Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109597 articles
Browse latest View live

hOJA YA hAJA: Makosa Katika Mchakato Wa Kupata .Viongozi Wa Kisiasa


Speaker Makinda attends the 36 Plenary Assembly of the SADC Parliamentary Forum in Victoria Falls Zimbabwe

0
0
The Speaker of the National Assembly of Tanzania Hon. Anne Makinda applauds the speech from the Guest of honor during the official opening of the 36 Plenary Assembly of the SADC Parliamentary Forum in Victoria Falls Zimbabwe today. With her is the Tanzania Higher Commissioner to Zimbabwe Hon. Adad Rajab and the SADC PF treasure Hon.  Seleman  Said Jaffo. For more CLICK HERE

DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA WAWEKEZAJI LA UKANDA WA ZIWA TANGANYIKA LEO SUMBAWANGA MKOANI RUKWA

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma. kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014  katika Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga, Mkoani Rukwa.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni kumi na tano kwa wajasiriamali wadogo wadogo wa Sumbawanga kwenye Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma.  kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014  katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni kumi  kwa wajasiriamali wa Halmashauri ya Mpanda mjini kwenye Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma.  kongamano hilo linafanyika leo                  01 Nov 2014  katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia mashati ya vitenge alipotembelea banda la Mkoa wa Katavi kwenye maonesho wakati wa Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma.  kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014  katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia ndizi za aina mbalimbali alipotembelea banda la Mkoa wa Kigoma kwenye maonesho wakati wa Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma.  kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014 katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa. Picha na OMR

SIMBA YAZIDI KUELEMEWA NA DROO, YATOKA SARE NA MTIBWA 1-1 LEO...

0
0
Hassan Ramadhan wa Mtibwa akijaribu kuudhibiti mpira huku akizongwa na Mohamed Hussein wa Simba, wakati timu hizo zilipopambana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom, Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro.
Mchezo ulimalizika kwa droo ya 1-1

YANGA YAKUNG'UTWA NA KAGERA SUGAR BAO MOJA KWA NUNGE

0
0
Timu ya Yanga leo imefungwa 1-0 na Kagera Sugar katika Uwanja wa Kaitaba katika Ligi Kuu ya Vodacom, mjini Bukoba, Kagera.


Na Faustine Ruta, Bukoba
Klabu ya Dar es salaam Young Afrika imekubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa wenyeji wao Kagera Sugar kwenye mchezo uliopigwa ndani ya Uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba.
Kipindi cha kwanza Timu zote mbili zilimaliza bila ya kufungana, Kipindi cha pili Kagera Sugar walitumia faida ya kucheza nyumbani na kufanikiwa kupata bao lililofungwa kiufundi na paul Ngwai na kuibuka na ushindi huo wa bao 1-0 na kuwaacha Yanga wakibaki na pointi zao 10 ambazo wamevuna katika michezo 6.

Profesa Mwandosya ahitimisha ziara yake ya siku sita nchini Ethiopia kwa kukagua ujenzi wa Ofisi za Bonde la Mto Abay - White Nile

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Kazi Maalum) Profesa Mark Mwandosya leo amemaliza ziara yake ya siku sita nchini Ethiopia kwa kukagua ujenzi wa Ofisi za Bonde la Mto Abay (White Nile),kutembelea chanzo cha Mto Abay,na kutembelea maporomoko maarufu ya Mto Abay (White Nile).
Waziri Mwandosya,kushoto,akiwa na Mhaidrolijia Mengistu,Mkurugenzi Mkuu wa Bone la Mto Abay baada ya kukagua kazi zinazoendelea za ujenzi wa Makao Makuu ya Bonde mjini Bahar Dar, Amhara.
Waziri Mwandosya kwenye mti uliopandwa na mwakilishi wa Tanzania wakati wa kuweka jiwe la msingi wa Jengo wakati wa sherehe za Siku ya Nile, mwaka 2013.
Waziri Mwandosya,kushoto,na Mhaidrolojia Mengistu, kulia,na Mama Lucy Mwandosya,katikati,wakiwa kwenye maporomoko ya Mto Abay,yaliyo 'Kebele'ya Tis Abay.
Waziri Mwandosya na Mama Lucy Mwandosya wakiwa na wenyeji wao wa Gish Abay, Wilaya ya Sekela,chanzo cha Mto Blue Nile, kilicho kilomita 150 kutoka Bahar Dar.

balozi seif azinduwa msikiti wa Kijiji cha Tasani Makunduchi

0
0
Wanazuoni, Masheikh na wazee wote nchini wana wajibu mkubwa wa kuisaidia Serikali Kuu katika jitihada zake za kukuza elimu, kujenga jamii iliyo bora, kulinda amani pamoja na kukataza maovu vikiwemo vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji wa kijinsia.
 Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al – hajj Dr. Ali Mohamed Shein wakati akiufunguwa msikiti wa Kijiji cha Tasani Makunduchi unaokadiriwa kusaliwa na waumini wapatao 200 kwa wakati mmoja wa sala. 
Dr. Shein ambae Hotuba yake ilisomwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema katika msaada huo Masheikh wana fursa nzuri ya kuzungumza na waumini wao hasa kupitia hotuba za sala za ijumaa ili kujenga jamii iliyo bora. 
Alisema Dini imekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa zaidi kwenye suala zima la kukuza maadili mema , malezi ya watoto sambamba na kuendeleza hali ya kuishi kwa upendo miongoni mwa jamii yote. 
Mapema asubuhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwa Niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi alilifungua jengo la Madrasatul Shafiat liliopo katika Kijiji cha Kajengwa Makunduchi. 
Akizungumza na waumini hao Dr. Shein alisema ufunguzi wa madrasa hiyo ni kielelezo cha jitihada za wananchi wa kajengwa kwa kushirikiana na viongozi wao katika kutilia maanani haja ya kuwapatia elimu ya dini watoto wao jambo ambalo limefaradhishwa na Mwenyezi Mungu. 
Alisema elimu nizawadi na urithi bora kwa watoto ambao huwajenga kuwa na ucha mungu, kujua utu, kuheshimu haki za watu wenye imani za dini nyengine sambamba na kumtukuza mola anayeteremsha neema kwa viumbe wote.
 Maustadhi wa baadae wakifurahia ufunguzi wa Madrasa yao ya Shafiiyat iliyopo Tasani Makunduchi uliofanywa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein.
 Ustaadhati Halima Rajab Hassan akimkabidhi zawadi ya kofia ya asili ya kiua iliyoshonwa Makunduchi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwa niaba ya Rais wa Zanzibar mara baada ya kufungua Madrasa ya Shafiiyat ya Tasani Makunduchi.
 Balozi Seif kwa niaba ya Rais wa Zanzibar akiufungua rasmi Msikiti wa Kijiji cha Kajengwa utakaotoa huduma za ibada za sala na madrasa kwa waumini wa Kijiji hicho.
Balozi Seif akiwapongeza akina mama wa Kijiji cha Kajengwa kwa ushirikiano wao na Viongozi wao na hatimae kupelekea kupata nyumba ya ibada. 
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

A UNIFIED APPROACH TO ENHANCING SECURITY IS VITAL – LEGISLATORS ASSERT AS NANYUKI VIII ENDS IN KIGALI

0
0
The Eighth Inter-Parliamentary Relations Seminar (Nanyuki Series) has ended with a call for a multi-dimensional and regional approach to security while bearing in mind that consequences of terrorism cannot be fully contained within national boundaries. 
 The legislators are calling for development of a conceptual framework on terrorism in the regional context that addresses relationship to other crimes such as money laundering, human and drug trafficking, poaching and the proliferation of Small Arms and Light Weapons (SALW). 
 The Resolution passed today further calls on EALA and National Assemblies to develop a joint platform to work on issues of peace and security in the region. Another consensus is to urge Partner States to expedite the ratification and implementation of all regional peace and security related protocols and commitment. 
 Further on, there is need to develop a deliberate programme of inclusion for persons and sectors of society that are often left out of the peace and security initiatives. Such include women, youth, children and various minorities. 
 To spur this aspect, delegates also want the establishment of twinning programmes between people and institutions of Partner States to facilitate social cohesion. This aspect, should accordingly start with border communities, creative industries, schools among others, to increase citizen participation in regional peace and security efforts.
 The Resolution further avers that a framework be established for working with other bodies, be they regional, continental and international on matters of peace and security. This is based on the premise that different Partner States have different commitments to one or more bodies and blocs. Delegates at the seminar called for the deepening of commitment to the development of a shared East African identity by promoting the use of Kiswahili as a lingua franca, observing the same driving side and adopting a common time zone Earlier on, the Heads of delegation made key statements speaking to the theme of the conference. 
 Hon Tony Ayoo of the Parliament of Uganda noted that Parliament of Uganda had passed legislation to integrate combatants back into the society. At the same time, community policing has been strengthened and capacities to share information enhanced. 
 He noted that the recommendations of the 8th Nanyuki series would be tabled on the floor of the House in the Parliament of Uganda. Hon Florence Kajuju of the Kenya National Assembly, remarked that integration was key. 
 The Kenya National Assembly according to Hon Kajuju ratified the Protocol of the Monetary Union last week on Thursday (October 30th, 2014). She maintained that sensitization was instrumental to enable ownership by the citizens. The legislator noted that Kenya had been hard-hit by terrorism and added that the Defence forces were on the high alert. 
 “We must engage in seeking lasting solutions to the challenges of peace and security,” Hon Kajuju said. 
 Hon (Prof) Juma Kapuya of the United Republic of Tanzania said peace and security was a pre-requisite to economic integration and called on Partner States to do all it takes to firmly rid the EAC of terrorism. 
 “We need to share security intelligence, and strengthen border community initiatives on the same”, Hon Kapuya said. “Joint mechanisms for policing framework and building joint capacity on counter-terrorism are likewise key”, Prof Kapuya added. 
 Hon Ramadhan Karenga of Burundi National Assembly cited cyber crime, kidnapping, terrorism, maritime piracy and internal conflicts as some of the areas that must be contained. “The dream of free movement will not become a reality if we do not address the problems. We must achieve peace and security to drive forth our economic growth”, Hon Karenga said. 
 He remarked that Burundi had set up a four point security framework, aimed at assuring internal public security, promoting good governance on security matters, capitalizing and valuing various resources of post-conflict gains and setting up special mechanisms to prevent and fight terrorism. The security situation in Burundi, Hon Karenga added, had improved away from the previous years’ cyclic strife. 
 “We are in fact now sending troops to war torn areas including Darfur, Sudan, Central Africa Republic and Chad. This is progressive”, Hon Karenga added. 
 Senator Jacqueline Muhongayire of Rwanda noted that genocidal ideology and extremisms such as youth radicalization were responsible for terrorism and trans-border crime. She said Rwanda had ratified all regional Protocols that were signed by the Partner States. The Protocols are on Foreign Policy Co-ordination, Protocol on Co-operation in Defence, Protocol on Peace and Security, Protocol on Anti-Narcotics and Drug trafficking. 
 “We call upon Partner States to ratify the same”, Senator Muhongayire said. Addressing participants yesterday, a political analyst and university don, Prof Adams Oloo told the Partner States to provide a clear hegemony in the securitizing process to contain terrorism, and strengthen regional security. Prof Oloo maintained that disunity in the approaches taken by each state in addressing security issues beyond borders was detrimental to security. 
 He called for shared understanding on what constitutes common threats to their survival as a region. The presenter cited several contemporary security challenges including intra-state conflicts, resource based conflicts, piracy and organized crime. Prof Oloo said that mistrust and suspicion between Partner States should be curtailed as this would contribute to the lack of progress in implementing a regional security strategy. 
 The seminar themed: “Insecurity and Terrorism as Threats to EAC Integration: How Can EAC Develop a Common Position” was organized by EALA in conjunction with the Association of European Parliamentarians with Africa (AWEPA). 
 An estimated 250 participants drawn from Partner States National Assemblies, EALA, academicians, high ranking Government officials as well as other regional stakeholders were in attendance.
A section of the delegates pay attention to the EAC Anthem
From left: Hon Tony Ayoo, MP, Parliament of Uganda, Amb Dr Richard Sezibera, Secretary General, EAC and the President of the Rwanda Senate, Rt. Hon Bernard Makuza share a moment on the sidelines of the Nanyuki VIII series


KUMBUKUMBU

0
0
           DONATA GASPAR TARIMO: 
7/8/1958 - 31/10/2013

Mama, ni mwaka mmoja sasa tangu ulivyoitwa na Bwana Mungu siku ile ya tarehe 31 Oktoba, 2013 saa Nne usiku. Kimwili hauko nasi, lakini kiroho tunaamini upo nasi. Daima tunakukumbuka mama, kwa upendo wako, ukarimu, ucheshi, busara zako, ushauri wako kwetu na kwa kuleta mshikamano katika familia. 
Mama, ulikua nguzo muhimu katika kuhimili mawimbi na kustawisha maendeleo katika familia na jamii inayotuzunguka. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa muda wote tuliokuwa na wewe hapa duniani, kwani malezi yako mema yamekua msingi mkuu wa maisha yetu. Tunaamini siku moja tutakutana huko uliko mama.
Ingawa maisha yanaendelea, tunakosa mengi sana tuliyoyazoea kutoka kwako na hatuwezi kufananisha hali ilivyo sasa hata chembe na namna tulivyokuwa na wewe. Tulikupenda sana mama, lakini Mungu amekupenda zaidi.
Unakumbukwa sana na mumeo Gaspar, wanao Martha, Michael, Kuki-Renatus, Charles na Emmanuel. Mkweo Jackline, na mjukuu wako Lance-Manase. Unakumbukwa pia na mama yako, kaka zako, dada zako, shemeji zako, wifi zako, wapwa zako, ndugu zako, majirani, jamaa na marafiki.
Mwenyezi Mungu Ailaze Roho yako mahali Pema Peponi. Amina.
….Mimi ndimi ufufuo na uzima, yeye aniaminiye ajapo kufa, atakuwa anaishi, nae kila aishie na kuniamini hatakufa kabisa hata milele…… 
Yoh 11: 25-26

FURSA KWA WANAFUNZI WA MBA VYUO VYOTE VYA TANZANIA

news alert: binti wa miaka 12 atoweka nyumbani kwao temeke, dar es salam, wazazi wanamtafuta

0
0

Jina: Mwasiti Abdulrazack Kakurwa. 

Umri miaka 12. 
Rangi ya mwili: Mweusi. 


Mara ya mwisho alivaa T-shirt iliyoandikwa Mnazi Mmoja primary School, na alijifunika mtandio mweusi. Ametoweka jana jioni maeneo ya mtaa wa Berege, Tandika, Temeke, Dar es salaam.
Yeyote atayemuina ama mwenye taarifa zake tunaomba taarifa zipelekwe katika kituo chochote cha polisi ama Kituo cha police tandika, Temeke,  na police Chang'ombe, Dar es salaam. Ama kwa Mzazi Abdurazack Kakurwa, namba ya simu 0713 835699, au Mubashiry Kakurwa, simu namba 0756/0717 -166438

FRANCO LWAMBO LWANZO MAKIADI NA TP OK JAZZ ENZI HIZO LIVE!

COPY & PASTE YA TP OK JAZZ YA KILWA JAZZ ENZI HIZO

0
0
Ukimaliza wimbo huu sikiliza wa hapo chini....

hoja ya haja: Suffer the pain of discipline now. Or else you will suffer the pain of REGRET later! Life Begins at 40 my friend.. How Old Are You?

0
0
Huo ni msemo wanao waingereza....

Today is your future kwa taarifa yako.. Ulipokuwa mdogo ulisema nikiwa mkubwa nitakuwa na gari na nyumba nzuri wazazi wangu wataishi hivi na vile. Je unayo? Je imetokea? Maybe yes. But maybe no.

Kama haijatokea je bado hujawa mkubwa? Basi kama ni mkubwa ujue kuna kitu hujafanya. 
Utasema tena nikifika miaka 40 nataka niwe na hiki na kile watoto wangu wasome international skul nk. Subiri uone miaka inavyoenda. Usishangae kufika 40 bado umeajiriwa kwa mtu na anakugombeza kwa nini mwanao anaumwa kila siku unachelewa kazini. Kazi nyingi. No bright future. No enjoyable present. Just existing and not living!
Hapo ndo unawaza kufuga ng'ombe wa maziwa Kibamba kwenye kiwanja chako cha miguu 12 kwa 15! Wenzako wa umri wako hapo unasikia wameanzisha bizness in Australia. Wamenunua kiwanja Mbezi Beach kwa 300M! Wanamiliki Apartment Johannesburg. Wakienda UK wanaenda kula The Ritz (Google that). Wanasomesha watoto zao the finest schools available wewe wa kwako wakati huo wamekosa nafasi Makongo wameenda Kibamba Secondary School wanapanda daladala sita kwenda na kurudi full kutukanwa na makonda.
Wenzako in their 40s wanasaidia wasio na uwezo katika jamii wewe ndo kwanza ukipokea simu kutoka kijijini una-mute! Wenzako in their 40s wakisikia kuna ujenzi wa nyumba ya ibada wanachangia 5M kimyakimya.. Wewe ukitoa laki moja basi mpaka mtaa wa saba watakujua! Halafu unashangaa wanazidi kuinuliwa. Mwenye nacho ataongezewa au hujui? Na asiye nacho..... (Malizia)
Wenzako in their 40s wana exposure ya uhakika. Walishafika kuanzia Sauzi, Botswana, Mozambique, Kenya, Ethiopia, Ghana, Naija, mpaka Egypt, The UK, Australia, Hawaii, Mexico, Croatia, The Netherlands, Switzerland, US, Panama mpaka Puerto Rico, Brazil na jirani zake, Hong Kong, Australia, Japan, China, (Incredible) India, Thailand, Singapore, New Zealand, Comorros, you name it..!! Wewe hata Kampala hujawahi fika. Kila siku Tegeta Posta ndo ruti yako miaka 15 mfululizo eti unatafutia watoto maisha! Unaishi au unaisha?
Acha mawazo mgando. Hiyo ajira ifanye serious sana tu lakini kwa muda tu. Jiandae kusimama mwenyewe. Kwani hujiamini? Na Mungu naye humwamini? Changamoto ni sehemu tu ya kufika kileleni. Don't be afraid. Don't dwell in that comfort zone!! Unasubiri kiinua mgongo? Utaenda kukiinvest wapi na kwa nguvu ipi. Na utaenjoy retirement kweli kama at 60 yrs ndo unafungua duka la vifaa vya ujenzi eti vinalipa. Kwa nini hukufungua ukiwa 30 ili uone vinalipa au la. At 60? With due respect.

Suffer the pain of discipline now. Or else you will suffer the pain of REGRET. Halafu ukianza kuregret ndo pressure zinakuja, stress, nk mwisho unawacha hata hao watoto in a far worse situation than your own lifetime.

Life Begins at 40 my friend.. How Old Are You?
Inbox me tushauriane fursa inayoweza kukupa hayo unayoona leo kama ndoto. Kamata fursa #twenzetu!

ngoma azipendazo ankal

0
0
Angela Chibalonza - Ebenezer

PRESIDENT KIKWETE GIVES NEW SUNDERLAND FC ACADEMY HIS SEAL OF APPROVAL

0
0
President Kikwete asks TFF President to support the project during the ceremony to mark a milestone in the start of the construction for a new community-based Sports Park in Dar es Salaam. 
 As part of Sunderland AFC’s ground-breaking football partnership with Tanzania, the club is lending its expertise to the creation of a football development programme in the country, in partnership with Symbion Power.

The kids are happy with  the project

Youths are invited to assist President Kikwete plant a commemorative tree
More applause as President Kikwete and one of the youths water the commemorative tree seedling. For More CLICK HERE

JK alipowatunuku Kamisheni maafisa wa ngazi ya chini 437 wa Jeshi la Kongo na JWTZ Monduli Arusha

Kila la Kheri Spika Makinda, Urais Bunge la SADC

0
0

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiteta jambo na Spika wa Bunge la Afrika Kusini Mhe. Baleka Mbete kabla ya kuanza kwa kikao cha Mkutano wa Jukwaa la Mabunge ya Nchi wanachama wa SADC jana mjini Victoria Zimbabwe. Uchaguzi wa Rais wa Jukwaa hilo unafanyika leo ambapo Spika Makinda anaungwa Mkono na Nchi nyingi za SADC .
Kwa habari kamili BOFYA HAPA

MBUNGE MBATIA ATEMBELEA SHULE YA SEKONDARI YA BISHOP MOSHI JIMBONI VUNJO

0
0
Mh  James Mbatia akizungumza jambo  katika chumba maalumu cha kujifunzia Kompyuta katika shule ya Sekpndri ya Bishop Moshi jimboni Vunjo.
Mh Mbatia akitizama baadhi ya vitabu katika maktaba ya shule hiyo,kulia ni mkuu wa shule hiyo Sophia Mushi. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Sherehe za KMKM za kufurahia Ushindi Misimu Miwili‏‎ mfululizo

0
0

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wapiganaji wa jeshi la KMKM katika sherehe za ushindi wa timu zake katika michezo mbali mbali kwa misimu miwili zilizofanyika leo viwanja vya maisara Mjini Zanzibar (kulia) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara maaalum za SMZ Haji Omar Kheri. 
 Kamanda Haidari akiwa kama kocha kwa Timu yake ya Makamanda waliostaafu wa KMKM katika sherehe za  sherehe za KMKM kwa ushindi wa timu zake kushinda misimu miwili mfulizo michezo mbali  mbali  kutoka 2013-2014 mpaka 2014/2015,zilizofanikisha kwa mchezo wa kuvuta Kamba na hatimaye timu hii ya wastaafu iliwashinda Maofisa walio kazini kwa kuwatoa katika raund zote mbili leo viwanja vya Maisara.


Viewing all 109597 articles
Browse latest View live




Latest Images