Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110095 articles
Browse latest View live

KIPINDI CHA DIRA YA DUNIA


CAF YAIPA TANZANIA UENYEJI FAINALI ZA U17

$
0
0

Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika -CAF leo hii limeipa Tanzania uenyeji wa fainali za michuano ya Afrika ya vijana umri chini ya miaka 17 mwaka 2019.

Uenyeji huu ni hatua muhimu sana kwa Tanzania katika kukuza soka la vijana na kwa hatua hii Tanzania itacheza moja kwa moja fainali hizi. 

Katika kuandaa kikosi bora cha kushiriki fainali hizi Tanzania, mwezi Juni mwaka huu TFF itaandaa mashindano ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 13 na wachezaji bora wa mashindano haya wataunda kikosi cha mwanzo cha Taifa kuelekea fainali za mwaka 2019.

TFF inamshukuru sana Rais Jakaya Kikwete na Mh. Fennela Mukangara Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kufanikisha maamuzi haya, na inaamini ushirikiano huu wa Serikali na wadau wengine utafanikisha mashindano haya mwaka 2019.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF).

MAKALA YA SHERIA; NI KOSA ASKARI KUONDOKA NA MTU MWINGINE BAADA YA KUMKOSA MTUHUMIWA NYUMBANI.

$
0
0
            
Na  Bashir  Yakub.

Malalamiko  ya raia  dhidi  ya  jeshi  la  polisi  hayataishi  kama  polisi  wenyewe hawatajirekebisha.  Na ieleweke kuwa  si  kweli  kwamba wanaolalamika  ni  wajinga  au hawana sababu  za  msingi.  Mara  zote  ukiangalia  malalamiko  ya  raia huwa  ni  ya  msingi  na  mzizi  wake ni  mmoja  tu.  Ni  utamaduni  wa  askari  wetu  kutopenda  kutenda  hatua  kwa  hatua  kama sheria  inavyoagiza. Sheria  imetoa  maelezo  mazuri  tu  ya namna  ya  kuyaendea  mambo. Tatizo  watekelezaji  ndio  hakuna. 

 Sheria  husema  kingine  na  watekelezaji  hufanya  kingine. Namna  hii  huwezi  kuepuka  chuki  na  migongano  kati  ya   hawa  watekelezaji  askari  na  raia. Na  migongano  na  kutokuelewana  kunapokuwa  kukubwa  na  usalama  nao  unayumba  kwakuwa   ili  askari  afanye  kazi  ya  usalama  vizuri   anategemea  msaada  wa  raia  karibia  kwa  asilimia  zaidi  ya  80.  '

 Na  raia  huyu hatatoa  ushirikiano  wakati  jana  umempiga  bila  sababu,  umemtukana   na  kumtolea  maneno  ya  kebehi. Makala  iliyopita  nilizumgumzia  namna  sheria  inavyomruhusu  raia  kukataa  kukamatwa  na  polisi  iwapo  polisi  huyo  atakiuka  taratibu  katika  ukamataji.  Leo  nazungumzia   namna  sheria  inavyokataza kumchukua  mtu  mwingine  baada  ya  kumkosa  mtuhumiwa  halisi  wa  kosa.  Tutaona  hili  likoje. 

1.ASKARI  KUONDOKA  NA  MTU  MWINGINE  BAADA  YA  KUMKOSA  MTUHUMIWA  HALISI.

Hii  ni  tabia  ambayo  imezoeleka  sana  na  ipo  kwa  muda  mrefu. Yumkini  kuzoeleka  kwake  na  kuwepo  kwake  kwa muda  mrefu hakuifanyi  hata  kwa  sekunde  moja  tabia  hii  kuwa  halali  kisheria.  Mara  nyingi  wanaokutwa sana  na tabia  hii  ni  watu  wa  vijijini  hasa  wa  hali  ya  chini.  Lakini  hata  mijini  pia  ipo  sana.  Nazungumzia   tabia  ya  kuondoka  na  mtu   mwingine  baada  ya  kumkosa mtuhumiwa  halisi.  Kwa  mfano  askari  wamekuja  nyumbani  kumtafuta  JOHN  kwa  kosa  analotuhumiwa  nalo.  Bahati  mbaya  au  nzuri  JOHN  hayupo  nyumbani. 

Kutokana  na hilo   askari  wanaamua  kuondoka  na  mke  wa  JOHN  au  mtoto  wake     ili  kumfanya  JOHN  aweze  kutokea. Hiki  ndicho  ninachozungumzia.  Na wanaokuwa  wakichukuliwa  mara  kwa  mara ni  mke  wa  mtuhumiwa  , mtoto  au  ndugu. Lengo   eti  ni kumfanya  mtuhumiwa  halisi  aweze  kujisalimisha. 

SOMA HAPA ZAIDI

MKURUGENZI MTENDAJI WA TAASISI YA MOI DKT. OTHUMANI KILOLOMA AFUNGUA MKUTANO WA TATU WA MADAKTARI WA MIFUPA JIJINI DAR

$
0
0
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa,ajali na upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) Dokta Othman Kiloloma (kulia) akifungua Mkutano wa tatu  wa Madaktari Bingwa wa Mifupa uliyofanyika katika Taasisi hiyo Dar es Salaa 
Daktari Bingwa wa Mifupa wa Taasisi hiyo Dk. Edmund Ndalama (kulia)  akizungumza na Makt. Bingwa tota Nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania na Marekani ambapo lengo ni kubadilishana ujuzi kwa Nadharia na Vitendo na unatarajia kumaliza  29-Mei 2015 
 Dokt. Zehrabanu Zulfikar akizungumza na Madkt. wakati wa Mkutano huo.
HABARI ZAIDI SOMA HAPA

Waziri Mwandosya akutana na Pele

$
0
0

Akiwa njiani kwenda Hanoi, Vietnam, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais ( Kazi Maalum),Profesa Mark Mwandosya, amekutana na  Edson Arantes do Nascimento (Pelé) mwanamichezo maarufu sana duniani. Pelé atatimiza umri wa miaka 75 ifikapo tarahe 23 Oktoba,2015. Katika uhai wake, Pelé aliweza kuingiza magoli 1283 katika michezo ya ushindani wa mpira wa miguu. 

Pelé aliichezea timu yake klabu ya Santos, Brazil kuanzia mwaka 1956 mpaka mwaka 1974.Baada ya kustaafu alijiunga na klabu ya New York Cosmos kwa muda mfupi kuanzia mwaka 1974 mpaka 1977. Pelé ametajwa kuwa mmoja wa watu maarufu zaidi duniani na hakika mwanasoka maarufu kuliko wote karne ya 20. 

Waziri Mwandosya alimshukuru Pelé kwa kuwa mfano bora katika mwenendo, maisha, ubunifu,na uongozi katika tasnia ya michezo na alimtakia afya njema na maisha marefu. Amewahi kuwa Waziri wa Michezo,Brazil. Katika picha ni Waziri Mwandosya, kulia;Pelé,katikati;na Mama Lucy Mwandosya, kushoto.

PATAKUWA HAPATOSHI DAR LIVE SIKU HIYO.

WAZIRI NYALANDU ASAINI MKATABA MSUMBIJI KULINDA SELOUS

$
0
0
 Waziri wa maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akibadilishana hati za makubaliano ya  kuhifadhi Pori la akiba la selous nchini Tanzania lililoungana na Hifadhi ya Nnyasa nchini Msumbiji na waziri wa Ardhi na Maendeleo vijijini Celso Coreia, ambapo mbali na uhifadhi watashirikiana kupambana na ujangili , utaalamu na vifaa, jana mjini Maputo Msumbiji.
  Waziri wa maliasili na Utalii, lazaro Nyalandu akimsikiliza waziri wa Ardhi na Maendeleo vijijini, Celso Coreia jana mjini Maputo kabla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kuhifadhi Pori la akiba la selous nchini Tanzania lililoungana na Hifadhi ya Nnyasa nchini Msumbiji ambapo mbali na uhifadhi watashirikiana kupambana na ujangili , utaalamu na vifaa.
 Waziri wa Maliasii na Utalii, Lazaro Nyalandu na waziri wa Ardhi na Maendeleo vijijini wa Msumbiji Celso Coreia wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa kabla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kuhifadhi Pori la akiba la selous nchini Tanzania lililoungana na Hifadhi ya Nnyasa nchini Msumbiji ambapo  mbali na uhifadhi watashirikiana kupambana na ujangili, utaalamu na vifaa.

MKUTANO WA MAJADILIANO YA RIPOTI YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAFANIKIO NCHI ZA AFRIKA WAFANYIKA MJINI ABIDJAN

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya fedha   na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile akiwaeleza Mawaziri wa Fedha kuhusu serikali ya Tanzania ilivyonufaika na fedha za Benki ya Maendeleo katika kutekeleza mipango yake hasa  kwenye miundombinu. Kutoka kulia ni Waziri wa Fedha wa Rwanda Bw. Claver Gatete  na kushoto kwake ni  Mchumi Mkuu Rugwabiza Minega Leonard.
Katibu Mkuu wa Wizara ya fedha   na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile akitoa ufafanuzi kuhusu Tanzania inavyoshirikiana na Benki ya Afrika kwa Mawaziri wa Fedha kutoka  nchini Rwanda, Ethiophia, Kenya na Visiwa vya Shelisheli wakati wa uwasilishaji wa ripoti ya utekelezaji wa mazimio ambayo kila nchi imejiwekea.
 Waziri wa Fedha wa Rwanda Mhe. Claver Gatete akitoa ufafanua wa masuala mbalimbali yanayohusu nchi za Afrika. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile ambaye amemwakilisha Waziri wa fedha na kulia kwake ni Waziri wa Fedha wa Ethiophia Mhe. Fisseha Aberra.

 Kamishna wa Fedha za Nje Bwana Ngosha Manyoga akiwa katika majadiliano yanayohusu ya ripoti ya utekelezaji wa mpango wa mafanikio  katika nchi za Africa.
 Wajumbe waliohudhuria Mkutano wa Kanda ya Afrika  wakimsikiliza na kufuatilia kwa makini Dkt. Mulu Ketsela ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Afrika alipokuwa akiwasilisha ripoti ya Benki hiyo.

TAARIFA YA MSIBA WA MZEE MGAYA

$
0
0
Familia ya mzee Richard Azza Mgaya inasikitika kutangaza kifo cha baba yao Mzee Richard Mgaya kilichotokea hospitali ya Apollo - India. Mwili wa marehemu utawasili Kilimanjaro International Airport tarehe 28/05/2015 saa nane mchana, msiba uko nyumbani kwake Arusha no. 59 Themi Hill. Marehemu ataagwa Ijumaa tarehe 29/05/2015 saa 6mchana katika kanisa la waadventista wa sabato Njiro Arusha.Mazishi yatafanyika Jumamosi tarehe 30/05/2015  Mamba Miamba - Same Kilimanjaro.

WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI UTALII NA MICHEZO AKUTANA NA BALOZI WA MALAWI ZANZIBAR.

$
0
0
  Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk  akisalimiana na Balozi wa Malawi Nchini Tanzania Hawa O. Ndilowe wakati alipowasili Ofisini kwake kwaajili ya kujitambulisha pia na kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusuUtalii Zanzibar.
 Afisa Ubalozi anaeshughulikia masuala ya Uchumi Tanzania Chinvano Kapeleta akizungumzia masuala ya Uchumi na Utalii na Viongoizi wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar.
 Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akifafanua jambo katika mazungumzo na Balozi wa Malawi Nchini Tanzania Hawa O. Ndilowe wakati walipokutana Ofisini kwake Zanzibar.
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk katikati akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Malawi Hawa O.Ndilowe kulia yake na baadhi ya viongozi waliofika Ofisini kwake Zanzibar.PICHA ZOTE NA MIZA OTHMAN-HABARI MAELEZO ZANZIBAR.

WAZIRI MKUU PINDA ATEMBELEWA NA MTOTO ALBERT

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na mtoto Albert Kanan wa darasa la tatu katika shule ya msingi ya Ilalangulu wilayani Mlele ambaye alikwenda nyumbani kwa Waziri Mkuu katika kijiji cha Kibaoni akiomba kupiga naye picha. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

tamthilia ya #Kitendawili sehemu ya tatu

MOAT WAPINGA MUSWADA WA SHERIA YA VYOMBO VYA HABARI

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA BALOZI WA TANZANIA NCHINI KENYA, JOHN HAULE

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi mpya wa Tanzania nchini Kenya, John Michael Haule, wakati Balozi huyo alipofika Osifini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kumuaga leo Mei 27 2015. Picha na OMR

Rais Kikwete afungua Mkutano Mkuu wa Chama Cha Waalimu Tanzania (CWT)

$
0
0
 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa Chama Cha Waalimu TANZANIA( CWT) uliofanyika katika hoteli ya Ngurdoto nje kidogo ya mji wa Arusha jana.Wakati wa mkutano huo wanachama wa CWT ulitarajia kuwachagua viongozi wapya wa chama Hicho.Akizungumza katika  mkutano huo Rais Kikwete ameahidi kutatua changamoto moto mbalimbali zinazowakabili waalimu nchini(picha na Freddy Maro).

Tangazo la Kozi ya Masters

JK ATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA ZA MZEE RUANGISA

$
0
0


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone:255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa masikitiko na huzuni nyingi taarifa ya kifo cha mwanasiasa mkongwe nchini na aliyepigania uhuru wa Tanganyika, Ndugu Samwel Ntambala Ruangisa, ambaye aliaga dunia mwanzoni mwa wiki hii nchini Marekani ambako alikuwa anatibiwa.

Katika salamu za rambirambi ambazo amempelekea Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mheshimiwa John Mongella kuomboleza kifo cha Mzee Ruangisa, ambaye pia alikuwa bado diwani katika Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Rais Kikwete amesema:

“Nimepokea taarifa za kifo cha Mzee Ruangisa kwa masikitiko na huzuni nyingi. Kwa zaidi ya nusu karne, Mzee Ruangisa amekuwa kiongozi wa kuigwa mfano katika nafasi zote ambazo zimepata kuzishikilia katika maisha yake kuanzia Ukuu wa Mkoa wa Ziwa Magharibi (sasa Kagera) na baadaye Mkoa wa Mara tu baada ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Ubalozi, Uwaziri, Ubunge, Umeya na Udiwani. Katika kila nafasi aliyoishikilia, Mzee Ruangisa alionyesha uongozi wa kiwango cha juu. Kwa hakika, tumepoteza kisima cha uzoefu wa uongozi.”

Rais Kikwete ameongeza katika salamu zake za rambirambi: “Mkuu wa Mkoa nakutumia salamu zangu za rambirambi kuomboleza msiba huu na kupitia kwako naomba uwape pole wana-Kagera wote kwa kuondokewa na mzee wao wa siku nyingi. 

Aidha, naomba unifikishe pole zangu nyingi kwa wanafamilia wote ambao wamepoteza baba, babu na mhimili wa familia. Wajulishe kuwa niko nao katika kipindi hiki kigumu. Waambie naelewa machungu yao kwa sababu machungu yao ni machungu yangu. Vile vile, naungana nao katika kumwomba Mwenyeji Mungu, Mwingi wa Rehema, aiweke peponi roho ya Marehemu Samwel Ntambala Ruangisa. Amina.”

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU,
DAR ES SALAAM.

27 Mei, 2015

MAADHIMISHO YA WIKI YA UKOMBOZI BARA LA AFRIKA,WANAWAKE WAELEZA NAMNA WALIVYOSHIRIKI KATIKA UKOMBOZI

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bodi ya AICC na Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya wiki ya Ukombozi wa Bara la Afrika, Balozi Christopher Liundi akikata utepe katika maadhimisho hayo ikiwa leo ni siku ya Kuona Mchango wa Wanawake katika Ukombozi wa Bara la Afrika, maadhimisho hayo yamefanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Profesa Ruth Meene akizungumza na baadhi ya wanafunzi na watu wengine waliohudhuria (hawapo pichani) ili kujua mchango wa wanawake katika ukombozi wa Bara la Afrika, wanawake hao ambao wamesaidia zaidi ni Mke wa Rais wa Mozambiq,Jocina Machel,Bi Ndaitwa wa Namibia,Winnie Mandela wa Afrika Kusini,Albetina Kisulu,Elizabeth Sebeko,Mariam Makeba wote wa Afrika kusini  na hapa nchini ni Bibi Titi Mohamed,Lucy Maulid na Sophia Kawawa ambao walikuwa wakihamasisha wananchi Kisiasa katika kulikomboa Bara la Afrika.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Victoria waliohudhuria katika Mkutano wa kujua jinsi wanawake walivyoshiriki katika kulikomboa Bara la Afrika, katika Mkutano uliofanyika Makumbusho ya Taifa jijiji Dar es Salaam leo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya AICC na Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya wiki ya Ukombozi wa Bara la Afrika, Balozi Christopher Liundi akizungumza leo na waandishi wa habari mara baada ya kutoka katika kumbi zenye  picha na vitu mbalimbali ndani ya jengo la Makumbusho ya Taifa vinavyoonyesha kumbukumbu ya matukio mbalimbali yalivyowahi kutokea hapa nchini.Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

RAIS KIKWETE AWAAPISHA KATIBU MKUU, NAIBU KATIBU MKUU WA MAMBO YA NJE NA BALOZI WA TANZANIA SAUDIA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha  Balozi Liberata Mulamula kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Balozi Mulamula anakuwa Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke kuongoza Wizara hiyo na kabla ya uteuzi huo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani. Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu tarehe 27 Mei, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Balozi Hassan Simba Yahya  kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kabla ya uteuzi huo Balozi Yahya alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu tarehe 27 Mei, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha, Mhe. Hemed Iddi Mgaza kuwa Balozi  wa Tanzania nchini Saudi Arabia. Kabla ya uteuzi huo Balozi Mgaza alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mkuu  na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu tarehe 27 Mei, 2015.
PICHA ZAIDI INGIA HAPA


DR. MENGI AZINDUA MPANGO WA AIRTEL FURSA 'TUNAKUWEZESHA' JIJINI DAR.

$
0
0
  Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi (wa pilikulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Airtel Tanzania, Balozi Juma Mwapachu (wapili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Sunil Colaso (kulia) na Menejawa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi wakiwa wameshika bango kamaishara ya uzinduzi wa mpango wa Airtel Fursa ‘Tunakuwezesha’, katika haflailiyofanyika jijini Dar es Salaam  jana.
  Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi (wa pili kulia), akikabidhi zawadi ya pasi na meza yake kwa muuza mitumba RashidSeleman (wa pili kushoto), ambaye ni mmoja wa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa ‘Tunakuwezesha’ katika hafla ya uzinduzi wa mpango  huo, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji   wa Airtel Sunil Colaso, Mwenyekiti wa Bodi ya Airtel Tanzania, Balozi Juma  Mwapachu (wa tatu kushoto) na Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi.
 Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi (wa pili kulia), akikabidhi zawadi ya mashine ya kutengeneza juisi kwa Abdulkarim  Ramadhan (wa tatu kushoto), ambaye ni mmoja wa vijana waliowezeshwa na mpango wa Airtel Fursa ‘Tunakuwezesha’ katika hafla ya uzinduzi wa mpango huo, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kutoka (kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Sunil Colaso, Mwenyekiti wa Bodi ya Airtel Tanzania, Balozi Juma Mwapachu na Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
 

Viewing all 110095 articles
Browse latest View live




Latest Images