Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

INTRODUCING "MY BRIDE PRICE" SHORT FILM BY IN FOCUS FILMS


MAALIM SEIF AFUTARISHA WATENDAJI WAKE

$
0
0

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akifutarisha watendaji wa Ofisi yake nyumbani kwake Mbweni Zanzibar. Miongoni mwao ni Watu Wenye Ulemavu wa aina mbali mbali. Picha na Salmin Said, OMKR



 Watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar wakijiandaa kufuturu  Mbweni Zanzibar. 
Watendaji wa Ofisi ya MAkamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar wakifuturu Mbweni Zanzibar. 

AFRICA MOUNTAINS REGIONAL FORUM SET FOR OCTOBER 2014 IN ARUSHA

$
0
0
cid:image001.png@01CF865E.938D6A00
The African Mountains Region Forum organized by East African Community in Partnership with Albertine Rift Conservation Society (ARCOS), African Mountains Partnership, United Nations Environment Programme (UNEP), the Austrian Development Cooperation and Swiss Agency for Development Cooperation is slated for 22nd - 24th October 2014 in Arusha, Tanzania.

The three-day forum, which aims at enhancing collaboration and framing a regional agenda for sustainable mountain development challenges in African mountains, will bring together senior officials from African government institutions, academia, civil society and private sector.

The specific objectives of this forum are to provide an opportunity for different sustainable mountain development stakeholders to enhance understanding of common conservation and development issues in the region; identify strategic actions to address major emerging issues such as climate change in the region as well as promote linkages and collaboration between different stakeholders for a regional framework on sustainable mountain development in Africa.

In addition, the forum will share lessons and experiences in meeting the conservation and development challenges including water, energy, food security and climate change in Africa Mountain regions as well as entail a special session devoted to UNEP’s inter-regional project‘’Climate Change action in developing countries with fragile mountainous ecosystems from a sub-regional perspective’’.

At the regional level,  according to the Treaty for the Establishment of the East African Community, Partner States agreed to cooperate in the management of shared natural resources and to take concerted measures to foster cooperation in the joint efficient management and sustainable utilization of natural resources within the Community for the benefits of the Partner States.

Article 9 of the EAC Protocol on Environment and Natural Resources Management puts emphasize on the need to promote the management of trans-boundary ecosystem in East Africa, while under article 20, Partner States agreed to protect mountain ecosystems such a critical water catchment, conservation of heritage areas and other areas of common strategic interest at local, national, regional and international levels.

Naibu Waziri wa Uchukuzi atembelea Shirka la Ndege Tanzania (ATCL)

$
0
0
 Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (kulia), akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mr. Salim Msoma wakati alipotembelea shirika hilo mwishoni mwa wiki kuongea na Bodi, Menejiment na wafanyakazi wa Shirika hilo. Nyuma ya Mr Msoma ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo, Kapteni Milton Lazaro.

 Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na wajumbe wa bodi na menejiment ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wakati alipoongea nao mwishoni mwa wiki katika ofisi za Makao ya Shirika hilo.

Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, akisisitiza jambo wakati alipoongea na Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Naibu Waziri aliwasisitiza watumishi hao kufanya kazi kwa bidii na kurudisha sifa ya shirika hilo. Picha na kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi

KATIZO LA UMEME MKOA WA TEMEKE

$
0
0

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataaarifu wateja wake wa Mkoa wa  Temeke kuwa kutakuwa na katizo la umeme kama ifuatavyo:-


TAREHE:      16/07/2014, 17/07/2014 NA 19/07/2014
MUDA:           03:00Asubuhi – 12 Jioni   
                                                                                   
SABABU:      Kubadilisha nguzo zilizooza maeneo ya Feri Kigamboni.
                            
MAENEO YATAKAYOATHIRIKA:
Feri, Tungi, Machava, Magogoni, Navy jeshini, Pikoli  na maeneo jirani.

Tafadhali usishike waya uliokatika toa taarifa kupitia simu zifuatazo 
2138352; 0222138352; 0788 499014,0736 501661 
au namba hii ya kituo cha huduma kwa Wateja:
2194400 au 0786985100.          
Uongozi unasikitika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.


Imetolewa na:          OFISI YA UHUSIANO,
                                    TANESCO – MAKAO MAKUU.

VIJANA WAASWA KUDUMISHA AMANI

$
0
0
 Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma akimvisha kofia ya ukamanda Profesa Peter Msolla baada ya kuteuliwa kuwa Kamanda wa UVCCM wilaya ya Kilolo sherehe zilizofanyika katika viwanja vya Kidabaga. 
 Mbunge wa jimbo la Kilolo,Profesa Peter Msola akila kiapo cha kuwa kamanda wa UVccm mbele ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma.
 Mbunge wa jimbo la Kilolo,Prof Peter Msola akiwaapisha makamanda wa vijana ccm katika wilaya ya Kilolo sherehezz ilizofanyika katika uwanja wa Kidabaga.

Na Denis Mlowe,Kilolo

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana  Chama  cha Mapinduzi (CCM)  Taifa, Sadifa Juma Hamis ametoa rai kwa   vijana kuepuka kutumika katika kuvuruga amani na utulivu uliopo nchini Tanzania kwa kutumika na baadhi ya vyama vya siasa na kuhatarisha amani  ya Taifa.
 
Sadifa alitoa rai hiyo mwishoni mwa wiki katika  viwanja  vya Kidabaga wakati akiwahutubia wananchi  wa Kidabaga kata ya Bomalang’ombe wilayani Kilolo wakati wa kusimikwa kwa mbunge wa jimbo la Kilolo Prof. Peter Msola kuwa kamanda wa umoja wa vijana CCM wa wilaya ya hiyo.
Alisema kuwa amani  ambayo tunajivunia  ipo  siku  itatoweka  na iwapo  vyama  vya siasa  vitaacha kufanya kazi yake ya  kisiasa kwa kunadi  sera  za vyama  vyao na kueneza  chuki  dhidi ya  serikali kama ilivyo  hivi  sasa kwa baadhi ya  vyama kuendesha siasa  za  chuki na  kuwatumia vijana kuvuruga amani yetu.
 
" Nawaombeni  sana vijana  wa   kuendelea   kuonyesha mfano  kwa  vijana  bora katika kudumisha amani iliyopo na kamwe msije iga siasa vya vyama  vya upinzani siasa ya  kufanya  vurugu ..... hiyo ni siasa mbaya  sana na itakuja  kuliweka Taifa katika umwagaji damu ambao hakika itakuwa ngumu sana kuweza kuishi tena kama mwanzo” alisemaSadifa
 
Alitoa mfano kuwa kuna ushahidi kwa nchi jirani unaonesha madhara ya kuichezea amani na kuongeza kuwa ni rahisi sana kupoteza amani na umoja lakini ni vigumu sana kuirejesha na kuwataka vijana kuacha kuandamana kwa kuiga tu kwa kuwa umeambiwa fanya jambo hilo
 
Mbali ya kuwataka  vijana kuacha kutumiwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa Sadifa aliwataka viongozi  wa vyama  vya siasa kutowatumia vijana hao  katika kuvuruga amani pia aliwataka vijana kutokubali siasa  chafu zenye chembe ya vurugu kwa watanzania na kuongeza kuwa sehemu yoyote yenye amani na utulivu, yapo maendeleo kwa sababu wananchi wanafanya shughuli za maendeleo kwa uhuru
 
 Kwa upande wake Kamanda mpya wa umoja wa vijana Ccm wilaya ya Kilolo, Prof Peter Msola aliwataka vijana kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuondokana na umaskini katika wilaya hiyo na kuwataka kushirikiana katika kudumisha amani iliyopo nchini Tanzania.
 
Alisema moja changamoto kubwa inayowakabili vijana na ambayo kwa kushirikiana nao atahakikisha inafanyiwa kazi kwa kutumia fursa mbalimbali zinazowazunguka ni ajira kwa kuwa fursa hizo zinaweza kuwa  katika sekta ya biashara, kilimo na ushauri kwa kupitia vikundi vya maendeleo.
 
Alisema ardhi na hali ya hewa nzuri ya wilaya ya Kilolo inaweza kuwaongezea fursa ya ajira vijana wa wilaya hiyo. 

Israel and Palestine, an animated introduction.

Jhikoman katika tizi la Uzee mwisho Chalinze ndani ya Ujerumani

$
0
0
 Mwanamuziki maaruffu wa Reggae barani Afrika Jhikoman ambaye anatarajia kupanda jukwaani wiki hii katika maonyesho ya 5th International African Festival Tubingen,2014,Germany. mwanamuziki (pichani) akiwa katika mazoezi ya viungo maarufu kama 'Uzee mwisho Chalinze' ndani ya Ujerumani. kwa wale wanataka kumpa Hi! +49(0)15211229655
 Kilomita 10 kila asubuhi si mchezo



Mario Gotze Scored This Unforgettable Goal To Win The World Cup For Germany

TBC YAFANYA HALFA YA KUHITIMISHA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA 2014, DAR

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bw. Clement Mshana (kulia) akiwakaribisha wageni walioalikwa katika hafla ya kuhitimisha michuano ya kombe la dunia 2014 iliyofanyika jana Julai 12, 2014 katika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof. Elisante ole Gabriel, akiongea machache katika hafla ya kuhitimisha michuano ya kombe la dunia 2014 iliyofanyika jana Julai 12, 2014 katika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Prof. Elisante ole Gabriel, akimkaribisha Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Mhe. Juma Nkamia ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuhitimisha michuano ya kombe la dunia 2014 iliyofanyika jana Julai 12, 2014 katika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. 
Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia akiongea akiongea katika hafla ya kuhitimisha michuano ya kombe la dunia 2014 iliyofanyika jana Julai 12, 2014 katika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. 


Mshehereshaji wa Hafla hiyo Elisha Elia akiongea machache.
Rais wa Bongo Movie, Steve Nyerere akitoa shukrani zake kwa niaba ya wasanii katika hafla ya kuhitimisha michuano ya kombe la dunia 2014 iliyofanyika jana Julai 12, 2014 katika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Malala DAY uly 14, 2014

$
0
0
Stand with me and the Nigerian girls: show the world we are #StrongerThan those who deny schoolgirls an education.  For more CLICK HERE

Dar tambarare

$
0
0
Hii ni sehemu ya jiji la Dar es salaam, hususan maeneo ya Mchafukoge na Kariakoo ambako kunaonekana Busatani ya Mnazi Mmoja Garden kuzitenganisha. Awali majengo ya upande wa kulia mwa bustani hiyo yalikuwa ya mbavu za mbwa.

DIAMOND PLATINUMZ ALIVYOTEMA YAI KWENYE BET RED CARPET CALIFORNIA

PADZ HOTEL, KIOTA KIPYA KABISA JIJINI MBEYA

$
0
0
 Padz Hotel ni kiota kipya kilichoota maeneo ya Forest kwenye Barabara Kuu ya Tanzania-Zambia, jirani na Chuo cha Mzumbe Univeristy, dakika kadhaa toka Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Songwe na katikati ya Jiji la Mbeya. 
Alama yake kuu ukitokea Songwe ni bendera za Tanzania na Marekani kwa nje na mjengo wa kioo tupu. Pazuri, huduma bomba msosi ndio usiseme. Na bei ni ya kiwandani...Kuwasiliana nao piga +255252500635 ama +255759851439 na +255652319139 ama email info@padtzhotel,com na pia nenda www.padzhotel.com



Introducing "WORUMO" BY FUTURE JNL MASTER Produced By Jmonster


NAIBU WAZIRI WA MAJI MHE AMOS MAKALLA ATEMBELEA MIRADI YA MAJI MIKOA YA PWANI NA DAR ES SALAAM

$
0
0
 Naibu Waziri wa Maji, Mhe Amos Makalla ameanza ziara yake ya siku nne ya kukagua miradi ya maji katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam kwa kutembelea tenki la maji la Chuo Kikuu cha Ardhi na mradi wa maji Ruvu Juu. 
 “Serikali hailengi tu kuleta maji, ila pia kutatua tatizo la upotevu wa maji. Bali, tumejiandaaje kupokea maji ya kutosha kutokana na mradi mkubwa unaoendelea Ruvu Juu. Hivyo, hatuna budi kukarabati au kujenga kabisa upya matenki yote mabovu kabla ya kuanza kupata maji tunayotegemea’’, alisema Naibu Waziri akiwa katika mradi wa maji wa tenki la Chuo Kikuu cha Ardhi. 
 Naibu Waziri aliendelea kwa kusema upotevu wa maji ambao ni asilimia 53 na hii inachangiwa na miundombinu mibovu na chakavu, na pia wizi wa maji uliokithiri. Nia kubwa ya Serikali ni kuhakikisha tatizo hilo linapungua kama sio kwisha kabisa. 
Pia, Naibu Waziri alitembelea mradi wa Ruvu Juu kuangalia maendeleo ya upanuzi wa mradi huo, ambao unahusisha ujenzi wa matenki na ulazaji wa mabomba mapya katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam, ambao unafanywa na kampuni mbili kutoka India na mojawapo ikiwa ni WABAG ukisimamiwa na DAWASA. 
Mhe. Makalla alisema kuwa mtambo wa Ruvu Juu ulijengwa miaka ya 70 na kwa sasa unahitaji ukarabati. Na ameridhishwa na matengenezo yanayoendelea katika mtambo huo, ambao unategemewa kuongeza uzalishaji wa maji kutoka lita za ujazo 82 mpaka 196. 
 Aidha, aliwahakikishia wakazi wa Pwani na Dar es Salaam kuwa Serikali iko makini na mradi huu na wategemee kero ya maji kutatuliwa mara baada ya kukamilika kwa ujenzi huo.
 Mbunge wa Kibaha Vijijini, Hamoud Jumaa aliishukuru Serikali kwa jitihada zake za kutatua kero ya maji katika mkoa wa Pwani na vitongoji vyake na kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo. 
Ukarabati wa tenki la maji la Chuo Kikuu cha Ardhi unategemewa kukamilika baada ya siku 90 na sio 120 kama ilivyokua ikitegemewa hapo awali kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Kryton inayosimamia ujenzi wa tenki hilo, Inj. Denis Kapella. 
Aidha, ujenzi wa chujio la maji unategemewa kukamilika mwezi Agosti na ulazaji wa mabomba, mwezi Septemba katika mradi wa Ruvu Juu.
  Ujumbe ulioongozana na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla ukiwa ndani ya tenki la maji lililopo Chuo Kikuu cha Ardhi.                                                                                                                                                                                  
    Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akiambatana na wakandarasi wa kampuni ya WABAG pamoja na Meneja Mradi DAWASA, Inj. Romanus Mwang'ingo (mwisho kulia)  wakikagua  mradi wa maji wa Ruvu Juu, Pwani.                                                                                                  
Mchoro wa mradi wa maji Ruvu Juu
     Meneja  Mradi DAWASA, Inj. Romanus Mwang'ingo akimuonyesha Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla ramani ya mpango wa ujenzi wa matenki ya mradi wa maji Ruvu Juu mkoani Pwani unaoendelea kujengwa.
  Naibu Waziri wa Maji, Mhe Amos Makalla akiwa na Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mhe Hamoud Jumaa wakiwa katika 'kijiko' katika eneo la ujenzi wa mradi wa maji Ruvu Juu, Pwani.

Qasida

KATIBU MKUU WA UVCCM AFANYA ZIARA MKOA WA ARUSHA

$
0
0

six14Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akiendelea na ujenzi katika uwanja wa michezo wa st.Benjamin uliopo Usa river kwa ufadhili wa edinburgh global partnerships na YES Tanzania katika ziara yake ya kwanza ya kikazi ya siku tatu katika Mkoa wa Arusha.

 six12Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mmoja wa wa vijana waliojitolea katika mradi wa ujenzi wa kiwanja cha michezo
six11Hapa viongozi na wadau wakishuhudia jiwe la msingi katika kiwanja hicho cha michezo kilichozinduliwa rasmi na Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda
six10Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mshindi wa mbio za pikipiki greengad maarufu kwa jina la Mjusi.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI LAZARO NYALANDU AKUTANA NA TAASISI ZA UHIFADHI WANYAMAPORI JIJINI NEW YORK

$
0
0
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Waandamizi wa Taasisi ya Vulcan ya nchini Marekani  Bw. Dave Stewart (kushoto) na Bi. Lauren Ryder, inayojihusisha na masuala ya kuidadi tembo katika nchi 18 barani Afrika ikiwemo Tanzania, baada ya kufanya mazungumzo maalum ya ushirikiano yaliyofanyika katika jiji la New York nchini Marekani jana.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu  akiagana na Bw. Dave Stewart kutoka Taasisi ya Vulcan inayojihusisha na masuala ya kuidadi tembo katika nchi 18 barani Afrika ikiwemo Tanzania mara baada ya kumaliza mazungumzo nao  jana jijini New York nchini Marekani.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu  (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Waandamizi wa Taasisi ya inaundwa na Wanajeshi Wastaafu wa jeshi la Marekani walioanzisha umoja wao ujulikanao kama (VETPAW)kwa ajili ya kusaidia Uhifadhi wa Wanyamapori barani Afrika mara baada ya kumaliza mazungumzo baina yao jana jijini New York, Marekani.  Kushoto ni Balozi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu  akizungumza na Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi  mara baada ya kukamilika kwa kikao jana baina ya Waziri Nyalandu na ujumbe wake pamoja na taasisi mbalimbali za uhifadhi jijini New York, Marekani. Kati ni Katibu wa Waziri Bw. Imani Nkuwi. 

AJALI YA MAGARI MAWILI NA PIKIPIKI YAPOTEZA MAISHA YA WATU WAWILI.

$
0
0
Gari aina ya Range Rover lenye likiwa limeharibika vibaya baada a kugongana uso kwa uso na gari dogo 
Gari dogo aina ya Toyota Corolla lilikiwa limeharibika vibaya baada ya kugongana uso kwa uso na Range Rover katika makutano ya barabara ya Arusha/Moshi jirani kabisa na kipita shoto(Keep left) cha Arusha

Mifuko maalumu ya kuzuia abiria asiumie wakati wa ajali ikiwa imefumuka baada ya ajali .
Pikipiki ikiwa chini ya gari aina ya Range Rover baada ya kugongwa.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images