Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

Mwongozo wa mh. Al Shaimaa bungeni dhidi ya albino

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MBUNGE wa Viti Maalum (CCM), Al Shaimaa Kweigyir, ameitaka serikali kuhakikisha kwamba hukumu za watu wanaokutwa na hatia dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), zinafanyika kwa uwazi, sambamba na kutocheleweshwa ili kulinda roho za Watanzania wanaoendelea kuangamia.

Al-Shaimaa aliyasema hayo bungeni jana wakati akitoa maelezo binafsi kwa kupitia Kanuni ya Kudumu ya Bunge ya (50) 1 inayomtaka mbunge kwa ruhusa ya Spika kutoa maelezo binafsi yanayomhusu au yanayoigusa jamii moja kwa moja.

Mbunge huyo ambaye pia ni mlemavu wa ngozi alisema kwamba endapo hukumu za kesi za wahalifu wa albino zitahukumiwa mapema na kwa uwazi itatoa funzo kwa wengine wanaofikiria kufanya unyama dhidi ya albino hapa nchini.
Mbunge wa Viti Maalumu, Al-Shaymaa Kweigyir, akiomba mwongozo wa Spika bungeni jana mjini Dodoma, kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya watuhumiwa wa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino). 
Akiendelea kuongea kwa msisitizo juu ya mauaji ya albino Tanzania.

“Na mimi ni mhanga katika jambo hili kwa sababu watu wanaishi kwa mashaka, hivyo naomba hukumu za wahalifu hao ziwe wazi kila mtu aone ili iwe fundisho kwa waliofanya na wale wanaofikiria siku moja wajiingize kwenye unyama huo.

“Pia naomba sheria za mauaji zirekebishwe ili kulinda haki za walemavu mara baada ya kufanyiwa unyama sambamba na kuwapa adhabu kali wale wote wanaokutwa na hatia dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi,” alisema Kweigyir.

Kweigyir ni miongoni mwa wabunge wanaopigania haki za kuishi za watu wenye ulemavu wa ngozi, likiwa ni janga lililoshika kasi katika maeneo kadhaa ya Tanzania, hususan katika mikoa ya Kanda ya Ziwa kunakoonekana kushamiri vitendo vya kuwadhuru na kuwaua walemavu hao wa ngozi.


BIASHARA YA MIAMVULI JIJINI DAR

$
0
0
 Msimu huu wa neema ya Mvua hapa jijini Dar ndicho kipindi muafaka kabisa kwa wafanyabiashara ndogondogo kubadili biashara zao.Pichani ni mmoja wa wafanyabiashara hao akiuza mwamvuli kwa mteja wake waliekuwa kwenye gari.
mmoja wa wafanyabiashara hao akielekea kilingeni kwake baada ya kutoka kujumua miamvuli tayari kwa kuiuza kwa wateja wake.

Diamond Motors wazindua gari jipya la Mitsubishi 2015 ASX jijini Dar es Salaam

$
0
0
Wema Sepetu akiwasha gari Jipya la ASX Mitsubishi katika uzinduzi wa gari hilo jijini Dar es Salaam.
  Hili ndilo gari la ASX Mitsubish jipya lililozinduliwa wiki iliyopita katika hoteli ya serena jijini Dar es Salaam 

Millard Ayo, Wema wasifia gari jipya la 2015 Mitsubishi ASX.
Mtangazaji wa Clouds FM, Millard Ayo na mwigizaji maarufu nchini, Wema Sepetu wamesifia gari jipya la Mitsubishi ASX la mwaka 2015 linalouzwa na kusambazwa na kampuni ya Diamond Motors (Hansa Group).

Katika uzinduzi wa kutambulisha gari hilo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine Kampuni ya Diamond Motors wauzaji pekee wa magari kutoka Mitsubishi waliwaalika Millard Ayo na Wema Sepetu kujaribu gari hilo toleo jipya Mitsubishi ASX kabla ya uzinduzi. 

Mastaa hao walivutiwa na mwonekano wa Mitsubishi ASX lenye vioo vya kisasa juu vyenye mwanga unaomwezesha dereva na abiria kufurahia mwonekano wa pande zote.

Meneja mauzo wa Diamond Motors, Reena Ganatra alisema Gari hilo lenye luninga ndogo inayocheza DVD, iPods, Bluetooth na sauti kutoka vyanzo mbalimbali ni maalumu kwa vijana wa kisasa na familia kwani Mitsubish ASX  limetengenezwa na teknolojia ya MIVEC yenye kulifanya liwe na nguvu ya 150 ps katika 6,000 rpm na nguvu ya kuzunguka kwa mwendokasi mkubwa na kwamba limetengenezwa maalum kutumia mafuta kidogo. 

“ASX ni mwanzo tu, tunazo aina nyingine za magari kama kama Pajero ambayo tunakaribia kuyatambulisha sokoni ili kuwapatia watanzania magari imara na yenye kuaminika kutoka Mitsubishi” Alisema Ganatra. 

ASX toleo la 2015 limebuniwa kwa ubora wa hali ya juu na imara likiwa na bodi gumu pia lina mfumo maalumu usiotegemea funguo hivyo kumfanya mwendeshaji kuwasha injini kwa kubofya kitufe.

 “ASX kutoka Mitsubishi, imetengenezwa maalumu kukidhi mazingira ya Tanzania hasa mijini kama Dar es Salaam ambapo muda wowote dereva wa kawaida anatoka kwenye barabara nzuri na kuingia kwenye barabara zenye makorongo” alisema  Ganatra

Injini ya gari hilo ambayo ni 2.0-liter imeunganishwa INVECS-III CVT inayoisaidia mwendelezo wake katika kubadili mwendo pamoja na uimara wa usukani unaosaidia mikono ya dereva  kuwa salama hata anapokuwa katika mwendo mkali.

Hansa Group inayofanya biashara kama Diamond Motors Limited, imekuwa ikifanya kazi ya katika sekta ya usafirishaji tangu mwaka 1980, ikitoa huduma kwa wasambazaji na wadau wa usafiri.Kampuni hiyo huhusika na bidhaa/ huduma mbalimabali. Shughuli za Hansa Group zimesambaa karibu nchi zote za jumuia ya Africa ikitoa huduma kama vile za uchimbaji, Umeme, Mafuta na Gesi, Reli,Ulinzi, Ujenzi, Usafiri, kimataifa na jumuhia za kimataifa.

JIHADHARI NA MATAPELI: AJIRA YA WALIMU WAPYA WA SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO VYA UALIMU MWAKA 2015/16

KIBONZO

MSAFARA WA KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA WAPOKELEWA KWA FARASI MIKOCHENI -WILAYA YA MOSHI VIJIJINI

$
0
0
 Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana ukipokelewa kwa farasi wakati wakiwasili katika kata ya TPC kijiji cha Mikocheni wilaya ya Moshi Vijijni mapema leo asubuhi,tayari kwa kuanza ziara ya jimbo la Moshi Vijijini mkoa wa Kilimanjaro.Ndugu Kinana alizungumza na Wananchi wa kijiji hicho na kuzisikiliza matatizo yao,hasa suala la Ardhi.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwa ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wako mkoani Kilimanjaro katika ziara ya siku tisa ya Kusimamia,kuhimiza,Kukiimarisha na kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na  ikiwemo pia kusikiliza matatizo ya wananchi
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na ujumbe wake wakiwasili katika kijiji cha Magomeni mapema leo asubuhi,kulia ni Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini Mh.Dkt.Cyril Chami.
 Mkutano ukiendelea katika kijiji cha Mikocheni
 Wananchi wa Mikocheni wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipozungumza nao mapema leo asubuhi,katika jimbo la Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro.
 Wakazi wa kijiji cha Mikocheni wakishangilia jambo wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipozungumza nao na kusikiliza matatizoo yao mbalimbali yakiwemo ya Ardhi.
 Mwenyekiti wa Chama cha CHADEMA tawi la Mikocheni,wilaya ya Moshi Vijijini akitangaza kuhamia chama cha CCM,amapo pia alikabidhiwa kadi mpya ya CCM na kukabidhi kadi yake ya zamani kwa Ndugu Kinana.Pichani kushoto ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisikiliza kwa makini.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiliki kupiga ngoma wakati wakipokelewa katika ukumbi wa CCM mkoa .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akizunguma katika Mkutano wa Halmashauri kuu ya wilaya na kikao cha jimbo,ambapo Ndugu kinana alipokea taarifa ya chama na taarifa ya utekelezaji wa Ilani

PICHA NA MICHUZI JR-MOSHI VIJIJINI.

TBL YATOA MSAADA WA MABATI, SARUJI KWA WAATHIRIKA WA JANGA LA MVUA KAHAMA

$
0
0
 Mwenyekiti wa kamati ya maafa ya watu waliopatwa na janga la  mvua ya mawe  katika  kata ya Mwakata  ambae ni mkuu wa wilaya ya Kahama,  Benson Mpesya  wa katikati akipokea msaada wa vifaa vya ujenzi  mabati 176  na mifuko ya saruji 130  vilivyotolewa na kampuni ya bia  ya TBL  kulia anayekabidhi ni  meneja mauzo na usabazaji Godwin Zakaria na kushoto ni mjumbe wa kamati Patrick Kalangwa ambae ni mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala lengo la msaada huo ni kuunga mkono ahadi ya Rais Jakaya Kikwete ya kuwajengea nyumba wahanga hao.
 Mwenyekiti wa kamati ya maafa ya watu waliopatwa na janga la  mvua ya mawe  katika  kata ya Mwakata  ambae ni mkuu wa wilaya ya Kahama,  Benson Mpesya  wa katikati akipokea msaada wa vifaa vya ujenzi  mabati 176  na mifuko ya saruji 130  vilivyotolewa na kampuni ya bia  ya TBL  kulia anayekabidhi ni  meneja mauzo na usabazaji Godwin Zakaria na kushoto ni mjumbe wa kamati Patrick Kalangwa ambae ni mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala lengo la msaada huo ni kuunga mkono ahadi ya Rais Jakaya Kikwete ya kuwajengea nyumba wahanga hao.

 Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya  kushoto  ambae ni mwenyekiti wa maafa wa janga la mvua ya mawe lililowapata wananchi wa kata ya Mwakata wilayani Kahama  akipokea msaada wa vifaa vya ujenzi  mabati 176  na mifuko ya saruji  130  toka kampuni ya bia ya TBL , anayekabidhi kulia ni Meneja idara ya mauzo na usambazaji Godwin Zakaria na katikati ni Juma Akida ambae ni meneja mauzo kanda ya ziwa .
Wananchi wa kijiji cha Mwakata wilayani Kahama wakishusha msaada wa mabati yaliyotolewa na kampuni ya bia tanzania TBL kwa lengo la kuunga mkono ahadi ya Rais Jakaya Kikwete  ya kuwajengea nyumba wahanga wa kata hiyo walioathiriwa na mvua ya mawe ambako  kampuni hiyo imetoa mabati 176 na mifuko ya saruji 130 .

WATEJA WA DUKA LA WOOLWORTHS KUNUNUA KWA NUSU BEI PASAKA

$
0
0
Meneja Masoko wa maduka ya Woolworths Tanzania,Edwina Barongo akisisitiza jambo kwa wateja waliofika katika Uzinduzi wa punguzo la bei ya bidhaa zote zinazouzwa katika Maduka yote ya Woolworths yaliyopo Arusha na Dar es Salaam, Punguzo hilo litadumu kwa muda wa wiki Nne ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka.Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mgeni rasmi (Loyal Customer) Manfred Ngantunga (kulia) akizindua duka la Woolworths lililopo mtaa wa Ohio jengo la PPF Tower ikiwa ni sehemu ya kuzindua punguzo la bei nafuu kwa bidhaa zinazouzwa na kampuni hiyo katika maduka yaliyopo Arusha na Dar es Salaa.Katikati ni Meneja Mkuu wa Woolworths Tanzania Joehans Bushiri na Mkurugenzi wa fedha Samson Katemi(kushoto).Uzinduzi huo wa Punguzo la bei kwa asilimia 50 utadumu kwa muda wa wiki Nne ulifanyika jijini Dar es Salaam.
Mteja wa muda mrefu wa bidhaa zinazouzwa kwenye maduka ya Woolworths ambaye pia alikuwa Mgeni rasmi Manfred Ngantunga (katikati) akikabidhiwa zawadi na mfanyakazi wa duka hilo, baada ya kuzindua punguzo la bei la bidhaa kwa asilimia 50%zinazouzwa kwenye maduka ya hayo Tanzania, Kulia ni Meneja Mkuu wa Woolworths Joehans Bushiri,Hafla ya uzinduzi ilifanyika makao makuu ya woolworths jijini Dar es Salaam.
Meneja Mkuu wa kampuni ya Woolworths Tanzania, Joehans Bushiri akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa punguzo la bei kwa bidhaa zinazouzwa katika maduka yote ya Woolworth, kwa kipindi cha wiki Nne ikiwa ni sehemu ya ponguzo la kununua bidhaa bora kwa kipindi hiki cha sikukuu ya Pasaka.Hafla ya uzinduzi ilifanyika jijini Dar es Salaam.


MAKALA MAALUM: Azania ni shule ya Serikali iliyoibua viongozi lukuki

$
0
0
 Na Maneno Selanyika, Dar es Salaam

SERIKALI na wadau wa sekta ya elimu wanatakiwa kuboresha shule kongwe zilizopo hapa nchini kwa kuwa zina mchango mkubwa katika kulifikisha Taifa hapa lilipo.

Wasomi wengi waliostaafu, wanasiasa, wabunge na viongozi waliopo sasa madarakani wengi wao walisoma kwenye shule hizo ambazo kwa sasa zinakabiliwa na changamoto nyingi hasa za kitaaluma, hivyo kupoteza umaarufu wake.

Ikumbukwe tu kwamba shule ni sehemu ya kumwandaa kijana ili baadae aweze kukabiliana na changamoto za mazingira yanayomzunguka.

Ukizitaja shule hizo za zamani ni lazima Azania Sekondari iwepo kwani ni shule ambayo May 2 mwaka huu itatimiza miaka 81  tangu ianzishwe mwaka 1943.
Nyingine ni Tambaza, Jangwani na Zanaki.

Historia ya Azania

Akizungumza na MTANZANIA kuhusu maadhimisho ya miaka 81 ya Shule ya Sekondari Azania, Mkuu wa Shule, Benardi Ngozye anasema shule hiyo ilianzishwa na watu ambao walikuwa ni jamii ya Wahindi Weusi waliotokea nchini India, ambapo wakati huo ilikuwa ikiitwa Government India Primary School – Mtendeni. 

Mwaka 1939 shule hiyo ilibaddilishwa ikaitwa Government India Secondary School, ambapo baada ya mji kukua ikagawanywa mara mbili ya wasichana ambayo ni Jangwani kwa sasa na wavulana – Azania.

Ngozye anasema mwaka 1952 wavulana walihamishwa kutoka Mtendeni wakajengewa shule yao ambapo iliandikisha wanafunzi sita tu wa Kiafrika ndipo jina la Azania likazaliwa.

Anasema shule hiyo wakati ikianzishwa asilimia 95 ya walimu walikuwa si Waafrika na shule ilibaki kuwa ya wavulana hadi mwaka 1967 ilipotaifishwa wakaandikishwa wasichana 15 lakini baadae iliendelea kuwa ya wavulana pekee.

WAZIRI SITTA AZUNGUMZA NA WANAHABARI JUU YA UELEWA WA TAARIFA ZA HALI YA HEWA

$
0
0
Waziri wa Uchukuzi,Mhe. Samuel Sitta akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dkt. Agness Kijazi kabla ya kuanza kwa mkutano na wanahabari,wakati akizungumzia maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani ambayo hufanyika kila ifikapo Machi 23 kila mwaka.
Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Samuel Sitta akizyngumza na wanahabari (hawapo pichani) kwenye maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani yanayofanyika kila ifikapo Machi 23 ya kila mwaka, yenye kauli mbiu isemayo 'Uelewa wa hali ya hewa kwa maamuzi stahiki'. Pembeni yake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dkt. Agness Kijazi.

Muswada wa Sheria ya Mifumo ya Malipo nchini Wasomwa Bungeni leo

$
0
0
Na Anitha Jonas-MAELEZO,Dodoma.

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya amesoma Muswada wa Sheria ya Mifumo ya Malipo nchini wa mwaka 2015 kwa mara ya pili Bungeni Mjini Dodoma,Sheria hii imelenga kudhibiti wizi unaofanyika kupitia mitandao pamoja na kuhakikisha serikali inanufaika kwa kujipatia mapato.

Mhe.Mkuya alisema chimbuko la Muswada huo ni matokeo ya maboresho yaliyofanywa na Serikali katika sekta ya fedha nchini yaliyoanza mwaka 1990 na yanayoendelea mpaka sasa pamoja na maboresho katika sekta ya fedha yaliyosababisha kutungwa kwa sheria ya mabenki na taasisi za fedha za mwaka 2006 pamoja na sheria ya Benki kuu ya mwaka 2006.

“Lengo la Muswada huu ni kuboresha Usimamizi,Udhibiti na Kuimarisha Mifumo ya Malipo nchini,pamoja na kuiweka nchi katika mazingira mazuri ya ushindani wa kibiashara,halikadhalika kudhibiti changamoto zinazoweza kutokea katika sekta ya fedha na kutengeneza mazingira bora ya kiufanisi,”alisema Mhe.Mkuya.

Kwa upande wa maoni ya Kamati ya Upinzani yaliyosomwa na Mhe.Christina Lissu (Viti Maluum -CHADEMA) kwa niaba ya Mwenyekiti wa kambi ya upinzani ya Wizara ya Fedha Mhe.James Mbatia,Kamati ilishauri Serikali kuondoa ukomo wa faini na badala yake iwe inasomeka (zaidi ya) kwa ajili ya kumwachia Hakimu kupanga ukomo wa faini hiyo,hivyo serikali ifanye mabadiliko katika cha 20 (a) na (b).

Katika kipindi cha uchangiaji wa maoni Mhe.Musa Azza (Mb) wa Ilala naye aliishauri serikali kuunda chombo kitakacho simamia mihamala yote inayofanywa kupitia mtandao ili serikali iweze kujipatia mapato ambayo yatasaidia kuendeleza nchi yetu tofauti na sasa fedha nyingi zinapotea na serikali inakosa mapato.

Naye Mhe.Suzan Lyimo Mbuge wa Viti Maalum Chadema aliishauri serikali kuwa sheria hii iangalie suala la mifumo ya mtandao kuwa chini kwani hili limekuwa liliwagarimu sana wananchi,halikadhalika gharama zinazotozwa na makampuni ya simu katika Kutoa Pesa na Kuhamisha Pesa kama Mpesa,Tigopesa na Airtel Money.

Muswada huu na jumla ya sehemu 12 na Ibara 59 ambazo zimezingatia kuleta manufaa makubwa kwa wananchi pamoja kuiletea mapato serikali.
Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu na Bunge Mhe.Jenista Mhagama (Mb) akimsikiliza kwa makini Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.William Lukuvi wakati wa kikao cha bunge kikiendelea Mjini Dodoma.
Waziri wa Fedha Mhe.Saada Mkuya akisoma Muswada wa Sheria Mifumo ya Malipo wa Mwaka 2015 katika Mkutano wa 19, Kikao cha Sita Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Maji Mhe.Amos Makalla akijibu swali kwa lililoulizwa na Mhe.Prof.David Mwakyusa (Mb) wa (Rungwe Magharibi) Bungeni Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Anne Kilango akijibu swali liliulizwa na Mhe.Amina Makilagi Mbunge wa Viti Maalum lilohoji juu ya mchang’anuo wa ada za Vyuo vikuu vya Umma,Bungeni Mjini Dodoma .Picha zote na Anitha Jonas-MAELEZO,Dodoma.

Mteja wa Benki ya NBC Tawi Bukoba akabidhiwa zawadi kubwa ya gari la Promosheni ya Weka Upewe

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Muda wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Pius Tibazarwa (katikati) akikabidhi funguo kwa mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe, Josephat Ruyongo mkazi wa Bukoba, ya gari lake jipya alilojishindia la Nissan Hardbody katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa NBC, Mussa Jallow. Gari hilo lina thamani ya zaidi ya sh milioni 54.
Mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya Benki ya NBC, mkazi wa Bukoba, Josephat Ruyongo akifungua gari lake mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Mkurugenzi Mtendaji wa Muda wa NBC, Pius Tibazarwa (katikati), jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa NBC, Mussa Jallow.
Mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya Benki ya NBC, mkazi wa Bukoba, Josephat Ruyongo akiwasha gari lake tayari kwa safari ya Bukoba mara baada ya kukabidhiwa jijini humo leo.
Mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya Benki ya NBC, mkazi wa Bukoba, Josephat Ruyongo (katikati) akipozi kwa picha ya kumbukumbu pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo mara baada ya kukabidhiwa gari lake.

KATIBA INAYOPENDEKEZWA

VIONGOZI WA TANZANIA NA KENYA WAKUBALIANA KUKOMESHA BIASHARA HARAMU YA MAZAO YA MISITU

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki nchini Tanzania,Gladness Mkamba akizungumza mara baada ya kutia saini makubaliano kati ya Tanzania na Kenya kupiga vita biashara haramu ya mbao pamoja na mazao ya misitu inayofanyika kupitia mipaka ya nchi hizo katika mkutano uliofanyika jijini Arusha na Kuandaliwa na Shirika la kimataifa la kulinda wanyama na viumbe hai World Wildlife Foundation (WWF) ambao ni waandaaji na washirika wa makubaliano hayo pamoja na shirika la TRAFFIC .Picha picha zote na Mahmoud Ahmad,Arusha.
Viongozi kutoka serikali ya Tanzania na Kenya pamoja na Mashirika binafsi wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutia saini makubaliano kati ya Tanzania na Kenya kupiga vita biashara haramu ya mbao pamoja na mazao ya misitu inayofanyika kupitia mipaka ya nchi hizo katika mkutano uliofanyika jijini Arusha na Kuandaliwa na Shirika la kimataifa la kulinda wanyama na viumbe hai World Wildlife Foundation (WWF) ambao ni waandaaji na washirika wa makubaliano hayo pamoja na shirika la TRAFFIC.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira na Maliasili nchini Kenya Richard Lusiambe (wakwanza kulia) akiongozana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki nchini Tanzania Gladness Mkamba mara baada ya kutia saini makubaliano ya Tanzania na Kenya kupiga vita biashara haramu ya mbao pamoja na mazao ya misitu inayofanyika kupitia mipaka ya nchi hizo katika mkutano uliofanyika jijini Arusha na Kuandaliwa na Shirika la kimataifa la kulinda wanyama na viumbe hai World Wildlife Foundation (WWF) ambao ni waandaaji na washirika wa makubaliano hayo pamoja na shirika la TRAFFIC .

Rais Kikwete akagua waathirika wa Mafuriko Buguruni jijini dar leo

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Mack Sadik akimuonesha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete mfereji ulioziba kutokana na uchafu na kusababisha mafuriko katika makazi ya watu eneo la Buguruni Mnyamani jijini Dar es Salaam leo.
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipita katika mitaa mbalimbali ya Buguruni leo wakati wa zoezi la kuwafariji waathirika wa mafuriko huko Buguruni Mnyamani leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsalimia mtoto Irene ambaye nyumba yao imeathiriwa na mafuriko huko Buguruni Mnyamani leo.


JK alipotembelea eneo la Buguruni kwa Mnyamani jijini dar es salaam lililokumbwa na mafuriko leo

WAPIGA PICHA ZA PASSPORT MJINI MOSHI WATWANGANA MAKONDE

$
0
0
Wapiga picha katika eneo la Kilima cha Mawenzi wakioneshana uwezo wa kupigana masumbwi hata hivyo chanzo cha ugomvi huo hakikuweza kufahamika mara moja.

Video na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

mahafali ya maafisa wa polisi katika chuo cha taaluma ya polisi kurasini jijini Dar es salaam

2nd HEALTH TANZANIA HEALTH SUMMIT

JK atembelea waathirika wa Mafuriko Buguruni kwa mnyamani Ilala Dar es salaam Machi 24,2015

Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images