Wananchi wa Kata ya Makuyuni wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye aliwaambia kwa miaka mingi sasa jimbo la Vunjo limekuwa linarudishwa nyuma na ushabiki wa kisiasa na kuwataka wananchi hao kufanya maamuzi sahihi mwaka huu kwa kuichagua CCM.Ndugu Kinana ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wapo kwenye ziara ya siku tisa mkoani Kilimanjaro ya Kutekeleza,Kukagua na Kuhimiza Utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2010.
katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisikiliza moja ya swali lililokuwa likiulizwa na mmoja wakazi wa himo,Bi.Pepetua Shayo kuhusiana na mradi wa maji uliopo katika eneo hilo,ambapo baadhi ya wananchi wamechukuliwa maeneo yao bila kulipwa fidia yoyote.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofali kwenye mradi wa vijana wa kijiji cha Oria ,kata ya Kahe Magharibi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na Naibu Kamanda wa UVCCM , Moshi Vijijini,Innocent Shirima alipokuwa akiwasili katika kijiji cha Oria,Kata ya Kahe Magharibi,jimbo la Vunjo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye uwanja wa polisi Himo ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa muda umefika sasa wa kufanya maamuzi ya msingi kwa kuchagua kiongozi anayeweza kuleta maendeleo katika Jimbo la Vunjo.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyiaka kwenye viwanja vya polisi himo na kuwaambia wananchi hao wapinzani hawana tena ubavu wa kuongoza kwani kwa zaidi ya miaka mingi sasa wamepata nafasi na hamna walichokifanya kwa wananchi hao wa jimbo la Vunjo.
PICHA NA MICHUZI JR-VUNJO-MOSHI VIJIJINI