Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live

Katibu Mkuu wa Yanga wa zamani, George Johnson Mpondela ‘Castor’ afariki dunia, kuzikwa tabora jumatano

0
0

Katibu Mkuu wa Yanga  wa zamani, George Johnson Mpondela ‘Castor’ (kulia) enzi za uhai wake akiwa katika moja ya mikutano ya klabu hiyo. Kushoto ni mmoja wa wazee maarufu wa klabu hiyo Mzee Yusuf Mzimba.
Na Mahmoud Zubeiry

 Katibu Mkuu wa Yanga SC wa zamani, George Johnson Mpondela ‘Castor’ amefariki dunia jana saa nne usiku katika hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu ya moyo.

Mtoto wa marehemu, Hilton Mpondela amemwambia mwandishi wa habari hii leo kwamba, baba yake aliyekuwa pia mwanasiasa na mwanachama wa Chama cha Demokrasia ya Maendeleo (CHADEMA) alikuwa amelazwa hospitalini hapo kwa wiki tatu katika wadi ya wagonjwa wa moyo. 

Hilton amesema kwamba baba yake aliyekuwa akiishi eneo la Machava, Kigamboni, Dar es Salaam amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo kwa miaka minne sasa. Amesema msiba upo nyumbani kwao, eneo la Karakata, Uwanja wa Ndege karibu na Kanisa Katoliki na kituo kidogo cha Polisi, maarufu Polisi Posti.

Marehemu ameacha mke na watoto tisa, ambao ni Pius, Robert, Hilton, Kennedy, Joseph, Collin, na wa kike Linda, Jaqcueline na Jennifer.

Hilton amesema mwili wa marehemu utasafirishwa Jumanne kwenda Tabora baada ya kuagwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hospitali ya Muhimbili tayari kwa mazishi yake Jumatano kijiji cha Misha wilaya ya Tabora vijijini.

Marehemu Mpondela alizaliwa kijiji cha Misha, Tabora, Septemba 28 mwaka 1942 na kipindi kirefu cha maisha yake alikuwa mtumishi wa Mamlaka ya Pamba Tanzania.

Alianza kujulikana zaidi Yanga SC miaka ya 1980 alipokuwa Meneja Utawala wa Mamlaka Pamba, makao makuu, Dar es Salaam alipoisiaida klabu hiyo kupata wachezaji nyota wa Pamba SC ya Mwanza kiulaini enzi hizo inatisha katika soka ya Tanzania na kutoa vipaji vingi.

Aliwakuna mno wana Yanga kuwa kuwasaidia kuwapata nyota kama Athumani Juma Chama ‘Jogoo’, Yussuf Ismail Bana, Juma Mhina, David Mwakalebela, Nico Bambaga, Fumo Felician na wengineo.

Haikuwa ajabu mwaka 1993 Mpondela alipochaguliwa kwa kishindo kuwa Katibu Mkuu wa Yanga SC  chini ya Mwenyekiti, Dk Jabir Idrisa Katundu.

Hata hivyo, pamoja na mafanikio katika uongozi wake ikiwemo kuiwezesha klabu hiyo kutwaa Kombe la Afrika Mashariki na kati, sasa Kagame mjini Kampala Uganda na ubingwa wa Bara na iliyokuwa Ligi ya Muungano mfululizo, lakini sera zake za kutaka kuifanya klabu hiyo kuwa kampuni zilimuingiza matatizoni.

Mpondela alianza kupingwa na wanachama waliokuwa wakiwaunga mkono wafadhili wa timu hiyo wenye asili ya kiasia enzi hizo, chini ya marehemu Abbas Gulamali na hatImaye akachemsha na kubwaga manyanga Yanga SC.

Alipewa jina Castor alipokuwa Yanga SC kwa kufananishwa na rais wa zamani wa Cuba, Fidel Castor kwa misimamo yake. 

Mwaka 1995 Mpondela alistaafu kazi Mamlaka ya Pamba na kwenda kugombea Ubunge wa jimbo la Kindondoni kwa tiketi ya CHADEMA, ambako hata hivyo aliangushwa na mgombea wa CCM, Peter Kabisa jimbo la kinondoni.

Mwaka 2007, Mpondela alirejeshwa Yanga SC na Mwenyekiti wa sasa na mfadhili wa klabu hiyo, Yussuf Manji kuwa Mjumbe wa Baraza la Wazee.

Mungu ampumzishe kwa amani marehemu George Johnson Mpondela -  Amin.





MBUNGE DEO FILIKUNJOMBE NA WAGENI WAKE KUTOKA LUDEWA WAPAGAWISHWA NA MJOMBA BENDI

0
0
Msanii Mrisho Mpoto  mkurugenzi  wa Mjomba Bend  akipiga picha na  viongozi  wa CCM kutoka  Ludewa katika  show iliyoandaliwa na mbunge  wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe usiku  huu jijini Dar es Salaam
Viongozi wa CCM kutoka  kata za  wilayaya Ludewa  wakijipongeza kwa  show kali kutoka kwa Mjomba Bendi baada ya kumaliza mafunzo ya uongozi  jijini Dar
Mkurugenzi  wa bendi ya Mjomba Mrisho  Mpoto  akicheza  na  wana Ludewa katika  show kali  iliyoandaliwa na mbunge wao  Deo Filikunjombe
Msanii Mrisho Mpoto  kulia  akisalimiana na kada wa CCM katikati ni mbunge Deo Filikunjombe. Picha zaidi BOFYA HAPA

TOYOTA AVENSIS FOR SALE

0
0
 TOYOTA AVENSIS SILVER D4-D, 1.8 DIESEL 
ENGINE, VERY ECONOMIC ON FUEL
        MODEL 2005 , MANUAL, AIR CONDITIONING,
5 DOORS,IN VERY GOOD CONDITION FOR YEARS TO COME,
   THE CAR IS IN DAR ES SALAAM  AND  DUTY HAS BEEN PAID.
PRICE IS T.SH 13,000,000 (13 MILLION) BUT ALSO NEGOTIABLE.
NO MADALALI  PLEASE!
            INTERESTED? CALL TEL: +255788741125 OR +255718030320


Wana Njia Panda washiriki kufanya usafi katika Hospitali ya Amana jijini Dar es salaam

0
0
  

 Mtangazaji wa Kipindi cha Redio cha Njia Panda kinachorushwa na Clouds FM Dkt. Isack Maro akizungumza na mwandishi wa habari wa Zanzibar Media Bi. Sophia Kingimali wakatika wa zoezi la usafi katika Hospilali ya Amana iliyopo Ilala, jana jijini Dar es Salaam. Wananjiapanda wamejitolea kufanya shughuli za usafi katika Hospitali hiyo ikiwa ni kutoa mchango wao kwa jamii inayowazunguka.
 Mtangazaji wa Kipindi cha Redio cha Njia Panda kinachorushwa na Clouds FM Dkt. Isack Maro akiwajibika
 Mmoja wa Wana Njia Panda Andrew Kwingwa kwa kushirikiana na Mfanaya usafi wa kampuni ya Care Sanitation yenye jukumu la kufanya usafi katika Hospitali ya Amana, Bi. Anna Mkonda wakimwaka takataka katika jaa la kuhifadhi taka la Hospitali ya Aman kabla ya kupelekwa Dampo. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Shamra shamra za kupokea wanachama wapya wa CCM ELIMU-UDOM Makao Makuu ya CCM Dodoma

0
0
 Chama Cha Mapinduzi CCM kimevuna Wanachama wapya Zaidi ya mia moja kutoka chuo Kikuu UDOM.Wanachama hao wapya  ambao walipokelewa jana na kupe wakadi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi Maalum Mhe.Prof.Mark Mwandosya (Prof.Mwandosya ni Mlezi wa Tawi hilo) katika Hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa NEC Makao Makuu ya CCM wamejiunga na tawi la CCM-Elimu (School of Education) UDOM Pichani Mhe.Prof.Mark Mwandosya akizungumza na wanachama wapya wa CCM Tawi la Elimu-UDOM katika Ukumbi wa NEC Makao Makuu ya CCM Dodoma.Wengine Pichani  ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu(kushoto) na Mwenyekiti wa CCM Tawi la CCM-Elimu-UDOM Bw.James Martin aliyekaa katikati.
 Wanachuo wakimsikilizaMhe.Prof.Mark Mwandosya
Mhe.Prof.Marck Mwandosya akiwa makao makuu ya CCM akisindikizwa na wanachama wa CCM Tawi la Elimu-UDOM mara baada ya kupokea wanachama wapya zaidi ya miamoja.
 Wanachama wapya wa CCM ambao walipokelewa jana na kupewa kadi na Mhe.Prof.Mark Mwandosya  katika Hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa NEC Makao Makuu ya CCM wamejiunga na tawi la CCM-Elimu (School of Education) UDOM wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri.


 Na Deusdedit Moshi Mtendaji Mkuu wa Photo Solutions  wawakilishi wa Michuzi Blog Kanda ya Kati. Picha zaidi BOFYA HAPA

Cesc Fabregas afunguka, asema Nimehamia Chelsea sababu Wenger kaniambia sina namba Arsenal

0
0
 Kiungo wa Spain  Cesc Fabregas (pichani) amefunguka leo kwa kusema alifanya mazungumzo na kocha wa Arsenal Arsene Wenge kabla ya kuhamia Chelsea, na kuambiwa kwamba nafasi yake tayari imeshacukuliwa na Mesut Ozil. 
Fabregas alikuwa chagua la kwanza la Arsenal baada ya mchezaji huyo alipoamua kuondoka Barcelona mwishoni mwa msimu uliopita, lakini akamua kwenda Chelsea kwa dau la pauni milioni 30. 
“Niliongea na Mzee Wenger naye akanambia atapata wakati mgumu kumpa nafasi ya kucheza kwani tayari Ozil alikuwa ameshachukua namba yangu”, Fabregas aliwaambia waandishi wa habari kwenye kambi ya Spain huko Brazil. 
“Kulikuwa na timu kadhaa ambazo ningeweza kuchagua kwenda name nikachagua moja ya timu mbili ama tatu zilizo bora”, aliongezea mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. 
“Nikaongea na Jose Mourinho naye akaongea mambo niliyotaka kusikia na mambo yakaendelea haraka haraka kuanzia hapo. 
“Huu si muda muafaka wa kuongelea hayo, hata hivyo, kwani tunachohitaji ni kujali zaidi mambo ya timu ya taifa na kombe la dunia”, alisema. 
Fabregas aliingia kipindi cha pili wakati Spain walipochapwa bao 5-1 na Holland katika mchezo wa kufungua dimba kwa kundi B. Amesema yeye na wenzake wanatafuta hamasa kutoka mchezo wao na Uswisi miaka minne iliyopita huko Afrika ya Kusini kwenye mechi ya ufunguzi. 
“Tunahitaji kufikiria ni jinsi gani tuliweza kuchuma katika miaka sita iliyopita,” alisema akimaanisha ushindi wa Spain katika michuano ya Ulaya kati ya miaka 2008 na 2012.





news alert: hackers waiba akaunti ya facebook ya meya wa ilala Mstahiki Jerry Silaa leo

0
0
Napenda kuwajulisha marafiki zangu wote kwamba akaunti yangu ya facebook ime-hackiwa na kuanza kutuma ujumbe kwa marafiki zangu kuwataka waingie kwenye link kwani nina maongezi ya siri.

Tafadhali puuzia ujumbe huo kwani utasababisha akaunti yako nayo ku-hackiwa.
Tafadhali sambaza ujumbe huu, wakati tunaendelea kujaribu kuiokoa. Nawaomba radhi wote walopatwa na usumbufu huu.
Asanteni sana
- Jerry Silaa

JE WAJUA MAANA HALISI YA NENO BRAZUCA?

0
0

 Na Sultani Kipingo

"BRAZUCA" 

ni neno jipya lililo midomoni pa wengi ulimwenguni hivi sasa, japo si watu wote wanaojua maana yake. Subiri nikupashe.
"Brazuca" si kitu kingine bali ni  jina la mpira  unaotumika katika michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea chini Brazil hivi sasa. 

Neno hilo lina maana mbili. Ya kwanza ni neno la nchi hiyo kwa wa-Brazil wanaoishi nje ya nchi – yaani Diaspora. Maana ingine, neno hilo lina maana ya kujivunia, kuufurahia na kutambia u-Brazil kwa watu wa nchi hiyo, ama kitu ama jambo lolote la kusisimua linalohusiana na nchi hiyo.

Baadhi ya mipira ya Kombe la Dunia imekuwa maarufu kuliko mingine, huku wachezaji wakiilalamikia kwa kile wanachosema mipira hiyo  husafiri kwa kasi zaidi hewani, kiasi hata kusumbua walinda milango

Adidas, watengenezaji maalumu wa mipira kwa ajili ya Kombe la Dunia tokea mwaka 1970, waliuita “Jabulani” mpira uliotumika katika fainali hizo mwaka 2010 huko Afrika Kusini, na kulakiwa na kila aina ya makelele kuwa mwendo wake hautabiriki.
Huu wa sasa jina lake rasmi ni "Adidas Brazuca" na umetengenezwa na kampuni ya Forward Sports  ya Sialkot nchini Pakistan. Jina “Brazuca” la mpira huo lilizinduliwa September 2, 2012 jijini Rio de Janeiro, kupitia kura ya maoni iliyoendeshwa na Fifa na Adidas, ambapo wapiga kura zaidi ya milioni moja wa Brazil walilichagua kwa kura 77.8% dhidi ya majina mengine mawili yaliyopendelkezwa – “Bossa Nova (14.6%) na Carnavelesca (7.6%)



Siku rais obama alipopiga misele mitaani

0
0
Kwa hisani ya White House

mdau ashuhudia ngoma ya argentina na Bosnia Herzegovina

0
0
Mdau Moody Kiluvia akiwa katika Uwanja wa Maracana jijini Rio de Janeiro kushuhudia mechi ya Argentina dhidi ya Bosnia Herzegovina ambapo Argentina wameshida kwa bao 2-1. Matokeo mengine ya leo ni Uswisi imeshinda 2-1 dhidi ya Ecuador, wakati Ufaransa imeizamisha Honduras kwa bao 3 mtungi. 


Christian Bella na Malaika band walivyodatisha wapenzi wao Tabora

PRIME PROPERTY FOR SALE AT MBEZI BEACH, DAR ES SALAAM

0
0
A two (2) storey house for sale at Mbezi beach behind Art Gallery in Dar es salaam. Plot size: 1,206 square metres. It is fully fenced by concrete blocks with two entrance gates at front and rear side; there are two access roads.

House: Ground floor: 5 bedrooms (1 master), 3 bathrooms, living room, dining room, kitchen and stores. 1st floor: 3 bedrooms (1 master), 2 bathrooms.
 Extras:
  1. The house can easily be converted into 2 family houses and each use its own gate on different access roads.
  2. Can also be converted into commercial use e.g. hotel, restaurant, office etc.
Price: USD 320,000
 Contact: 0788 077 098 
or email: rodgers@eaunique@gmail.com
 Note: No agents please

Best regards,
MDAU MBEZI BEACH

Dkt Liky Abdallah na vibweka vya wa-Brazil wanaopinga Kombe la dunia kufanyika kwao

UN KUZINDUA MFUMO MPYA WA KUHABARISHA UMMA NDANI YA TAMASHA LA ZIFF 2014 JIONI HII

0
0
un1
Ofisa habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vusso (kushoto) akionesha taarifa ya Umoja wa Mataifa ya utekelezaji wa mpango wa pamoja wa mashirika ya Umoja wa mataifa hapa nchini. Taarifa hiyo imo katika documentary (taarifa ambayo iko katika mfumo wa video) ya dakika saba inayoonyesha kazi mbalimbali Umoja wa Mataifa nchi itazinduliwa leo kwenye ukumbi wa Ngome Kongwe kuanzia saa moja jioni katika mpango wa Umoja wa Mataifa wa kutumia mitandao ya kijamii kuwafikia wadau wake wa maendeleo.(Picha na Zainul Mzige).
Un2
Mkuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini Anna Liboro Senga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo kuhusu uzinduzi wa mfumo mpya wa utoaji wa taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa wadau wake.Mpango huo unazinduliwa leo jioni katika ukumbi wa wazi wa Ngome Kongwe. Kushoto ni Ofisa habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vusso .(Picha na Zainul Mzige wa Mo Blog)
   

Ndovu Special Malt yasherehekea ushindi wake jijini Dar

0
0
Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt, Pamela Kikuli akionyesha Kikombe alichoshinda kupitia bia ya Ndovu kutoka katika Kampuni ya Kimataifa ya Monde Selection nchini Ufaransa kama bia yenye ubora wa kimataifa wakati wa hafla ya kupongezanma na wadau wa bia hiyo iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt, Pamela Kikuli na Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Nchini(TBL) wakionyesha Kikombe walichoshinda kupitia bia ya Ndovu kutoka katika Kampuni ya Kimataifa ya Monde Selection nchini Ufaransa kama bia yenye ubora wa kimataifa wakati wa hafla ya kupongezanma na wadau wa bia hiyo iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki
Mkurugenzi wa Masoko TBL,Kushila na Meneja masoko TBL, Fimbo Butallah wakizungumza na wadau.   


Professor Benezeth Mutayoba apata tuzo ya 2014 National Geographic Buffett for leadership in conservation

0
0
Professor Benezeth Mutayoba , Profesa chuo kikuu cha Sokonne na makamu mwenyekiti wa Tanzania Elephant Protection society akipokea tuzo ya Buffet For Leadership In Conservation kutoka National Geographic siku ya Alhamisi June 12, 2014 Washington, DC. Wanaomkabidhi tuzo ni Dr. John Francis (kushoto) ambaye ni makamu wa Rais National Geographic kwenye Utafiti na Gary E. Knell ambaye ni Ris National Geographic na Afisa Mtendaji Mkuu
Professor Benezeth Mutayoba , Profesa chuo kikuu cha Sokonne na makamu mwenyekiti wa Tanzania Elephant Protection society akiotoa shukurani na kuelezea kuguswa kwake kwa Natianal Geographic kutambua mchango wake na kumpa tuzo ya 2014 National Geographic Buffett For Leadership in Conservation.
Professor Benezeth Mutayoba , Profesa chuo kikuu cha Sokonne na makamu mwenyekiti wa Tanzania Elephant Protection society katika picha ya pamoja na maafisa Ubalozi  wa Tanzania nchini Marekani siku alipotembelea Ubalozi huo kutoka kushoto ni Afisa Switebert Mkama, Professor Benezeth Mutoyoba, Mkuu wa Utawala na Fedha Mama Lily Munanka Afisa Paul Mwafongo na Amon Mutayoba mtoto wa Profesa Benezeth Mutayoba aliyemsindikiza baba yake kwenye tuzo hiyo.

MAMA SALMA KIKWETE ATEMBELEA BANDA LA NHIF KIGOMA

0
0
Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete akimsikiliza kwa makini Ofisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Dr. Emmanuel Francis wakati akitoa taarifa ya huduma zilizotolewa na Mfuko katika maadhimisho ya uchangiaji damu mkoani Kigoma, pembeni ni Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dr. Kebwe S. Kebwe.
Baadhi ya Wananchi wa Mkoa wa Kigoma waliojitokeza kwenye siku ya Uchangiaji Damu.

Job opportunity

0
0
BM Hair & Beauty Clinic Ltd, is looking for office manager to manage its growing business and look on the day to day operations of the company.

Quarification
Minimum of diploma in either of the folliwing disciplin bisiness administration, law, public administration, political science and account

Experience.
One year experience in the relevant field.

Remuneration
Competitive package will be offered to successfull candidate.

Deadline will be on 24th june 2014. Only shortlisted candidate will be cantacted.

Send your application to
Managing director
BM Hair & Beauty Clinic Ltd
Box  78586
Dsm , Tel +255 784 259967

PPF YATOA HUDUMA Wiki ya Utumishi Mnazi Mmoja Dar

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Utawala Bora), George Mkuchika, akisalimiana na Meneja Kumbukumbu wa Mfuko wa Pesnheni wa PPF, Gladness Mteta, alipotembelea banda la PPF, kwenye maonyesho ya wiki ya Utumishi yaliyoanza jana kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika, akimsikiliza Meneja Kumbukumbu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Gladness Mteta (Wakwanza kushoto), alipotembelea bandfa la Mfuko huo kwenye ufunguzi wa Wiki ya Utumishi kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Jumatatu Juni 16, 2014
Maafisa wa PPF wakihudumia wateja kwenye maonyesho ya wiki ya utumishi kwebnye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
Maafisa wa Mfuko wa Pesnheni wa PPF, wakiongozwa na Meneja wa Kumbukumbu, Gladness Mteta (Wapili kushoto), Sereki Michael (Wakwanza kushoto), Paulina Msanga na Nelusigwa Mwalugaja, wakisubiri kuhudumia wateja kwenye banda lao wakati wa ufunguzi wa wiki ya Utumishi kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, Juni 16, 2014.

MAKAMU WA RAIS AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA NCHI ZA G77+CHINA NCHINI BOLIVIA

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza katika mkutano wa maadhimisho ya miaka 50 ya nchi za G77 na China, uliofanyika jijini Santa Cruz, Bolivia jana Juni 15, 2014.
Sehemu ya washiriki na wawakilishi wa viongozi wa mataifa mbalimbali katika mkutano huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (katikati) akiwa na baadhi ya Viongozi kutoka mataifa mbalimbali wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo yaliyofanyika juzi usiku Juni 14, jijini Santa Cruz, Bolivia.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kushoto mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wenzake waliohudhuria na kuzungumza katika mkutano huo wa sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya nchi za G77 na China uliofanyika jana Juni 15, 2014, jijini Santa Cruz, Bolivia. Picha na OMR.

Na Mwandishi Maalum, Santa Cruz, Bolivia
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal amezitaka nchi wanachama wa G77+China, kuhakikisha zinaboresha kilimo ili ziwe na hifadhi ya kutosha ya chakula kwa wananchi wake. 

Akihutubia mkutano wa mwaka kwa nchi za G77+China ambao pia ni kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya umoja wa nchi hizi, unaofanyika jijini St Cruz De Sierra, Dkt Bilal alisema nchi za umoja huu zina maeneo mazuri kwa kilimo na hivyo ni muhimu kuyatumia maeneo haya katika kuzalisha chakula kwa lengo la kuhifadhi na kuwa na usalama wa chakula nyakati zote.

Dkt. Bilal alisema, nchi hizi kwa pamoja zinahitaji kuwa na kauli moja kuhusu masharti yanayowekwa na nchi kubwa hasa katika kilimo na kuelezea kuwa ili mafaniio makubwa yapatikane, lazima uwepo uwekezaji wa ndani katika kilimo sambamba na serikali za nchi hizi kuchangia shughuli za uzalishaji ili kuwa na kilimo chenye tija kwa wakulima na kinachoweza kuchangia usalama wa chakula.

Kuhusu suala la mazingira, Mheshimiwa Makamu wa Rais aliwaeleza wajumbe wa G77+China kuwa, maazimio yaliyofikiwa Rio+20 na mapendekezo kuhusu ‘Kesho tunayoitaka’ yanazihitaji nchi hizi kupaza sauti zake kwa pamoja kuhusu kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwani suala hili kwa sasa haliwezi kutatuliwa na nchi moja bali linahitaji nguvu ya kila mtu duniani.

Makamu wa Rais alifafanua kuwa bila kuwa na mazingira bora maendeleo endelevu yatabakia ndoto na pia kufanikisha Malengo ya Milenia kwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa itakuwa vigumu kama suala la mazingira litaachwa kwa kila nchi kufanya inavyotaka.

“Kundi hili lina kazi kubwa iliyo mbele yetu na hasa kuhusu malengo mapya ya maendeleo baada ya kukamilika kwa muda wa Malengo ya Milenia mwakani. Tunahitajika kubuni njia za kuzipatia nchi zetu maendeleo katika Nyanja za uchumi, kijamii na mazingira ili tufanikiwe vema,” alisema Mheshimiwa Makamu wa Rais.

Katika hotuba hiyo Mheshimiwa Makamu wa Rais pia alizungumzia kuhusu umuhimu wa nchi hizi kuweka msisitizo wa kuwapa wananchi maji safi na salama, umuhimu wa kuwa na nishati inayotosheleza matumizi ya uzalishaji, uwepo wa huduma bora za afya na elimu ili kupiga hatua kwa haraka baina ya wananchi wa nchi hizi. “Nafahamu kufanikisha haya yote ni kazi kubwa lakini hatuna muda wa kusubiri. Ni lazima tufanye kazi ili kubadili hali iliyopo,”alifafanua.

Mkutano huo ambao umekamilika jana kwa mwenyeji wake Rais Evo Morales kuwashukuru wanachama wa G77+China walioweza kushiriki mkutano huo, pia ulionesha nia kwa wanachama wa nchi hizi kutafuta majibu ya changamoto ya ukosefu wa ajira unaokabili wananchi wengi wa nchi hizi. Viongozi wengi walisisitiza kuwa, suala la ajira hasa kwa vijana linatakiwa kutazamwa upya na hasa ukizingatia rasilimali zilizopo katika nchi za G77+China ili zitumike katia kutengeneza ajira mpya zitakazoweeza kusaidia kuboresha maisha ya watu wa nchi hizi kwa miaka mingi ijayo. 
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live




Latest Images