Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live

REGIONAL CHAMPIONS LEAGUE (RCL) 2014


MISA YA MSIBA DMV

$
0
0
Dada Sarah Mushi wa Ashburn, VA anapenda kuwajulisha na kuwaomba mjumuike nae katika misa ya mpendwa mama yake mzazi Mrs. Aruken Geoffrey Mushi itakayofanyika Jumamosi June 7, 2014 katika kanisa OUR SAVIOR'S WAY LUTHERAN CHURCH liliko Ashburn.

Our Savior's Way Lutheran Church,
43115 Waxpool Rd,
Ashburn,
VA 20148
Ibada itaanza saa 6:00 mchana.
Kwa taarifa zaidi unaweza kuwasiliana na
David Kisanga: 703-932-0540
Mercy Ligate: 240-461-9477.
Bwana ametoa, Bwana ametwaa na jina lake lihimidiwe - AMEN

VITUO VYA MWENGE, MAKUMBUSHO KABLA NA BAADA YA MABADILIKO LEO

$
0
0

 Mwenyekiti wa soko la Makumbusho, Bi Mary John (kulia), akiongea na Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Kinondoni, SP Awadhi  Haji (kati), na Mkuu wa Usalama Barabarani, Kituo cha Kinondoni, Solomon Mwangamilo (kushoto).
  Huduma ya usafiri ikiendelea kama kawaida eneo la Makumbusho
 Stendi ya Makumbusho kabla haijaanza kutumika.
  Muonekano mpya wa kituo cha Mwenge baada ya kuhamishwa.
Picha na GPL

TANZANIA NA QATAR ZASAINI MKATABA WA USHIRIKIANO WA KAZI NA AJIRA

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira wa Qatar wakisaini Mkataba wa Kazi ambao unalenga kuwawezesha Watanzania hususan vijana wenye ujuzi/taaluma katika fani mbalimbali kupata fursa za ajira na kazi za staha, ujira stahiki, kujiunga na hifadhi za jamii nchini Qatar.  Mkataba huo pia unazingatia sheria na viwango vya kazi kulingana na Mikataba ya Kimaataifa ikiwemo ya Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira wa Qatar mara baada ya kusaini Mkataba wa Kazi kati ya nchi hizo mbili. Kulia ni Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo  ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mazungumzo yakiendelea.

UHURU KWA VYOMBO VYA HABARI UNA I "SHAPE" JAMII ASEMA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII-NYARANDU

$
0
0
Video imepigwa na Dixon Busagaga wa 
Globu ya Jamii aliyekuwa jijini Mwanza.

DKT. BILAL AZINDUA KITUO CHA TIBA, UCHUNGUZI NA MAFUNZO YA MAGONJWA YA SARATANI, MATUMBO NA INI UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI CHAFUNGULIWA MUHIMBILI

$
0
0
Kituo cha uchunguzi na mafunzo ya magonjwa ya saratani, matumbo na ini Ukanda wa Afrika Mashariki kimefunguliwa rasmi mwishoni mwa juma. Sherehe hizo zilifanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili mwishoni mwa juma ambapo Mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Fuatilia katika picha matukio wakati wa ufunguzi.
Description: DSC_1474
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal akipongezana na Profesa Meinrad Classen wa Chama cha Madaktari wa Matibabu ya Mfumo wa Chakula ya Ujerumani ambaye alisaidia kutafuta fedha za kujenga na kuweka vifaa tiba vya kituo hicho kutoka Kampuni ua Else Kroner Fresenius ya nchini Ujerumani  baada ya kufungua rasmi kituo hicho.
Description: DSC_1477
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal
akisaini kitabu cha wageni mara tu baada ya kufungua kituo hicho.
Description: DSC_1482
Dkt. John Rwegasha, Bingwa wa Magonjwa ya Matumbo na Ini akitoa ufafanuzi kwa  Makamu wa Rais, Dkt. Bilal
Description: DSC_1501
Dkt. Edwin Masue Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani akitoa maelezo kwa Dkt. Bilal kuhusu matumizi ya kifaa cha kufanyia uchunguzi.

UPDATES ZA MSIBA WA GEORGE TYSON

$
0
0
Mwili wa Marehemu George Tyson (pichani) utapelekwa nyumbani kwa marehemu Mbezi Beach (eneo la Makonde) kesho Jumanne Juni 3 kuanzia majira ya saa kumi jioni kwa ajili ya kuaga.
 
Mwili utakuwepo nyumbani hapo mpaka siku ya Jumatano Juni 4,ambapo mwili utapelekwa kwenye viwanya vya Leaders Club,Kinondoni kwa ajili ya shughuli ya kuaga mwili na ibada fupi.

Baadae mwili utapelekwa kwenye Uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere tayari kwa kusafirishwa kwenye jijini Nairobi nchini Kenya kwa mazishi.

Tutaendelea kuwaletea taarifa kadri zitakavyokuwa zikitufikia.

introducing Mzazi Montana's 1st solo project out of Chikwaso Family


Najua wajua ya Capt. Gardiner G. Habash kuanza hivi karibuni ndani ya Michuzi TV - kaa chonjo

$
0
0
Hiki ni kipindi kingine tena kitachokujia hivi punde kupitia MICHUZI TV, kama ulivyoambiwa hapo. Usikonde. Show hii na nyingine nyingi za kusisimua utazipata kirahisi sana kiasi utashangaa. Kaa chonjo, mboga ipo jikoni - karibu itaiva. We kaa mkao wa kula tu...

mama mzazi wa mwanalibeneke Kazikupenda "KK" Chale afariki dunia leo

$
0
0
Mdau Kazikupenda Kk Chale anasikitika kutangaza kifo cha mama yake mzazi Bi.Fides Chale (pichanii) kilichotokeo ghafla leo huko Nyumbani kwake Ubungo Msewe.
Mipango ya mazishi inaendelea nyumbani kwa mwanae, Ubungo-Msewe, Dar. Maziko yanatarajia kufanyika Dar. Taarifa zaidi zitotelewa baadae.
Bwana ametoa, Bwana ametwaa 
jina la Bwana Lihimidiwe - Amen

KK anaendesha blog ya Tembea Tanzania BOFYA HAPA

KHITMA YA MAREHEMU AMINA ZAHRA MTENGETI KUSOMWA KESHO

$
0
0

Asalaam aleykum. 
Khitma ya wanawake ikiwa ni Duaa kwa marehem AMINA ZAHRA MTENGETI itasomwa kesho Tarehe 3 JUNE, saa 10 alasiri eneo la REGENT ESTATE, Mlingotini, jijini Dar es salaam,  nyumbani kwa Hajjat Mwantumu MALALE.

Wote mnakaribishwa

TANZIA

$
0
0
MAREHEMU REDEMPTA 
KATONDAABELA (MAMA RWEKAZA)

Familia ya Prosper Mutafurwa wa Mtaa wa Mwale, Tandika Maguruwe, Dar es salaam. Inasikitika kutangaza kifo cha Mke wake mpendwa Redempta KatondaAbela ai Mama Rwekaza (Pichani) kilichotokea alfajiri ya Jumapili tarehe 01/06/2014 akiwa usingizini.
Habari ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki wote popote walipo.
Mipango ya mazishi inafanyikia Nyumbani kwa Mume wa marehemu Tandika Dar es salaam.
Mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa siku ya Jumatano tarehe 04/06/2014 kwenda Katoke, Buyango, Kiziba, Bukoba na mazishi yatafanyika Siku ya Ijumaa tarehe 06/06/2014 huko huko Katoke,Buyango, kiziba, Bukoba.
Glob ya Jamii  inatoa  pole kwa 
familia nzima, ndugu, jamaa na marafiki wote

BWANA AMETOA NA BWANA 
AMETWAAJINA LAKE NA LIHIMIDIWE
AMEN

Tigo enters new partnership with DTBi and COSTECH to promote ICT and create youth employment in the country

$
0
0
 Eng Mulamula CEO of DTBi making welcome remarks
 Dr Hassan Mshinda DG of Costech making a statement.
 Mr Diego Gutierrez GM of Tigo making a statement.
 Hon Minister Makame Mbarawa making his speech.
 Eng Mulamula & Mr Gutierrez sign the MoU
Handshake after signing MoU between Tigo & DTBi

DStv Rewards Customers over Tshs 26m/-

$
0
0
Wateja wa DStv walioshinda malipo ya mwezi ya mwaka mzima wakipongezwa na Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (kulia) na Operations Manager wa kampuni hiyo Ronald Shelukindo (Kushoto).
DStv, the leading pay television service has awarded its customers over Tshs 26,000,000 worth of subscription, in a campaign aimed at thanking and rewarding subscribers for their sustained loyalty and support. The campaign dubbed DStv Rewards has given out free annual subscriptions to customers who remained connected uninterrupted between January and March 2014.

In a brief handover ceremony held at DStv Offices Oysterbay, Public Relations Manager of MultiChoice Tanzania Barbara Kambogi said that “the DStv Rewards Campaign was open to subscribers on each of our five bouquets Premium, Compact Plus, Compact, Family and Access, all a customer had to do was to ensure they paid their subscription on time and automatically were entered into an electronic draw.

Commenting further was MultiChoice Tanzania General Manager, Peter Fauel: We are delighted to award our loyal subscribers and recognize their contribution towards our business. This is our way of thanking them. DStv has without a doubt the best programming be it in sports, movies, kids, news, lifestyle, documentary and music.


He further continued “this is an exciting period for our customers especially with the World Cup being around the corner. Our winners will be able to watch in-depth coverage of the World Cup through the dedicated SuperSport channels. We congratulate our winners and urge others who are not connected to take advantage of our hardware special offer of fully installed DStv at just Tshs 129,000.

TAASISI YA FARIDA FOUNDATION KUFANYA UZINDUZI TAREHE 28/06/2014

$
0
0


 Taasisi ya Faridas foundation inatarajia kufanya uzinduzi wake rasmi siku ya tar 28/6/2014 siku ya jumamosi katika ukumbi wa crystal hall, blue pearl hotel, ubungo plaza kuanzia saa 6 hadi 12 jioni. 
Katika siku hyo taasisi itatoa misaada mbali mbali kwa walemavu ikiwemo baiskeli za walemavu, vyerehani, vifaa vya shule na vifaa vingine muhimu kwa walemavu ukiwa kama mdau au mtanzania unayeguswa na walemavu na ungependa kuhudhuria siku hyo maalumu kadi zinapatikana kwa mchango wa shilingi laki moja na kuendelea hii ikiambatana na chakula cha mchana vinywaji na burudani mbalimbali pia utakuwa umesaidia kuongeza idadi ya vifaa vitakavyotelewa kwa walemavu mbali mbali. Kutoa ni moyo sio utajiri. 
Endapo una kampuni au ungependa kushiriki kama kampuni au taasisi kwa kudhamini pia nafasi bado zipo wazi wasiliana nasi kupitia +255715186262 au email faridasfoundation@gmail.com

MBUNGE WA JIMBO LA SIMANJIRO,OLE SENDEKA ALIVYOUNGURUMA MERERANI

Polisi Feki watiwa mbaroni mkoani Iringa

$
0
0

Kamanda wa  polisi mkoa wa Iringa,Ramadhan Mungi akiwaonyesha maaskari  feki ambao  walikuwa wakifanya utapeli katika mikoa ya Iringa na Morogoro ,kulia ni Bazil Nyakunga ambae ni mwalimu akiwa na sare za polisi na katikati ni bossi wake Godlack Mbehale.
Askari polisi Mkoani Iringa (kushoto) akiwa na maaskari  feki katika ofisi ya kamanda wa polisi  leo 


Na Francis Godwin,Iringa

MATAPELI washindwa  kubaki njia  kuu sasa waanza  michepuko  mipya ni baada ya jeshi la  polisi mkoa  wa Iringa kumkamata  mwalimu aliyejifanya askari akiwa na fullu kombati za jeshi la polisi na  bossi wake aliyevalia kiraia ambae pia ni  feki  na ni  mmiliki wa studio eneo la Kihesa mjini hapa.

Upo usemi  usemao  kuwa usiombe  likukute usilo litegemea kukukuta katika maisha yako na ukipenda kudanganya uwe tayari kudanganywa  ,hakuna asiyepata  kusikia ama kusoma habari kuhusu utapeli  unaoendelea hapa nchini kwa  watu wa kada mbali mbali na mazingira  yanaonyesha matapeli hawa  siku  zote ni watu  wanaopenda wengine yawakute na sio  wao na hata kupenda kudanganya na sio kudanganywa kama ambavyo mwalimu huyo Bazil Nyakunga (20) ambae anatuhumiwa  kutapeli  wazazi wengi Iringa na Morogoro ambao  wanataka  watoto wao kwenda kusomea uaskari .

Mwalimu Nyakunga  akiwa na bossi  wake  feki Godlack Mbehale (21) walijikuta matatani kwa  kukutwa na wasilotegemea  kulipata  baada ya  jeshi la  polisi kuweka mtego kufuatia wananchi wengi kufika  polisi  kulalamikia utapeli huo wa  ajira  kwa vijana  wao katika  jeshi la  polisi.

Ramadhan Mungi ni kamanda  wa  polisi  wa mkoa  wa Iringa alilitonya gazeti  hili kuwa jeshi  lake  lilipopata stori   hiyo ya utapeli  waliweka mtego eneo la Ipogolo ambapo askari huyo feki alikuwa amepiga kambi la kitapeli kwa  kuwasanua mavumba wazazi wenye uchu wa  watoto  wao kuwa mageda (ma Askari).

Alisema  kuwa  vijana  hao ambao  mmoja  Nyakunga ambae ni mkazi wa Ilula Mtua katika  wilaya ya Kilolo mkoani Iringa ni kijana  aliyepata  kusoma kozi ya ualimu mkoani Shinyanga  na kuwa ndie  alikuwa akijifanya na askari  polisi na muda  wote  alikuwa akivaa sare za jeshi  hilo.

Mungi  alisema  kuwa  kijana  huyo na mwenzake  wamepata  kuwaliza  watu wengi  sana Iringa na Morogoro na  kuwa mtu wa mwisho  wamemliza kiasi cha Tsh 900,000 na kuwa njia  wanayotumia ni Nyakunga kama askari  baada ya  kumpata  mazazi na mtu mwinye uhitaji na ajira ya  polisi amekuwa akipiga simu kwa boss  wake Bw Mbehale na kuiweka simu hiyo katika mfumo wa Laudi spika ili mtu anayetapeliwa  kupata  kusikiliza vema mazungumzo hayo.

“ Nyakunga kama askari  feki  baada ya  kumpata mteja  wa kumtapeli amekuwa akiweka simu yake katika  sauti  kubwa na huyo boss  wake amekuwa akisikika akipanga gharama za mtapeliwa  kulipia na baada ya  kutoa  pesa  wamekuwa  wakiingia mitini kwa kumta ahadi feki….mfano anapopiga simu anajifanya samahani boss naomba maelekezo ya mwisho huyu mzazi /kijana anataka kazi anapaswa kutimiza nini kwa  sasa kabla ya kuitwa katika usaili ”.

Hata  hivyo kamanda Mungi alisema  kuwa ni  vema  wananchi kuchukua  tahadhari juu ya utapeli huo na kuwa kazi za polisi kwa  sasa haziingizwi kwa mtindo huo na kuwa jeshi  hilo lina utaratibu wake wa kuingiza  vijana ikiwa ni pamoja na kuwachucha toka  sekondari  kwa kujaza fomo huku wale  wa elimu ya  juu  upo utaratibu na  wale  wanaochukuliwa kwa utaalam  wao pia  wanautaratibu wao  na si vinginevyo.

Alisema  kuwa  hakuna  usaili  wa askari  unaofanywa  mitaani ama  wilayani  hivyo vijana  hao  walikuwa  wakifanya utapeli  na ni vema  wananchi  kuchukua tahadhari  kubwa .

Pia  alisema jeshi lake  linafanya uchunguzi  ili  kubaini eneo  ambalo matapeli hao  walipata  sare  hizo za  jeshi la  polisi na mbinu  waliyotumia  kuzipata sare  hizo ikiwa ni pamoja na kuwafikisha  mahakamani.

Hata  hivyo kwa  upande wao matapeli  hao  walidai kuwa   ni kweli  wanafanya kazi na ualimu na mmoja na mmiliki wa  studio eneo la Kihesa mjini  Iringa na  kuwa sare  hizo  walizipata kutoka kwa rafiki yao ambae ni askari polisi aliyewatuma kuzifikisha kwa ndugu yao askari .

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI SHEREHE ZA MAKABIDHIANO YA URAIS NCHINI MALAWI

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akimpongeza Rais mpya wa Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika  baada ya Rais huyo mpya wa Malawi kukabidhiwa madaraka  jijini Brantyre kwenye hoteli Sunbird. Baada ya kukutana viongozi hao walipata fursa ya kuzungumzia masuala la kidiplomasia baina ya nchi hizi mbili na kukubaliana kuendelea kuwa na mahusiano mema kama nchi zinazoishi ndugu na jirani. Picha kwa Hisani ya Ikulu ya Malawi
Makamu  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DkT. Mohammed Gharib Bilal leo Jumatatu Juni 02, 2014 ameshiriki katika sherehe za kukabidhi madaraka kwa Rais mpya wa Malawi Profesa Arthur Peter Mutharika katika sherehe zilizofanyika kwenye uwanja wa Kamuzu Banda jijini Blantyre. Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Rais wa Botswana sambamba na wawakilishi wa nchi za Zimbabwe, Msumbiji, Afrika Kusini na nyinginezo.
Akihutubia baada ya kukabidhiwa sime ambayo ni ishara ya kuwa kiongozi wa watu wa Malawi, Rais Mteule Mutharika alisisitiza kuwa, katika kipindi cha utawala wake atahakikisha kuwa anaifanyia makubwa Malawi sambamba na uhakikisha kuwa anaifanya Malawi itimize majukumu yake ya kimataifa kufuatia kutambua kuwa kujitenga kunaweza kuifanya Malawi kutonufaika na fursa zilizopo duniani.
“Nchi hii ipo katika dunia na siyo rahisi tena kuwa na fikra kwamba Malawi inaweza kubaki peke yake kama kisiwa. Tunahitaji kuwa na wenzetu wa kusaidia maendeleo ya Malawi. Tunawahitaji wahisani toka Kusini ama Mashariki, tunayahitaji mataifa tajiri na mataifa yanayoendelea. Tutafanikiwa sana kama tutaendeleza urafiki kwa wote. Tufanye hivi bila kujali kuwa sisi ni taifa kwani hali ya sasa inahitaji kila mmoja wetu kushirikiana na mwenzake,” alisema.
Katika hotuba hiyo pia amesisitiza kuwa kipindi chake cha utawala atajitahidi kukabiliana na rushwa na kwamba hatakuwa na mchezo kwa wala rushwa katika kipindi akiwa madarakani. Pia alisisitiza kuhusu umuhimu wa kuiunganisha Malawi kwa miundombinu bora ili kuboresha maisha ya wananchi sambamba na kusogeza huduma za wananchi karibu.
Rais Mutharika aliapishwa juzi baada ya kuwashinda washindani wake akiwemo Rais aliyemaliza kipindi chake Joyce Banda ambaye hata hivyo hakuweza kutokea katika sherehe hizi za kukabidhi madaraka. 

Akizungumzia suala la kutohudhuria kwa Rais  Joyce Banda, Rais Mteule Mutharika alisema alitegemea Rais Banda kuwepo lakini hakufika na yeye anatambua kuwa wakati wa uchaguzi kulikuwa na tofauti baina yao lakini kwa sasa uchaguzi umeisha na amesahau yaliyopita ili kuanza ukurasa mpya wa kuijenga Malawi. Katika shughuli hiyo pia Rais wa zamani wa Malawi Kamuzu Banda alihudhuria.
Makamu wa Rais Dkt. Bilal na msafara wake walitarajiwa kurejea nyumbani leo hii Jumatatu mara tu baada ya kukamilika kwa kazi hii ya makabidhiano.

KATIBU MKUU WA CCM,AKUTANA NA MCHIMBAJI MDOGO WA MADINI,MERERANI,SUZIE DIDAS KENEDY.

BALIMI EXTRA LAGER KUDHAMINI MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI 2014

$
0
0
Meneja wa Bia ya Balimi Extra Lager(kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu udhamini wa mashindano ya ngoma yajulikanayo kama “Balimi Ngoma Festival 2014” TBL Dar es Salaam.Kushoto ni Meneja matukio wa Taifa TBL, George Mombeki.
Meneja matukio wa Taifa TBL, George Mombeki(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu udhamini wa mashindano ya ngoma yajulikanayo kama “Balimi Ngoma Festival 2014” TBL Dar es Salaam.
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live




Latest Images