Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

KAMATI YA MUDA YA BLOGGERS TANZANIA YAANZA KUPITIA RASIMU YA KATIBA

$
0
0
  Mwenyekiti wa Muda wa Jumuiya ya Wamiliki wa Mitandao ya Jamii Tanzania (Bloggers), Joachim Mushi (kulia), akizungumza wakati akifungua majadiliano kwa wajumbe wa kamati ya muda ya Jumuiya ya wamiliki wa mitandao ya jamii Tanzania ya kujadili rasimu ya Katiba ya umoja huo Dar es Salaam leo. 
Majadiliano hayo yameanza jana kujadili rasimu ya katiba kabla ya kuipitisha kwa hatua za usajili wa Jumuiya ya Wamiliki wa Mitandao ya Jamii Tanzania (Bloggers).  Kushoto ni Mjumbe wa Kamati hiyo ya muda kutoka Zanzibar, Othman Maulid "Mapara".
 Katibu Msaidizi wa Jumuiya ya Wamiliki wa Mitandao ya Jamii Tanzania , Shamim Mwasha (kushoto),akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo wakati wa mapitio ya rasimu hiyo. Kulia ni Mjumbe wa Kamati,  Henry Mdimu.
 Mwenyekiti wa Muda wa Jumuiya ya Wamiliki wa Mitandao ya Jamii Tanzania (Bloggers), Joachim Mushi (wa pili kushoto), wakati akifungua majadiliano kwa wajumbe wa kamati ya muda ya Jumuiya ya wamiliki wa mitandao ya jamii Tanzania ya kujadili rasimu ya Katiba ya umoja huo Dar es Salaam leo. Majadiliano hayo yameanza jana kujadili rasimu ya katiba kabla ya kuipitisha kwa hatua za usajili wa Jumuiya ya  Wamiliki wa Mitandao ya Jamii Tanzania (Bloggers). Kutoka kushoto ni Mjumbe, Othman Maulid, Katibu Msaidizi wa Wamiliki wa Mitandao ya Jamii Tanzania , Shamim Mwasha,  Henry Mdimu (Mjumbe), Mariam Ndabaganga (Mjumbe) na William Malecela (Mjumbe).
Wajumbe wa kamati hiyo wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mkutano wao uliofanyika katika Mgahawa wa MOG Lounge, jijini Dar es Salaam leo asubuhi.

WAZIRI WA UCHUKUZI DK. HARRISON MWAKYEMBE AZINDUA JENGO LA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA

$
0
0
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe (wa tatu kutoka kulia ) Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya kudumu ya Miundombinu Mhe. Peter Serukamba , Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu Serikali ya Mapunduzi ya Zanzibar, Dk. Juma Akir (kushoto) Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usafii wa Anga Tanzania(TCCA) ambaye pia ni Msaidizi wa Rais wa Mambo ya Kanda, Dk. Nyamajeje Weggoro, wakishirikiana kukata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la TCAA. Uzinduzi huo ulikua sehemu ya maadhimisho ya Siku yaKimataifa ya Usafiri wa Anga Duniani(ICAD)
Waziri wa Uchukuzi, Mh. Dk. Harrison Mwakyembe, akizindua jengo la Makao Makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA). Uzinduzi huo ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga Duniani(ICAD). Anayeshuhudia kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu TCAA, Bw. Charles Chacha.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania, Charles Chacha(Kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Uchukuzi, Mh. Dk. Harrison Mwakyembe wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga Duniani(ICAD) yaliyofanyika kwenye viwanja vya TCAA. Katiti ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Peter Serukamba.

TAHADHARI KUTOKA MICHUZI MEDIA GROUP.

$
0
0

MKURUGENZI MTENDAJI WA KAMPUNI YA MICHUZI MEDIA GROUP (MMG) ANAPENDA KUTAHADHARISHA WADAU POPOTE WALIPO KUHUSIANA NA UJUMBE (PICHANI) AMBAO UPO KWENYE FACE BOOK NA HATA KWENYE TWITTER) KWAMBA UJUMBE HUO  HAUHUSIANI KWA LOLOTE NA ANKAL MUHIDIN ISSA MICHUZI,  WALA MMG AMA WAKALA WAKE. 

HIVYO TUNAWASIHI TUSIHUSISHWE NAYO NA PIA TUNAWAOMBA KUWA MACHO NA MAMBO KAMA HAYA,MAANA ULAGHAI NA UTAPELI MITANDAONI NI MWINGI MNO.

AHSANTENI SANA
ANKAL

USIKUBALI KUIBIWA

KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA AMANI ORPHANAGE CENTER CHA POKEA ZAWADI NA MSAADA WA MAANDALIZI YA KRISMASI KUTOKA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF.

$
0
0
Kushoto ni Meneja wa Pwani wa PSPF Msafiri S. Mugaka  akiwa na Afisa Mahusiano wa PSPF Coleta Mnyamani wakiwakabidhi zawadi ya Mbuzi  kwa ajilli ya Krismasi watoto wa kituo cha kulelea yatima cha Amani Orphanage Centre tarehe 5.12.2014
 Afisa Mahusiano wa PSPF Coleta Mnyamani akimkabidhi zawadi ya vinywaji mmoja wa watoto katika kituo hicho
 Meneja wa Pwani wa PSPF Msafiri S. Mugaka akimkabidhi mmoja wa watoto msaada wa mafuta ya kupikia kwa niaba ya watoto wenzake walipo watembelea katika kituo chao huko  Zinga Bagamoyo.

JHIKOMAN & AFRIKABISA BAND KUTINGISHA JIJI LA DAR DSEMBA 12, 2014

$
0
0
 Mfalme wa mziki wa Reggae barani Afrika Jhikoman mwenye makao yake mijini Bagamoyo,aiongoza bendi yake Afrikabisa katika shamra shamra za sherehe za kuadhimisha siku ya uhuru wa Tanganyika. Onyesho hilo linawashirikisha wasanii wengi.
Mahali; Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni,mkabala na chuo cha usimamizi wa fedha (IFM).Barabara ya Samora, mtaa wa Shaabani Robert kati ya Jiji la Dar-Es-Salaam.
  Sehemu ya ukumbi wa  Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni,mkabala na chuo cha usimamizi wa fedha (IFM).Barabara ya Samora, mtaa wa Shaabani Robert kati ya Jiji la Dar-Es-Salaam. 
  Mfalme wa mziki wa Reggae barani Afrika Jhikoman akiwa na mwanamuziki Mkongwe Tabia Mwanjelwa katika moja ya shoo zake nchini Ujerumani hivi karibuni
 Sehemu ya ukumbi wa  Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni,mkabala na chuo cha usimamizi wa fedha (IFM).Barabara ya Samora, mtaa wa Shaabani Robert kati ya Jiji la Dar-Es-Salaam.

SIMBA YASHINDWA KUIFUNGA EXPRESS YA UGANDA NYUMBANI, ZATOKA 0-0, UWANJA WA TAIFA LEO

$
0
0
 Magolikipa wa Simba, Manyika Peter na Ivo Mapunda  wakifanya mazoezi ya viungo kabla ya mchezo wao wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya The Express ya Uganda, katika mchezo huo timu hizo hazikufunga. 
(Picha zote na Francis Dande)
Katongole Henry akimtoka mshambulia wa Simba, Ramadhani Singano 'Mess'.
Kipa wa The Express, Mutumba Ivan akiruka juu kuokoa moja ya hatari langoni mwake.
Beki wa Simba, Nasoro Masoud akimtoka mchezaji wa The Express ya Uganda wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

 Ramadhani Singano 'Mess' akitafuta mbinu za kumtoka beki wa The Express, Katongole Henry.
Kipa wa The Express ya Uganda, Mutumba Ivan.
Elius Maguri akipata matibabu baada ya kuumia.

wadau hassan na Emmanuel walamba nondozzzz Chuo Kikuu Mzumbe

$
0
0
Wadau wakipozi  Hassan  Kindole (kulia) na Emmanuel Gasper    baada ya kula nondozzzz zao katika mahafali ya 13 ya Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro Ijumaa. Wadau wamelamba nomndozzz za  shahada ya menejimenti ya Rasilimali witu (Bachelor of Human Resource Management) 

kampuni ya selcom wireless yaipiga jeki Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini (taswa)

$
0
0

Meneja  Biashara, ukuzaji na Masoko wa kampuni ya Selcom Wireless, Juma Mgori (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na udhamini wa Tuzo za wanamichezo bora za Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa). Kampuni hiyo imetoa udhamini wa Sh Milioni 30. Kushoto ni Gallus Runyeta ambaye ni Meneja Miradi wa kampuni hiyo na kulia ni Mwenyekiti wa Taswa, Juma Pinto

ngoma azipendazo ankal

JESHI LA POLISI-KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI NA VODACOM WAENDESHA ZOEZI LA UTOAJI ELIMU NA UPIMAJI WA VILEVI MWILINI KWA MADEREVA

$
0
0
 Afisa wa Jeshi la Polisi – Kikosi cha Usalama Barabarani akimpima kiwango cha pombe mwilini dereva wa basi la kwenda mikoani, Steven Mwakibolo kwa kutumia kifaa maalum wakati wa upimaji madereva ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni ya Usalama Barabarani  inayodhaminiwa na Vodacom Tanzania. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa kampuni hiyo Rosalynn Mworia, akifuatilia kwa karibu zoezi hilo lililofanyika leo katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, akimuelimisha dereva wa basi liendalo mkoani Elias Samu kuhusiana na pete ya kidoleni inayotolewa na Vodacom Tanzania kwa ushirikiano na jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani yenye ujumbe “Wait To Send” unaohamasisha madereva wa vyombo vya moto kutokutumia simu za mkononi wakati wakiwa wanaendesha vyombo hivyo. Zoezi hili lilifanyika leo katika kituo cha mabasi yaendayo mkoani cha Ubungo jijini Dar es Salaam katika mwendelezo wa kampeni ya Usalama Barabarani inayodhaminiwa na kampuni hiyo.
 Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga akiwafafanulia jambo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia (kushoto) wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na  Henry M. Bantu wakati wa zoezi la upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva wa mabasi yaendayo mikoani lililofanyika leo katika kituo cha mabasi cha Ubungo jijini Dar es Salaam. Zeozi hilo ni mwendelezo wa kampeni ya Usalama Barabarani  inayodhaminiwa Vodacom Tanzania.
 Maafisa wa Kikosi cha Usalama Barabarani wakimsomea dereva wa basi la kwenda mikoani matokeo yake ya vipimo vya kilevi mwilini wakati wa zoezi la upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva wa mabasi lililofanyika leo katika kituo cha mabasi yaendayo mkoani cha Ubungo jijini Dar es Salaam,anaeshuhudia kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia ambapo kampuni yake ni wadhamini wa kampeni ya Usalama Barabarani.
 Mjumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Mzee Hamza Kassongo pamoja na maafisa wa Vodacom Tanzania wakionyesha pete zenye ujumbe wa “Wait to Send” wakati wa zoezi la upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva wa mabasi yaendayo mikoani lililofanyika leo katika kituo cha mabasi cha Ubungo jijini Dar es Salaam ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya Usalama Barabarani  inayodhaminiwa na Vodacom Tanzania. Pete hizo ziligawiwa kwa madereva wa mabasi yaendayo mkoani zikiwa na ujumbe huo unaowakumbusha kusubiri hadi wakiwa wamesimamisha vyombo hivyo ndipo watumie simu zao za mkononi.
Afisa wa Jeshi la Polisi – Kikosi cha Usalama Barabarani akimpima kiwango cha pombe mwilini dereva wa basi la mkoani, Elias Samu kwa kutumia kifaa maalum wakati wa zoezi la upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva wa mabasi yaendayo mikoani katika mwendelezo wa kampeni ya Usalama Barabarani  inayodhaminiwa na Vodacom Tanzania. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, akifuatilia kwa karibu zoezi hilo liliofanyika leo katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo jijini Dar es Salaam.

STATOIL YATOA ZAWADI KWA WASHINDI WA SHINDANO LA MASHUJAA WA KESHO

$
0
0
Kampuni ya Statoil Tanzania imewatangaza na kuwazawadia washindi wa shindano la Mashujaa wa Kesho katika hafla iliyofanyika siku ya Alhamisi Desemba 4. Mashujaa wa Kesho ni shindano la biashara lililoandaliwa kwa lengo la kukuza dhana ya ujasiriamali kwa vijana mkoani Mtwara.

Bwana Nassibu Hamimu Lilumba ameibuka mshindi wa shindano la Mashujaa wa Kesho baada ya kutoa wazo la biashara na kIsha kuandaa mpango wa biashara na kutoa maelezo yake katika jopo la majaji. Mshindi alizawadiwa fedha taslimu za Kitanzania zenye thamani ya dola elfu tano (5,000) za Kimarekani katika hafla iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Mpango wa biashara uliolenga kufungua kampuni ya utoaji wa huduma za boda boda kwa utaalamu mkoani Mtwara, uliibuka mshindi kutokana na vigezo ambavyo ni kama vile fursa katika soko, kiwango cha ushindani wa mwenye wazo, uwezo wa kusimamia biashara, uelewa wa masuala ya fedha pamoja na fursa za uwekezaji.

Sosthenes Njelekela, Zawadi Yusuph Washaru, Vivian Charles na Ali Hassan waliingia katika hatua ya fainali na kupatiwa zawadi zao. Kila mshiriki aliyeingia katika fainali alijipatia fedha taslimu za Kitanzania zenye thamani ya dola elfu moja (1,000) za Kimarekani.

Shindano lilipata muitikio mkubwa kutoka kwa vijana wa Mtwara ambapo vijana 500 wenye mawazo mbalimbali ya kibiashara katika kilimo, ufugaji wa wanyama na kuku, teknolojia ya habari na mawasiliano, viwanda vidogo na huduma nyinginezo za kibiashara walishiriki. Baadhi ya mawazo hayo yalitoka kwa washiriki mmoja mmoja na mawazo mengine yalitoka kwenye vikundi, kama vigezo vya ushiriki vilivyoelezea.

Washiriki 40 waliofanikiwa kuvuka mchujo wa awali walipatiwa mafunzo ya ujasiriamali ambapo waliweza kujifunza kuhusu njia za kuandaa na kuendesha biashara kwa ufanisi na namna ya kuandaa mipango ya biashara kutokana na mawazo yao ya biashara. Mipango hiyo ya biashara ilikusanywa na kupitiwa kabla ya mipango kumi ya biashara kupelekwa kwa majaji ili kupata mipango mitano ya biashara kuelekea kwenye fainali. Washiriki wa mipango hiyo mitano walitakiwa kutetea mipango yao ya biashara mbele ya majaji.

Jopo la majaji watano liliongozwa na Bi. Victoria Tunu Chale, Mwanzilishi na Mkurugenzi wa People Dynamics Tanzania LTd na Mhandisi, Bwn. Andrew Mnzava ambaye ni mtaalamu kutoka Tanzania Renewable Energy Association, Bwn. Mosses Nkanda, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Mnazi Bay Consulting Ltd ya Mtwara pamoja na Bwn. Justine Lusasi, Mkufunzi Msaidizi kutoka chuo cha Stella Maris ambaye alishiriki kwa ukaribu katika kutoa miongozo kwa washiriki wa shindano hilo na pia katika kusimamia matumizi ya kompyuta zilizotolewa na Statoil kwa ajili ya matumizi ya washiriki wa shindano la Mashujaa wa Kesho.

“Tuna furaha kumpata mshindi wa shindano hili. Vijana wengi wa Mtwara walijitokeza kushiriki katika shindano, jambo lililotupa ari kubwa katika kutekeleza shindano hili. Statoil ni kampuni inayopenda kuunga mkono vijana wenye vipaji katika nchi ambazo kampuni hii inafanya shughuli zake. Hii ni njia yetu ya kukuza maendeleo katika jamii zinazotuzunguka,” alisema meneja wa Statoil nchini, Øystein Michelsen.
 Mkurugenzi wa kampuni ya statoil-tanzania bwana Oystein Michelsen iliyofanyika katika ukumbi wa Zanzibar uliopo Hyatt Regency Dar es Salaam.
 Balozi wa Norway nchini Tanzania Mh Hanne Marie Kaarstad akinena jambo wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mashujaa wa kesho  iliyofanyika katika ukumbi wa Zanzibar uliopo Hyatt Regency Dar es Salaam.
Bwa. Nassibu H. Lilumba ambaye ndiye Mshindi wa kwanza aliyejishindia dola 5000.

COURT PARTICIPATES IN THE 15TH EAC JUA KALI - NGUVU KAZI EXHIBITION

$
0
0
The East African Court of Justice (EACJ) for the first time is participating in the EAC Jua Kali/Nguvu Kazi that is currently ongoing at the Gikondo Expo Ground in Kigali, Rwanda. The court has seized the opportunity to sensitize the public on the role, operations and procedures of the regional court.

At the expo, exhibitors and the general public have shown interest in learning more about the Court especially how to approach and use its services in settling disputes regarding business within the EAC Partner States.

The exhibitors and show-goers have registered their complaints of lack of information and knowledge on the existence of the Court rather than calling it the UN International Criminal Tribunal for Rwanda (UN ICTR) and appealed for continuous sensitization on the role of the Court among the East African citizens.

Over 1,000 participants attending the 15th Jua Kali appreciated the judicial services provided by the EACJ to protect the rights of the business community through ensuring adherence and compliance of the Treaty for the Establishment the East African Community and the EAC Customs Union and Common Market Protocols during their implementation.

The exhibitors also commended the EACJ for realizing the needs of the citizens to be given justice they deserve and opening of the EACJ Sub-registries in the Partner States’ Capitals where the aggrieved parties can file their complaints for settlement in Court.

In the implementation of integration agenda conflicts may raise, therefore there is need for EACJ to increase awareness and the support to reach to the East Africans through these exhibitions and other sensitization mechanisms to educate the Public on the existence of the Court and how to use it.

The Court pledged to continue working closely with EAC Organs and Institutions, EAC Ministries in various outreach programs to increase awareness to the EAC citizens on the activities of the East African Court of Justice in promoting the regional integration agenda.

During the exhibition a number of EACJ publication materials were distributed to the participants and these included; the EACJ Rules of Procedure, Rules of Arbitrations, Court User’s Guide, and the 10th Anniversary Reports and also encouraged the participants to make use of website of the Court http://www.eacj.org for further information.
The in charge of EACJ Sub registry in Kigali Germain Rusingiza receiving promotional materials from Annah Nabaasa at the EAC stand.
Burundi Ambassador to Rwanda HE Alexis Ntukamazina (in suit) receiving promotional materials and EACJ publications at the EAC stand.

MKURUGENIZ WA JIJI LA ARUSHA APANIA KUIREJESHA TIMU YA AFC LIGI KUU

$
0
0
Na Woinde Shizza,Arusha

Mkurugenzi wa jiji la Arusha, Juma Iddi amepania kuipandisha ligi timu ya Arusha FC inayoshiriki ligi daraja la pili msimu huu, huku akiwataka viongozi wa sasa wa timu hiyo kuwa kama kamati na jiji hilo kuhakikisha swala hilo linafanikiwa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mapema ofisini kwake alisema kuwa kwa kuwa tayari usajili umekwisha fanyika kwa sasa wanatafuta kocha mwenye ujuzi na uwezo wa kimataifa wa kuwanoa vijana hao ili kuweza kumudu mikiki ya ligi daraja la pili bila kuwa na woga.

“Kiukweli mimi napenda michezo na niko hapa halmashauri ambapo kazi kubwa ni pamoja na kuitangaza michezo na kuonyesha mfano hivyo kwa kuanzia tumeipa nguvu ya kushiriki michuano hiyo kwa vifaa vyote walivyohitaji vya michezo lengo wasianze kulalama na vifaa”

“Na baada ya vifaa sasa tutahakikisha inakuwa mikononi mwetu mapema mwezi ujao baraza la madiwani litakapokaa na kuridhia na baadhi ya watendaji wa halmashauri hii watakuwa miongozi mwa viongozi watakaochaguliwa kuiongoza lengo ni kuileta karibu na kujua mahitaji yao” alisema Juma Iddi.

Alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi wa Arusha kuhakikisha wanakuwa karibu zaidi na timu hiyo na ilete chachu ya soka mkoani hapa kwa kuishangilia na mawazo pia maoni yao.

“sisi kama halmashauri kuimiliki timu hii siyo kuwaweka mbali wananchi bali ni kuweza kuwajulisha kuwa pia kuwa timu hiyo ni yao kwani itakuwa inatangaza jiji pia kodi zao ndio zitatumika na wajue kuwa pia hatutachukua moja kwa moja bali kwa mda ili tu kuipandisha”

Alitumia fursa hiyo kuwataka mashabiki wa soka wa mkoani hapa pamoja na benchi la ufundi na wachezaji kuwa kitu kimoja na wasiruhusu migogoro kati yao kwani kufanya hivyo kutakatisha matumaini ya kupanda ligi bali wawe kitu kimoja kuhakikisha lengo linafanikiwa.
Juma Iddi (mwenye suti nyeusi) ni Mkurugenzi wa jiji la Arusha

KUMBUKUMBU

$
0
0
Mpendwa baba Alex Safi Maridadi, ingawa umetutoka kimwili miaka 26 iliyopita, tunasheherekea zawadi ya maisha Mungu aliyokujalia na uwepo wako katika maisha yetu. Tunakumbuka upendo, ukarimu na uongozi wako katika familia. Unakumbukwa na mke wako mpendwa Therese Maridadi, watoto wako, wajukuu, ndugu, jamaa na marafiki wote.

Bwana akupatie pumziko la milele, na mwanga wa milele akuangazie, upumzike kwa amani

KITUO CHA RADIO 5 CHAANDAA “KAMPENI YA RADIO 5 VIWANJANI”MSIMU HUU WA SIKUKUU YA XMASS NA MWAKA MPYA

$
0
0
SAM_0369
Radio 5 FM 105.7 imeandaa "kampeni ya RADIO 5 viwanjani" katika mkoa wa Arusha ambapo itawakutanisha watangazaji  na madjs na wasikilizaji wao katika kumbi za starehe kwa takribani wiki tano ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki wa Redio hiyo kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima huku mashabiki wakijipatia zawadi mbalimbali katika kampeni hiyo(katika picha ni Mtangazaji wa kituo cha Redio 5 Julius Kamafa aliyejizolea umaarufu mkubwa jijini Arusha kupitia kipindi chake cha funiko base kinachosikilizwa zaidi na vijana akishow love na msikilizaji wake katika kampeni  ya "Redio 5 viwanjani"ndani ya ACTIVE CLUB - Mbauda jijini Arusha
SAM_0349
Timu kazi ya Redio 5 wakifatilia show 
SAM_0350
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa  kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akiwa anauliza maswali kwa vijana wa Arusha waliofika katika kampeni ya Redio 5 viwanjani ndani ya ACTIVE CLUB - Mbauda jijini Arusha.
SAM_0353
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa  kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akimuuliza maswali shabiki wa redio 5 katika kampeni ya Redio 5 viwanjani yenye nia ya kuwashukuru wasikilizaji wa kituo hicho kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima

Your Last Chance to VOTE SWAHILI FASHION WEEK 2014

$
0
0

SWAHILI FASHON WEEK & AWARDS 2014

POP UP SHOP on Sunday 7th December hosted By Alexis Grahamwife of Candaian High Commissioner to Tanzania at her residence onToure Drive from 1-5PM - FREE ENTRY

VOTING
 Lines close at Midnight (EAT) VOTE NOW

Tickets available ONLYEPIDOR in Masaki @30,000TZS
Tickets at entrance is priced at 40,000TZS
5-7 December 2014
HOTEL SEA CLIFF
DAR ES SALAAM


CONTACTS:
General
+255757828832
POP-UP SHOP:+255787747918

VIP FRONT ROW Tickets SMS:+255767222441
Share
Tweet
Forward
+1
Share
Copyright © 2014 Swahili Fashion Week, All rights reserved.
you are receiving this email due to your patronage to our event

Our mailing address is:
Swahili Fashion Week
Plot 48B Drive inn
Dar Es Salaam
Tanzania

Add us to your address book


u

 

Usiku wa Old Is Gold wahamia Thai Village - Spice Modern Taarab kuendeleza makali Jumapili hii

$
0
0

NA ANDREW CHALE
USIKU wa ‘Old Is Gold’ na Spice Modern Taarab, unatarajiwa kurindima kwa kishindo Jumapili ya kesho Desemba 7, ndani ya   ukumbi wa Thai Village  uliopo Masaki, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia Idarous Khamsin, mwandaaji na mdhamini wa onyesho hilo, mashabiki  wa Old Is Gold  watakuwa wakikutana katika kiota hicho kipya cha burudani kila jumapili kukumbushana enzi.
“Kwa kiingilio cha sh 5,000 tu, wadau watafurahia shoo kabambe kutoka kwa Spice Modern Taarab ndani ukumbi wa Thai Village. Huku wadau wkijumuika pamoja na kubadilishna mawazo” alisema Asia Idarous.
Asia Idarous alilielezea kundi hilo ni la magwiji wa muziki huo wa mwambao ikiwemo kupiga nyimbo za taarab za zamani na zile za sasa ambapo miongoni mwa nyimbo  hizo ni pamoja na ‘Pendo kitu cha hiari’, ‘Dunia ina fisadi,’ ‘Kasha’ na nyingine nyingi.
Onyesho  hilo litakuwa kila siku kwenye ukumbi huo wa Thai Village huku likidhaminiwa na Fabak Fashions (Mikocheni) pamoja na Thai Village huku wadau wengine wakiwa ni pamoja na Clouds tv, Michuzi Media Group, G, One Media wengine wengi.

Vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakutana Arusha kujadili Sera ya Vijana wa EAC

$
0
0
 Mbunge kutoka Kenya Mhe. David Ocheng akitoa hotuba wakati wa mkutano wa kwanza wa Vijana wa EAC kuhusu Sera ya Vijana wa EAC unaoendelea makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha Tanzania.
 Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Mhe. Jesca Eriyo (kushoto) akitoa mada wakati wa mkutano wa kwanza wa Vijana wa EAC kuhusu Sera ya Vijana wa EAC unaoendelea makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha Tanzania. Kulia ni mwenyekiti wa Mkutano huo ambaye ni Mwanasheria wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester Riwa.

 Mmoja wa vijana kutoka Uganda Bi. Helena Okiring akichangia wakati wa mkutano wa kwanza wa Vijana wa EAC kuhusu Sera ya Vijana wa EAC unaoendelea makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha Tanzania.
 Bi. Stella Massekwe kutoka Uganda akitoa mchango wake kuhusu masuala mbalimbali yaliyozungumzwa wakati wa mkutano wa kwanza wa Vijana wa EAC kuhusu Sera ya Vijana wa EAC unaoendelea makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha Tanzania, Kushoto ni kijana Baraka Chelego kutoka Tanzania.
Baadhi ya Vijana kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambazo ni Tanzania bara na visiwani, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi wakifuatilia matukio yaliyokua yanaendelea wakati wa mkutano wa kwanza wa Vijana wa EAC kuhusu Sera ya Vijana wa EAC unaoendelea makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha Tanzania.



Picha na: Genofeva Matemu - Maelezo.

mdau Peter Samanya Msacky alamba nondozzzz Chuo Kikuu Mzumbe

$
0
0
Katika mahafali ya 13 katika chuo kikuu Mzumbe yaliyofanyika Ijumaa katika kampasi kuu Mzumbe, Morogoro mdau Peter Samanya Msacky alilamba nondozzz ya Uzamili ya Uhasibu na Fedha (MSc in Accounting and Finance) ya Chuo Kikuu Mzumbe (MU).
Bwana Msacky akipongezwa na mke wake mpendwa Judith mara tu baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili
Glad akimpongeza baba yake kwa mafanikio aliyopata kwa kutunukiwa Shahada ya Uzamili, anaonekana akimhakikishia baba yake kuwa hata yeye atajitahidi katika mafunzo yake ili kufikia ndoto yake.
Mdau Msacky akipongezana na rafiki yake Bwana Mawalla baada ya kutunukiwa shahada za Uzamili
Picha ya pamoja ya familia ya bwana na bibi Peter Msacky baada ya tafrija fupi iliyofanyika katika viwanja vya Magadu mjini Morogoro.
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images