Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109597 articles
Browse latest View live

UK Islamic NGO support Muhimbili Cardiac equipment worth 300,000USD

0
0
By Aminiel Aligaesha

The Muntada Aid which is an Islamic NGO based in UK has supported medical equipment to Muhimbili National Hospital (MNH) worth over 300,000 USD to save lives of children with congenital heart diseases. Speaking to the press in Dar es Salaam, the Acting Executive Director of MNH Dr. Hussein Kidanto said the equipment donated includes stents and other surgical devices.

He said with stent children with congenital heart diseases have undergone high tech procedures of unclogging and dilating blood vessels without opening the chest whilst with devices the same procedure has been applied to new born with defects (holes) hearts.

“Muntada Aid apart from supporting the equipment, it also sent a mission with 29 different experts to mention few; interventional pediatric cardiologists, perfusionists, anaethiologist, nurses, ICU physician to join efforts with our local experts to perform the said procedures” said Dr. Kidanto.

He said the mission who arrived in Tanzania in May 8th and left on 16th, 2015 managed to perform 23 open heart surgeries and 41 devices pediatric procedures, which has significantly helped the nation to save over 290,000 USD, would have incurred if they were to be sent abroad.

“I appreciate for this support from Muntada Aid and will be happy to extend this collaboration with Muhimbili National Hospital hence to increase a number of beneficiaries under this program,” said Dr. Kidanto.

He said the world estimates that congenital heart disease stands at 8 per 1000 live births whereby in Tanzania with approximate 46 million population and 1.7 million annual birth rate (2014), it is estimated that 13,600 babies were born with congenital heart disease in Tanzania and approximate 25% of them will need some form of intervention within the first year of diagnosis. And indeed some were operated in the current mission with the aid of Muntada.
From left, the fifth one is the Minister for Health and Social Welfare in Tanzania Dr. Seif Rashid in a posing picture in one of the ICU at MNH with the a team of cardiologist and surgeons from Prince Sultan Cardiac Centre in Riyadh, Kingdom of Saud Arabia. The first one on right side is Dr. Hussein Kidanto the Acting Executive Director of MNH. This mission was proudly sponsored by Muntada Aid.

BREAKING NEWZZZZ: MWIGULU LAMECK NCHEMBA AJIUZULU NAFASI YA NAIBU KATIBU MKUU WA CCM, RAJABU LUHWAVI ACHUKUA NAFASI YAKE

0
0
Habari za uhakika kutoka Dodoma zinaeleza kwamba Naibu Katibu Mkuu wa CCM ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (kushoto) amejiuzulu nafasi hiyo katika chama tawala. Kulia ni Ndg Rajabu Luhwavi ambaye anachukua nafasi yake. Taarifa kamili soma hapo chini:

7th Welcoming Ramadhan Conference Sunday June 14, 2015 @ Julius Nyerere International Conference Centre, Dar es salam

LAZIMA TUSOME ALAMA ZA NYAKATI...CHAMA KWANZA MTU BAADAE - JK

OFFICE ACCOMODATION FOR LEASE @ KINONDONI, DAR ES SALAAM

SIKU MAGUFULI ALIPOKATAA KUIPOKEA BARABARA YA KILWA (MTONGANI - MBAGALA RANGI TATU YA KM 5.1

0
0
UJENZI wa Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam ambayo Waziri wa Ujenzi, Dkt John Pombe Magufuli alikataa kuipokea mwaka 2011, baada ya kujengwa chini ya kiwango. Ujenzi wa kipande hicho cha kilomita 5.1 kutoka Mtongani hadi Mbagala Rangi Tatu, ulikamilika mwaka 2012. Mafundi wa Kampuni ya Kajima ndio waliokuwa wakijenga kipande hicho cha barabara . 
Dkt.  Magufuli alikataa kuipokea barabara hiyo kutoka katika Serikali ya Japan, iliyotoa msaada wa fedha na ujenzi kufanywa na Kampuni ya Kajima, baada ya kujiridhisha kuwa ilijengwa chini ya kiwango. 
Dkt. Magufuli alimweleza Balozi wa Japan nchini, Mhe. Masaki Okada kwamba asingeipokea barabara iliyo chini ya kiwango hata kama imetolewa kama msaada kwa Tanzania. 
 Baada ya msimamo huo wa Serikali, Japan ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa kampuni hiyo ilijenga barabara hiyo chini ya kiwango. Kutokana na hali hiyo, Balozi Okada aliahidi kurudia ujenzi wa kilometa 5.1 kipande ambacho waligundua kuwa kampuni hiyo ilijenga chini ya kiwango. 
 Baada ya kauli hiyo ya Balozi, Dk Magufuli alimtaka mkandarasi huyo kuondoa tabaka la lami na kuweka tabaka jingine gumu lenye sentimita saba jambo ambalo limetekelezwa baada ya marudio.
Ujenzi wa Barabara ya Kilwa yenye urefu wa kilomita 13.5 kutoka bandarini hadi Mbagala Rangitatu ulizinduliwa kwa kuwekwa jiwe la msingi na Rais Jakaya Kikwete mwaka 2007.

Dk. Salim atembelewa na Ugeni wa Jeshi la Uchina

0
0
Waziri Mkuu Mstaafu na pia Rais wa Chama cha Mahusiano Mema kati ya Uchina na Tanzania akiwa na Kamisaa wa Siasa katika Chuo Kikuu cha Ulinzi cha Uchina (Political Commissar of the National Defense University of China) Jenerali Liu Yazhou pamoja na ujumbe wake walipomtembelea ofisini kwake leo Jumatatu. Jenerali Liu Yazhou amekuja nchini kwa ziara ya siku mbili.

Private Sector Stakeholders meet in Mwanza to discuss Non Tariff Barriers

0
0
Mwanza 25th  May,2015: Tanzania Chamber of Commerce Industry and Agriculture (TCCIA) has organized a two days Private Sector Stakeholders Forum from 26th to 27th May to discuss on the Non Tariff Barriers (NTBs) impeding transit trade and exportation of Tanzania originating products to the East African Community Region and other regions such as Southern African Development Community (SADC).

The Private Sector Stakeholders' forum will bring together key players in the trade including Private Sector Organizations (PSOs) and some economic operators. The participating PSOs includes; Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC), Tanzania Horticultural Association (TAHA), Tanzania Freight Forwarders Association (TAFFA), Association of Tanzania Employers (ATE), Agriculture Council of Tanzania (ACT), Tanzania Milk Processors (TAMPA), Leather Association of Tanzania (LAT), Tanzania Truck Owners Association (TATOA), Vikundi vya Biashara Ndogondogo (VIBINDO). They meet to share the success stories realized so far in fighting against NTBs, Share the existing challenges, share experience in the work of advocacy for the better business environment and deliberate on a new combined strategy in addressing the pending NTBs.

The forum is organized by TCCIA in partnership with Trademark East Africa. Trade Mark East Africa has been supporting TCCIA to implement the Non Tariff Barriers (NTBs) Project since 2012.The support includes technical support, supply of important equipments including computers, servers, scanners and facilitation of various project related trainings, seminars, meetings and promotional campaigns. Trade Mark East Africa has invested in the project about USD 1.2million.

Through this project TCCIA has managed to develop two systems that have been helpful in creating a conducive business environment by lowering the cost of doing business in Tanzania and in the EAC region as a whole. The two systems are; NTBs SMS and Online Reporting and Monitoring System an IT based tool that enables exporters and importers to report NTBs once they are encountered along the trade corridors, at the borders or at government institutions' offices. Since its establishment in 2012 the system has captured 85 NTBs and 54% of them have been eliminated.  Electronic Certificate of Origin is another new system of its kind in the EAC region developed by TCCIA under the support of TMEA. 

This system enables exporters to apply for Certificates of Origin electronically and get them approved on line by the competent authority. This system cuts down transporter's cost of processing the document by 50%. Since it started its operation in July, 2014 it has facilitated issuance of about 300 certificates. More than 300 exporters are trained throughout the country on the usage of the system. TCCIA has also supported Uganda to develop the NTBs SMS and Online System and it is currently working  with Burundi and Kenya to extend similar support.

UNFPA WAKABIDHI MSAADA WA GARI LA WAGONJWA, JENGO NA VIFAA VYA UPASUAJI GEITA

0
0
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani(UNFPA) limekabidhi msaada wa gari la wagonjwa lenye thamani ya shilingi milioni 80 katika kituo cha afya cha Masumbwe kilichopo katika Wilaya mpya ya Mbogwe Mkoani Geita.

Shirika hilo limetoa vifaa vya kutoa huduma ya upasuaji vyenye thamani ya shilingi milioni 250 katika kituo hicho mbali na kutumia shilingi zaidi ya shilingi milioni 100 kusadia ujenzi wa jengo la upasuaji katika kituo hicho.

Misaada hiyo kwa pamoja ilikabidhiwa Jumamosi iliyopita katika halfa ambaye mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh. Kassim Majaliwa.

Majaliwa alishuruku UNFPA kwa msaada huo na kutaka utumike vizuri ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

“ Nimeona vifaa vya hospitali vingi na vya gharama kubwa, sasa ni wajibu wetu kuvitunza na kuvitumia vizuri. Mfano gari tu limegharimu shilingi milioni 80. Huu ni msaada mkubwa sana na kwa niaba ya serikali nawashukuru sana UNPFA, tutaendelea kushirikiana”, alisema Majaliwa .

Hata hivyo Naibu Waziri huyo aliwaagiza vingozi wa Halmashuri ya Wilaya ya Mbogwe kuhakikisha kuwa gari hilo linatumika kusafirisha wagonjwa tu na sio vinginevyo.
DSC_0360
Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh. Kassim Majaliwa akikata utepe kuzindua gari la wagonjwa (Ambulance) lenye thamani ya Tsh. Milioni 80 kwa ajili ya kubebea wakinamama wajawazito na watoto wanaohitaji huduma za dharula za upasuaji kutoka vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika wilaya ya Mbogwe kwa ufadhili wa Shirika la UNFPA. Kushoto anayeshuhudia tukio hilo ni Mwakilishi msaidizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania, Dkt. Rutasha Dadi.
DSC_0289
Mganga mfawidhi wa kituo cha Afya Masumbwe wilayani Mbogwe, Dkt. Peter Shilogile akitoa maelezo ya mashine ya kisasa ya kuongezea damu wakina mama watakaokua wakijifungulia kwenye kituo hicho kwa Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh. Kassim Majaliwa.
DSC_0062
Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya CCBRT, Haika Mawalla (kushoto) na Mwakilishi msaidizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania, Dkt.Rutasha Dadi wakipitia ratiba ya sherehe za maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kutokomeza Fistula ambapo kitaifa yamefanyika katika Wilaya Mbogwe, Geita.

NEC yatoa Ratiba Rasmi ya Uchaguzi Mkuu.

0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa ratiba rasmi kwa vyama vya Siasa na wananchi wote itakayotumika katika Uchaguzi Mkuu wa Serikali  unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo  Jaji wa Rufaa (Mst.) Damian Lubuva imesema kuwa kwa Mamlaka waliyopewa kwa mujibu wa vifungu vya 35B(1), (3) (a), 37 (1) (a) na 46 (1) vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi,  Sura ya 343, shughuli za uchaguzi zinatarajia kuanza hivi karibuni.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa  Uteuzi wa wagombea Urais, Ubunge na Udiwani unatarajia kufanyika Agosti 21, 2015, na  kampeni za Uchaguzi kwa wagombea hao zitatarajia kuanza Agosti 22 mpaka - Oktoba 24 mwaka huu.

Halikadhalika siku ya kupiga kura kwa wananchi wote inatarajiwa kuwa Oktoba 25, 2015 kwa wale waliojitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.

NEWS ALERT: KOMAA CONCERT kuadhimisha miaka 16 ya kuwika kwa msanii JUMA NATURE kufanyika Mei 30, 2015 Dar Live

0
0
Tamasha kubwa la kuadhimisha miaka 16  ya kutamba katika Bongo Fleva ya msanii JUMA NATURE maarufu kama Kiroboto pamoja na hitimisho la sherehe za mwaka mmoja za 93.7 EFM linalofahamika kama KOMAA CONCERT kwa mara ya kwanza litafanyika rasmi jumamosi hii ya tarehe 30 mwezi mei katika ukumbi wa Dar Alive –Mbagala, kuanzia saa kumi na mbili jioni. 
 Tamasha hili limeandaliwa na Juma nature akishirikiana na EFM kwa lengo la kuwaburudisha Mashabiki wa juma nature na wasikiliazaji wa 93.7 EFM ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki kwa ushirikiano wao kwa miaka kumi na sita ya muziki tangu kuanza msanii huyo Juma Nature aingie kwenye game ya Muziki nchini Tanzania. 
 Aidha, mashabiki watapata burudani kutoka kwa kiroboto ambaye atatumia dakika 180 akiwa jukwaani kuhakikisha anakonga nyoyo za mashabiki wake ambapo ataimba nyimbo zake zote kali zilizofanya vizuri na kusindikizwa na wasanii kibao. 
 Miongoni mwa wasanii hao ni pamoja na Profesa Jay, Shetta, Snura, Makomando, Msagasumu na wengine wengi. Tunatoa wito kwa mashabiki wote wa juma nature , Efm Radio, wadau na wengine kujitokeza kwa wingi siku ya tamasha hili ili kupata burudani hii ya kihistoria ambapo kiingilio kitakuwa ni shilingi 7,000 tu. 
 Tunaamini Juma nature ni msanii mwenye kipaji kikubwa na aliyewahamasisha wasanii kibao kuingia katika muziki huu wa kizazi kipya hivyo anastahili kupewa heshima kubwa kwa mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa kizazi kipya. 
 Lakini kwa Efm huyu ni msanii wa Kwanza tu na itaendelea kufanya hivyo kwa wasanii wengine kwa kuwa kwetu sisi tunaamini Muziki unaongea.

 IMETOLEWA NA DENIS SSEBO, 
MENEJA MAWASILIANO NA MAMBO YA SHERIA WA EFM.
Mfalme wa Mchiriku Msaga Sumu akiongea. Kushoto ni msanii Snura na Kulia ni Meneja wa Mawasiliano na Mambo ya Sheria wa EFM Dennis Ssebo
Msanii wa kundi la Makomando akiongea akiwa na Snura na Msaga Sumu
Juma Nature, Snura na Makomando
Meneja mawasiliano na Mambo ya Sheria wa 93.7EFM Dennis Ssebo (mwenye suti) akiongea leo na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu onesho la hitimisho la sherehe za mwaka mmoja za 93.7 EFM linalofahamika kama KOMAA CONCERT ambalo kwa mara ya kwanza litafanyika rasmi Jumamosi hii ya tarehe 30 mwezi mei katika ukumbi wa Dar Alive –Mbagala. Kushoto na kulia ni wanaofanya kundi la Makomando, wakiwa na Snura (wa pili kushoto), Mfalme wa Mchiriku Msaga Sugu (wa tatu kushoto), Ssebo na Juma Nature.
Msanii JUMA NATURE a.k.a Kiroboto akiongelea onesho la hitimisho la sherehe za mwaka mmoja za 93.7 EFM linalofahamika kama KOMAA CONCERT ambalo kwa mara ya kwanza litafanyika rasmi Jumamosi hii ya tarehe 30 mwezi mei katika ukumbi wa Dar Alive –Mbagala


CHANGIA UJENZI WA MSIKITI KIJIJI CHA MLAMLENI, MKURANGA, MKOA WA PWANI

0
0
 Katika Maisha yetu Wanaadamu Ibada ni Jambo Muhimu saana. Uzuri , Usafi wa sehemu ya kuabudu ni Moja katika mambo mazuri yenye kupendeza katika kila Nafsi ya Binaadamu.

Nyumba hii ya Ibada ama Msikiti  huu  Ndugu zetu wanafanya Ibada ya Swala 5 kwa siku , Msikiti huu upo Mkoa wa Pwani , Wilaya ya Mkuranga , Kijiji cha Mlamleni Kitongoji cha Kimbangulile. Wenzetu wameanza kwa Nguvu zao kwa Ujenzi wa Msikiti huu. Na Jitihada nyengine ni kuwa na Matofali yasiyo pungua 300 kwa Ajili ya kuanza Ujenzi Mpya.



Mambo kutoka kwako ukiwa umeguswa na hili .
Tunaomba MCHANGO WAKO WA VIFAA VYA UJENZI.



Kwa Mwanzo Tunahitaji
1.Cement
2.Tofali
3.mchanga
4.Vifaa vya Kuchimbia Majembe, Panga , chepe N.k



Maazimio yetu tuanze Ujenzi pale tu tutakapo pata uwezo wa kulifanya hili.



Tunawakaribisha mtembelee eneo la tukio kwa wale ambao watakuwa Na Muda.



Michango yenu tunaomba muwasilishe kwa Namba ya Simu.

0715800772( Tigo Pesa ) GHALIB MONERO.


Kwa wale waliopo Nje ya Tanzania : WESTERN UNION : GHALIB NASSOR MONERO



Waliopo KENYA tafadhali wasiliana ALI BAJIY NASOR no' 0725113783.



More Update kuhusu Michango ya Msikiti huu Tafadhali tembelea : facebook : Kijana wa Kiislam Dsm or Whatssap Number : +255689604780



Au Piga Simu : +255715800772



WABILLAHI TAUFIQ WENU KATIKA UTUMISHI WA DINI KATIKA JAMII.


JK afungua Mkutano wa Shirikisho la Vyuo vya elimu ya Juu Dodoma

0
0
Mwenyekiti wa CCM Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akinyanyua juu nakala za kanuni za Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo Vya Elimu ya Juu kuzizindua rasmi wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Shirikisho hilo uliofanyika katika ukumbi wa Kilimani mjiini Dodoma leo. Kulia ni katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,watatu kulia ni Makamu Mweyekiti wa CCM Bara Ndugu Philip Mangula na kushoto ni mlezi wa shirikisho hilo ambaye pia ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknologia Ndugu January Makamba.
Rais Kikwete akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa kwanza wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo Vya Elimu ya Juu mjini Dodoma.
Rais Kikwete akisalimiana na baadahi ya wanafunzi baada ya kufungua mkutano.(picha na Freddy Maro)

UPENDO NKONE, MIKE KALAMBAY WANOGESHA TAMASHA LA GOSPEL COLUMBUS, OHIO

0
0
Mwimbaji wa nyimbo za injili wa Columbus, Ohio Enock Mwamba(kati) akiimba moja ya nyimbo za injili huku akiwashirikisha Mike Kalambay aliyekuja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Upendo Nkone aliyekuja toka Tanzania maalum kunogesha tamasha la Gospel lililofanyika siku Jumapili May 24, 2015 na kuhitimisha tamasha hilo lililokua la siku 3 mjini humo lililoanzia siku ya Ijumaa May 22, 2015.
Mike Kalambay akiimba moja ya nyimbo za injili kwenye tamasha la gospel lililofanyika siku ya Jumapili May 24, 2015 mjini Columbus, Ohio.
Mike Kalambay toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo akishambulia jukwaa na nyimbo za injili.
Mwimbaji mahili wa nyimbo za Injili Upendo Nkone akiimba moja ya nyimbo zake kwenye tamasha hilo.

MAKALA YA SHERIA: JE WAJUA SHERIA INAKURUHUSU RAIA KUKATAA KUKAMATWA NA ASKARI TARATIBU ZINAPOKIUKWA ?

0
0
Na  Bashir  Yakub.
Siku  zote  wananchi  wamekuwa    wakililalamikia jeshi  la polisi  kwa  namna  linavyoendesha  shughuli  zake hasa wakati  wa  ukamataji (arrest). Matumizi  ya  nguvu, ubabe    na  kutofuata  sheria    na  taratibu  maalum  limekuwa  ndio  tatizo  kubwa  kwa  wananchi  dhidi  ya  askari.  

Sio  siri  askari wamekuwa  wakitumia  nguvu  na  ubabe  mno  katika  kuwakamata raia.  Hata  pale pasipo  na  haja  yoyote  ya  kutumia  nguvu    bado  wao  wamekuwa  wakilazimisha  nguvu  nyingi  hali  ambayo  hupelekea   vurugu , kuumizana  na  hata  mauaji. Mara  nyingi  unapochunguza  matukio   mbalimbali  ya  vurugu ambayo  huwahusisha raia  na polisi  utagundua  kwa haraka kuwa  ubabe    wa askari  ndio  uliopelekea  vurugu.  Basi  leo  nitaeleza nini  ufanye  askari  anapokiuka  taratibu   hasa  wakati  wa  kukamata/kuweka  chini ya ulinzi.

1.NINI  MAANA  YA  KUKAMATA ( ARREST ).
Sura  ya  20  Sheria  ya  Mwenendo  wa  Makosa  ya  Jinai  kama  ilivyofanyiwa  marekebisho  2002  ndiyo  sheria  inayotoa  mwongozo   wa  namna  na  jinsi  ya  kumkamata  mtu.  Pamoja  na  hayo sheria  hii  haikueleza   moja  kwa  moja  nini  maana  ya  kukamata. Hata  hivyo  kutokana  na  miongozo mbalimbali  ya  kimahakama  ambayo  hutumika  kutafsiri  sheria  hii  tunaweza  kupata  tafsiri  ya  neno  kukamatwa  kwa  kusema  kuwa  ni  tendo  la  kumzuia  kwa  muda   raia  ambaye  inatuhumiwa  kwa  kosa  fulani,   ambalo  hufanywa  na  mamlaka  husika. 

Kwa tafsiri  hiyo  tendo la kuzuia  lazima  liwe    la  muda,  raia  anayekamatwa  lazima awe  ametuhumiwa, na pia  ukamataji  lazima  ufanywe  na  mamlaka.  Huo  ndio  utakuwa  ukamataji ( arrest).


Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa EAC kuhusu Burundi kufanyika mwishoni mwa mwezi Mei

0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) tarehe 25 Mei, 2015 kuhusu Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2015 kuhusu masuala ya amani na usalama nchini Burundi. Mkutano huo ambao umeitishwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya EAC, Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete utatanguliwa na Mkutano wa Baraza la Mawaziri.
Mhe. Membe akiendelea na mkutano wake na Waandishi wa Habari.Picha na Reginald Philip

TANZANIA PASSPORT RENEWAL – 2015, OHIO

0
0
Dates: May 29 – 31, 2015 (Friday & Sunday)
Time: 9:00am – 6:00pm
Location: 2432 Home Acre Dr, Columbus, OH 43231
Fees: $70 - only Cash and Money Order (Passport Fees & FedEx return)
Service Cost: $30/person - only cash.
All Tanzanians living OH & nearby states are welcome.
FOR MORE INFORMATION AND REQUIREMENTS, PLEASE VISIT: http://tanzaniaembassy-us.org/?page_id=79

For any question please contact Tanzania Columbus Community Association (TCCA):  jumuiyatanzaniaohio@yahoo.com
Tel: 614-378-8655, 614-312-6955, and 614-226-4216

Also, there will be Social Network hour for those who want to promote their business and want to learn what others are offering. Don’t forget your business cards and fliers to promote your business. Please do not miss this opportunity.

MAONYESHO YA PICHA ZA ALBERT MANIFESTER YAFANA JIJINI DAR

0
0
Mpiga Picha maarufu nchini, Albert Manifester, Mei 24 mwaka huu alifanya maonyesho ya baadhi ya picha alizopiga ikiwa ni sehemu ya kazi zake na baadhi ya picha zilizouzwa siku hiyo zilifanikisha kupatikana kwa kiasi cha shilingi milioni kumi na laki Tatu ambapo asilimia 50 ya mauzo hayo yalitolewa ili kusaidia huduma ya afya ya uzazi katika kijiji cha Kipamba kinachoishi watu wa jamii ya Wahadzabe.

Akizungumza katika hafla hiyo, Manifester alisema kuwa "picha inaongea haraka zaidi kuliko maneno, hivyo na amini kupitia jicho langu nitabadilisha maisha ya watanzania wengi, naanza na watanzania wenzetu Wahadzabe kuboresha huduma ya afya ya uzazi kwa wakina mama".
Mgeni rasmi katika hafla ya maonyesho ya picha zilizopigwa na Albert Manifester (kushoto), Mama Mwantum Malale (kulia) akipokea moja ya picha kama zawadi kutoka kwa mpiga picha huyo.
Mpiga Picha maarufu, Albert Manifester (kushoto) akionyesha sehemu ya kazi zake kwa Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya maonyesho ya picha, Mama Mwantum Malale wakati alipokuwa akitembelea shemu mbali mbali kuona picha hizo. Hafla hii ilifanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency, Jijini Dar es salaam.
Mpiga Picha maarufu, Albert Manifester (kushoto) akiwaeleza jambo, Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya maonyesho ya picha, Mama Mwantum Malale pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mh. Edward Ole Lenga wakati wa hafla hiyo.

GEPF WAANZA WIKI MAALUM (GEPF WEEK) KWA BONANZA LA WADAU WA MFUKO KUELEKEA MKUTANO MKUU WA SITA WA WADAU

0
0
Timu ya Mfuko wa Pensheni wa GEPF ikipasha kabla ya kuanza kwa bonanza maalum la wiki ya GEPF (GEPF Week) katika viwanja vya shule ya sekondari ya Popatlal.
Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa Mfuko wa GEPF Bi Joyce Shaidi akitoa neno la ufunguzi kabla ya kuanza rasmi kwa bonanza la wadau wa Mfuko wa GEPF. aliye mkono wake wa kushoto ni kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, Omary Ntungu.
Washindiwa Bonanza la GEPF timuya Chuo cha Utumishi cha Tanga wakifurahia ushindi baada ya kipenga cha mwisho kupulizwa.

NGOMA AFRICA BAND KUTUMBUIZA MJINI BREMEN,UJERUMANI JUMAMOSI 30 MAY 2015

0
0
 Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band almaarufu kama FFU-Ughaibuni yenye maskani yeke nchini Ujerumani,siku ya jumamosi 30 Mei 2015 bendi hiyo italitingisha hekalu la Uebersee Museum mjini Bremen,kuanzia Saa moja Usiku hadi kumekucha. 

Onyesho hilo la usiku usiokwisha limeandaliwa na utawala wa hekalu hilo la makumbusho la Uebersee Museum,ambapo utawala huo umeiomba bendi ya Ngoma Africa band kwenda kutumbuiza,kwa kuwa bendi hiyo ilitumbuiza mwaka 2013 na  kuvunja rekodi ya kuwavuta washabiki wengi kuliko bendi yeyote katika historia ya matamasha yafanyikao katika hekalu hilo.
Ngoma Africa band inayoongozwa na kamanda  Ras Makunja ni bendi pekee ya kiafrika yenye mvuto mkubwa barani ulaya,na washabiki wake wameipachika majina mengi ya kiusanii kama vile FFU-Ughaibuni,Viumbe wa ajabu  ANUNNAKI Alien's (himaya ya mazimwi wa Anunnaki), pia maarufu kwa majina kama Mzimu wa Muziki,na "Watoto wa Mbwa" . 

Ngoma Africa band pia inatajiri wa wanamuziki wenye vipaji vya hali ya juu wakiwemo yule mpiga solo mahiri Afande  Chris Bakottesa aka Afande Chris-B, Sanjint major Jo jo Sousa, wanamuziki chipukizi wengi walizalishwa na bendi hiyo ambayo inawanamuziki kumi.

Ngoma Africa band ilianzishwa mwaka 1993 na kiongozi wa bendi hiyo ambaye pia ni mtunzi wa nyimbo nyingi za bendi hiyo Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja.
unaweza kuwasikiiza FFU


unaweza kujumuika nao pia at ngoma4u@gmail.com
Viewing all 109597 articles
Browse latest View live




Latest Images