Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109597 articles
Browse latest View live

Court declines to grant ex parte order in an application by a Tanzanian resident

0
0
The First Instance Division declined to grant ex parte order (meaning to grant order to one party in the absence of the other parties involved in the matter) to a Tanzania resident seeking for an interim order that the government of Kenya deposit the amount of 28,475,737 Ksh. to EACJ being decretal amount awarded to him in the civil case at the High Court of Kenya as required under Rule 21 (2) of the East African Court of Justice Rules of Procedure.

The Court said that the Applicant failed to convince the Court the urgency of granting the order in the absence of the other parties and the irreparable damages the Applicant would suffer if the order was not granted.

The subject of the main case is that the Applicant (Alfred Koroso) a business man from Moshi, Tanzania, was arrested and placed in custody at Taveta police station; he was charged of robbery with violence and later acquitted after he was found not guilty.

The Applicant after being acquitted he filed a case in Nairobi High Court Kenya for payment of damages for wrongful arrest, confinement and prosecution by the government of Kenya.

The Applicant claims that the amount awarded to him was supposed to be paid within 30 days from the Date of the judgement of the High Court of Kenya on 25th March 2013 which has never been paid up to date.
Karoso (the Applicant) therefore alleges that the refusal and failure and frustration the decree by the government of Kenya to comply with the Court order is an infringement of Article 6 (d) and 7 (2) of the Treaty for the Establishment of the East African Community.

He further alleges that he has continued to suffer and incurring more damages therefore claiming in the main case to be paid additional amount of 5,086,465 Ksh. plus the decretal amount that was awarded to him earlier by the High Court of Kenya.

The Court has therefore declined to grant the ex parte order and ruled that the Applicant serves other parties in the case and the matter be heard and determined inter party (Hearing the case in the presence of all the parties involved in the matter). The Permanent Secretary Ministry of State for provincial Administration and Internal Security is also a party in the case.

Rule 21 (2) provides that; No motion shall be heard without notice to the parties affected by the application. Provided, however, that the First Instance Division, if satisfied that the delay caused by proceeding in the ordinary way would or might entail irreparable injustice, may hear the motion and make any ex parte order upon such terms as to costs or otherwise, and subject to such undertaking, if any, as the Division deems just.

Article 6 (d) of the Treaty provides that, good governance including adherence to the principles of democracy, the rule of law, account ability, transparency, social justice, equal opportunities, gender equality, a s well a s the recognition, promotion and protect ion of human and peoples right s in accordance with the provisions of the African Charter on Human and Peoples’ Rights;

Article 7 (2) provides that; The Partner States under take to abide by the principles of good governance, including adherence to the principles of democracy, the rule of law, social justice and the maintenance of universally accepted standards of human rights.

Tanzania, Thailand kushirikiana katika madini na vito

0
0
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo (mwenye shati la batiki), akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Wafanyabiashara wa Madini ya Vito wa Thailand, walipotembelea Banda la Tanzania katika Maonesho ya 54 ya Vito na Usonara ya Bangkok, yaliyofanyika Septemba 9 hadi 13 mwaka huu.
Makamu wa kwanza wa Rais wa Taasisi ya Wafanyabiashara wa Madini ya Vito na Usonara wa Thailand, Bw. Sutipong Dumrongsakul, akimkabidhi zawadi maalumu Mkuu wa Ujumbe kutoka Tanzania ulioshiriki maonesho ya vito ya Bangkok, Archard Kalugendo, mara baada ya kikao kati ya Ujumbe huo na Viongozi wa Taasisi hiyo ya Wafanyabiashara wa Thailand.
Wateja mbalimbali wakihudumiwa katika Banda la Tanzania kwenye maonesho ya vito na usonara ya Bangkok yaliyofanyika hivi karibuni nchini   Thailand.

BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI KAMILI

WANANCHI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA WATAALAM WA UTAFITI WA HALI YA UMASIKINI WA KAYA TANZANIA

0
0
Naibu Waziri wa Fedha –Sera, Mhe. Mwigulu Nchemba akifungua mafunzo ya wiki tatu ya wakufunzi, wasimamizi na wadadisi kutoka Tanzania Bara na Zanzibar watakaoendesha utafiti wa kufuatilia hali ya umasikini katika kaya mwaka 2014/15.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Joel Bendera akiwakaribisha washiriki wa mafunzo ya wiki 3 ya utafiti wa kufuatilia hali ya umasikini katika kaya mwaka 2014/15 mkoani Morogoro.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumzia umuhimu wa matumizi ya takwimu sahihi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya wakufunzi, wasimamizi na wadadisi kutoka Tanzania Bara na Zanzibar watakaoendesha utafiti wa kufuatilia hali ya umasikini katika kaya nchini mwaka 2014/15.

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI

APPRECIATION

0
0
THE LATE MR. EDWARD ELIEZER NDALAMA 

We; the family of the late Mr Edward Eliezer Ndalama wishes to express our sincere heartfelt thank you for your support you have given us during the difficult time of the death of our dearest husband, father, grandfather, brother and a friend Mr Edward Eliezer Ndalama who died on the 06/07/2014 and was laid to rest on 11/07/2014 at Kinondoni cemetery in Tanzania.

Words cannot express how we appreciate each one of you; you have supported us.

Please join us to celebrate the life of our dearest husband, father, grandfather, brother and a friend;
Mr Edward Eliezer Ndalama
whom we loved dearly but Our Almighty Father loved him more.
We are kindly inviting you to the thanksgiving mass which will be held on the 20/09/2014 at 5pm and thereafter the thanksgiving dinner.
The mass and thanks giving dinner will be held at St Mary's Church Hall, 1 Mount, Acton High Street, London, W3 9NW.
R.S.V.P
Ms Gladys
Mobile: 07771645260
Jacq
Mobile: 07983886022

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA MPANGO WA UTAMBUZI WA UJUZI ULIOPATIKANA NJE YA MFUMO RASMI WA MAFUNZO, JIJINI DAR LEO

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kama ishala ya kuzindua rasmi mpango wa Utambuzi wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa mafunzo, kwa ajili ya kutathimini na kutambua ujuzi na elimu ua ufundi Stadi kwa Vijana waliojifunza fani mbalimbali, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika leo Septemba 19, 2014 kwenye Hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Kazi, na Ajira, Gaudensia Kabaka (kushoto) ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dkt. Shukuru Kawambwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti, mmoja kati ya wahitimu 30, wa mafunzo hayo, Charles Gwambassa, wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango wa Utambuzi wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa mafunzo, kwa ajili ya kutathimini na kutambua ujuzi na elimu ua ufundi Stadi kwa Vijana waliojifunza fani mbalimbali. Hafla hiyo ilifanyika leo Septemba 19, 2014 kwenye Hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti, mmoja kati ya wahitimu 30, wa mafunzo hayo, Mwajuma Massoud, wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango wa Utambuzi wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa mafunzo, kwa ajili ya kutathimini na kutambua ujuzi na elimu ua ufundi Stadi kwa Vijana waliojifunza fani mbalimbali Hafla hiyo ilifanyika leo Septemba 19, 2014 kwenye Hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam.

WASTAAFU WA JESHI LA MAGEREZA WAAGWA RASMI LEO MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA JIJINI DAR

0
0
Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja akitoa nasaha fupi katika hafla fupi ya kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza ambao wamestaafu rasmi Utumishi wa Umma tangu Julai 1, 2014. Hafla hiyo imefanyika leo Septemba 19, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
Wastaafu wa Jeshi la Magereza(katika picha) wakiwa na familia zao wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) wakati akitoa nasaha fupi kwa Wastaafu hao ambao wamestaafu Utumishi wa Umma tangu Julai 1, 2014.
Kwaya ya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza inayoundwa na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza ikitumbuiza kwenye hafla hiyo ya kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza. Hafla hiyo imefanyika leo mchana Septemba 19, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Jijini Dar es Salaam.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakishangilia Wimbo Maalum uliotumbuizwa na kwaya ya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza katika hafla fupi ya kuwaaga Maafisa na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza ambao wamestaafu Utumishi wao kwa mujibu wa Sheria tangu Julai 1, 2014.
Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(kulia) akikabidhi zawadi kwa Sajin Taji wa Jeshi la Magereza, Kessy Ngwengwe(kushoto) ambaye alikuwa ni Dreva wa Magari ya Viongozi Makao Makuu ya Jeshi Magereza. Askari huyo amestaafu Utumishi wake wa Umma tangu Julai 1, 2014.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wastaafu wa Jeshi la Magereza(waliosimama mstari wa nyuma) kwenye hafla fupi ya kuwaaga Wastaafu hao ambao amestaafu Utumishi wao wa Umma tangu Julai 1, 2014(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

PPF YAWANOA WAAJIRI KUHUSIANA NA HUDUMA ZAKE MPYA IKIWEMO PPF TAARIFA APP

0
0
Prof. Betria Mapunda ambae amemwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar Es salaam akifungua semina iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa Waajiri kwa lengo la Kutoa elimu juu ya huduma zitolewazo na mfuko huo wa Pensheni wa PPF katika ukumbi wa Seaescape, Uliopo Mbezi Beach Jijini Dar Es Salaam.
Meneja wa Kanda ya Kinondoni wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Zahara Kayugwa akitoa mada wakati wa semina iliyoandaliwa na Mfuko wa Penhsheni wa PPF kwaa Waajiri wa Makampuni na mashirika mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa Seaescape, Mbezi Beach Jijini Dar Es Salaam leo.
Majaliwa E Mkinga, Mchambuzi na Mtengenezaji wa Mifumo ya Teknolojia ya habari na mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF akielezea jinsi PPF ilivyotengeneza mfumo wa kupata taarifa za wanachama kupitia simu aina za Smartphone na kuutaja mfumo huo kuwa ni PPF TAARIFA App ambayo mteja ataweza kuiweka katika simu yake ya mkononi.
Baadhi ya waajiri wakielekeza kuhusu jinsi ya kuweka mfumo wa PPF Taarifa katika simu zao za Smartphone leo katika semina iliyofanyika katika Ukumbi wa Seascape hotel Mbezi beach Jijini Dar Es Salaam.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Unamkumbuka Bingwa wa zamani mbio za mita 400 Tanzania??

0
0
Unamkumbuka Morris Okinda? Yule bingwa wa zamani wa mbio mita 400 kuruka viunzi, hivi sasa ndiyo Mkuu wa Polisi (OCD) wilaya ya Monduli.Okinda aliweka rekodi ya mita 400 kuruka viunzi katika mashindano ya Afrika mwaka 1985 jijini Cairo Misri akitumia sekunde 51:20 ambayo kitaifa haijavunjwa mpaka hii leo.Waalifu wakikimbia jamaa akiwepo hawachukui raundi maana alikuwa anawakamata dakika tu maana anakimbiza upepo balaa.

ORIJINO KOMEDI NA UJIO WAO MPYA

MDAU AKIPUNGA UPEPO UFUKWENI

0
0
Kamera ya Globu ya Jamii katika pita pita zake imefanikiwa kuinasa Taswira ya mdau huyu akiwa kaketi kwenye kiti chake huku pembeni akiwa kaegesha usafiri wake wakati akipunga upepo katika ufukwe wa bahari ya Hindi,jijini Dar jioni hii.

MKUU WA MKOA WA RUVUMA AKUTANA NA WAENDESHA PIKIPIKI SONGEA

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akizungumza na waendesha pikipiki (Maarufu kama  Boda Boda) leo hii katika ukumbi wa Songea Club uliopo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma. Mwambungu amewataka dereva Boda boda kuepusha ajali za barabarani kwa kufuata sheria,kutotumiwa katika maandamano ya kisiasa ambayo yanapelekea uvunjifu wa amani na kuwafanya wapoteze maisha ama kuwafanya kuwa walemavu.
 Pichani ni umati wa waendesha pikipiki wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wakimsikiliza mkuu wa Mkoa  ambaye hayupo pichani. Ambapo katika mkutano huu amewaasa mambo mengi ikiwemo suala lililotokea hivi karibuni la kuwarushia bomu askari polisi waliokuwa kwenye doria na kuwajeruhi askari wa tatu.
Madereva pikipiki hawa wakimsikiliza mkuu wa mkoa kwa umakini huku wakiahidi kutoa ushirikiano wa kuwafichua wahalifu ambao wamejiingiza katika huduma ya kusafirisha abiria kwa lengo la kuwachafua na wao kukidhi mahitaji yao.
Piki piki zikiwa zimepaki nje ya mkutano.(Picha zote na demasho.com)

MAADHIMISHO YA SIKU YA UTALII 2014 KUFANYIKA JIJINI ARUSHA

0
0
Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha pamoja na Wadau wa Sekta ya Utalii nchini wanayofuraha ya kuwakaribisha Wananchi wote na Wadau mbalimbali katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani kwa mwaka 2014 ambayo Kitaifa yatafanyika Mkoani Arusha kwenye viwanja vya Nane Nane (TASO) kuanzia tarehe 20 hadi 28 Septemba, 2014.

Siku ya Utalii Duniani huadhimishwa tarehe 27 Septemba ya kila mwaka ambapo kila nchi mwanachama wa Shirika la Utalii Duniani (UNWTO) husherekea siku hii, kwa lengo la kuweka uelewa kwa Jamii kuhusu umuhimu wa utalii na thamani yake, kijamii, kisiasa, kitamaduni na kiuchumi.

Kauli Mbiu ya Mwaka huu ni “Utalii na Maendeleo ya Jamii’’ (Tourism and Community Development) kwa kuzingatia Kauli Mbiu hii, tunawajulisha wadau wote katika nyanja mbalimbali za Utalii, Maliasili na Uhifadhi, vikundi vya jamii na wajasiriamali, viongozi na wataalamu kwa pamoja kushiriki kikamilifu katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani kwa nia ya kujifunza na kutambua fursa za kiuchumi zilizopo katika Sekta ya Utalii na kutumia fursa hizo kujikomboa katika umaskini.

Shughuli zitakazofanyika ni pamoja na kuwasilisha na kuonesha na kwa vitendo juu ya tafsiri ya Kauli Mbiu kwa kufanya kongamano la ushirikishwaji wa jamii kwenye sekta ya Utalii kwa ajili ya kujiletea maendeleo, mashindano ya Uchoraji wa picha kuhusiana na kauli mbiu, michezo na burudani mbalimbali.

Vilevile kutakuwa na maonesho ya utalii, malikale, misitu na masuala ya uhifadhi kwa ujumla na bila kusahau ziara ya kutembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Arusha kwa nia ya kuhamasisha wananchi kushiriki kwenye shughuli za utalii wa ndani.

Wito unatolewa kwa kuwaalika wadau wote wa utalii na jamii husika kuja kwa pamoja na kuadhimisha siku hii kama ishara ya jitihada za pamoja za kufanya utalii nguzo ya kweli ya maendeleo ya Jamii nchini.

KINANA , NAPE WAITEKA KIBAHA

0
0
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wakazi wa Kibaha mjini wakati wakiwasili kwenye uwanja wa mkutano .
 Kikundi cha ngoma cha Kisamamwe kikitumbuiza ngoma ya Afrika kabla ya kuanza kwa mkutano wa hadhara ambapo Katibu Mkuu wa CCM alihutubia wananchi wa Kibaha mjini.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kibaha mjini ambapo aliwaambia wapinzani wamekosa hoja ya msingi kiasi cha kuamua kufanya maandamano ya kuleta vurugu nchini.
 Sehemu ya Umati wa watu wakisikiliza mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Wana CCM wakiwa kwenye mkutano
 Mbunge wa Kibaha mjini Silvestry Francis Koka akihutubia wakazi wake na kuwaambia kuwa pamoja na jitihada zote anazofanya maji bado ni donda sugu ila ufumbuzi upo njiani.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kibaha mjini wakati wa mkutano wa hadhara ambapo aliwaambia viongozi wa halmashauri hawana budi kukaa na wafanya biashara ndogo ndogo kujadili kodi kabla ya kuwapangia kuona kama wana uwezo wa kulipa ama hapana hii itasaidia kupunguza lawama na mikingamo baina ya wafanya biashara na halmashauri.

MHE. BALOZI PHILIP MARMO AWEKA SAINI MKATABA WA MKOPO KUTOKA MFUKO WA MAENDELEO YA KIMATAIFA

0
0
Mhe. Balozi Philip S. Marmo wa Ubalozi wa Tanzania Ujerumani yuko Vienna, Austria tarehe 9 Septemba, 2014 kuweka saini Mkopo kwa mradi wa tatu wa kupunguza umasikini wa Dola za Marekani 16,350,000 na mradi wa kuendeleza Elimu wa Dola za Marekani 10,200.000. Miradi hiyo itatekelezwa na serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Mheshimiwa Balozi Marmo anawakilisha pia Austria kutoka Ujerumani. Mkataba huo ulisainiwa katika ofisi za OFID, Vienna, Austria kati yake na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa OPEC kwa ajili ya Maendeleo ya Kimataifa, OPEC Fund for International Development(OFID) Bw. Suleiman J. Al-Herbish.
Balozi Philip S. Marmo akiweka saini Mkataba wa Mkopo kutoka Mfuko wa OPEC , OFID Ofisi ya OFID iliyopo Austria, Vienna tarehe 9 Septemba, 2014.
Balozi Marmo akipokea Nakala ya Mkataba wa Mkopo kutoka Mfuko wa OPEC kutoka kwa Bw. Suleiman J. Al-Herbish, Mkurugenzi Mkuu wa OFID-Mfuko wa Maendeleo wa OPEC , Austria, Vienna tarehe 9 Septemba.

INTRODUCING ITS GOING DOWN- AY FEATURING MS TRINITI & LAMYIA


TANZIA

0
0
Familia ya aliekua mwanamuziki wa bendi za super matimila na tanzania one theatre TOT Fredy Mwalasha inasikitika kutangaza cha baba yaompendwa Fredy Mwalasha kilichotokea saa 5 asubuhi ya leo tarehe 19/9/2014,mazishi yanatarajia kufanyika mkoani morogoro mara baada ya mwili kuwasili...

KIGOMA MWISHO WA RELI

0
0
Mdau Hassan aliopo safarini Mkoani Kigoma,ametuletea taswira hii aliyoidaka leo alipotembelea eneo la mwisho wa Reli mkoani Kigoma.

MAMBO YA GADO

ngoma azipendazo ankal - kindly sponsored by Isumba lounge

0
0
Brenda Fassie - Weekend Special

WANACHAMA WA NHIF MKOANI KIGOMA WAUOMBA MFUKO HUO KUGHARAMIA KIPIMO CHA VINA SABA (DNA)

0
0
BAADHI ya wanachama wa mfuko wa Bima ya afya (NHIF) wameutaka mfuko huo kugharamia kipimo cha vina saba (DNA) kwa wananchama wake pamoja na gharama za nauli na posho kwa wanachama wanaokwenda kupata matibabu nje ya vituo vyao vya kazi.

Wanachama hao waliyasema hayo katika kijiji cha Mwamgongo wakati wa kikao cha pamoja baina ya wanachama hao na uongozi wa mfuko wa Bima ya afya(NHIF) Mkoa wa Kigoma.

Nassib Ally mtumishi wa afya katika kituo cha mwamgongo alisema kuwa pamoja na kwamba malipo ya posho na nauli kwasasa ya kwenda kutibiwa nje ya kituo hulipwa na mwajiri lakini malipo hayo hayalipwi kwa wakati.

Alisema kuwa hali hiyo imekuwa ikiwafanya wanachama kuhangaika wanapofuatilia matibabu nje ya vituo vyao vya kazi.

Naye Mussa mwalimu wa shule ya Msingi Nyambusho iliyopo kijijini hapo alisema kuwa aliutaka mfuko kugharamia upimaji wa vinasaba(DNA)pamoja na kugharamia matibabu ya nje ya nchi kwa wananchama wake.

Akijibu juu ya maombi hayo Meneja wa Bima ya afya Mkoa wa Kigoma Elias Odhiambo alisema kuwa kwasasa mfuko wa Bima ya afya haugharamii malipo ya posho na nauli kwa wanachama wake wanaopata rufaa ya matibabu nje ya vituo vyao vya kazi,Alisema suala hilo linabaki kuwa la muajiri.

Odhiambo alisema pia suala la kugharamia matibabu nje ya nchi litabaki suala la Wizara ya afya na huku suala la upimaji wa vinasaba likibaki kuwa la gharama za mtu binafsi.
Meneja wa mfuko wa Bima ya afya (NHIF)Mkoa waKigoma Elias Odhiambo akikabidhi moja ya mashuka 50 kwa uongozi wa Kituo cha afya cha Mwamgongo kilichopo mwambao wa kaskazini mwa Ziwa Tanganyika Wilaya ya Kigoma.
Mkuu wa kituo cha afya Mwamgongo Dkt Swagala akipokea msaada wa mashuka 50 toka kwa meneja wa Bima ya afya(NHIF)Mkoa wa Kigoma Elias Odhiambo.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha mwamgongo waliojitokeza kupima afya zao katika shule ya msingi mwamgongo zoezi lililokuwa likiratibiwa na mfuko wa Bima ya afya(NHIF) Mkoa wa Kigoma.Picha zote na Editha Karlo
Viewing all 109597 articles
Browse latest View live




Latest Images