Ndugu, Issa Wahichinenda Mkurugenzi wa uendeshaji wa UTT AMIS akitoa maada kuhusiana na fursa za uwekezaji katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja kwa wafanyakazi wa ofisi ya Mkaguzi wa hesabu za serikali katika kikao cha baraza la wafanyakazi kilicho fanyika hivi karibuni Mtwara.
UTT AMIS ndiyo magwiji katika kuanzisha na kuendesha Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja (Mutual Funds) hapa nchini. Mpaka sasa UTT AMIS inaendesha mifuko mitano ambayo ni Mfuko wa Umoja, Mfuko wa Wekeza Maisha, Mfuko wa Watoto, Mfuko wa Kujikimu na Mfuko wa Ukwasi yenye jumla ya thamani ya Shilingi bilioni 235.
Mifuko yote hii imeweza kukidhi vigezo muhimu vya uwekezaji ambavyo ni Usalama,Ukwasi na Faida (Safety, Liquidity and Returns). Mifuko hii inayoendeshwa na UTT AMIS ni kwa ajili ya watanzania wote, vikundi, Saccos, taasisi, kampuni na mifuko ya hifadhi za jamii. Wawekezaji wote wananufaika kwa kupata faida shindani, uwekezaji mseto ili kupunguza hatari za uwekezaji,utalaamu wa meneja wa mifuko,unafuu wa mkubwa wa gharama na uwazi kwani bei halisi ya vipande vya mifuko hutangazwa kila siku za kazi.
Baadhi ya washiriki wa kikao cha baraza la wafanyakazi la ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali wakifuatilia uwasilishwaji mada kuhusiana na fursa za uwekezaji katika mifuko ya Pamoja inayoendeshwa na UTT AMIS.