Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

Mafundisho: Matumizi sahihi ya Facebook kwa Wafanyabiashara

$
0
0
Katika dunia ya leo, kama wewe ni mfanyabiashara basi hauwezi epuka ushawishi wa mitandao jamii. Ingawa wengi wetu tumekuwa tukiitumia mitandao jamaa kwa ajili ya mawasiliano pekee, ila kuna mengi yanaweza kufanyika na kusaidia kukuza ufannisi wa biashara yako.
Kwa kulitambua hilo, Dudumizi Technologies LTD inakuletea mafunzo juu ya njia na namna sahihi za kutumia Facebook kukuza na kuboresha Biashara.

Mafunzo haya yatakuwa ya wiki mbili, bila kukuchosha (tukitambua muda ni kitu muhimu kwa mjasiriamali), tutakutumia dondoo (kwa email fupi) iliyojikita moja kwa moja kwenye utendaji. Hivyo, kila siku utapokea email moja inayokufundisha jinsi ya kutekeleza hatua husika. Mwisho wa siku, utakuwa umejijngea uwezo mkubwa wa kutumia Facebook kwa ajili ya biashara yako.

 Pia, washiriki wote watapata nafasi ya kuuliza maswali kwa email kwenda kwa wataalamu wetu kwa muda wote wa mafunzo bila gharama yoyote. Pia washiriki watajumuishwa kwenye muendelezo wa mafunzo ya matumizi mbalimbali IT kwenye biashara kwa Video.

Walengwa: Wamiliki wa biashara wadogo na wa kati
Gharama: Bure, unachotakiwa ni kujiunga tu na fomu ya mlisho wa email chini
Muda wa mafunzo:  July 21 - Agosti 5
Muda wa mwisho kujiunga: July 20
Idadi ya Washiriki: 100
Lugha: Kiswahili
Muandaaji: Dudumizi Technologies LTD

Fomu ya Kujiunga bofya Hapa


KITABU CHA KWANZA KINACHOELEZA KWA KINA HISTORIA YA KLABU YA SIMBA TANGU 1920 HADI SASA

$
0
0
                                                 Mwina Kaduguda

Balozi wa Tanzania Nchini Urusi Lt.Gen Wynjones Mathew Kisamba amuaga Rais wa Zanzibar Dkt Shein

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi  wa Tanzania Nchini  Urusi  Lt.Gen Wynjones Mathew Kisamba alipofika kumuaga Rais leo Ikulu Mjini Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na  Balozi  wa Tanzania Nchini  Urusi  Lt.Gen Wynjones Mathew Kisamba alipofika kumuaga Rais Ikulu Mjini Zanzibar
Picha na Ramadhan Othman,Ikulu. 

MTOTO WA RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI AJUMUIKA NA WADAU WA BENKI YA FNB KUPATA IFTARI YA PAMOJA JIJINI DAR

$
0
0
Pichani kulia ni Mgeni rasmi,Mtoto wa Rais Mstaafu awamu ya pili,Mh,Ali Hassan Mwinyi,Abdallah Ali Hassan Mwinyi kwenye hafla ya Iftari ilioandaliwa na benki ya FNB,na kufanyika kwenye bustani ya Serena Hotel jijini Dar hapo jana,anaefuatia kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa benki ya FNB,Ndugu Dave Aitken akiwa na baadhi ya wageni waalikwa wengine.
Mgeni rasmi Abdallah Ali Hassan Mwinyi sambamba na Mkurugenzi Mkuu wa benki ya FNB,Ndugu Dave Aitken wakijumuika pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakiwa pia na baadhi ya wateja wa FNB benki waliolikwa kwenye hafla ya Iftari, ilioandaliwa na benki hiyo jana jioni katika bustani ya Serena Hotel jijini Dar hapo jana. 
Pichani kulia ni Mgeni rasmi,Mtoto wa Rais Mstaafu awamu ya pili,Mh.Ali Hassan Mwinyi,Bwa. Abdallah Ali Hassan Mwinyi akiongoza wageni waalikwa kupata Iftari ya pamoja ilioandaliwa na benki ya FNB,kwenye bustani ya Serena Hotel jijini Dar hapo jana.

 Baadhi ya Wadau wa benki ya FNB wakiwa kwenye hafla ya Iftari
Baadhi ya wadau wa FNB Benki wakijadiliana jambo huku wakipata Iftari iliyoandaliwa na benki hiyo maalum kwa wateja wao katika bustani ya Serena hotel jijini  Dar hapo jana.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS KIKWETE AKUTANA NA WASANII KUTOKA MAREKANI

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wasanii nyota wa filamu na muziki kutoka Marekani walioko nchini kwa ziara ya kutoa mafunzo kwa wasanii wa Tanzania. Wasanii hao ni na Terrence J. Jenkins, mwendeshaji wa kipindi cha muziki kwenye televisheni ya E! Entertainment (wa pili kulia) Chaka Zulu, Mtendaji wa Shughuli za Muziki kutoka Kampuni ya Disturbing The Peace Records (wa pili kushoto) na Davis Banner, mwigizaji, mwanamuziki, mtunzi na msimamizi wa shughuli za muziki ambaye amepata kushinda tuzo maarufu ya Grammy.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitumia simu yake ya mkononi kuwaonesha vivutio vya kitalii wasanii nyota wa muziki na filamu wa Kimarekani walioko nchini kwa ziara ya kutoa mafunzo kwa wasanii wa Tanzania. Wasanii hao ni Terrence J. (Jenkins), mwendeshaji wa kipindi cha muziki kwenye televisheni ya E! Entertainment, mwigizaji wa filamu na mtunzi wa vitabu na Revi Shelton, Mtendaji wa Shughuli za Muziki katika Kampuni ya Outlet Media Group. Wengine ni Chaka Zulu, Mtendaji wa Shughuli za Muziki kutoka Kampuni ya Disturbing The Peace Records na Davis Banner, mwigizaji, mwanamuziki, mtunzi na msimamizi wa shughuli za muziki ambaye amepata kushinda tuzo maarufu ya Grammy.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibadilishana mawazo na wasanii nyota wa muziki na filamu kutoka Marekani walioko nchini kwa ziara ya kutoa mafunzo kwa wasanii wa Tanzania. Wasanii hao ni Terrence J. (Jenkins), mwendeshaji wa kipindi cha muziki kwenye televisheni ya E! Entertainment, mwigizaji wa filamu na mtunzi wa vitabu na Revi Shelton, Mtendaji wa Shughuli za Muziki katika Kampuni ya Outlet Media Group. Wengine ni Chaka Zulu, Mtendaji wa Shughuli za Muziki kutoka Kampuni ya Disturbing The Peace Records na Davis Banner, mwigizaji, mwanamuziki, mtunzi na msimamizi wa shughuli za muziki ambaye amepata kushinda tuzo maarufu ya Grammy.PICHA NA IKULU.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na wasanii hao.

I SHOT BI KIDUDE - PREVIEW of work in progress - Friday July 19th - Durban International Film Festival

$
0
0
Bi Kidude during her lifetime. Picture taken by Muhidin Issa Michuzi.
More coverage of Bi Kidude by this blog CLICK HERE
Award-winning UK film-maker Andy Jones will enter the final leg of a decade long journey when he brings a preview of his latest film to Durban International Film Festival in South Africa on 19th July.
 ‘I Shot Bi Kidude’ recounts the dramatic final months in the life of the world’s oldest singer, Zanzibar’s Bi Kidude who died last year at a reported age of 102. 
The film is yet to be completed, but this hasn’t deterred the programmers in Durban who invited Andy to screen a version as soon as they heard that the film was being made. 
 “Bi Kidude played in Durban, and it is fantastic to share the new film with people in a city with such a strong connection to her, and to Zanzibar,” says Andy. 
 ‘I Shot Bi Kidude’ tells the tale of Andy’s friendship with the legendary singer, from their first encounter in 2002 up to her funeral in April 2013.
 His acclaimed first film ‘As Old As My Tongue’, won numerous awards and is regarded as the seminal work about this extraordinary performer.
 “When I heard rumours that Bi Kidude had been kidnapped, I thought ‘somebody should make a film about that!’ And then I realised that I had all the archive, so it might as well be me! We’d stayed in touch, but I hadn’t seen her for about three years,” says Andy, who persuaded South African cinematographer Natalie Haarahoff to join him as they captured Bi Kidude’s final moments.
 “She was always someone around whom stories grew, and her final years were no less extraordinary. She was even kidnapped and taken away from the music which fuelled her life.” When Andy heard that Bi Kidude had died he knew he just had to be at her funeral, due to take place the following day. Dropping everything, he travelled to Zanzibar, arriving in the nick of time to film the extraordinary scenes as the whole island came to a halt to honour this amazing woman. 
“This film is my account of that day and what happened in the months beforehand. It completes Bi Kidude’s story. I’ve spent a lot of time thinking about whether to make this film, but there are some myths which need to be set straight. Bi Kidude was a larger than life character and this film is for everyone who knows the value of true friendship and believes in the power of music.” 
‘I Shot Bi Kidude’ (work in progress preview) screens with Andy Jones in attendance. 
19 July at 17:00 Elangeni Hotel.
 22 July at 10:00 Luthuli Museum;
 22 July at 17:30 Suncoast 6;
 For more information or to arrange an interview please contact: 
 Andy Jones on +44 7960 393785:
 andy@radiofilm.co.uk

Msaada tutani: mtoto aibwa changanyikeni leo, ataemuona atoe taarifa polisi

$
0
0
MTOTO KAIBIWA CHANGANYIKENI LEO ANAITWA MARLYN.
ATAKAEMUONA NNAOMBA ATUSAIDIE KUTOA TAARIFA KITUO CHOCHOTE CHA POLICE. AMEIBIWA NA MKAKA KANYOA PANK. 
Please upatapo ujumbe huu mfowardie na mwenzako

Vijana wa Kiislam Wilayani Kilwa washiriki Mashindano ya Kusoma Quraan

$
0
0
Na Abdulaziz Video,Lindi.

Viongozi wa Dini wilayani Kilwa mkoani Lindi wametakiwa kuhubiri Amani,umoja na mshikamano wanapokuwapo kwenye ibada zao ili kuliombea Taifa lisiingie kwenye vurugu zinazoweza kusababisha uvunjivu wa amani ya nchi Hususan katika mchakato wa katiba mpya

Akihutubia waislam walioshiriki katika shindano la kila mwaka la Usomaji wa Quran,Mkuu wa wilaya ya kilwa,Abdallah Ulega ameeleza kuwa viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika Kuelimisha na kukemea waumini wao kufanya mambo ambayo yanaweza kusababisha kuleta madhara ya kuwagawa watanzania.

Aidha alibainisha kuwa nchi yetu kwa sasa iko katika kipindi cha mpito cha kutafuta katiba ambapo alitumia nafasi hiyo kutoa wito kwa waislam kukemea tabia za Rushwa,wizi,zinaa,Uharibifu wa Mazingira na inawezekana ikiwa Quran itasomwa na kuhifadhiwa kuzingatiwa Ipasavyo "Hakika nyie ni mashuhuda Mwezi huu wa Ramadhan hali ni ya Utulivu sana katika mji wetu hakuna Disco,Rusha Roho pamoja na mikusanyiko katika mabar Tena Hata kimavazi watu wanavaa mavazi ya Heshima hali imekuwa ya Amani sana Naomba waislamu wenzagu msiache Tumche Mola wetu"Alimalizia Ulega.

Kwa upande wake kaimu Shekhe mkuu wa wilaya za Kilwa,Sheikh Muhidin Matuta alisema kuwa ni wajibu wa waislamu kujenga upendo baina yao na pamoja na kufundisha maadili kwa watoto ili wawe viongozi bora wa baadaye.

Aidha Sheikh Muhidin alieleza kuwa shindano hilo linaloratibiwa na kamati ya kusimamia Mashindano ya Quran Kilwa(QUROU)licha ya usimamizi huo tayari inamiliki Ardhi ambayo imekusudiwa kujengwa kwa shule itakayowalea na kuwasomesha Mahafidh wa Quran na viozi jana wengine waweze kuwa miongoni mwa Jamii na Viongozi bora wa Taifa.

"Waislamu wenzangu tupo katika mfungo wa Ramadhan,Mwezi ambao utukufu wake kila mmoja anaujua na jitahada zinafanywa na masheikh na waalimu wa Dini kukumbusha na kuelimisha Faida zinazopatikana katika Mwezi huu hivyo usiaharibu wema wote kwa kufurahia sikukuu ya IDD"Alimalizia kaimu Sheikh wa Wilaya ya Kilwa

Katika shindano hilo Khadija Kaudunde aliibuka na ushindi katika usomaji wa Juzuu 1,Mariam Suleiyman alishindika usomaji wa juzuu 3,Shaweji Mwichande Juzuu 5,Amir Hassan Mkwachu Juzuu 10 huku Abdallah Yusuf Kombo akifanikiwa katika usomaji wa Juzuu 30 Zawadi mbalimbali zilitolewa kwa washindi ikiwemo magodoro,Cherehani,Radio,Baiskeli kwa washindi na walimu wao pamoja na Pesa Taslimu

kikao cha 98 cha watayarishaji wa vipindi vya elimu kwa umma kupitia TBC chafanyika Mkoani Morogoro

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 98 wa watayarishaji wa vipindi vya elimu kwa umma kupitia shirika la utangazaji Tanzania (TBC) mkoani Morogoro iliyoanza julai 14 hadi 23 mwaka huu mkoani Morogoro, mkutano huo unafadhiliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF. kutoka kulia ni Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa pensheni wa PSPF, Adam Maingu na (katikati) ni Mkurugenzi wa uendeshaji wa mfuko huo wa PSPF, Neema Muro. mkutano huo unafadhiliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF. kutoka kulia ni na (katikati) ni Mkurugenzi wa uendeshaji wa mfuko huo wa PSPF, Neema Muro.
Mkurugenzi wa shirika la habari Tanzania (TBC) Clement Mshana akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 98 wa watayarishaji wa vipindi vya elimu kwa umma kupitia shirika la utangazaji Tanzania (TBC) mkoani Morogoro iliyoanza julai 14 hadi 23 mwaka huu mkoani Morogoro, Mkutano huo umefadhiliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF.
Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa pensheni wa PSPF, Adam Mayingu akizungumza na watayarishaji wa vipindi vya elimu kwa umma kupitia shirika la utangazaji Tanzania (TBC) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 98 wa mkoani Morogoro ulioanza julai 14 hadi 23 mwaka huu mkoani Morogoro, Mkutano huo umedhaminiwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera akijaza fomu ya kujiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF baada ya kufungua mkutano wa 98 wa watayarishaji wa vipindi vya elimu kwa umma kupitia shirika la utangazaji Tanzania (TBC) ambao ulidhaminiwa na Mfuko wa Pensheni wa Pensheni PSPF mkoani Morogoro ulioanza julai 14 hadi 23 huku akishuhudiwa na Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa pensheni wa PSPF, Adam Maingu kulia na kushoto Mkurugenzi wa uendeshaji wa mfuko huo wa PSPF, Neema Muro na nyuma yao ni Costantina Martin ambaye ni Meneja Mawasiliano, Masoko na Uenezi wa PSPF

Feza Boys and Girls Secondary Schools emerge Top in Dar es salaam

$
0
0
The National Examination Council of Tanzania ( NECTA) has  released the Form Six National Examination results for 2014 indicating better performance over last year’s record.

The results from the examination sat on may this year showed  Feza Boys High school topping the lists of schools in terms of best performance in Daresalaam  and ranked 2nd nationalwise followed by the sister school Feza girls High school which became 2nd in Daresalaam and 12th nationalwise.

A  total of 60 candidates sat for the exam where 36 got division I, 18 students got division II and 6 students got division III which made the school 2nd nationalwise, and Feza girls had 41 candidates where 19 students got division I, 13 division II, and 9 division III’s .

The results further showed that Feza boys High school as the overall best school in science subjects as it topped chemistry, biology, history and Economics nationalwise.

The 2 students from Feza boys high school, Innocent Sabas Yusuf (3rd) and Ramadhan   Msangi(10th), managed to become among the top ten best students in Tanzania.


Since its commencement in the year 1998, Feza Schools have been pioneering provision of quality education to the Tanzanian Youth. From nursery, primary, secondary to high level education the school has established spacious compounds with home touch, teaching by Tanzanian curriculum for both boys and girls. 
Feza Schools have even recently opened an International school for both boys and girls, following the Cambridge Curriculum to suit more needs of the Tanzanians seeking for alternative education systems.

RAIS WA TFF AANDAA FUTARI KWA WADAU

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameandaa futari kesho (Julai 17 mwaka huu) kwa wadau mbalimbali wa mpira wa miguu.

Shughuli hiyo itafanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam ambapo waalikwa wataanza kuwasili saa 11.30 jioni.

Waalikwa katika futari hiyo wametoka katika makundi mbalimbali. Makundi hayo ni wadhamini, klabu za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza za Dar es Salaam ambazo zitawakilishwa na watu wawili wawili.

Viongozi wa zamani wa TFF, Said El Maamry, Leodegar Tenga, Muhidin Ndolanga, Athuman Nyamlani, Mwina Kaduguda, Michael Wambura, Fredrick Mwakalebela na Ashery Gasabile. Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF waliopo Dar es Salaam, Wizara ya Michezo na Ofisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Vyama shiriki; TWFA, TAFCA, TASMA, SPUTANZA, FRAT ambavyo vitawakilishwa na watu watatu watatu, viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Baraza la Michezo la Taifa (BMT), wahariri wa habari za michezo, Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) na Polisi kanda Maalumu- Dar es Salaam.

Wajumbe wa kamati ndogondogo za TFF waliopo Dar es Salaam, wazee wa Simba na Yanga- watano kutoka kila klabu, timu ya Serengeti Boys, klabu ya Saigon, Bodi ya Ligi Kuu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Wakuu wa wilaya za Dar es Salaam, wabunge wa Dar es Salaam, Meya wa Dar es Salaam, Meya wa Kinondoni, Meya wa Ilala na Meya wa Temeke.

Waalikwa wengine ni Omari Abdulkadir, Amin Bakhresa, Harudiki Kabunju, Hamis Kissiwa, Ismail Aden Rage, Masoud Sanani, Jamal Bayser, Hassan Dalali, Imani Madega na Mbaraka Igangula.

KITABU CHA "HISTORIA YA KLABU YA SIMBA"KILICHOANDIKWA NA MWINA KADUGUDA CHAZINDULIWA RASMI LEO

$
0
0
 Mwina Kaduguda Mtunzi wa kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" akielezea kwa kina Magumu gani amepitia wakati anaanza kuandaa kitabu hicho,Wa kwanza Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia na Katikati ni Mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Bwana Mkuki Bgoya ambao ndio wachapishaji wa kitabu hicho.Akielezea kwa ufupi Mwina Kaduguda amesema kwamba Dhumuni kubwa la Kutunga kitabu hicho ni kutaka kutunza historia ya soka ya Timu hiyo isipoteee ili iweze kusomwa kizazi na kizazi.




 Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia Akijiandaa kukata utepe ili kuweza kuzindua rasmi kitabu hicho cha historia ya Simba,Wanaoshuhudia kulia ni mtunzi wa kitabu hicho Mwina Kaduguda akifuatiwa na Bwana Mkuki Bgoya mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Ambao ndio wachapishaji wa kitabu hicho
Mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Bwana Mkuki Bgoya  Akielezea namna walivyochapa kitabu hicho na ubora wake .
 Mjumbe wa kamati ya Utendaji Klabu ya Simba Bwana Collin Frisch akiongea kwa niaba ya Rais wa Simba,ambapo amempongeza sana Mwina Kaduguda na kusema ameiweka Klabu ya Simba kwenye Kumbukumbu muhimu sana kwenye soka la Tanzania hivyo inatakiwa aungwe mkono kwa nguvu zote.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia akitoa neno kumpongeza Mwina Kaduguda  kwa kufikiria mbali sana kwa kuweka soka la Tanzania kwenye maandishi namna klabu ya simba ilivyoanza,Akaongeza kuwa Klabu za soka Tanzania zinatakiwa kuwa na watu kama Mwina Kaduguda ili kuleta maendeleo ya soka.Naibu waziri pia akasisitiza ni wakati wa kila mwanachama kujituma kwa bidii na kuacha kukaaa kwenye korido za Klabu na kupiga Zoga.
Mwina kaduguda Mtunzi wa Kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" Akimkabidhi  Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia Zawadi ya Kitabu ambayo ameomba apelekewe Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

KATIBU MKUU KIONGOZI AKUTANA NA UJUMBE TOKA CHUO CHA ST THOMAS CHA MAREKANI

$
0
0
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiongea na ujumbe kutoka Chuo cha St. Thomas cha Marekani uliomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 16, 2014 Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue leo tarehe 16 Julai, 2014 amekutana na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mt. Thomas cha Minnesota, Marekani wanaotembelea Tanzania kujifunza uzoefu wa Tanzania katika masuala ya kiuongozi na anuwai ya tamaduni. 

Wanafunzi hao ambao kwa idadi yao ni wanafunzi 14 wanaochukua Shahada za Uzamivu na Uzamivu katika masuala ya Uongozi wa Kimataifa pamoja na Wakufunzi wao wawili, Dkt. Jean Pierre Bongila na Dkt. Artika Tyner. Mkutano huu ni mwendelezo wa mkutano kama huu ambao Katibu Mkuu Kiongozi aliufanya mwaka jana na kundi jingine la wanafunzi kutoka Chuo hicho ambapo aliwapa uzoefu wa uongozi na anuwai ya tamaduni katika Tanzania, Afrika na katika medani za kimataifa. Kwa kutambua umuhimu wa nasaha walizozipata wanafunzi wa mwaka jana, Chuo hicho kiliomba na kukubaliwa fursa nyingine ya kuonana na Katibu Mkuu Kiongozi. Ziara ya wanafunzi hao ilianzia Arusha tangu tarehe 12 Julai, 2014 na itamalizika tarehe 17 Julai, 2014. 

 Pamoja na kupata fursa ya kuonana na kuzungumza na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Arusha, wanafunzi hao walipata pia muda wa kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo Arusha na baadaye Zanzibar. Na matarajio ni kuwa wanafunzi hao watakuwa mabalozi wazuri wa kuitangaza Tanzania sehemu mbalimbali za dunia watakakokwenda kufanya kazi. Kwa ujumla, wanafunzi wamepata fursa nzuri ya kuuliza maswali yaliyogusa maeneo yote yanayohusu uongozi, siasa, uchumi, elimu, afya na utamaduni ambayo yalipata ufafanuzi wa kutosha kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

RAIS KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM LEO

$
0
0
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM jijini Dar es salaam leo. PICHA NA IKULU

Tanzania kupata mafunzo Kamisheni ya Mafuta na Gesi Canada

$
0
0
Serikali ya Tanzania inatarajia kutuma wataalam kwenda nchini Canada katika Kamisheni ya Mafuta na Gesi ya jimbo la British Columbia (BC Oil& Gas Commission), ili kupata uelewa zaidi katika masuala ya udhibiti wa mafuta na gesi nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Charles Kitwanga wakati akiongea na watendaji wa Kamisheni ya Mafuta na Gesi ya Jimbo la British Columbia katika Ofisi za kamisheni hiyo zilizo katika mji wa Victoria nchini Canada.

Akiongoza ujumbe wa Tanzania uliotembelea Kamisheni hiyo ili kujifunza masuala ya udhibiti wa sekta ndogo ya gesi asilia, na mafuta, Naibu Waziri alisema kuwa lengo la serikali ya Tanzania ni kuhakikisha kuwa rasilimali zilizopo zinaendelezwa na faida yake kuonekana kwa wananchi hivyo wataalam watakwenda nchini Canada katika Kamisheni hiyo ili kuongeza uelewa katika masuala ya udhibiti ambao kwa kiasi kikubwa unachangia katika kuhakikisha kunakuwa na maendeleo endelevu ya rasilimali zilizopo Tanzania.

" Mtazamo wa wananchi wengi ni kuwa makampuni ya kigeni yanakuja nchini Tanzania kuchukua rasilimali na kuondoka nazo bila wananchi hao kufaidika hivyo serikali inafanya kila jitihada ili faida za rasilimali zetu ziwafikie wananchi wote na moja ya vigezo vya jitihada hizo ni kuwa na mamlaka madhubuti za udhibiti zitakazohakikisha makampuni ya nje na ndani ya nchi yanafanya kazi kwa kuzingatia kanuni na sheria zinazoongoza sekta husika" alisema Kitwanga.

Naibu Waziri alieleza kuwa Tanzania ikiwa katika mchakato wa kutengeneza sheria na kanuni zitakazoongoza sekta ya gesi asilia na mafuta, inahitaji kupata maoni na uelewa zaidi kutoka katika nchi zilizopiga hatua katika uendelezaji wa rasilimali hizo ikiwemo jimbo la British Columbia ambalo limegundua gesi asilia kiasi cha zaidi ya futi za ujazo trilioni 2900.

Naye Ofisa Mkuu wa Operesheni katika Kamisheni ya Gesi na Mafuta ya British Columbia, Mhandisi Ken Paulson alieleza kuwa Kamisheni hiyo ambayo imeanzishwa zaidi ya miaka 15 iliyopita ina jukumu la kudhibiti shughuli zote za mafuta na gesi asilia ikihusisha, utafiti, uendelezaji na usafirishaji wa rasilimali hizo kwa njia ya bomba.

Mhandisi Paulson alieleza kuwa Kamisheni hiyo pia ina jukumu la kukusanya takwimu za kijiolojia zinazotumika katika shughuli za utafutaji wa gesi asilia na mafuta na kuzitangaza kwa njia ya tenda ili makampuni yanayohitaji kufanya shughuli za utafutaji mafuta na gesi katika jimbo hilo yanunue takwimu hizo kutoka Kamisheni hiyo.

Kuhusu matumizi ya gesi asilia, Afisa Mkuu wa Operesheni aliueleza ujumbe huo kutoka Tanzania kuwa asilimia 15 ya kiasi cha gesi kilichogunduliwa katika jimbo hilo kinatumika ndani ya jimbo la British Columbia kwa matumizi mbalimbali na kiasi kinachobaki kinasafirishwa kwenda bara la Amerika Kaskazini.

" Ingawa tunasafirisha gesi kwenda Amerika Kaskazini, mahitaji ya soko hilo yanashuka kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa gesi nchini Amerika, hata hivyo tumejipanga kukabiliana na hali hiyo kwa kutumia gesi hii kwa masuala mengine ikiwemo kuzalisha methano, matumizi ya majumbani na kutumika katika vivuko ambavyo vitakuwa vinatumia mafuta na gesi" alisema Mhandisi Paulson.

Kuhusu mfumo wa ugawanaji mapato (PSA) kati ya makampuni ya utafutaji na uchimbaji gesi asilia na mafuta, Bw. Mhandisi Paulson alieleza kuwa kampuni ikianza uzalishaji wa gesi au mafuta, serikali ya jimbo hilo hukusanya mrabaha wa asilimia 10 hadi 20 ya Mapato.

Katika ziara hiyo ya mafunzo nchini Canada, Naibu Waziri Nishati na Madini ameambatana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Victor Mwambalaswa pamoja na baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo akiwemo, Murtaza Mangungu (Mb.), Raya Ibrahim (Mb.), Richard Ndasa (Mb.), Deogratias Ntukamazina(Mb.), Shafin Sumar (Mb.) na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (wa tatu kutoka kushoto), Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa (wa pili kutoka kushoto) na Mbunge wa Sumve, Richard Ndasa (wa kwanza kushoto) wakimsikiliza Eng. Ken Paulson, Afisa Mkuu wa Operesheni katika Kamisheni ya Gesi na Mafuta ya Jimbo la British Columbia nchini Canada mara walipofika katika Kamisheni hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara ya mafunzo kwa ujumbe huo katika sekta ya uziduaji.
Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu (wa kwanza kushoto) akieleza kitu katika mkutano kati ya watendaji wa Kamisheni ya Gesi na Mafuta ya Jimbo la British Columbia nchini Canada pamoja na ujumbe kutoka Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri Nishati na Madini, Charles Kitwanga (wa tano kutoka kushoto).Wengine katika picha ni Mwenyekiti Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa (wa nne kutoka kushoto) Mbunge wa Ngara, Deogratias Ntukamazina (wa pili kutoka kushoto), Richard Ndasa (Mb. Sumve), (wa tatu kutoka kushoto), Raya Ibrahim (Mb.) (wa pili kutoka kulia) pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Nishati . Katikati ni Eng. Ken Paulson, Afisa Mkuu wa Operesheni katika Kamisheni ya Gesi na Mafuta ya Jimbo la British Columbia nchini Canada.

Majadiliano ya masuala ya kodi Afrika yafanyika Arusha

$
0
0
 Waziri wa Fedha, Mh. Saada Mkuya akizungumza na Waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa  mkutano wa siku 3 wa majadiliano ya masuala ya kodi Afrika uliofanyika jijini Arusha jana katika hotel ya naura spring. 
Waziri wa fedha Saada mkuya akijadiliana jambo na rais wa kituo cha kimataifa cha ukusanyaji kodi na uwekezaji Daniel Witt wakati wa mkutano wa siku 3 wa majadiliano ya masuala ya kodi Afrika uliofanyika jijini Arusha jana katika hotel ya naura spring.
 Waziri wa Fedha,Mh. Saada Mkuya katikati  akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TRA,Bw. Rished Bade (wa tatu kulia) na Dr. Jeffrey Owens mtaalam mshahuri wa kodi na mhadhiri chuo kikuu cha uchumi na biashara Viena (kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wadau walioshiriki kwenye mkutano hio mara baada ya waziri kufungua mkutano wa majadiliano ya masuala ya kodi unaofanyika jijini Arusha katika hotel ya Naura spring.

AFRICAN REGGAE AMBASSODOR JHIKOMAN KUTINGISHA JUKWAA TUBINGEN,UJERUMANI

$
0
0
Mwanamuziki maarufu wa reggae barani Afrika Jhiko Manyika aka Jhikoman kutoka Bagamoyo,Tanzania,anatarajiwa kupanda jukwaani katika maonyesho makubwa ya kimataifa ya 5th.International African festival Tubingen 2014,nchi ujerumani. Mwanamuziki huyo nguli wa reggae amepewa nafasi ya pekee ya kutumbuiza mara mbili kwa siku tofauti katika viwanja vya onyesho hilo Festplatz,Europa str. mjini Tubinge kusini mwa ujerumani, ambako maonyesho yatafunguliwa 17.julai 2014 hadi 20.Julai 2014,maonyesho ya Tubingen yategemewa kukusanya umati wa watu zaidi ya 100,000 na yanazishirikisha bendi na wasanii mbali mbali wa nchi za kiafrika.Pia Mabalozi na wawakilishi wa nchi mbali mbali za kiafrika wameshaanzakuwasili katika mji huo wa Tubingen ,kuudhuria maonyesho hayo.

biashara matangazo...

Mtwara, Lindi to host grand ‘southern’ expo

$
0
0
THE southern Tanzanian regions of Mtwara and Lindi will have a good opportunity of showcasing their rich but largely untapped tourism and economic potential through a two-day festival starting August 16.

Dubbed ‘Mtwara Festival’, the first ever annual event, to take place at the Lawi Nangwanda Sijaona Stadium in the fast developing municipality, will be coloured by an assortment of rhythms, music, arts and culinary flavour on display.

The festival, whose theme this year is ‘Fursa Zimefunguka, Tuzitambue, Tujiandae, Tuzichangamkie’ (Opportunities have opened up, let’s identify them for exploitation), is expected to be officiated by the Prime Minister, Mr Mizengo Pinda.

According to a press release issued by the Tanzania Creative Industries Network (TACIN), Mtwara Festival “is born of the collaboration between it, the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) and supported by the Tanzania Tourist Board (TTB)’’.

The festival is part of TTB strategy to attract visitors and create tourism and economic opportunities to the deep-water port regions.

It is also deemed as a communication strategy and platform from which the community will learn about abundant opportunities around them as well as enhance their pride through the promotion of Mtwara and Lindi as places to visit, live, work and do business.

“Mtwara and Lindi are both coastal regions with pristine beaches and abundant wealth of history, culture and creativity, which through this festival will attract more foreigners and stimulate tourism in these two communities,’’ the statement quoted Mr Anic Kashasha, the Executive Chairman of TACIN, saying.

Mr Kashasha has further noted that the recent discovery in 2012 of natural gas in Mtwara and Lindi will also contribute to the economic development in the two regions as it will create more opportunities for job creation and income generation.

Mtwara has for many years been seldom touched by the outside world and reasons for its late development may be traced all the way to the colonial era when the Germans and Portuguese needed a buffer zone and used Ruvuma River as a border.

Acting TTB Managing Director Devota Mdachi has called on businesses and organizations to come out and support the festival in addition to taking advantage “of this great opportunity to showcase their products and services for the world to see’’.

The festival has been supported by several institutions, including the Mtwara Regional Commissioner’s Office, Mtwara Mikindani Municipal Council and Mtwara Rural District Council. Media partners are Tanzania Standard (Newspapers) Limited, publishers of Daily News, Sunday News, HabariLeo, HabariLeo Jumapili, Spoti Leo, Mtwara’s Pride FM Radio and Strictly Communications.

SOURCE: DAILY NEWS

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2014 YATOKA

$
0
0
Matokeo ya mtihani wa kidato cha 6 yaliyofanyika tarehe Mei 5 – 21, yametoka. Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia 95.98 ya watahiniwa waliofanya mtihani kidato cha 6 wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 12,080 na wavulana waliofaulu ni 26,825.

Watahiniwa waliopata division IV ni 4,420 sawa na asilimia 12.54
Watahiniwa waliopata zero (0) ni 612 sawa na asilimia 1.74.

SHULE 10 ZILIZOONGOZA
1. Igowole
2. Feza Boys
3. Kisimiri
4. Iwawa
5. Kibaha
6. Marian Girls
7. Nangwa
8. Uwata
9. Kibondo
10. Kawawa

SHULE 10 ZA MWISHO
1. Ben Bella
2. Fidel Castro
3. Tambaza
4. MuhezaHigh School
5. Mazizini
6. Mtwara Technical
7. Iyunga technical
8. Al- falaah Muslim
9. Kaliua
10. Osward Mang'ombe
MATOKEO KIDATO CHA 6: 95.98% wafaulu kidato cha 6 kutoka 87.9% mwaka jana. Tambaza ndani ya shule 10 za mwisho, K/Katibu Mtendaji Necta C. Msonde atangaza leo.
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live


Latest Images