Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live

Hatua za mwisho za Maandalizi Mbio za Kilimanjaro Marathoni 2015

$
0
0
Mabango mbalimbali yakiwa yamewekwa maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi kuashiria kuanza kwa shamrashamra za mbio za Kilimanjaro Marathoni.
Baadhi ya wageni wakijiandikisha kukimbia mbio ndefu za kilometa 42 ambapo zoezi la uandikishaji linafanyika katika hotel ya Keys mjini Moshi.
Washiriki wa mbio za Kilometa 21 zinazodhaminiwa na kampuni ya mawasiliano ya Tigo wakijiandikisha kwa ajili ya kupata namba maalumu wakati wa kukimbia mbio hizo. 
Baadhi ya wakimbiaji wakijaza fomu kwa ajili ya kukimbia mbio ndefu za km 42. Picha zaidi BOFYA HAPA

DKT.MAGUFULI AFANYA UKAGUZI WA KIVUKO CHA MV DAR ES SALAAM

$
0
0
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amekagua kivuko cha MV Dar es salaam kinachotarajia kutoa huduma zake kati ya Dar es salaam na Bagamoyo na kuahidi kuwa kivuko hicho kitaanza kazi siku chache zijazo mara baada ya kukamilika kwa vituo vya maegesho. 
Akizungumza mara baada ya ukaguzi huo, Waziri Magufuli amewataka wakazi wa Dar es salaam na Bagamoyo kukitumia kivuko hicho ambacho kitawawezesha kufika katika maeneo yao kwa haraka na kuepuka usumbufu wa msongamano katikati ya jiji la Dar es salaam. 
“Tumieni kivuko hiki kwa uangalifu ili kidumu kwa muda mrefu, na sisi Serikali tutahakikisha tunaweka nauli nafuu ili kuwezesha wananchi wengi kumudu kutumia usafiri wa kivuko hiki, amesema Waziri Magufuli”. 
Waziri Magufuli amemtaka mkandarasi wa Ujenzi wa maegesho ya kivuko hicho ambae ni Kamandi ya Wanamaji wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kukamilisha ujenzi wa maegesho ya kivuko hicho mapema iwezekanavyo ili huduma za usafirishaji zianze mara moja. 
Kwa upande wake Mkuu wa MKoa wa Pwani Eng. Evarist Ndikilo ameipongeza Wizara ya Ujenzi kwa kuwezesha kupatikana kwa kivuko cha MV Dar es salaam ambacho kitafungua fursa za kiuchumi na kuleta maendeleo kwa wananchi. Aidha, Eng. Ndikilo ameiomba Wizara ya Ujenzi kuiendeleza barabara ya Bagamoyo- Zinga hadi Mbegani na kuhakikisha kuwa na usafiri wa basi moja kutoka Bagamoyo kwenda Mbegani na kuwepo maegesho ya magari yenye usalama. 
 Nae Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) Eng. Marceline Magessa, amesema kuwa maandalizi kwa ajili ya kuanza kazi kwa kivuko hicho yamekamilika ambapo tayari manahodha, mabaharia na mafundi watakaohudumia kwenye kivuko hicho wameshaajiriwa. 
 Aidha Eng. Magessa alibainisha kuwa Kivuko cha MV Dar es salaam kimetengenezwa na kampuni ya Western Marine Shipyard kutoka Denmark kwa takriban Shilingi bilioni 8 na kina uwezo wa kubeba abiria 300 wakiwa wamekaa. 
 Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Wanamaji ya JWTZ Meja Jenerali Rogasian Laswai, amemshukuru Waziri kwa kupewa kazi ya kujenga maegesho hayo na kuahidi kukamilisha kazi hiyo kwa wakati ili wananchi wanufaike na huduma za kivuko hicho mapema. 
Takriban vituo saba vinatarajiwa kujengwa kwa ajili ya maegesho ya kivuko hicho ikiwemo Magogoni, K awe, Jangwani, Rungwe Oceanic, Mbweni, Kaole na Mbegani. 
 IMETAYARISHWA NA KITENGO 
CHA MAWASILIANO SERIKALINI, WIZARA YA UJENZI.

Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akiwaita wakazi wa jiji la Dar es Salaam katika eneo la Ferry kwa ajili ya safari ya kwenda Bagamoyo na kurudi kwa safari ya majaribio kwa kutumia kivuko cha MV Dar es Salaam alichokikagua leo.

Kivuko cha MV Dar es Salaam kikiwa njiani kuwasili eneo la Magogoni kwa ajili ya kuanza safari ya kwanza ya majaribio ya kwenda Bagamoyo mkoani Pwani.Kivuko hiki kinauwezo wa kubeba abiria zaidi ya 300.

Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakipanda kivuko cha MV Dar es Salaam kwa ajili ya Safari ya majaribio ya kwenda Bagamoyo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo akimpokea Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili Bagamoyo na Kivuko cha MV Dar es Salaam.

Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli katikati akiwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Raymond Mushi kushoto wakiwa safarini kuelekea Bagamoyo Mkoani  Pwani, akiwa na Kamanda wa Navy, Meja Jenerali Rogastian Laswai
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliopata fursa ya kupanda kivuko hicho wakitazama madhari ya jiji wakati wakiwa safarin

WAZIRI MKUU AENDELEA NA ZIARA YAKE MKOA WA MBEYE,LEO YUPO WILAYANI KYELA

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mkuu wa Zamani wa Mkoa wa Mbeya Mzee John Mwakipesile baada ya kuwasili kwenye makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela kwa ziara ya siku moja wilayani humo Februari 26, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu wa CHADEMA wa kata ya Mwaya, Ageni Pamesa kabla ya kufungau maabra ya shule ya sekondari ya Mwaya akiwa katika ziara ya Mkoa wa Mbeya Februari 26, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikata utepe kufungua maabara ya shule ya sekondari Mwaya wilayani Kyela akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Februari 26, 2015. Kushoto ni Mkewe Tunu na wapili kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kyela anayeondoka Margareth Malenga.

USIKOSE KUFATILIA MICHEZO YA LIGI KUU YA UINGEREZA KUPIA SUPERSPORT NDANI YA DSTV

BLOGGERS KUKUTANA KESHO KATIKA HOTELI YA SERENA JIJINI DAR ES SALAAM KATIKA PATI YA KIHISTORIA

$
0
0
 Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network  (TBN) na mmiliki wa Blog ya The Habari.com Joachim Mushi (katikati) akizungumza wakati wa mkutano na waandishi. Kutoka kushoto ni  mjumbe wa TBN Mkala Fundikira,  Afisa wa kampuni ya mawasiliano na matangazo ya AIMS, Shafiq Mpanja wa AIM, Ofisa Uhusiano wa NMB Doris Kilale na mjumbe wa TBN Khadija Kalili.
Katika mkutano huo TBN imesema kesho Jumamosi jioni Bloggers takriban 100 kutoka sehemu mbalimbali nchini watakutanika katika ukumbi wa hoteli ya Serena jijini Dar es salam kwa ajili ya hafla ya mwaka mpya itayohudhuriwa pia na wadhamini na marafiki wa Bloggers.
 Ofisa Uhusiano wa NMB Doris Kilale akifafanua jambo wakati wa mkutano.
 Mmiliki wa Blog ya Bongoweekeend Khadija Kalili akizungumza wakati wa mkutano.
 Father Kidevu (kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano.
Baadhi ya Bloggers na waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari wakifuatilia jambo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari Maelezo Dar es Salaam.

MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHI MASHINE YA KUPIMIA SARATANI YA MATITI KWA AKINA MAMA HOSPITALI KUU YA JESHI LUGALO

$
0
0
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete akikabidhi mashine ya kupimia saratani ya matiti kwa akina mama kwa uongozi kwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Luteni Jenerali Samuel Ndomba (kulia). Hafla ya makabidhiano hayo ilifanyika kwenye Hospitani Kuu ya Jeshi Lugalo kwenye Kitengo cha Uzazi na Mtoto kilichoko Mwenge tarehe 27.2.2015. Aliyesimama pembeni kwa Mama Salma ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donan Mmbando na aliyesimama kulia kwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi ni Mkuu wa Hospitali Kuu ya Jeshi ya Lugal Brigedia Jenerali Josia Mwita Makere.
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Samuel Ndomba akitoa hotuba wakati wa hafla ya kukabidhi mashine ya kupima saratani ya matiti kwa akina mama katika Hospitali ya Lugalo tarehe 27.5.2015.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akitoa hotuba yake muda mfupi kabla ya kukabidhi mashine ya kupimia saratani ta matiti kwa akina mama kwenye Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo. Hafala hiyo ilifanyika kwenye Kitengo cha Uzazi na mtoto cha hospitali hiyo kilichoko eneo la Mwenge hapa Dar tarehe 27.2.2015.

KINANA AKUTANA NA KAMATI KUU YA CHAMA CHA SPLM CHA SUDANI YA KUSINI

$
0
0

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumzana na Kamati Kuu ya Chama Cha SPLM ambapo alipeleka ujumbe maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,kikao hicho kilikuwa chini ya Mwenyekiti wa chama cha SPLM ambaye pia ni Rais wa Sudan ya Kusini Rais Salva Kiir, Ikulu mjini Juba.
 Mwenyekiti wa chama cha SPLM ambaye pia ni Rais wa Sudan ya Kusini Rais Salva Kiir akiongoza kikao maalum cha Kamati Kuu ambacho Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alihudhuria.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiagana na Rais wa Sudan ya Kusini Rais Salva Kiir mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu cha chama cha SPLM ,kikao hicho kilimalizika usiku wa manane mjini Juba ,Sudan.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa kikao maalum cha Kamati Kuu ya chama cha SPLM mjini Juba,kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa SPLM ambaye pia ni Makamu wa Rais wa nchi hiyo James Wani.

TUZO ZA WASANII BORA WA MUZIKI WA ZANZIBAR MWAKA 2015

$
0
0
Mkurugenzi wa Biashara Zanzibar Nd. Mohamed Baucha wa kulia akimkabidhi Tunzo ya Video bora ya mwaka muziki wa kizazi kipya Nassir Hassan (Vanila) mara baada ya kuibuka mshindi, tunzo hizo zimeandaliwa na Kampuni ya Zanzibar Media Corporation LTD katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Salama Hall  Bwawani Mjini Zanzibar.
 Mwanamitindo marufu wa Zanzibar Farouk Abdillahi akimkabidhi Tunzo ya Video bora mwaka ya Taraab Bi. Saada Nassor
 Meneja wa Zenji Entertainment Seif Moh'd (kushoto) akimkabidhi tunzo Mwanamuziki Bora wa kiume wa tarabu asili Cholo Ganun
 
 Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora)  Dkt. Mwinyihaji Makame akimkabidhi tunzo ya muandaaji bora wa Tamasha Zanzibar Music Award mwaka 2015 Mbunge wa Jimbo la Uzini na Mkurugenzi wa Redio ya Zenji FM Mohamed Seif Khatib katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Salama Holl Bwawani Mjini Zanzibar. 
 Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Dkt. Mwinyihaji Makame katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Kampuni ya Zanzibar Midia Corporation LTD. Picha zote na Makame Mshenga wa Maelezo Zanzibar. Picha zaidi BOFYA HAPA


JAJI MKUU AENDELEA NA ZIARA YA KIKAZI MKOANI TABORA

$
0
0
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania (kulia), akijadili jambo na Mhe. Ludovick Mwananzila, Mkuu wa Mkoa wa Tabora alipotembelea Ofisi ya Mkoa wa Tabora alipokuwa katika ziara yake ya kikazi ya kutembelea Mahakama mkoani humo.
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania (kulia), Mhe. Ludovick Mwananzila, Mkuu wa Mkoa wa Tabora (katikati), Mhe. Jaji Amir Mruma, Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Kanda ya Tabora (kushoto), wakitoa nje ya jengo la Ofisi ya Mkuu wa Tabora, mara baada ya Mhe. Jaji Mkuu na ujumbe alioambatana nao kumsalimia Mkuu huyo wa Mkoa.
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikati), Mhe. Jaji Amir Mruma, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Tabora (wa pili kushoto), Mhe. Sam Rumanyika, Jaji wa Mahakama Kuu,Kanda ya Tabora (wa pili kulia), Mhe. David Mrango, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Tabora (wa kwanza kulia),na Mhe. Jaji Leila Mgonya, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora (wa kwanza kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Mahakama ya Mkoa wa Tabora. (Picha na Mary Gwera, Mahakama)

Mh. Al Shaimar kwa ushirikiano na Bayport wa wazitembelea familia za watoto Albino waliopoteza maisha Jijini Mwanza

$
0
0
Meneja Mauzo wa Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services Kanda ya Ziwa, Lugaano Kasambala, akimpa pole Ester Jonas, mama wa Yohana Bahati, mtoto mwenye ulemavu wa ngozi albino, aliuawa mkoani Mwanza, hivi karibuni. Mama huyo anatibiwa katika Hospitali ya Bugando baada ya kupata mareraha katika tukio la kuvamiwa na kuporwa mtoto wake. Kulia kwa Kasambala ni Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir mwenye miwani waliyeambatana katika safari hiyo kwa ajili ya kuwapa pole na kuwafariji.

Na Mwandishi Wetu, Mwanza
MBUNGE wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir kwa ushirikiano na Taasisi ya Kifedha, inayojihusisha na mikopo ya Bayport Financial Services yenye Makao yake Makuu jijini Dar es Salaam, Tanzania, walifanya ziara ya siku mbili jijini Mwanza kwa ajili ya kutembelea familia mbili zilizopoteza watoto wao wawili ambao ni walemavu wa ngozi.

Familia hizo ni ya Ester Jonas, mama wa marehemu Yohana Bahati na ile ya Sofia Juma mama wa mtoto Pendo Emmanuel, wote wakiwa ni watu wenye ulemavu wa ngozi, huku familia zote mbili zikipewa Sh Milioni 2 kila moja.
Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir mwenye miwani akimfariji mama wa Yohana Bahati (Ester Jonas) aliyelazwa Hospitali ya Bugando, Mwanza, pamoja na kumpaa mafuta ya kupaka kwa ajili ya watoto wake wawili ambao nao ni albino,. Kushoto kwa Mh Shaimar ni Meneja Mauzo wa Bayport Financial Services Kanda ya Ziwa, Lugano Kasambala na wafanyakazi wengine wa Bayport waliombatana pamoja kwenye msafara huo wa kutoa pole.

ZIARA YA WAZIRI MKUU WILAYANI RUNGWE

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka jiwe la Misingi la ujenzi wa nyumba za watunmishi wa Halmashauri ya Busokeleo wilayani Tukutu unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika kijiji cha Rungwa akiwa katika ziara ya mkoa wa Beya Februari 27, 2015. Wapili kushoto ni mkewe Tunu.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akigua nyumba zinazojengwa na Shirikal la Nyumba la Taifa (NHC) karika kijiji cha Rungwa kwa ajili ya watumishi wa Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Februari 27, 2015. Watatu kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mark Mwandosy na wapili kushoto ni Mkurugenzi wa NHC, Haikaman Mlekio.
Mke wa Waziri Mkuu, Mamam Tunu Pinda akivalishwa kitenge na bibi Hilda Mwasikili katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda mjini Tukuyu Februari 27, 2015. 

Waziri Fenella akutana na wasanii nchini

$
0
0
Waziri wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akimueleza jambo Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Francis Michael wakati wa mkutano na wasanii uliofanyika katika ukumbi wa uwanja mpya wa Taifa leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Idara ya Utamaduni kutoka Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Prof. Herman Mwansoko akiongea na wasanii nchini na kuwaeleza kuhusu umuhimu wa sekta hiyo kushiriki kikamilifu katika masuala ya kitaifa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea upatikanaji wa Katiba Mpya, Kulia ni Katibu wa Bodi ya Filamu Bi. Joyce Fisoo.
Waziri wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akiongea na wasanii nchini na kuwaasa wasanii kuielimisha na kuhamasisha Jamii kuhusu Katiba Inayopendekezwa kupitia kazi mbalimbali za sanaa, wakati wa mkutano na wasanii nchini uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

WAVAMIZI NA WAMILIKI WA ARDHI KINYUME CHA SHERIA JIJINI DAR KUKIONA, KUKUMBWA NA BOMOA BOMOA

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Alphayo Kidata (kulia) bakitoa tathmini ya zoezi la bomoa bomoa awamu ya tatu linaloendelea katika Manispaa ya Kinondoni jana jijini la Dar es salaam.Kulia ni Muhandisi wa Manispaa ya Kinondoni Baraka Mkuya.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Bw. Alphayo Kidata (hayupo pichani) alipokuwa akitoa tathmini ya zoezi la bomoa bomoa kwa wananchi waliovamia maeneo yanayomilikiwa kisheria na watu wengine katika manispaa ya Kinondoni jana jijini Dar es salaam.
Moja ya ukuta uliojengwa kinyume cha sheria katika eneo lisiloruhusiwa eneo la Tegeta ukibomolewa jana.

Rais Kikwete aongoza kikao cha Kamati kuu ya CCM ikulu Dar es Salaam

$
0
0
Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya taifa ikulu jijini Dar es Salaam leo.Wapili kulia ni Rais wa Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein na wawatu kulia ni makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal.Kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwaongoza wajumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kusimama kwa dakika chache kumkumbuka mjumbe wa baraza la wawakilishi wa jimbo la Magomeni Zanzibar ambaye pia alikuwa mjumbe wa kamati hiyo leo wakati wa kuanza kikao cha kamati hiyo ikulu jijini Dar es Salaam.(picha na Freddy Maro)

MKOA WA DODOMA UMEPOKEA NAKALA 61,290 ZA KATIBA INAYOPENDEKEZWA KWA AJILI YA KUZIGAWA KWA WANANCHI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mapokezi ya nakala za katiba inayopendekezwa na maendeleo ya usambazaji wake kwa wananchi Mkoani Dodoma mapema leo.
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (hayupo pichani) wakati akiwasilisha taarifa ya mapokezi na usabazaji kwa wananchi wa Nakala za katiba inayopendekezwa Mkoani Dodoma mapema leo.

Kumekucha ‘Chicken Wings Bonanza & Family Day Out’ leo Februari 28

$
0
0
Na Andrew Chale
Bonanza kubwa la Nyama ya kuku ‘’Chicken Wings’ linaendelea muda huu huku watu mbalimbali wameanza kumiminika marafiki na familia mbalimbali leo  Februari 28, ndani ya Azura Beach Club, Kawe, Jijini Dar es Salaam.
Akieleza hilo muda huu haapa katika viwanja ghivi linapoendelea Bonanza hili la Chicken Wing, Bonanza & Family oUT', Mkurugenzi Mtendaji  wa kampuni ya Jaunt Africa Ltd, Acquiline  Mlulla waandaji wa Bonanza hilo  Amesema watu mbalimbali wameanza kujitokeza tokea asubuhi huku wakifurahia vyakula, vinywaji na muziki bila kusahau nyama safi ya kuku ambayo inapamba Bonanza hili kwa leo.
“Bonanza la ‘Chicken Wings,  ni  la kipekee kwani si la kukosa kabisa leo Februari 28,  kwa kiingilio cha sh 10,000 kwa watu wazima na sh 4,000 kwa watoto. mlango tiketi zote zinapatikana. ni kuanzia sasa hadi usiku" alieleza Acquilina Mlulla.
Mtandao huu utaendelea kukuletea matukio mbalimbali hapo baadae.Kwa muda huu michezo mbalimbali inaendelea ikiwemao watoto kufurahia michezo ya swiming pool, castle camp, muziki na matukio ya ‘surprise’ kwa anayefika.
Bonanaza hilo limedhaminiwa na Jaunt Africa Ltd, Dodoma Wine, Hot Spot Magazine, Coca- Cola, Michuzi Media Group na wengine wengi.
For updates or to find out more about CHICKEN WINGS BONANZA, please contact us at: +255 755 048 362 or +255 658 289 737 Email: info@jaunt-africa.com  or SKPE: acquiline.mlulla

SIMBA YAIPIGISHA KWATA TANZANIA PRISONS, YAIFUNGA 5-0

$
0
0
 Beki wa Simba, Mohamed Hussein akiwatoka wachezaji wa Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Beki wa Tanzania Prisons akichuana na mshambuliaji wa Simba.
Wachezaji wa timu ya Simba wakishangilia ushindi wa timu yao baada ya kuifunga Tanzania Prisons 5-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Mohamed Hussein wa Simba akiwania mpira na beki wa Tanzania Prisons, Lugano Mwangama.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Mnuso wa Tanzania Bloggers Network (TBN) funika bovu dar es salaam serena hotel usiku huu

$
0
0
Mgeni Rasmi Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania Mhe Kajubi Mukajanga (kati) akiwa na Ankal na Anko John Kitime
Kutoka kushoto ni Woinde Shizza, Othman Michuzi, Pam Mollel, Zainul Mzige  na Karim 
Mgeni Rasmi Mhe Kajubi Mukajanga akikata ndafu wa TBN. Kushoto kwake ni mwakilishi wa Ubalozi wa Marekani na kulia ni Kelvin Twissa, Mdhamini mkuu wa Mnuso huo pamoja  na Rachel Pallangyo wa TBN
Mkuu wa ukumbi (floor manager) Monica Joseph Mara akiongoza wana TBN kuserebuka

 Ankal akiwa na ubavu wake (kulia) na ubavu wa Bongo Celebrity a.k.a Mama Amaya
 Nyota wa mchezo hapa ni Gadiola toka Arusha (mbele kati)
 Msoma risala mkuu wa TBN Henry Mdimu akiwa na bloggers wenzie 
 Wana TBN katika picha ya pamoja
 Ankal akiwa na Max wa Jamii Forums ambao wote ni waasisi wakuu wa TBN

 Nyota hapa ni blogger toka Bukoba Ruta (Blue T-shirt) akiwa na blogger wa Dar, Arusha  na Kilimanjaro
Mwanachama mkongwe wa TBN Kaka Omar Swai (wa pili kushoto) akiwa na wana libeneke toka Arusha Pam Mollel (shoto), Woinde Shizza (kulia) na Mama Ankal

HAFLA YA TANZANIA BLOGGERS NETWORK YAFANA SANA,SERENA HOTEL JIJINI DAR

$
0
0
Sehemu ya Wamiliki wa Blogs mbali mbali hapa nchini wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi katika hafla maalum ya mwaka kwa Tanzania Bloggers Network,ambaye ni Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT),Ndg. Kajubi Mukajanga pamoja na baadhi ya wadhamini waliofanikisha hafla hiyo,iliyofanyika usiku huu kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam.
Mgeni Rasmi katika hafla maalum ya mwaka kwa Tanzania Bloggers Network,Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT),Ndg. Kajubi Mukajanga (wa pili kulia) akizungumza jambo na baadhi ya Wamiliki wa Blogs Tanzania,waliokutana pamoja leo kwa lengo la kufahamina na kuunganisha vyema umoja wao.

Mkurugenzi wa Masoko kwa Kampuni ya Simu ya Vodacom Tanzania ambao ndio walikuwa wadhamini wakuu,Kelvin Twissa akizungumza machache katika hafla hiyo. 

AU 

MAAMUZI YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM HAYA HAPA

Viewing all 110025 articles
Browse latest View live




Latest Images