Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

TRA yaendelea na Maadhimisho ya Wiki ya Mlipa Kodi Tanzania,Yatoa Msaada Hospitali ya Temeke na Kukabidhi Madawati 100 Shule ya Msingi Misitu,Kivule

$
0
0
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),leo Novemba 18,2014 walitembelea Hospitali ya Rufaa ya Temeke jijini Dar es Salaam,ambapo waliweza kutoa msaada wa vitu mbali mbali kwa watoto waliolazwa Hospitalini hapo pamoja na kukabidhi baadhi ya vifaa vya Usafi kwa Uongozi wa hospitali hiyo Mbali na kukabidhi vifaa hivyo,pia walijumuika pamoja na kujitolea kufanya usafi wa Mazingira ya Hospitali hiyo.

Mara baada ya kukamilisha shughuli zote za hospitalini hapo,Wafanyakazi hao walielekea moja kwa moja katika Shule ya Msingi Misitu,ilipo katika Kata ya Kivule,Kitunda na kuweza kukabidhi msaada wa Madawati 100 ambayo yatapunguza adha ya kukaa chini kwa asilimia 74 ya wanafunzi wote wa shule hiyo ambao idadi yake imefikia 590.

Hapo awali wanafunzi hao wote walikuwa wakikaa chini na kuendelea na masomo yao.

TRA imefikia kufanya hivyo,ikiwa katika muendelezo wa Maadhimisho ya Wiki ya Mlipa Kodi chenye kauli mbiu isemayo "Risiti ni Haki Yako,Unaponunu Dai Risiti na Unapouza ni Lazima Utoe Risiti" ambayo kilele chake ni Novemba 21,2014 huku Mgeni Rasmi akitazamiwa kuwa Makamu wa Rais,Dkt. Mohamed Bilal.
Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Kanda ya Temeke,Victor Msuya (kulia) akizungumza na mmoja wa wauguzi wa zamu katika Wadi ya Watoto ya Hospitali ya Rufaa ya Temeke jijini Dar es Salaam leo Novemba 18,2014,wati Timu TRA ilipotembelea Wadi hiyo.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
 Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Kanda ya Temeke,Victor Msuya (kulia) akiwaongoza maafisa wengine wa TRA kutoa bidhaa mbali mbali walizokwenda kuwagawia watoto wanaopatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Temeke,Jijini Dar es Salaam leo Novemba 18,2014.
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakijadiliana jambo wakati wakijiandaa kwenda kufanya usafi wa Mazingira wa Hospitali ya Temeke,Jijini Dar es Salaam leo Novemba 18,2014.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Misitu,Ilipo katika kata ya Kivule,Kitunda jijini Dar es Salaam wakiwa wameketi kwenye madawati mapya yaliyokabidhiwa leo na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).Nyuma yao ni Baadhi ya Maofisa wa TRA waliofika shuleni hapo. 
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Misitu,Hyasinta Hugo akizungumza wakati akiukaribisha Uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Shuleni hapo. 
 Mkurugenzi wa Walipakodi na Elimu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Richard Kayombo akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki kuzungumza na uongozi wa Shule hiyo na kukabidhi madawati.
 Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki akizungumza na uongozi wa Shule hiyo pamoja na wanafunzi kabla ya kukabidhi madawati,yaliyotolewa na TRA kwa shule hiyo.
Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki akipena mkoni na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Misitu,Hyasinta Hugo wakati akimkabidhi madawati 100 yaliyotolewa na TRA kwa shule hiyo.


Serikali kudhibiti utoroshwaji wa madini nje ya nchi

$
0
0
Serikali imekua ikipoteza mapato mengi kutokana na utoroshwaji wa madini aina ya Tanzanite yanayopatikana nchini Tanzania pekee.

Kamishna wa Madini nchini,Eng Paul Massanja amesema leo wakati wa maonesho ya madini ya Vito yanayofanyika jijini hapa ambayo yanahudhuriwa na washiriki kutoka mataifa mbalimbali.

Amesema kwa takwimu za mwaka 2013,Tanzania ilipata dola za marekani 38 milioni wakati nchi ya Kenya ilijipatia kiasi cha dola 100 milioni na India ilijikusanyia kitita cha dola 300 milioni.

"Wote mnafahamu haya madini yanapatikana Tanzania pekee huu ni ushahidi kuwa kumekuwa na utoroshwaji wa madini haya kwa kiwango kikubwa jambo linalotunyima mapato ya kutosha"anasema Eng Massanja

Hata hivyo amesema wataendelea kudhibiti mianya ya utoroshaji wa madini nje ya nchi ambayo hayajaripiwa kodi sitahili huku kukiwa na mipango ya kujenga jengo kubwa ambalo litatumika kufanyia biashara ya madini.
Naibu Katibu Mkuu,Wizara ya Nishati na Madini,Mhandisi Ngosi Mwihava(katikati)akikata utepe kufungua Maonesho ya Tatu ya Madini ya Vito ya kimataifa mkoani Arusha leo.
Kamishna wa Madini nchini,Mhandisi Paul Massanja(kushoto)akimpongeza mmoja wa wafanyabiashara ya madini ya Vito jijini Arusha.
Viongozi mbalimbali wa Wizara ya Nishati na Madini wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyabiashara kutoka nchini DRC.
Meneja Uhusiano wa Wizara ya Nishati na Madini,Badra Masoud(kushoto) akizungumza na mmoja wa wadau wa sekta ya madini nchini,Pandit katikati ni Kamishna wa Madini nchini,Mhandisi Paulo Massanja.

SIMAMIENI IPASAVYO MIUNDOMBINU YA MAJI: MH. MWANRI

$
0
0
Na Saidi Mkabakuli – Ruvuma

Serikali imetoa wito kwa taasisi za umma kusimamia kwa umakini miundombinu ya miradi ya maji pindi inapokamilika ili kuweza kuwapatia wananchi huduma ya maji ya uhakika mara miradi hiyo inapokabidhiwa kwa kamati za usimamizi wa maji.

Wito huo umetolewa na kiongozi wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati timu hiyo ilipokuwa ikifanya ukaguzi wa ujenzi wa miundombinu ya maji ya utekelezaji wa program ya maji na usafi wa mazingira katika vijiji 10 vya manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Bibi Mwanri ambaye pia ni Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango anayeshughulikia Huduma za Jamii na Masuala ya Idadi ya Watu, alisema kuwa kwa miaka mingi kumekuwepo na ubadhirifu wa miundombinu ya miradi mingi ya maji hali inayorudisha nyuma juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa wananchi wanafikiwa na maji safi na salama kote nchini.

“Kumekuwa na tabia mbaya ya ubadhirifu wa miundombinu hii, msikubali waiharibu ama kuiba vifaa vya ujenzi wa miradi yote 10 maana kama munavyoona serikali na wafadhili wamejitolea ili kuhakikisha munafikiwa na huduma hii muhimu,” alisema.

Akizungumza wakati timu hiyo ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo ilipotembelea na kukagua Mradi wa Maji wa Ruhuiko Kanisani utakaohudumia zaidi ya wakazi 3000 wa kitongoji ya Kijiji cha Ruhuiko Kanisani na maeneo ya jirani, Msanifu wa mradi huo, Bw. Elezear Ndunguru alisema kuwa mpaka sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 55.

“Kasi ya utekelezaji wa mradi huu ni ya kuridhisha kwani mpaka sasa tumeweza kujenga vituo 12 vya kuchotea maji kati ya 15, kinachongojwa kwa sasa ni kukamilika kwa tanki la kuhifadhia maji,” alisema.

Msanifu huyo ameongeza kuwa hadi kukamilikwa miradi yote 10 jumla ya shilingi bilioni 2.77 zitatumika na kuweza kuwahudumia zaidi ya wakazi 9000 wa vijiji vitakavyopitiwa na miradi hiyo.

Kwa mujibu wa Mpango wa Kwanza wa Maendeleo, lengo kuu kwa upande wa maji ni kuongezeka kwa upatikanaji wa maji safi na salama ni mojawapo ya maeneo yanayotiliwa mkazo ili kuweza kuongeza kasi ya maendeleo na kupunguza umaskini miongoni mwa Watanzania.
Timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikishuka kutoka kwenye tanki la kuhifadhia maji ya Mradi wa Maji wa Ruhuiko Kanisani utakaohudumia zaidi ya wakazi 3000 wa kitongoji ya Kijiji cha Ruhuiko Kanisani na maeneo ya jirani.
Timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikishuhudia kazi ya utandazi wa mabomba ya maji ya Mradi wa Maji wa Ruhuiko Kanisani. Hadi kukamilika kwake mradi huo utatumia zaidi ya shilingi milioni 480.
Msanifu wa Mradi wa Maji wa Ruhuiko Kanisani Bw. Elezear Ndunguru (Kulia) akitoa maelekezo kuhusu maendeleo ya mradi huo. Mradi huu unafadhiliwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia na unagharimu zaidi ya shilingi milioni 480 za Kitanzania.
Kiongozi wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Mwenye koti jekundu) akihoji masuala mbalimbali kuhusu utekelezaji wa miradi ya maji kwenye manispaa ya Songea.
Kiongozi wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akizungumza mara baada ya timu yake kukagua Mradi wa Maji wa Ruhuiko Kanisani. Wanaomsikiliza kutoka kulia ni Naibu Katibu Mtendaji (Uchumi Jumla), Prof. Longinus Rutasitara, anayemfuatia ni Msanifu wa Mradi huo Bw. Elezear Ndunguru na Mratibu wa ukaguzi huo Bw. Senya Tuni (Wapili kulia).

Vijana waaswa kushiriki mashindano ya teknolojia

$
0
0
Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania,Abigail Ambweni akiwafafanulia jambo baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kutoka Kitivo cha Sayansi ya Kompyuta kuhusiana na shindano la AppStar linaloendeshwa na kampuni hiyo linalowalenga wataalam wa kutengeneza mobile applications na kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo pesa taslim na safari ya kwenda nchini India kushiriki katika shindano hilo ngazi ya kimataifa.
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wa Kitivo cha Sayansi ya Kompyuta,John Marolera akimuulizawa swali Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania,Abigail Ambweni kuhusiana na shindano la AppStar linaloendeshwa na Vodacom Tanzania linalowalenga wataalam wa kutengeneza mobile applications na kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo pesa taslim na safari ya kwenda nchini India kushiriki katika shindano hilo ngazi ya kimataifa.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wa Kitivo cha Sayansi ya Kompyuta,wakielekea katika sehemu maalum ya kupatiwa maelezo ya jinsi ya kushiriki katika shindano la AppStar linaloendeshwa na Vodacom Tanzania linalohusiana na wataalam wa kutengeneza mobile applications kushiriki katika shindano hilo na kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo pesa taslim na safari ya kwenda nchini India kushiriki katika shindano hilo ngazi ya kimataifa.

Ndoto za wanafunzi wa vyuo vikuu wanaosoma masomo ya sayansi ya teknokojia ya habari na mawasiliano nchini ya  kuwa magwiji wa fani hiyo zinaelekea kutimia. Hali hii inatokana na  kuzinduliwa kwa shindano la kusaka vipaji vya ugunduzi wa program za simu  - App Star – mwezi huu.

Shindano hili la kimataifa lilizinduliwa na Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania na linajumuisha Watanzania wote wenye hamasa ya kutumia teknolojia kuboresha maisha yao na ya jamii zao kwa ujumla.  Aidha, ngwe ya kwanza ya kuchuja majina ya wale watakaoshiriki  katika  duru ya mwisho ya mashindano hayo itakayofanyika mjini Bangalore, nchini India itafanyika tarehe 5 Disemba 2014 jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Meneja wa Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania, Abigail Ambweni ambaye aliyekuwa katika harakati za kuwahamasisha wanafunzi wanaosoma masomo ya kompyuta katika Kitivo Cha Sayansi ya Kompyuta cha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, aliwasihi vijana hao  kushiriki katika shindano hilo ambalo pamoja na mambo pengine pia linalenga kuibua vipaji vya vijana kwenye nyanja ya  ubunifu wa teknolojia.

“Dunia ya sasa ni ya sayansi na teknolojia hivyo tunaamini kuwa ubunifu wa programu za kiteknolojia haunufaishi mbunifu peke yake bali pia hurahisisha maisha ya wananchi wote wanaoitumia program hiyo. Hivyo basi, huu ni wakati wenu vijana kujitokeza  na kuvinadi vipaji vyenu kupitia shindano hili”, alisema Ambweni.

Baadhi ya wanafunzi wa Chuo hicho walihamasika kushiriki na wameipongeza Vodacom kwa kuandaa shindano kama hili lenye mwelekeo wa kuinua vipaji na wametoa ushauri kuwa shindano hilo lisiishie kwenye ubunifu wa programu za simu bali ubunifu wa kila aina wa matumizi ya kompyuta.

Ambweni aliendelea kusema kwamba Shindano hili liko wazi kwa wabunifu  na watumiaji wote wa teknolojia wanaotumia mifumo mbalimbali kama vile  Android, Windows, IOS, Sumbian na nyinginezo na wanapaswa kuwasilisha kazi zao kabla ya tarehe ya mwisho ya kujisajili ya Novemba 25, 2014. Mshindi wa kwanza mwaka huu atazawadiwa pesa taslimu na atagharamiwa safari ya kwenda India kushiriki kwenye ngazi ya kimataifa ya shindano hili ambapo atakayeibuka mshindi huko atapata fursa ya kuhudhuria mkutano mkuu wa kimataifa  wa masuala ya simu za mkononi utakaofanyika Barcelona nchini Hispania.

Wabunifu wanaotaka kushiriki wametengwa katika makundi mawili mojawapo likiwa ni lile la wenye makampuni na tayari wana mitandao na wale ambao ndio kwanza kabisa wanawiwa kutangaza ubunifu wao. Washiriki wana uhuru wa kuchagua kushiriki katika kundi lolote wanalodhani linakidhi mahitaji yao.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Intaneti wa Vodacom Tanzania Saurabh Jaiswal alisema, washiriki  wa shindalo hili mwaka jana walijikita katika ubunifu kwenye nyanja za michezo ya kwenye simu, elimu, burudani, michezo, afya, kilimo na mazingira.

“Tunawahimiza washiriki kutumia fursa hii kutangaza vipaji vyao na kuonyesha ubunifu wao wa kidijitali tulinao nchini Tanzania, “ alisema Jaiswal.

Tangu kuanzishwa kwa mashindano haya mwaka 2012, washiriki wengi wenye vipaji vya ubunifu wa teknolojia wamendelea kuingia katika mchuano huu wa kiteknolojia. Wabunifu kutoka nchi za  Tanzania, Afrika ya Kusini, Misri, Kenya, Ghana na  India watashiriki katika mashindano ya mwaka huu. Maelezo zaidi ya shindano hili la App Star yanapatika dev.info@vodafone.com

WIZARA YA UJENZI KUJENGA DARAJA JIPYA LITAKALOPITA BAHARINI PEMBEZONI MWA DARAJA SELANDER

$
0
0
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akionesha sehemu ambazo daraja hilo jipya litakapojengwa pembezoni mwa daraja Selander kuanzia hospitali ya Aghakan hadi barabara Kenyata. Sehemu ya Daraja hilo pekee litakuwa na urefu wa km 1.03
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile akiwa na ujumbe kutoka Serikali ya Korea Kusini pamoja na Wizara ya Ujenzi mara baada ya kusaini Mkataba wa Muhtasari wa Majadiliano leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile kulia akimshukuru Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli mara baada ya hafla ya utiaji sahihi wa Muhtasari wa Majadiliano.
Tukio la utiaji sahihi likiendelea kama inavyoonekana pichani.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Eng. Patrick Mfugale akionesha mchoro wa nguzo kubwa za daraja hilo litakalopita baharini pembezoni mwa daraja la Selander huku Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe wakifatilia kwa makini.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akifafanua kuhusu ujenzi wa daraja hilo. Picha kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini (GCU) Wizara ya Ujenzi

MOTO WATEKETEZA SOKO LA BIDHAA ZA UTAMADUNI LIJULIKANALO KAMA MT.MERU CURIOS & CRAFTS MARKET JIJINI ARUSHA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo ameagiza uchunguzi wa kina kufanyika kufuatia soko la wafanyabiashara wa Vinyago na bidhaa mbalimbali za kitalii la Maasai Market kuteketea kwa moto.

Mulongo ambaye alifatana na kamati ya Ulinzi na Usalama alishangaa kuona maduka hayo ambayo yapo jirani na Kikosi cha Zima Moto kushindwa kuzima moto na kusababisha hasara kwa wananchi.

"Sitakubali kuona uzembe unaendelea katika mkoa wetu,lazima watu wawajibishwe kwa uzembe hasa Kikosi cha kuzima moto ambao mko karibu na Ofisi za Chama Cha mapinduzi wilaya yalipo maduka haya"amesema Mulongo

Chanzo cha moto bado hakijaweza kufahamika huku maduka hayo yapatayo 188, huku yakiwa hayajaunganishwa na Umeme kwa lengo la kuepusha hatari ya moto kwani bidhaa nyingi ni vinyago vinavyotengenezwa kwa mbao.
Habari picha kwa hisani ya woindeshizza blog
Baadhi ya Mabaki ya bidhaa zilizoteketea kwa moto katika SOKO la bidhaa za utamaduni lijulikanalo kwa jina la MT.MERU CURIOS& CRAFTS MARKET usiku wa kuamkia leo. 
Bango la Soko hilo.
Sehemu ya Wafanyabiashara wa SOKO la bidhaa za utamaduni lijulikanalo kwa jina la MT.MERU CURIOS & CRAFTS MARKET wakiwa wameduwaa bila kujua la kufanya mara baada ya Soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo na kuunguza bidhaa zote za wafanya biashara zililopo katika soko hilo

Mahakama ya Kisutu yasema Hans Macha ana kesi ya kujibu

$
0
0
Na Mwandishi Wetu

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imetoa uamuzi katika kesi inayomkabili mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam, Hans Aingaya Macha (pichani) kuwa ana kesi ya kujibu.

Uamuzi huo, umetolewa na Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Devotha Kisoka katika kesi inayomkabili mfanyabiashara huyo ya kugushi hati ya kiwanja cha Ramadhan Balenga chenye namba 183 kilichopo Kigogo, mkataba wa mauziano na hati ya uhamishaji miliki.

Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Devotha alisema baada ya kupitia ushahidi wa awali wa upande wa mashitaka, mshitakiwa(Macha) una kesi ya kujibu na mahakama inakutaka uanze utetezi katika kesi yako inayokukabili na dhamana yako inaendelea kama kawaida.

Kutokana na hali hiyo, Hakimu Devotha aliiharisha kesi hiyo hadi Desemba Mosi na Mbili kwa upande wa mshitakiwa kuanza kutoa ushahidi wake, mahakamani hapo katika kesi hiyo inayoonekana kuvuta hisia kubwa za wananchi jijini Dar es Salaam.

Kabla ya mahakama kutoa uamuzi huo, Wiki iliopia Hakimu Devotha alisikiliza ushahidi wa mwisho kutoka kwa upande wa mashitaka, ambaye alikuwa Mkuu wa Maabara ya Uchunguzi wa Hati wa Polisi, Mrakibu wa Polisi, Amaan Renatus Saad.

Renatus alidai mahakamani hapo, mbele ya Hakimu Devotha kuwa alipokea nyaraka kutoka kwa Ofisi ya Msajili wa Hati ikiomba ifanyiwe uchunguzi katika nyaraka za uhamishaji miliki kutoka kwa Balenga kwenda kwa Macha.

"Nina uzoefu wa miaka zaidi 10, ambapo nimeupata sehemu mbalimbali ikiwemo Bostwana. Polisi ilipokea barua kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutaka kufanyiwa uchunguzi,''alidai.

Renatus alidai baada ya kupokea barua, walifanya uchunguzi na kutoa taarifa kwa Wizara ya Ardhi kuwa saini walizochunguza hazikusaini na mtu mmoja, ambaye ni Balenga, hivyo zimegushiwa.

Alidai uchunguzi wao, ulizingatia mambo mengi ikiwemo mgandamizo wa peni, spidi ya peni, hivyo aliiomba mahakama ipokee ushahidi wake kama kielelezo sahihi katika kesi hiyo na upande wa mashitaka unaoongozwa na Wakili wa serikali, Nassoro Katuga, alidai mahakamani hapo kuwa, wamefunga ushahidi na kutoa nafasi ya upande wa utetezi nao kutoa ushahidi wake.

mabalozi wa Hifadhi za Taifa wa TANAPA watembelea Bungeni Dodoma leo

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akisalimiana na mabalozi wa Hifadhi za Taifa zilizo chini ya TANAPA,waliotembelea Bungeni mjini Dodoma leo.
Kikundi cha Vijana ambao ni mabalozi wa hifadhi za Taifa zilizo chini ya TANAPA wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu.Vijana hawa wako mjini Dodoma katika ziara ya kimafunzo.Picha na Deusdedit Moshi.


IGP MANGU AONGEZA ASKARI KITETO

$
0
0
E88A9486
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP Ernest Mangu akimsikiliza Diwani wa Kata ya Matui Wilayani Kiteto Bw.Athuman Kidawa wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea kwa  vifo.kushoto ni Afisa tarafa wa Matui Bw.Eliakimu Ndelekwa.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)E88A9514
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP Ernest Mangu akizungumza na wananchi  wa Kata ya Matui Wilayani Kiteto wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea kwa  vifo. (Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)E88A9421
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP Ernest Mangu akizungumza na Mtendaji wa Kijiji cha Chekanao, Kata ya Kiperesa , Wilayani Kiteto Bw.Omar Ndee (kulia) wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea kwa vifo.Katikati ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Deusdedit Nsimike pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bw.Japhet Chafu (Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
 
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi, Kiteto.
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu ameahidi kuongeza idadi ya Askari katika kijiji cha Chekanao, kata ya Kiperesa wilayani Kiteto Mkoani Manyara kufuatia wananchi katika kijiji hicho kujitolea nyumba kwa ajili ya kuishi Askari kwa lengo la kuimarisha usalama katika maeneo yao kufuatia kuwepo kwa migogoro ya ardhi inayosababisha kutokea kwa mauaji.
 
IGP Mangu aliyasema hayo jana wakati alipokuwa katika ziara Wilayani Kiteto ya kujionea uharibifu uliojitokeza pamoja na kutafuta ufumbuzi wa migogoro hiyo iliyopelekea kutokea kwa vifo vya wakulima na wafugaji hivi karibuni katika wilaya hiyo ambapo watu kadhaa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na vurugu hizo.
 
Alisema kufuatia kuwepo kwa umbali mrefu wa kituo cha Polisi na kijiji hicho atahakikisha askari wa kudumu wanakuwepo ili kushirikiana na wananchi katika kuwabaini wahalifu wanaofanya vurugu na kuendeleza migogoro hiyo ambapo wananchi nao waliahidi kujenga kituo cha Polisi.
 
Kwa upande wake Mtendaji wa Kijiji cha Chekanao Bw.Omar Ndee alisema wamekuwa wakipata shida kutokana na umbali mrefu wa kituo cha Polisi jambo ambalo limekuwa likifanya kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu vinavyochangiwa na migogoro ya ardhi katika wilaya ya Kiteto.
 
Naye Mwenyekiti wa Kijiji hicho Japhet Chafu alilishukuru Jeshi la Polisi kwa kuimarisha usalama kijijini hapo tangu kutokea kwa mauji ya wakulima na wafungaji ambapo alibainisha kuwa bila kuwepo wao hali ingekuwa mbaya zaidi kutokana na kutokuwepo na muafaka baina ya wakulima na wafugaji.
 
“IGP hawa askari wako wasingekuwepo hapa usingekuta mtu lakini tunawashukuru sana hawa askari kwa kuwa hivi sasa hali ya usalama imerejea na hata shambani tumeanza kwenda” Alisema Bw.Chafu.
 

IGP Ernest Mangu alitumia ziara hiyo kuzungumza na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, Wakaguzi wa Tarafa pamoja na Askari Kata ili kutafuta ufumbuzi wa migogoro hiyo na kuimarisha hali ya ulinzi na usalama.

KATIBU MKUU MPYA WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII AKABIDHIWA OFISI

$
0
0
  KATIBU MKUU WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII DKT.ADELHELM  JAMES MERU AKIFANYA MAKABIDHIANO YA OFISI  NA ALIYEKUWA KATIBU MKUU WA WIZARA YA MALISILI NA UTALII, BI. MAIMUNA  TARISHI YALIYOFANYIKA JANA JIONI TAREHE 17/11/2014  MPINGO HOUSE JIJINI DAR ES SALAAM.          

 Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Maimuna  Tarishi, akimkabidhi vitendea kazi  Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt.Adelhelm  James Meru, yaliyofanyika jana jioni tarehe 17/11/2014  Mpingo House Jijini Dar es salaam.
 Aliyekuwa Katibu Mkuu  wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Maimuna Tarishi,  akipeana mkono   mara  baada ya kumkabidhi vitendea kazi Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Dkt.Adelhelm 
Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt.Adelhelm  James Meru,  Akiwa kwenye picha ya pamoja  na aliyekuwa  Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Maimuna  Tarishi, mara  baada ya kukabidhi  vitendea kazi  yaliyofanyika jana jioni tarehe 17/11/2014  Mpingo House Jijini Dar es salaam. Mwingine ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Selestini Gesimba.

MISHUMAA YA KALE...Kipindi kipya kutoka VIJIMAMBO na KWANZA PRODUCTION

$
0
0
Photo Credits: Ye Olde Vivyl Shoppe
Baada ya pilika za wiki nzima, na mchamchaka wa maisha, sasa unakuja wakati wa kuburudika na muziki halisi wa zamani.
Katika kipindi hiki, utaweza "kuruka majoka" na "kula mangoma" kwa kusikiliza nyimbo ziliotamba miaka ya zamani, kupata historia ya wasanii na vikundi mbalimbali na pia kusikiliza mazungumzo na maDj na wasanii mbalimbali wa zamani.
Ungana na MixMaster Dj Luke Joe kwenye "one and two" na Mubelwa Bandio nyuma ya kipaza sauti kwenye kipindi kipya cha MISHUMAA YA KALE kitakachokujia kila Ijumaa kuanzia saa 11 kamili jioni mpaka saa 1 kamili usiku kwa majira ya Marekani ya Mashariki (5:00pm - 7:00pm EST)
Ungana nasi kupitia www.kwanzaproduction.com
MixMaster DJ Luke Joe. Photo Credits: IskaJojo Studios
Mubelwa Bandio


Shinda na Vodacom Kabumbu

FOREVER NUTRI-LEAN PROGRAMME

$
0
0
FOREVER NUTRI-LEAN PROGRAMME
Has two step process, combining a 9-day cleansing plan followed by a long –term weight loss plan.
  1. Clean 9- Detoxify-leaves you clean, healthier, happy and helps you to loose between 3kg to 8kg. @ Tsh 265,000.
  2. Forever Nutri-Lean (Life style 30)- burns fats, loose weight between 10kg to 15kg & maintain your weight, leaves you with good eating habits.  @ Tsh 440,000.
  3. Body Toning Kit- Removes cellulites and fats deposits under the skin. Wrap the arms, thighs, stomach and loose up to 2 inches per Wrap. @ Tsh 145,000.
Loose weight with FOREVER NUTRI-LEAN PROGRAMME and improve quality of your life (Sexual desire and performance, reduce possibilities of diabetes, Cancer and Sleep apnea).
FOREVER NUTRI-LEAN PROGRAMME has No Drugs (Caffeine, Topiramate, sibutramine, xenical, phentermine, methamphetamine)

How do you know one is overweight?
  By finding the Body mass Index (B.M.I.) i.e. a ratio of the weight over the height squared
       BMI  =      Weight  (kg)   
              Height (m) X Height (m)
Less Than 18.9       =    Underweight
                 19 - 24.9 = Normal weight
                  25 - 30    =   Overweight
              Above 30   =   Obese
Recommended Weight (kg) = Height (m)*Height (m)*24.9
WEIGHT TO LOSE= YOUR WEIGHT- CALCULATED (Recommended) WEIGHT
FOR MORE INFORMATION CALL   0769888605/0786139316



Balozi Seif Ali afungua Mkutano wa Kimataifa wa Tano wa Ushirikiano kati ya China na Afrika

$
0
0
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiufungua rasmi Mkutano wa Tano wa Ushirikiano kati ya China na Afrika unaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Days Hotel & Suites Shinei Bay Mjini Haikou Jimboni Hainan.
  Gavana wa Jimbo la Hainan Bwana Jian Dingzhi akitoa neno la makaribisho kwa wajumbe wa mkutano wa Tano wa Ushirikiano kati ya China na Afrika unaoendelea katika ukumbi wa Kimataifa wa Days Hotel i& SuitesShiney Bay Mjini Haikou.
 Meya Wa Manispaa ya Zanzibar Mstahiki Khatib Abdullrahman Khatib kulia pichani na kushoto yake Mwakilishi wa Jimbo la Chanani Mh. Ussi Jecha Simai wakiwa makini kufuatilia Hotuba  ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hayupo pichani wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tato wa Kimataifa wa Ushirikiano kati ya China na Afrika uliofanyika Katika Mji Mkuu wa Jimbo la Kisiwa cha Hainan – Haikou.
 Washiriki wa Mkutano wa Kimataifa wa Tano wa auashirikiano kati ya China na Afrika, waliopo mbele wane kuanzia  kulia ni Meya wa Manispaa ya Zanzibar Mstahiki Khatib Abdulrahman Khatib,Mwakilishi wa Jimbo la Chaani Mh.e Ussi Jecha Simai, Waziri wa Ardhi Mh. Ramadhan Abdulla Shaaban,Waziri wa Habari Mh. Said Ali Mbarouk na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi.
Waandishi wa Vyombo mbali mbali vya Habari wa Jimbo la Hainan wakipata ufafanuzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Tano wa Ushirikiano kati ya China na Afrika kutoka kwa Mgeni rasmi wa ufunguzi wa Mkutano huo Makamu wa Pili wa Rais wa ZanzibarBalozi Seif Ali Iddi. Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

The Economist Health Care in Africa Summit 2014

$
0
0
 Katibu mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donan Mmbando akiwa kwenye kipindi cha maswali na majibu toka kwa Vivek Muthu pembeni yake na maswali mengine toka kwa wadau waliohudhuria kwenye mkutano wa Afya wa Afrika unaoendelea jijini Dar es Salaam.
 Mmoja ya wadau akiuliza swali kwa Katibu mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donan Mmbando.
 Wadau toka nchi mbalimbali duniani wakifuatilia kwa karibu yanayoendelea mkutanoni.
Mkutano ukiendelea

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA

MDAU ANDREW CHALE KUTOA VITABU VYA MAISHA YAKE

$
0
0
Andrew Chale (kulia) akiteta jambo na 'Mwenyekiti' Mjengwa  wa Mjengwa blog
Andrew Chale (kulia) akiteta jambo na 'Mwenyekiti' Maggid Mjengwa wa Mjengwa Blog. ..

Ni vya 'Who Is Andrew Chale', 'Nimnukuu Nani?' na ''Mimi ni Historia',

Mwandishi wa Habari nchini Tanzania, Andrew Chale anayeandikia magazeti ya Tanzania Daima na Sayari yanayotolewa na kampuni ya Free Media ya jijini Dar es Salaam, ambaye pia mwandishi 'msaada' wa blog za habari mbalimbali za hapa nchini na nje ya Tanzania ameanza mchakato rasmi wa kuandika vitabu vitatu (3) vitakavyokuwa vikielezea juu ya Maisha yake.

Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari leo Novemba 19, Andrew Chale alibainisha juu ya kusudio hilo la kutoa Vitabu vya kuelezea Maisha yake ni ndoto aliyonayo kwa miaka mingi na kwa sasa imetimia.

"Wengi watajiuliza sasa nimepata wapi ujasiri wa kufanya jambo hili kubwa la kuelezea Maisha yangu?.Ni rahisi sana, Unapokuwa na Mungu kila jambo linawezekana hivyo vitabu hivi vitakuwa ni muongozo kwa Vijana wote hapa Duniani kuelewa kuwa yale yote wanayopitia si ya kuyakatia tamaa, bali kuangalia wapi wataweza kujikomboa na hata kuendana na hali iliyopo kwa kujithamini, kujielewa, uvumilivu na kufikia malengo stahiki ya maisha" alifafanua Andrew Chale.

Alivitaja vitabu hivyo kuwa ni: "Who Is Andrew Chale?" Sehemu ya Kwanza), 'Who Is Andrew Chale 2?"- 'Nimnukuu Nani?' (Sehemu ya Pili) na Kitabu cha mwisho kitakachojulikana kama "Mimi ni Historia".


Akifafanua vitabu hivyo vya 'Who Is Andrew Chale' cha kwanza na kile cha pili cha 'Who Is Andrew Chale 2- 'Nimnukuu Nani?', alibainisha kuwa vitaelezea kwa kina Historia yake tokea kuzaliwa hadi alipofikia sasa huku cha Pili cha 'Who Is Andrew Chale 2-'Nimnukuu Nani' kikielezea yale mambo yote yaliyojificha nyuma ya pazia na ukakasi wa maisha aliyopambana nayo kutoka kwa walimwengu na mwishowe anauliza "Nimnukuu Nani?".
Aidha,kwa upande wa kitabu cha : "Mimi ni Historia" ameweza kuelezea ujumbe juu ya Vijana kutokata tamaa na baadala yake wasonge mbele kwa magumu yote waliyopitia, ikiwemo yeye.

"Mimi ni Historia", mimi mwenyewe naogopa sana, kwanza kuanzia jina la Kitabu, Nakumbuka nilimuuliza Mama yangu Mzazi juu ya jambo fulani la kifamilia baina yake na Baba, lakini jibu alilonipa ndilo lililonifanya nishike neno hili 'Mimi ni Historia'. 

Kikubwa kwenye kitabu hichi nitafafanua mambo mbalimbali ya kihistoria bila shaka hata atakayesoma ambaye alipitia mambo kama yangu naye itakuwa ni Historia" alimalizia Andrew Chale. Vitabu hivyo vyote vitajaa Historia ya kweli, itakayotoa mafunzo kwa kila mmoja atakayebahatika kuvisoma Pia vitakuwa ni kama mafunzo, mfano wa kuigwa, na kukuacha ki mdomo wazi na hata kububujikwa machozi.

Aidha, Andrew Chale, aliomba ushirikiano kwa wadau kujitokeza kumsapoti ilikufanikisha juhudi za vitabu hivyo ikiwemo gharama za kuandaa Mswada, mapitio na uchapaji. "Kwa sasa nipo katika andalio la Simulizi, na lengo kuu nije nichapishe Mkuki na Nyota.Kwa sasa natafuta watu watakao kuwa msaada wa awali wa kufanikisha dhumuni langu hili Ikiwemo ushahuri, msaada wa kifedha, mchango wa kimawazo na mengineo. Tuwasiliane kupitia 0719076376 au 0767076376 au 0688076376 au chalefamily@yahoo.com" alimalizia Andrew Chale.

Andrew Chale, ambaye kwa sasa anaishi Bagamoyo, Mkoani Pwani akifanya shughuli zake hizo za Uandishi wa Habari, Pia ni Mwanaharakati wa Haki za Watoto nchini, msanii wa masuala ya Vichekesho, Mtunzi wa filamu, maigizo na mshahuri kwenye matamasha ya sanaa na Muziki, mbali hayo pia ni Mjasiriamali katika Sanaa na Utamaduni ikiwemo kukuza Sanaa na Utamaduni kwa Mkoa wa Pwani.

DK SHEIN AHUDHURIA MKUTANO WA MABALOZI MKOA WA MAGHARIBI UNGUJA

$
0
0
  Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi alipowasili viwanja vya Ofisi ya CCM Mkoa Amani alipohudhuria katika mkutano wa Mabalozi wa Mkoa wa Magharibi Unguja akiwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama cha Mapinduzi katika Mikoa ya Unguja
 Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono Mabalozi waliofika kumpokea  alipowasili viwanja vya Ofisi ya CCM Mkoa Amani alipohudhuria katika mkutano wa Mabalozi wa Mkoa wa Magharibi Unguja akiwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama cha Mapinduzi katika Mikoa ya Unguja,
 Baadhi ya Mabalozi   wa CCM wa jimbo la Kwamtipura wakimsikiliza Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akihutubia Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika Mkoa wa Magharibi Unguja katika ukumbi wa CCM MKoa Amani leo,
 Baadhi ya Mabalozi   wa CCM wa majimbo mbali mbali ya Mkoa wa Mgharibi wakiwa katika mkutano wa  Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika Mkoa wa Magharibi Unguja katika ukumbi wa CCM MKoa Amani leo uliohutubiwa na Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,
 Baadhi ya Mabalozi   wa CCM wa majimbo mbali mbali ya Mkoa wa Mgharibi wakiwa katika mkutano wa  Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika Mkoa wa Magharibi Unguja katika ukumbi wa CCM MKoa Amani leo uliohutubiwa na Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,

REPORT OF A STUDY ON BLOOD NEED ASSESMENT IN TANZANIA

$
0
0

Ministry of health and social welfare through National Blood Transfusion service (NBTS) in collaboration with Center for Disease control (CDC), American Association of Blood bank (AABB) and FELTP launched the study to establish current clinical pattern of blood use, quantification of the National blood demand and estimation of National blood needs in Tanzania in June 2013 and ended in October 2013.


The study involved 42 Transfusion facilities in both Tanzania mainland and Zanzibar; dissemination meeting on the findings of the study was officially opened by acting chief medical officer Dr Margareth Mhando on 18th November 2014.


Speaking to CDC officers, Hospital directors, Regional medical officers, medical officers in charge and NBTS officers, acting Chief medical officer Dr Mhando said “before the study NBTS did not know how much blood was needed to meet demands for Blood transfusion treatments of patients in Tanzania, NBTS was using WHO formula to estimate blood needs using 1% of population or when at least 10 whole blood units is collected per 1000 population”.


According to recent census of about 45 million people, NBTS need to collect at least 450,000 units of whole blood per year to meet country demand, Dr Mhando said that “it was important for NBTS to determine exactly blood consumption, collection demand and needs for all transfusion facilities including government, private and faith base”.

The study findings shows that infectious disease were major cause of anemia requiring blood transfusion in both adults and children while malaria accounted for majority of blood transfusion in adults (52%). Maternal hemorrhage was the leading cause of anemia in pregnant women (73%).  Study findings shows that estimate annually blood demand nationally is 278,372 units which is base on blood transfusion request at all the transfusion hospitals in mainland Tanzania and Zanzibar,” she said.



She added that study is complete; data analysis has been done, it is important to share the findings with various stakeholders from different institutions to get their inputs and that responsible authority to implement some of the recommendations from the study to improve blood transfusion practices in the country.

Huduma ya Simu Dokta yanufaisha maelfu ya watanzania

$
0
0

Idadi ya wanaojiunga nayo yazidi kuongezeka


Kulwa Saiduni wa Bombo,mkoani Tanga ni miongoni mwa maelfu ya watanzania wanaoweza kupata taarifa zinazohusu afya katika hali ya utulivu wakiwa majumbani mwao.Hii inatokana na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom kuanzisha huduma ya Simu Dokta ambayo inawawezesha wateja wake waliojiunga na huduma hii kupata taarifa za afya kupitia simu zao za mkononi.

Hii huduma ni ya aina yake kuanzishwa nchini Tanzania ikiwa inatolewa na Vodacom.Inashirikisha madaktari bingwa wa fani mbalimbali  ambao wamejitolea kutoa utaalamu wao kuhusiana na masuala ya afya na taarifa hizo zinawafikia watanzania kwa njia ya mtandao wa simu popote walipo nchini.

Kulwa, kwa muda mrefu amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya mwili ambayo amekuwa hakijitibia kwa muda mrefu bila kupona.Hivi sasa amepata nafuu ya ugonjwa huu baada ya kupokea ushauri wa kitaalamu kupitia huduma ya simu dokta “Sikuweza kumudu kumuona daktari bingwa wa ugonjwa uliokuwa unanisumbua kwa muda mrefu,nimepata ushauri ambao umenisaidia kupitia huduma ya simu dokta.nimebadilisha vyakula ,natumia zaidi matunda na mboga za majani na hali yangu imebadilika kwa haraka naendelea vizuri”.Alisema.
Huduma ya simu Dokta ilizinduliwa rasmi tarehe 4,Novemba ambapo mbali na kutumika kupata taarifa za afya kutoka kwa wataalamu pia inamuwezesha mtumiaji wake kupata taarifa za madhara ya kiafya yasababishwayo na mtindo wa maisha wa mtu pia masuala mbalimbali yanayohusiana na afya kwa ujumla.Kupata huduma mteja akijiunga anakatwa shilingi 100/-kwa siku,ambapo mteja huweza kupata jumbe zipatazo mbili au zaidi kuhusiana  na masuala ya afya.

Kama ilivyokusudiwa huduma hii imekuwa msaada kwa jamii za watu wanaoishi maeneo ya vijijini ambako upatikanaji wa taarifa maeneo hayo ni mgumu pia huduma hii inakidhi juhudi za serikali kufikia malengo ya millennia ambapo lengo mojawapo namba 6 ni kukinga na kuondoa magonjwa mbalimbali.Huduma hii inawawezesha watumiaji kupata taarifa kwa wakati kuhusianana magonjwa na jinsi ya kujikinga nayo na kutunza afya zao.

“Sote tunajua kinga ni bora kuliko tiba.Wateja wetu wanaweza kupata taarifa kuhusiana na magonjwa yanayowasumbua kutoka kwa madaktari bingwa ambao wamejitolea kuelimisha jamii kupitia huduma hii na tuna imani wananchi wengi wanaendelea kunufaika nayo”.Alisema Kelvin Twissa,Mkuu wa Masoko na Mawasiliano na Masoko wa Vodacom Tanzania.

Amewataka watanzania kuchangamkia fursa ya kutumia huduma hii na kuongeza kuwa jamii ambayo inapata taarifa za kutosha ni rahhisi kujikinga na maradhi na kuchukua hatua sahihi yanapotokea magonjwa ya dharura.
Twissa aliendela kusema:”Kupata huduma hii  na ushauri kutoka kwa madaktari bingwa mteja anachotakiwa kufanya ni kutuma neno DAKTARI kwenda namba ya simu 15542”.

Baadhi ya madaktari bingwa wanaotoa ushauri kupitia huduma hii ni pamoja na Dk.Meshack Shimwela,Dk.Sulende Kubhoja ambao ni madaktari bingwa wa  magonjwa ya watoto na moyo na Dk.Munawar ambaye ni daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake.
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live


Latest Images