwa na Tume ya Uchaguzi Kuanzia mapema Alfajiri kesho,Kanda ya Tano ni Mikoa ya Mara,Arusha,Manyara na Kilimanjaro.

USIKOSE KUCHEKI FAINALI YA FA CUP KUPITIA DSTV

Orodha ya vyama vya kijamii vinavyokusudiwa kufutwa na wizara ya mambo ya ndani ya nchi

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images