Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live

Brian Tracy Talk about His Leadership Seminar in Tanzania this June


SSRA yawapa somo wananchi wa Jiji la Mwanza

$
0
0
 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,Mhandisi Warioba Sanya, akifungua semina ya Mamlaka ya Uthibiti wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii Nchini (SSRA) inayoendeshwa kwa Wananchi wa Jiji la Mwanza juu ya umuhimu wa Wananchi kujiunga na Mifuko ya Hifadhi za Jamii hapa nchini.Semina hiyo imefanyika hivi karibuni kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
  Sehemu ya Wajumbe wa Semina hiyo wakifatilia mambo mbali mbali.
Picha ya Pamoja baada ya Kufumguliwa na Semia hiyo.

HAFLA YA KUZAWADIA WACHEZAJI WA BWAWA LA MAINI

$
0
0
 Kikosi cha Bwawa la Maini kwenye mnuso wa kuzawadia wachezaji bora uliofanyika usiku huu katika hoteli ia Hilton Liverpool na kuhudhuriwa na wapenzi na wanachama kutoka kila pembe ya dunia ikiwemo Tanzania ambayo iliwakilishwa na viongozi wa The Kop In Tanzania
 Sehemu ya wageni kwenye mnuso huo katika hoteli ya Hilton Liverpool
 Katibu wa The Kop in Tanzania Issa Batenga akiwa na kocha wa Bwawa la Maini Brendan Rodgers kwenye mnuso huo usiku huu hoteli ya Hilton Liverpool
Katibu wa The Kop in Tanzania Issa Batenga katika mnuso huo

SHINE A LIGHT 3 ON 3 CHARITY BASKETBALL TOURNAMENT

$
0
0
Shine A Light :This is a group founded by KCMC (Kilimanjaro Christian Medical College)students in June 2010 aimed at helping children who are less fortunate (orphans ,street children etc ) achieve their dreams, have a chance at life and a bright future.
 If you feel you can participate or support us in any way or means (currently based in Moshi, Tanzania).
 Contact us: email-sal.kcmc@gmail.com 
 OR VISIT OUR WEBSITE www.shine-a-light.or.tz 
 SHINE A LIGHT HOSTED A 3 ON 3 CHARITY BASKET TORUNAMENT ON THE 3RD OF MAY 2014 AT THE KCMC HOSPITAL BASKETBALL GROUNDS!!! 128,000 Tsh was raised !!!We would like to thank all those who participated!!!
NO TO RACISM !!!!
LAYUP...!
Coming through....
In action...

TUNAWEZA KUJIFUNZA KUTOKA UHISPANIA- BALOZI MANONGI

$
0
0
 Na Mwandishi Maalum 
 Tanzania inaweza kuongeza zaidi kasi yake ya ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi wake, kwa kujifunza uzoefu wa nchi nyingine marafiki kama vile Uhispania. Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, ameyasema hayo siku ya jumanne, wakati alipokuwa akichangia majadiliano ya mada kuhusu “Kuendelea kwa Pamoja: misaada ya maendeleo ( ODA), biashara na uwekezaji”. 
Muwasilishaji wa mada hiyo alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Uhispania, Bw. Jose Manuel Garcia- Margallo Y Marfil, alipokutana na kubadilishana mawazo na Balozi wanaoziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa. 
Balozi Manongi amesema katika majadiliano hayo, kwamba Tanzania kama nchi inaaamini kuna maeneo ambayo inaweza kujifunza zaidi na kutumia uzoefu wa Hispania katika kusukuma mbele kasi ya ukuaji wa uchumi wake na maendeleo. 
 Akabainisha kuwa maeneo ambayo Tanzania kwa kushirikiana na Uhispania inaweza kujifunza na kubadilishana uzoefu ni uwekezaji, biashara na uvutiaji wa misaada ya maendeleo. 
“Tanzania inapenda kukushukuru kwa kuadaa mkutano huu na fursa hii ya kubadilisha mawazo kuhusu dhana nzima ya maendeleo ya pamoja, misaada ya maendeleo, biashara na uwekezaji
“Maeneo haya ni muhimu sana kwetu na nina amini tunaweza kubadilisha uzoefu na kujifunza namna ambavyo nyinyi mumefanikiwa” akasema Balozi.
Aliongeza kwamba hata katika majadiliano yanayoendelea hivi sasa kuhusu ajenda mpya za maendeleo endelevu baada ya 2015, maeneo yanayotiliwa mkazo mkubwa pamoja na mambo mengine , ni hayo ya uwekezaji, biashara na misaada ya maendeleo. 
“ Ni kwa kutumia fursa zilizopo za uhusiano baina ya nchi na nchi na ushirikiano katika ngani ya kimataifa, tunaweza kuendelea kwa pamoja”, akaongeza Balozi Manongi 
Aidha Mwakilishi huyo wa Tanzania kama ilivyokuwa kwa wawakilishi wengine waliochangia majadiliano yao, akatumia fursa hiyo kuishukuru Uhispania, kwa uamuzi wake wa kuanzisha Mfuko wa Maendeleo Endelevu kwa ubia na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa ( UNDP). 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Uhispania, pamoja na mambo mengine, aliwaeleza mabalozi kwamba, nchi yake ambayo ilikumbwa na mtikisiko mkubwa wa kuyumba kwa uchumi angalau imeanza kutengemaa kwa kuchukua hatua kadhaa wa kadhaa, ingawa amekiri kwamba safari bado ni ndefu. 
Baadhi ya mambo ambayo anasema serikali yake iliamua kuyafanyia kazi kwa kuyapa umuhimu ni pamoja na, kufungua milango ya uwekezaji ndani na nje ya nchi yake, kukuza na kupanua biashara na upatikanaji wa ajira kwa vijana wao. 
Akabainisha kwamba kama si kupanua wigo wa biashara, kuongeza kasi ya uwekezaji ndani na nje, Uhispania isingeweza kujifunia mafanikio iliyonayo hivi sasa ikiwa ni pamoja na kuyatafsri mafanikio hayo katika ushirikiano wa kimaendeleo. 
 Na kwa sababu hiyo akasema nchi yake imekuwa mstari wa mbele katika utoaji wa misaada ya maendeleo kwa nchi mbalimbali yenye uhusiano nao ikiwa ni pamoja Umoja wa Mataifa. Akatoa mfano kwa kusema kati ya 2007 na 2012 nchi yake imechangia zaidi ya dola za kimarekani 30 billion kwenye eneo la maendeleo, misaada ambayo ilitolewa kupitia uhusiano baina yake na nchi nyingine na katika ngazi ya kimataifa. 
Ambapo Afrika Kusingi mwa Jangwa la Sahara ilipata jumla ya dola 4 billioni kama msaada wa maendeleo. Kuhusu uwekezaji akasema nchi yake inamtaji wa dola bilioni 640. Vile vile Uhispania ni nchi ya saba kama msafirishaji wa huduma katika nchi mbalimbali na ni ya 17 kama msafirishaji mkubwa bidhaa. 
 Akasema ni katika kuamini kwake katika dhana nzima ya ushirikiano wa kimaendeleo ndio maana nchi yake licha ya kutoa misaada kwa nchi moja moja na katika ngazi ya Umoja wa Mataifa, ndiyo maana imeamua kwa kushirikiana na UNDP kuunda mfuko wa maendeleo endelevu kama ilivyofanya kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Millenia ( MDGs). 
Akasisitiza kwamba nchi yake imeamua kuunda mfuko huo kwa kile inachoamini kwamba utakuwa daraja au kiungo kati ya Malengo ya Maendeleo ya Millenia ambayo yanaishia ukiongoni, na malengo mapya ya maendeleo endelevu.
Sehemu ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa, wakati wa majadiliano  kuhusu dhana ya  maendeleo ya pamoja,  uwekezaji, biashara na misaada ya maendeleo,  majadiliano hayo yaliongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Uhispania, Bw.Jose Manuel Garcia- Margallo Y Marfil ambapo pia alielezea nafasi ya nchi yake katika  kukuza  ushirikiano na  misaada  ya kimaendeleo  

ngoma azipendazo ankal

$
0
0
Mambo ya "Night Nurse" na Gregory Isaacs

Visit Mikono Speakers at BuildExpo Africa 2014

$
0
0
Tickets for the High Performance 
Leadership seminar are quickly selling out...
Visit Mikono Speakers booth at the BuildExpo Africa 2014 at Mlimani City Conference Centre from 8th to 10th May 2014 and get your ticket at 15% discount. Do not miss out on this once-in-a-lifetime opportunity to witness the legendary Brian Tracy and Azim Jamal live in Dar Es Salaam
For details:
 |Email info@mikono.biz 

KINANA KUANZA ZIARA YA SIKU 26 TABORA, SINGIDA NA MANYARA

$
0
0
*NI YA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM 
*KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI 
* KUKAGUA MAANDALIZI YA CHAMA
YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye  akiwa na baadhi ya waandishi wa habari watakaoungana na Katibu Mkuu wa CCM, Andulrahman Kinana, katika ziara ya siku 26 katika mikoa ya Tabora, Singida na Manyara itakayoanza kesho katika jimbo la Igunga mkoani Tabora. Nape alipiga picha na na waandishi hao leo baada ya kuzungumza nao kuhusu ziara hiyo, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba , Dar eSalaam. Kulia na kushoto ni baadhi ya magari maalum yatakayotumiwa na waandishi hao. 

RAIS KIKWETE AWASILI ABUJA, NIGERIA, KUHUDHURIA MKUTANO WA UCHUMI DUNIANI (WORLD ECONOMIC FORUM)

$
0
0
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea shada la maua mara baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Nnamdi Azikiwe jijini Abuja, Nigeria, usiku wa Mei 6, 2014 ambako atahudhuria Mkutano wa siku 3 wa Uchumi Duniani kuhusu Afrika (World Economic Forum for Africa).
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Waziri wa Nishati wa Nigeria Profesa Chinedu Ositadinma Nebo na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Mhe Daniel Ole Njoolay katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Nnamdi Azikiwe jijini Abuja, Nigeria, usiku wa Mei 6, 2014 ambako atahudhuria Mkutano wa siku 3 wa Uchumi Duniani kuhusu Afrika (World Economic Forum for Africa).
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay, Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdallah Kigoda na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Mhe. Mohammed Aboud Mohammed baada ya kuwasili jijini Abuja, Nigeria, usiku wa Mei 6, 2014 ambako atahudhuria Mkutano wa siku 3 wa Uchumi Duniani kuhusu Afrika (World Economic Forum for Africa). 

TASAF YAWAFUNDA WATAALAM WA KISEKTA JUU YA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI-PSSN

$
0
0
Mkurugenzi mtendaji wa TASAF, bwana Ladislaus Mwamanga amesema utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya Masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii nchini TASAF utasisimua shughuli za maendeleo kwenye maeneo mbalimbali ya nchi ambako utatekelezwa na hivyo kuwa chachu ya maendeleo na  kuondoa kero zinazowakabili wananchi hususani suala la umasikini.

Bwana Mwamanga amesema hayo jiji Dar es salaam alipofungua  warsha ya wataalamu wa kisekta kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambao sekta zao zinahusika kwa namna moja au nyingine katika utekelezaji wa shughuli za TASAF kwenye maeneo yao.

Mkurugenzi mtendaji huyo wa TASAF amesema kwa kiwango kikubwa  utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya masikini umeanza kutekelezwa kwa mafanikio ambapo mwelekeo umeonyesha kuwa maeneo ambako Mpango huo umefanyiwa majaribio kumekuwa na mafanikio ya kujivunia hususani katika sekta za Elimu, Afya, na hata Lishe kwa kaya ambazo hapo awali hazikuwa na uhakika wa kupata lishe.

Hata hivyo, bwana Mwamanga amewataka wataalamu hao wa kisekta kutumia utaalamu wao ipasavyo ili waweze kuielewa dhana nzima ya Mpango wa kunusuru kaya masikini na kuhakikisha kuwa wanawawezesha wananchi hususani walioko katika kaya masikini ili waweze kuondokana na umasikini.

Mkurugenzi huyo mtendaji wa TASAF pia ametaka mkakati maalum uwekwe ili kuhakikisha kuwa huduma muhimu hususani za upatikanaji wa elimu na Afya  unakuwapo  ili walengwa wa mpango huo waweze kunufaika nazo.

Zifuatazo ni picha za ufunguzi wa warsha hiyo ya wataalamu wa kisekta iliyofanyika leo katika hoteli ya Golden Jubelee jijijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akifungua warsha ya wataalam wa  Kisekta (hawapo pichani) jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi wa Miradi wa TASAF Bwana Amadeus Kamagenge (aliyesimama)akitoa maelezo ya utangulizi katika warsha ya wataalamu wa kisekta   jijini Dar es salaam katikati ni Mkurugenzi mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga  na kushoto kwake ni mkurugenzi wa uratibu wa TASAF  Alphonse Kyariga.
 Mkurugnezi wa uratibu wa shughuli za Muungano katika Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Bwana Issan Ibrahim Mohmond (aliyevaa  koti )akimsikiliza mkurugenzi mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga (hayupo pichani) alipofungua warsha ya wataalam wa kisekta jijijin Dar es salaam  mbele yake ni Mkurugenzi wa Ukaguzi wa TASAF Bwana Christopher Sanga.
Baadhi ya washiriki wa warsha ya wataalamu wa Kisekta wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa warsha ya wataalam wa kisekta iliyotolewa na mkurugenzi mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga(hayupo pichani).
Baadhi ya washiriki wa warsha ya wataalamu wa Kisekta wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa warsha ya wataalam wa kisekta iliyotolewa na mkurugenzi mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga(hayupo pichani).
Mtaalamu wa teknolojia ya habari na mawasiliano ICT wa TASAF Bwana Peter Luanda(wa kwanza  kushoto)na meneja wa uhawilishaji wa fedha Bwana Omar Malilo (mwenye miwani katikati)wakiwa katika warsha ya wataalamu wa kisekta iliyoandaliwa na TASAF jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga (aliyeketi katikati )akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya wataalam wa kisekta  iliyoandaliwa na kwa lengo la kuwaelewesha namna ya utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya masikini nchini unaoratibiwa na Mfukowa Maendeleo ya Jamii TASAF.

KATIBU MKUU WA CCM,KINANA KUANZA ZIARA YA SIKU 26 KESHO, MIKOA YA TABORA, SINGIDA NA MANYARA

$
0
0

  *NI YA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

*KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

* KUKAGUA MAANDALIZI YA CHAMA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye  akiwa na baadhi ya waandishi wa habari watakaoungana na Katibu Mkuu wa CCM, Andulrahman Kinana, katika ziara ya siku 26 katika mikoa ya Tabora, Singida na Manyara itakayoanza kesho katika jimbo la Igunga mkoani Tabora. Nape alipigapicha na na waandishi hao leo baada ya kuzungumza nao kuhusu ziara hiyo, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba , jijini Dar eSalaam. Kulia na kushoto ni baadhi ya magari maalum yatakayotumiwa na waandishi hao.

VIONGOZI WA DINI WAWASILI KUTOKA NCHINI THAILAND

$
0
0
Baadhi ya viongozi wa dini kutoka katika Mikoa ya Lindi na Mtwara wakiwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) kutokea nchini Thailand. Viongozi hao walifanya ziara nchini humo kwa ajili ya kujifunza na kupata uzoefu wa uendelezaji wa sekta ya gesi.
Viongozi wa dini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) kutokea nchini Thailand.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Abdallah Hamis Ulega akizungumza na waandishi wa habari jinsi wananchi wa Thailand walivyonufaika na rasilimali ya gesi.

HIKI NDIO KIPITA SHOTO BABKUBWA KUPITA VYOTE JIJINI DAR

$
0
0
Libeneke la Glogu ya jamii bado linaendelea kukuletea Kipita shoto bora na Babkubwa kupita vyote ndani ya jiji la Dar,kilichopo katika barabara ya Jamhuri mbele kabisa ya Makao Makuu ya Benki ya NMB.kuna fununu kwamba,kipita shoto hiki kinaweza kuwa ndio kipita shoto bora kabisa katika isti afrika mashariki.

DKT. SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI IDARA MAALUM ZA SMZ IKULU ZANZIBAR LEO

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dkt.Ali Mohamed Shein(katikati) akizungumza na Uongozi wa Idara Maalum za SMZ katika mkutano wa utekelezaji mpango kazi wa robo tatu ya mwaka Julai-Machi 2013/2014,katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Unguja leo asubuhi.
Baadhi ya makamanda wa Idara maalum za SMZ wakimsikiliza Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ,Mhe,Haji Omar Kheri (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji mpango kazi wa robo tatu ya mwaka Julai-Machi 2013/2014,mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dkt.Ali Mohamed Shein,katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Unguja leo asubuhi.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.

Dk. Kigwangala aitaka TAMISEMI kuwashirikisha Wananchi kubuni Vyanzo vya Mapato

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dk Hamis Kigwangala amezitaka Sekretarieti za mikoa na halmashauri zote nchini kuhakikisha kwamba inawashirikisha wananchi katika maandalizi ya bajeti kubuni vyanzo vya mapatao.

 Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bungeni leo kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha 2013, mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Kigwangala amesema pia wananchi washirikishwe katika utungaji wa sheria ndogo za ukusanyaji ili kurahisisha zoezi la makusanyo bila manung’uniko.

Amesema ushiriki wa wananchi pia utasaidia katika zoezi zima la kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo hasa pale ambapo Serikali kuu pamoja na Serikali za Mitaa zitakapokuwa zinatoa mchango wake kikamilifu katika miradi husika na hivyo nguvu ya wananchi kutopotea.


President Kikwete has sent a congratulatory message to His Excellency Miloš Zeman, President of the Czech Republic on the occasion his country’s Liberation Day on the 8th May

$
0
0
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency Miloš Zeman, President of the Czech Republic on the occasion his country’s Liberation Day on the 8th May.

The message reads as follows;

“His Excellency Miloš Zeman,
 President of the Czech Republic,
 Prague,
 CZECH REPUBLIC.

Your Excellency,

On behalf of the people and government of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, I wish to convey my sincere congratulations to you, the people and the government of Czech Republic on the occasion of the Liberation Day of Czech Republic.
Tanzania values the close ties of friendship and co-operation and the warm and friendly relations between our two countries and the people.
I am confident that with the good will and understanding on both sides, the bilateral relations between Tanzania and Czech will continue to flourish as both countries pursue the shared ideas and objectives for the benefit of the two countries and peoples.
Please accept, your Excellency, my best wishes for your personal good health and peace and prosperity for the people of Czech Repulic”.
Issued by:  Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation of the United Republic of Tanzania, Dar es Salaam.

7th May, 2014

DKT. BILAL AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA VIONGOZI WA CCM NA WAFANYAKAZI WA KIWANDA CHA MGOLOLO (W) MUFINDI, IKULU DAR

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Viongozi wa CCM Wilaya na Mufindi wlioongazana na baadhi ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha Mgololo, wakati walipofika Ofisini kwa Makamu Ikulu Jijini Dar es Salaam, leo Mei7, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa CCM Wilaya ya Mufindi na baadhi ya wafanyakazi wa Kiwanda cha Mgololo, waliofika Ofosini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Mei 7, 2014 kwa mazungumzo. Picha na OMR

PRESIDENT KIKWETE MEETS FORMER BRITISH PM GORDON BROWN AND MARK SUZMAN OF THE GATES FOUNDATION IN ABUJA, NIGERIA, TODAY

$
0
0
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete shakes hands with Rt. Hon. Gordon Brown (MP), UN Special Envoy for Global Education and Former British Prime Minister in the sidelines of the World Economic Forum on Africa in Abuja, Nigeria, May 7, 2014.


President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete in a bilateral meeting with Rt. Hon. Gordon Brown (MP), UN Special Envoy for Global Education and Former British Prime Minister in the sidelines of the World Economic Forum on Africa in Abuja, Nigeria, May 7, 2014.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete shakes hands with Mr Mark Suzman, President of Global Policy and Advocacy and Country Programmes of the Gates Foundation after holding bilateral talks in the sidelines of the World economic Forum on Africa in Abuja, Nigeria, today May 7, 2014.Photos by State House.

BREAKING NYUZZZ: BASI LA PRINCESS MURO LAPATA AJALI JIONI HII ENEO LA MIKUMI MKOANI MOROGORO

$
0
0
Baadhi ya abiria waliokuwemo kwenye basi la Princess Muro walilokuwa wakisafiri nalo kutoka Mkoani Mbeya kuja jijini Dar es Salaam wakiwa hawajui la kufanya baada ya Basi hilo kupinduka jini hii katika eneo la Hifadhi ya Wanyama ya Mikumi,Mkoani Morogoro.

Twanga Pepeta kuzindua ukumbi wake Ijumaa

$
0
0
Bendi ya muziki wa dansi ya The African Stars ‘wana twanga pepeta’ ijumaa itazindua ukumbi wa kisasa wa burudani na mikutano wa Machinga Lounge uliopo maeneo ya uwanja wa mpira wa wa miguu wa Karume jijini.

Ukumbi huo unamilikiwa na kampuni ya African Stars Entertainment Tanzania (ASET), umetengenezwa  kisasa zaidi kwa lengo la kuwapa burudani mashabiki wa Manispaa ya Ilala, Temeke na Kinondoni kwa mujibu wa mkurugenzi wa Twanga Pepeta, Asha Baraka.

Asha alisema kuwa kwa muda mrefu sasa wakazi wa maeneo ya Ilala hawana ukumbi mkubwa kwa ajili ya shughuli za burudani na yeye kuamua kutengeneza ukumbi huo uliopo eneo maarufu la Machinga Complex.

“Hii ni fursa pekee kwa wadau wa burudani kuzindua ukumbi huo ambao ni wa kisasa, lengo ni kuwapa burudani mashabiki wetu wa maeneo hayo na majirani zake, hasa kwenye ukumbi wa kisasa ambao hata shuguli za mikutano mbali mbali inaweza kufanyika,” alisema Asha.

Alisema kuwa ukumbi huo unauwezo wa kuingiza watu zaidi ya 500 waliokaa kwenye viti na lengo lao kubwa pia kutumika kwa vikundi vingine vya burudani. “Twanga haitakuwa inafanya shoo zake mara kwa mara kwenye ukumbi huu, vikundi vingine, anamuziki wa bongo fleva na taarabu pia wanakaribishwa, kuutumia,” alisema.

Hii ni mara ya pili kwa ASET kumiliki ukumbi ambapo mwanzoni mwa miaka ya 2000 walimiliki ukumbi wa ASET Club (zamani FM Club au Lang’ata) uliopo eneo la Kinondoni
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live




Latest Images