Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

CHAMA CHA MAPINDUZI UINGEREZA CHAPATA MWENYEKITI MPYA

$
0
0
KAPINGA KANGOMA MWENYEKITI MPYA CCM UK - AIBUKA NA USHINDI WA KISHINDO  WA ASILIMIA 94.6% YA KURA ZOTE HALALI.

Aanza kwa kuunda timu itakayounda upya Jumuiya ya Watanzania UK na kuhusisha wadau wote;Azungumzia suala la uraia pacha na Rais Ajaye katika uchaguzi 2015;Kuunda Saccoss ya watanzania UK na Jumuiya ya Wanawake.Na Abraham Sangiwa Itikadi Siasa na Uenezi - CCM – UNITED KINGDOM.
 Mwenyekiti Mpya wa CCM UK Ndugu Kapinga Kangoma akitoa nasaha na shukrani zake.
 Mwenyekiti Mstaafu wa CCM UK Ndugu Maina Owino akimkabidhi vifaa vya ofisi Mwenyekiti Mpya CCM UK Ndugu Kapinga Kangoma.

 Wajumbe, wanachama wa CCM UK na watanzania waishio uingereza wakimsikiliza Kwa makini Mwenyekiti Mpya wa CCM Ndugu Kapinga Kangoma (hayupo pichani).

 Mwenyekiti Mstaafu Ndugu Maina Owino akipiga kura yake katika Uchaguzi wa Mwenyekiti Mpya wa CCM UK.

Promoter Britts Events Wafunguka juu ya kAshafa nzito ya kuharibu shoo ya Diamond nchini ujerumani

$
0
0
1384142_505866609511143_1668869613_n
Awin Williams Akpomiemie.


MY PEOPLE FIRST OF ALL, I WOULD LIKE TO EXPRESS MY HEART BY TELLING THE GENERAL PUBLIC AND THE FANS OF DIAMOND PLATNUMZ, THAT WE FROM BRITTS EVENTS MANAGEMENT IS VERY SORRY FOR WHAT HAPPENED LAST NIGHT, DURING THE CONCERT OF DIAMOND PLATNUMZ. IT WAS NEVER PLANNED FOR THE CONCERT TO BE DELAYED OR FOR THE ARTIST NOT TO PERFORM. 

HERE I WOULD TELL YOU ALL THE TRUTH OF WHAT REALLY HAPPENED ABOUT THIS EVENT FOR YOU ALL TO KNOW THE TRUTH.

THE PROJECT OF DIAMOND CONCERT WAS A VERY EXPENSIVE PROJECT,
BECAUSE THE BRITTS EVENTS MANAGEMENT WANTED EVERYTHING TO BE PROFESSIONAL, AS A COMPANY WE DECIDED TO LOOK OUT FOR INVESTORS WHO WOULD INVEST IN THIS PROJECT, THEN WE APPROACHED THREE INVESTORS WHO INVESTED BUT ONE OF THEM DID’NT INVEST TOO MUCH AS HE SAID HE WONT BE IN THE COUNTRY.


THE TWO INVESTORS ARE WELL KNOWN PEOPLE LIVING IN STUTTGART
ONE WORK WITH THE USA MILITARY THE SECOND ONE OWNS A SHIPPING COMPANY IN STUTTGART, THESE WERE THE TWO MAJOR INVESTORS THAT WE GOT, WE GAVE THEM A CONTRACT TO SIGN AND ONE OF THEM SIGNED BUT THE SHIPPING GUY REFUSE TO SIGN THE CONTRACT OF THE PROJECT THAT HE WANTS TO HAVE A PRIVATE CONTRACT WITH THE USA GUY, THEN I TOLD MR.USA THAT WAS A WRONG MOVE BUT MR.USA SAID BRITTS DO NOT WORRY,ALL WILL BE FINE, 


MY PEOPLE THE PROJECT STARTED AND THEN THE TWO INVESTORS THEN NOTICE THAT DIAMOND IS A BIG ARTIST AND HE WOULD PULL LOTS OF CROWD AND PEOPLE LOVE HIM, THEN THEY TEAMED UP AGAINST BRITTS WHO INVITED THEM AS INVESTORS ON THIS CONCERT AND WANTED TO TAKE THE PROJECT AWAY FROM BRITTS BECAUSE THEY ARE THE ONE WHO BRINGS PART OF THE MONEY FOR THIS PROJECT WHILE BRITTS IS THE ONE WHO OWNS THE ARTIST AND THE PROJECT,.

JUST BECAUSE BRITTS IS A NEW COMPANY IN STUTTGART MR. SHIPPING GUY DECIDED TO TEAM UP WITH THE USA GUY AND DJ -WANTED, TO TAKE OVER THE PROJECT, WHEN BRITTS SITS DOWN AND HOLD MEETINGS WITH THEM, THEY WOULD DO THEIR OWN MEETING AND THEN,CHANGE ALL THE PLANS BEHIND BRITTS MANAGEMENT, SO THEY WERE OPPRESSING AND PUSHING THE PROJECT BEHIND BRITTS.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

KUMBUKUMBU YA VICTORIA WILBERT NKWABI

$
0
0
Leo ni miaka miwili sasa tokea  Mpendwa wetu VICTORIA,uliposikia sauti ya Mungu  wetu ikikuita nawe ukaitika. Bado tunakukumbuka kwa namna ya pekee kwa Ucheshi, Upendo na Upole.Kwetu kumbukumbu hizi ni hazina zetu.
Victoria unakumbukwa sana na mimi mama yako LYDIA,Baba yako mlezi mpendwa Japheth Mbwana,Mumeo mpenzi Emmanuel Kilato, Ndugu zako Godfrey, Mercy, Viollah, na wengine  wengi sana kama  Mama mkubwa, Wajomba zako, Wakwe zako, wanaukoo wote,Majirani wa Lumala,- Mwanza,Geita,Dodoma, Walimu wako wa Shule, na Chuo UDOM, wafanyakazi wa Benki kuu Mwanza,wanaparokia ya Pasiansi Mwanza,Wanaparokia wa Pasiansi – Mwanza,Wanajumuiya wa Mt.Fidel – Lumala Mwanza,Ndugu jamaa na marafiki hasa Masista wa Poor Clares wa Nyanguingi Mwanza.

MWENYEZI MUNGU AKUANGAZIE MWANGA WA MILELE UPUMZIKE KWA AMANI.AMINA.



Hope FM 98.0 - Iringa's newest and hottest radio station on air!

$
0
0
The University of Iringa in Iringa region has just launched  its radio known as Hope  Fm, covering Iringa and its neighbouring areas on the  98.0 frequency. This radio, that aims at informing, entertaining as well as unite Iringa and her neighbourhood,  is part of the university's broadcasting teaching and learning process for  students and lecturers under the department of journalism. Tune in now!

INTRODUCING IMPERIAL SECONDARY SCHOOL AT MSOLWA, CHALINZE, COAST REGION

$
0
0
Imperial Secondary School is a friendly, co-educational, boarding school that caters for students throughout their secondary education. At Imperial Secondary School we cultivate students’ desires to learn through questions and think critically. Personal excellence is the goal for each student, as they are inspired to achieve at the best level in ways best suited to each individual .
The school has a committed team of teachers who are at best in their chosen fields. The methodology followed to impart education is a good mix of conventional and sophistications utilizing the latest in teaching gadgets and techniques. We put in our best efforts to help students pursue their goals, achieve their dreams and find their niches in society. Our main goal to equip every student not only with the best education, but create in each student a character of high moral standards, who will become in future a responsible citizen of his country.

TASWIRA ZA UFUNGUZI WA MRADI WA NYUMBA ZA MAKAZI ZA MEDELI WA NHC DODOMA

$
0
0
1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma wenye nyumba 150, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Rehema Nchimbi (wa kwanza kushoto) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene. Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Christopher Kangoye. (Picha zote kwa hisani ya Shirika la Nyumba la Taifa)
2
Rais Jakaya Kikwete akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma wengine wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC, Nehemia Mchechu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma wenye nyumba 150, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene. Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Christopher Kangoye.4Majengo ya Nyumba za Makazi za Medeli Mjini Dodoma kama yanavyoonekana pichani.5Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Zakhia Meghji huku Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Christopher Kangoye na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene wakishuhudia wakati wa ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za makazi za Medeli zilizopo Mjini Dodoma. Mradi una jumla ya nyumba 150. (Picha zote kwa hisani ya Shirika la Nyumba la Taifa)6 

ngoma azipendazo ankal

$
0
0
Tabu Ley Rochereau - "Mokolo Nakokufa"

TAARIFA YA MSIBA WA BAHATI MWAKABUNGU

$
0
0
MAREHMU BAHATI MWAKABUNGU ENZI ZA UHAI WAKE

WANAFUNZI AMBAO TUMEPITA CHUO CHA BIASHARA KITUO CHA DAR ES SALAAM (CBE) TUNASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA ALIYEKUWA MWANAFUNZI MWENZETU BAHATI MWAKABUNGU AMBAYE AMEFARIKI JUZI HAPA DAR ES SALAAM.

MSIBA UPO KWA KAKA YAKE NOEL MWAKABUNGU MAENEO YA BUZA JIJINI DAR ES SALAAM, TAARIFA KUTOKA KWA WANA FAMILIA WANASEMA MAZISHI YATAFANYIKA LEO TAREHE 3/09/2014 KATIKA MAKABURI YA KINONDONI MUDA WA ALASIRI.

KWA TAARIFA ZAIDI UNAWEZA KUWASILIANA NA NAMBA HII:

0718277409

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.

USHAURI WA KAMANDA RAS MAKUNJA KWA WASANII KUHUSU SOKO LA MUZIKI ULAYA

$
0
0
WASANII TUSIWE WATU KULAUMIWA KILA WAKATI! BALI KUSHAURIWA,

WASANII LAZIMA WAANGALIE KWA MAKINI MIKATABA NA MUDA KUTUMBUIZA

Baada ya vyombo vya habari kuandikia kwa wingi tukio la fujo zilizotokea wikiendi ya 30.Augost 2014 katika show ya mwanamuziki Diamond, Blog ya jamii na timu ya Michuzi Media  imefanya juhudi za kutaka kusikia maoni na mtazamo wa mwanamuziki wa Tanzania aliyeupigania muziki wa Tanzania katika soko la ughaibuni kwa miaka 21 si mwingine bali ni Kamanda ras Makunja wa FFU
au Ngoma Africa Band.

Michuzi media ilianza kwa swali ?: Ras Makunja nini mtazamo wako  kwa
Yaliyotokea Stuttgart.?

Kamanda Ras Makunja: " Kwanza nianze kwa kuwapa pole wale wote waliopatwa  na usumbufu na maumivu yawe ya mwili,hisia au hali kutokana na tukio lile,kwa kweli tuliposikia tulistuka sana sana" ,Ras Makunja alisema.

Kwa kuwa sisi sote tunajua ugumu wa msanii anapokuwa On Tour hususan ugenini ,kuna taarifa za awali ambazo msanii ni vigumu sana kuzipata,taarifa ambazo ,pengine zinaweza kumsaidia msanii kwa namna moja au nyingine,kwa kweli msanii anapokuwa ugenini ni sawa na usiku wa kiza.Ras Makunja alisisitiza

Tunacho shukuru Mungu pamoja na yote yaliyotokea pale hatukusikia kama kuna mtu aliyepoteza uhai,maana uhai ni zawadi ya Mola kwa viumbe wake.

Wito wangu kwa wadau na washabiki kwa kuwa nyinyi ndio ma-boss zetu,na sisi wasanii au wanamuziki ni watumishi wenu,ningewaomba msichoke kuunga mkono mara mnaposikia msanii au mwanamuziki,au bendi inapiga sehemu fulani,Kwa sababu Chereko Chereko na mwenye mwana.

Fujo zilizotokea pale Stuttgart kila moja kasoma katika vyombo vya habari na nyinyi ndio mahakimu,lakini mimi si msemaji wa upande wowote pale bali kama msanii ningeomba msimuhukumu msanii kwa kosa la mtu mwingine.

MICHUZI MEDIA : Unawashauri nini wanamuziki  wenzako kutoka nyumbani  wanaokuja   kutumbuiza ?

Ras Makunja: Ushauri wangu nimeshausema mara nyingi katika vyombo vya habari kuwa, Wasanii wa nyumbani lazima wanapopata mikataba waipeleke kwa mameneja na mwanasheria ili isomwe na kueleweka kipengele kimoja baada ya kimoja mfano: taratibu za malipo cash au? na muda wa kulipwa kabla au baada ya show: Hotel,Bima ,VAT,Ulinzi na Kingine muhimu ambacho mara nyingi  ndicho chanzo cha mizozo ni malipo na muda wa kutumbuiza hili lazima liwe wazi tena ndani ya mkataba,Mfano show inaanza saa 4 usiku hadi 7.usiku basi lilwe wazi.

Unajua kuna baadhi ya mapromota wanapenda sana kutufanya wasanii kuwa mashine, mara nyingi wanavunja utaratibu "anakuweka hoteli na yeye anasubiri watu wajae ukumbini au wanunue vinywaji kwanza ,sasa 
watu wakishalewa unategemea nini? ni fujo tu lakini kama mkataba unaeleza time ya kutumbuiza na mwisho wa show,ata kama kuna watu wawili msanii anatumbuiza.

"WASANII WA AFRIKA MASHARIKI WAPENDWA SANA ULAYA"
Ras Makunja alisema baada miaka 21 ya kupigania soko na moyo wa wadau na washabiki wa sanaa za Afrika Mashariki sasa sanaa zetu zimeshika soko na baadhi ya wasiopenda maendeleo wanatutazama kwa macho ya makengeza ! 

Wasanii lazima tuangalie sana sana nani wa kufanya nae kazi,katika music Industry kuna baadhi ya watu wanamfanya msanii ni kipande cha ndimu "anakamua na kutupa ganda" 

Msanii anapata tabu kujenga jina kwa miaka,eti promota anataka kulibomoa kwa dakika usipokubaliana na yake,lazima wasanii wajichunge sana.

Wasanii wa Afrika Mashariki tunawapa wakati mgumu wapinzani wetu,na wapinzani wetu wanajua vema kuwa pia sisi ni wakarimu hapo ndipo wanapojaribu kutumaliza na ukarimu wetu.

Nawashauri wasanii wezangu wale wanaokuja ujerumani,kabla hujasafiri jaribu kuwasiliana na umoja wa waTanzania Ujerumani(UTU) email yao hii kamati.utu@googlemail.com ili upate information muhimu,hakuna
atakaye kuingilia katika biashara au mkataba wako lakini ushauri ni muhimu.

Pia lazima tujijue kuwa kwa sasa tunatishia soko na tayali lipo mikononi mwetu kwa maana hii wapinzani wanajaribu kujifanya wao ndio mapromota lazima tujipange na kutambua nani wa kufanya nae kazi na kwa makubaliano yepi.

Habari za uhakika tunazo kuwa mwaka 2015 wasanii wa Afrika Mashariki ndio wanaotakiwa kwa wingi hapa ughaibuni,tumieni nafasi hiyo.

KARIBUNI SANA KATIKA SOKO LA UGHAIBUNI NA MKIPATA NAFASI ZA
KUTUMBUIZA LAZIMA MKAMUE BILA YA HURUMA.
Asanteni, pia nawashukuru sana Michuzi Media kwa kunipa nafasi.

Kishapu bila Maafa ya Ukame inawezekana - Mutagurwa

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Bi.Jane Mutagurwa akiwasisitiza Wataalam katika Sekta ya Kilimo, Mifugo, Afya, Elimu na Utawala wa kata ya Mwamalasa, Masanga na Langana Wilayani Kishapu wakati akifungua mafunzo ya jinsi ya kutekeleza Mradi Wa Kuijengea Jamii Uwezo wa kupunguza Athari Za Maafa katika kata zao, mafunzo hayo yanaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa Maafa kwa Tarehe 1-5 Septemba, 2014. (Kulia) ni Mratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Harison Chinyuka (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Bi.Jane Mutagurwa amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu inaweza kupunguza athari za maafa ya ukame ikiwa Wataalam katika Sekta ya Kilimo, Mifugo, Afya, Elimu na Utawala wa kata ya Mwamalasa, Masanga na Langana Wilayani Kishapu watashirikishwa katika Kuijengea Jamii Uwezo wa kupunguza Athari Za Maafa katika kata zao.

Akiongea wakati akifungua mafunzo ya kuijengea uwezo jamii wa kuzuia, kupunguza na kukabiliana na maafa yanayotokana na ukame kwa Wataalam waliopo katika Ngazi ya Kata yanayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa Maafa kwa Tarehe 1-5 Septemba, 2014, wilayani Kishapu, Mutagurwa alibainisha kuwa kupitia mafunzo hayo wataweza kuvieimisha vikundi vya kata zao husika juu ya kuzuia, kupunguza na kukabiliana na maafa yanayotokana na ukame.

“Katika mafunzo haya nimeambiwa mtafundishwa matumizi ya Taarifa za Hali ya Hewa, Dhana ya Maafa ikiwa ni pamoja na Sera na sheria ya maafa, namna ya kubainisha viashiria vya upungufu wa chakula, tathmini ya upungufu wa chakula pia na mwongozo wa ugawaji wa chakula cha msaada. Napenda niwasihi tumieni fursa hii ya mafunzo haya vizuri ili muweze kuwaelimisha wananchi wa Wilaya yetu namna bora ya kupunguza na kukabiliana na maafa yanayotokana na ukame nami naahidi nitafuatilia kuona jinsi mnavyo elimisha wananchi katika kata zenu” alisisitiza Mutagurwa.

Mutagurwa alifafanua kuwa Kishapu bila athari zitokanazo na maafa ya ukame inawezekana ikiwa wataalam wa ngazi ya kata watashirikishwa kwa kuwa wao ndio wanao uwezo mkubwa kwa ngazi ya kata wa kutambua viashiria na vihatarishi vinavyoweza kusababisha maafa na hatimaye kutoa ushauri sahihi kwa wananchi wa kupunguza na kukabiliana na maafa yanayotokana na ukame.

“Kwa mfano Maafisa Ugani kwa utaalam wao kutokana na mvua kutonyesha mara kwa mara katika wilaya yetu, kupitia mafunzo haya wataelewa matumizi ya Taarifa za Hali ya Hewa ili waweza kuwashauri wakulima matumizi ya mbegu na pembejeo za kilimo kwa kipindi muafaka cha kulima mazao yanayostahimili ukame, na hatimaye kuepukana athari ya ukame ambayo ni wilaya yetu kuwa na upungufu mkubwa wa chakula” alisema Mutagurwa.

Aliongeza kuwa waratibu wa Elimu katika kata na Watendaji wa Kata hawana budi kuhimiza upandaji wa miti katika kata zao, kwakuwa miti ikipandwa kwa wingi wilayani humo inaweza kukabiliana vyema na athari za mabadiliko ya Tabia Nchi ikiwemo ukame.

Awali akimkaribisha Mkurugenzi huyo, Mratibu wa mafunzo hayo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu Maafa, Bw.Harison Chinyuka alibainisha kuwa mafunzo hayo ni sehem ya utekelezaji wa Mradi Wa Kuijengea Jamii Uwezo Wa Kupunguza Athari Za Maafa Kwa Mikoa Iliyoathirika Zaidi Na Ukame ambao unafadhiliwa na Benki ya Dunia na kusimamiwa na UNICEF chini ya Uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Halmashauri husika wakiwa Watendaji Wakuu wa Mradi huo. Mradi huo unatekelezwa kwa kipindi cha miezi 18 uliozinduliwa Wilayani Same, mkoani Kilimanjaro tarehe 11 Desemba2013.

MAWAKALA WA MAKOMANDOO WA NEPAL WALIOTUA NCHINI KINYEMELA NA KUJIFANYA 'WALINZI' WAPANDISHWA KORTINI

$
0
0
MKURUGENZI wa Kampuni ya Ulinzi ya Advanced Limited, Juma Ntinginya (47) na wenzake wawili, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kuwahifadhi raia wa Nepal.

 Washtakiwa hao walipanda kizimbani jana mbele ya Hakimu Mkazi, Devotha Kisoka na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali kutoka Idara ya Uhamiaji, Patrick Ngayomela.

Ngayomela alidai washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja uendeshaji wa kampuni hiyo, Henry Mwakipunda (34) na dereva Hamza Sefu (30).

Akiwasomea mashtaka yao, Ngayomela alidai kuwa Agosti 29 mwaka huu, maeneo ya Kijitonyama, wilayani Kinondoni, kinyume na sheria, washtakiwa waliwahifadhi raia wa Nepal huku wakijua kufanya hivyo ni kosa.

Washtakiwa wote walikiri kutenda makosa hayo na kwamba waliwaingiza raia hao kwa nia ya kufanya kazi katika kampuni yao.

Inadaiwa viza walizokuwa nazo zilikuwa kwa ajili ya kutembea nchini na si kufanya kazi.

Hakimu Kisoka aliwahukumu washtakiwa kwenda jela mwaka mmoja au kulipa faini ya Sh 100,000 kila mmoja. Wote walilipa faini na kuachiwa huru.

Wakati huo huo, mshtakiwa Halit Gurbuz (33) ambaye ni raia wa Uturuki, alipandishwa kizimbani katika mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Emilius Mchauru, kwa makosa mawili ya kuishi nchini na kufanya kazi bila kibali.

Ngayomela akimsomea mashtaka, alidai Agosti 30 mwaka huu maeneo ya Mikocheni, mshtakiwa akiwa raia wa Uturuki, alikutwa akiishi nchini bila kibali.

Katika shtaka la pili, anadaiwa huku akijua hana kibali cha kuishi nchini, alikuwa anafanya kazi Kampuni ya Techno Plus bila kibali cha kumruhusu kufanya hivyo.

Mshtakiwa alikiri kosa na Hakimu Mchauru aliahirisha kesi hiyo hadi leo kwa ajili ya kumsomea hukumu. Hata hivyo, mshtakiwa alikwenda mahabusu Keko.
Komandoo Sidhee Bahadurkatuwal (kulia) kutoka Nepal akionesha nyumba ya Mrwanda aliyokuwa akiilinda kupitia kampuni ya Ulinzi ya Advanced Security karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, akiwa na makomandoo wenzake kutoka Nepal.

Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim ashiriki Fistula Ice Bucket Challenge

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim Tanzania, Bw. Yogesh Manek akishiriki zoezi la Ice Bucket Challenge kuunga mkono kampeni dhidi ya ugonjwa wa fistula nchini Tanzania, baada ya kuteuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, Sunil Colaso. Tukio hilo lilifanyika katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim Tanzania, Bw. Yogesh Manek akizungumza na waandishi kabla kushiriki zoezi la Ice Bucket Challenge kuunga mkono kampeni dhidi ya ugonjwa wa fistula nchini Tanzania, baada ya kuteuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, Sunil Colaso. Tukio hilo lilifanyika katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 
========  ====== =========

Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim Tanzania, Bw. Yogesh Manek ameshiriki katika Ice Bucket Challenge, kuunga mkono kampeni dhidi ya ugonjwa wa fistula nchini Tanzania, baada ya kuteuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, Sunil Colaso.

Kabla ya kumwagiwa maji yenye barafu Bw. Manek aliwateua, Ali Mafuruki Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Infotech Investment Group, Shabir Abji, Mwenyekiti wa Hotel ya New Africa na Veena Jog, Mkurugenzi Mtendaji wa Advent Constructions Ltd kushiriki katika zoezi hilo ikiwa ni jitihada za kuwaokoa wanawake wakitanzania wenye tatizo la ugonjwa huo wa fistula.

Akizungumza kabla ya kushiriki, Jumapili, Bw. Yogesh Manek alisema amehamasika kukubali shindano hilo kutokana na idadi kubwa ya maisha inayopotea na ulemavu unaosababishwa na ugonjwa huo: pamoja na zoezi hilo kunakshiwa na mpango wa utunzanji mazingira wa benki hiyo ujulikanao kama ‘Exim Go Green’ Maji kwa matumizi mazuri.

“Namshukuru Bw. Sunil Colaso, Mkurugenzi wa Airtel Tanzania, kwa kunichagua kufanya zoezi hili ambalo nimelipokea kwa heshima kubwa sababu nafahamu urishiriki wangu utaukoa maisha ya walio wengi na kusaidia Tanzania kuwa huru dhidi ya fistula. Kwa mujibu wa takwimu zilizopo zaidi ya wanawake 8000 ufariki kutokana na fistula, 160,000 upata ulemavu na zaidi ya watoto 40,000 wa chini ya mwaka mmoja ufariki kutokana na ugonjwa huu unaotibika,” alisema.

Alibainisha kuwa Benki ya Exim, imekuwa ni katika mstari wa mbele kuunga mkono shughuli mbali mbali zenye manufaa kwa wanawake, ndiyo maana kampeni ya fistula imekuja kwa wakati muafaka.

“Benki ya Exim imekuwa ikiunga mkono miradi mbali mbali ya kimaendeleo ya kijamii, hususani katika sekta za afya, mazingira na elimu.

“Hii imethibitishwa na baadhi ya shughuli za kijamii tulizofanya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na kuchangia magodoro katika hospitali ya Mwananyamala, kuijengea shule ya msingi Kilakala vyoo na kushiriki kikamirifu katika shughuli za usafi wa mazingira nchi nzima, ili kuwa na mazingira safi. 

“Na leo hii, ninashiriki katika Ice Bucket Challenge kuonyesha jitihada zetu kama benki katika kuendelea kuunga mkono shughuli hizo,” alisema Bw. Manek. Alisema kuwa wafanyakazi wote wa Benki ya Exim wameunga mkono zoezi hili la Ice Bucket Challenge ambalo limeanzishwa kwa lengo zuri.
“Tunafuraha kubwa na kiwango cha huruma, ukarimu na hisia zilizoonyeshwa na wafanyakazi wote, wao pia wakishiriki katika zoezi hili muhimu kikamirifu," alisema Bw Manek.
Bw. Manek alibainisha pia, zoezi hilo pia limelenga katika kukuza ushiriki wa wafanyakazi na watu wengine katika shughuli za kijamii ambazo benki imekuwa ikianzisha mara kwa mara ikiwa na lengo la kusaidia kukuza sekta mbali mbali za kiuchumi na kijamii nchini.

Benki ya Exim ni moja kati ya benki kubwa nchini kwa upande wa mali zake za jumla, na kuwa na matawi 32 nchi nzima ikisambaa katika uchumi wa nchi tatu Afrika.  

YOUNG AFRICANS NA BENKI YA CRDB WAINGIA MAKUBALIANO YA UTENGENEZAJI WA KADI ZA KISASA ZA UANACHAMA

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei (kulia) akisaini mkataba na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Klabu ya Yanga, Fatma Karume kwa ajili ya kutengeneza kadi za kisasa za uanachama wa klabu hiyo za mfumo wa kieletroniki 'Gold Premium Card'. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa klabu ya Yanga, Mama Fatma Karume akipitia mkataba walioingia na Benki ya CRDB. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akionyesha kadi ya kisasa ya uanachama wa Yanga ikiwa katika mfumo wa kieletroniki kabla ya kumkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa klabu hiyo, mama Fatma Karume.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei (kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga,  Fatma Karume kadi namba moja ya mfumo wa kieletroniki 'Gold Premium Card' mara baada ya benki hiyo kuingia mkataba wa kutengeneza kadi hizo. Hafla hiyo ilifanyika Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam. 
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

HUC YATANGAZA UFADHILI WA MASOMO YA UFUNDI VETA, VIJANA CHANGAMKIENI

$
0
0
Na Nathan Mpangala wa HUC.

Shirika lisilo la kiserikali la Help for Underserved Communities Inc. (HUC), linatangaza nafasi za ufadhili wa masomo ya ufundi VETA kwa vijana wa Kitanzania. Kozi hizo ni ufundi wa magari, umeme wa magari, udereva magari/pikipiki, ufundi cherehani, hair dressing (urembo), mapambo ya ukumbi na nyinginezo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika hilo, inasema, HUC, itafadhili wanafunzi 15 wa kozi mbalimbali za awali VETA kwa mwaka 2014-2015.

Walengwa ni vijana wa kike na kiume waliomaliza shule za msingi ambao wamethibitika kuwa wazazi/walezi wao wameshindwa kuwalipia ada. Imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa, mwanafunzi atatakiwa kujaza kwa usahihi fomu ya maombi (imeambatanishwa hapa), akiambatanisha na barua akieleza sababu za kuomba ufadhili huu na barua ya utambulisho toka ofisi ya serikali za mitaa na mwisho wa kupokea barua za maombi ni Jumatano, Oktoba 01, 2014, saa 11 jioni.

Barua za maombi zitumwe kupitia:

Maombi ya ufadhili wa masomo,
Help for Underserved Communities Inc.
P. O. Box 7022,
Dar es Salaam,
Tanzania.

Au

Help for Underserved Communities Inc.
P.O.Box 6822,
Ellicott City, MD 21042 

Au

Kupitia baruapepe:
info@myhuc.org OR kijasti@hotmail.com

fomu ya kujiunga

Taarifa hiyo imesema, majina ya watakaopata ufadhili yatatangazwa Oktoba 10, 2014 na kwamba ada italipwa moja kwa moja chuoni.

HUC ni shirika lisilo la kiserikali toka nchini Marekani lenye lengo la kuziwezesha jamii zipatazo huduma hafifu kupata maji safi na salama, vifaa vya elimu na ufadhili wa masomo ya ufundi. Mwaka jana, shirika hili lilifadhili vijana 11 VETA.

Wamiliki, Waombaji leseni za madini watakiwa kufuata Taratibu

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisaini moja ya leseni za uchimbaji madini kwa wamiliki waliokidhi vigezo vya kuapatiwa leseni. Anayeangalia ni Mwanasheria Wizara ya Nishati na MadinI Phines Sijaona.

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akimsikiliza mmoja wa waombaji wa Leseni za uchimbaji madini, Mark Stanely mmiliki wa kampuni ya Bafex Tanzania Limited (Kanda ya Kusini Magharibi) wakati wa kikao cha kusaini leseni za uchimbaji madini zilizokidhi vigezo

Kamishna Msaidizi anayeshuhgulia Leseni, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi John Nayopa, akifafanua jambo wa wamiliki wa kampuni ya Gemini Exploration & Mining Service Limited mara baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo kumaliza kusaini leseni hizo.




MICHEZO YA SHIMIWI SASA KUFANYIKA MKOANI MOROGORO KUANZIA SEPTEMBA 27 MPAKA OKTOBA 11

MABOSS WA AIRTEL TANZANIA WAENDELEZA MAPAMBANO DHIDI YA FISTULA

$
0
0
Wakuu wa makampuni tofauti pamoja na wakurugenzi wa vitengo mbali mbali vya kampuni ya Airtel Tanzania wameendelea kuonyesha kuguswa kwa kushiriki kutimiza shinikizo toka kwa Mkurugenzi mkuu wa Artel Tanzania alilolitoa wiki moja iliyopita kuhamasisha mapambano dhidi ya Fistula kwa akina mama kwa kuchangisha pesa zitakazotumika kusaidia shughuli mbalimbali wakati wa matibabu kwa wale waliopatwa na tatizo hilo Angalia video hizi kuona kila mmoja alivyofanya mara baada ya kuguswa na kujitoa kuchangia.Adriana Lyamba- Mkurugenzi Huduma kwa wateja Airtel Tanzania. Levi Nyakundi- Mkurugenzi Masoko Airtel Tanzania.

The Journey of 10 BG Tanzania Scholars who will join University of Aberdeen and Robert Gordon University in UK to pursue their MSc Degree studies in Oil and Gas

$
0
0
The British Council Tanzania started the journey of BG Tanzania scholarship on February 2014 with promotion and awareness creation to the Universities in different regions in Tanzania, receiving applications and selection of 10 scholars followed by scholarship awarding to 10 scholars.

The British Council conducted a pre-departure briefing on 15 August, 2014 as part of preparation for their studies in UK to 10 BG Tanzania Scholars who won the award to study Master’s degree in oil and gas in UK for the 2014/15 Academic Year.

On 27 August, 2014 the BG Tanzania organized a special lunch and press conference to 10 BG Tanzania Scholars who will depart in early September 2014 to commence their Master’s studies in Oil and Gas for engineering and geology studies at 2 universities in the UK: University of Aberdeen and Robert Gordon University The British Council and BG Tanzania hosted a Farewell Reception to 10 BG Tanzania Scholars on 28th August 2014 The one year BG Tanzania scholarships will cover the cost of tuition fees, books, thesis, study field trip, accommodation and return flight.

The BG Scholars were selected on the basis of academic merit from a field of geo- science and engineering who received admission from the two (2) UK Universities namely University of Aberdeen and Robert Gordon University.

Eight (8) of the Scholars are men and two (2) are women, and virtually all intend to obtain a Master’s of Science Degree majoring in Geo-science and Engineering for Oil and Gas industry.

The scheme is funded by BG Tanzania and administered by the British Council, Tanzania. It offers Tanzanian graduates the opportunity to pursue postgraduate education at universities in the UK with focus on specific geoscience and engineering courses that are particularly relevant for Tanzania’s emerging natural gas and related sectors.

Since its first award in 2012, the BG Tanzania has bestowed 4 scholarships for the two academic years: 2012/13 and 2013/14. As a long-term commitment to promote science in Tanzania, The BG Tanzania plans to award twenty (20) more postgraduate scholarships in Oil and Gas for the 2015–2016 and 2016 - 2017 academic years.

Launch of Big Brother Hotshots postponed

Mahakama Yamfunga Jela Mwizi wa Nyaya za TTCL

$
0
0
Mmoja wa watuhumiwa wa nyaya za simu. Picha hii haina uhusiano na habari hii.  
Mmoja wa watuhumiwa wa nyaya za simu. Picha hii haina uhusiano na habari hii. [/caption] Na Mwandishi Wetu MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu ya jijini Dar es Salaam imemuhukumu kwenda jela miaka minne, Shaibu Muhidin Ndina baada ya kupatikana na kosa la kuiba nyaya za Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Hukumu hiyo imetolewa Agosti 25, 2014 katika mahakama hiyo na B. Mashabara baada ya mshtakiwa kutiwa hatiani kwa kosa hilo la wizi wa nyaya(cables) za kampuni ya TTCL zenye thamani ya shilingi milioni 15. 

Awali akisomewa shitaka hilo, Muhidin Ndina anadaiwa kutenda kosa hilo Januari 11, 2013 maeneo ya Boko Katika Wilaya ya Kinondoni kabla ya kufikishwa mahakamani na kufunguliwa kesi namba 12/2013. “…Aliiba nyaya (cables) za thamani ya milioni 15…alitenda kosa hilo Januari 11, 2013 Boko Katika eneo la Kinondoni, jijini Dar es Salaam…” ilisomeka sehemu ya hukumu ya kesi hiyo.

 Uharibifu wa miundombinu ya umma zikiwemo nyaya za simu za Kampuni ya TTCL umekuwa ukishamiri maeneo kadhaa jambo ambalo limekuwa likisababisha hasara kubwa kwa kampuni na usu mbufu kwa wananchi na watumiaji wa huduma za TTCL. *Imeandaliwa na www.thehabari.com
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live


Latest Images